Unakumbuka Nini kuhusu maisha shule za bweni A level share kisa chako.

Unakumbuka Nini kuhusu maisha shule za bweni A level share kisa chako.

marco polo jr

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2020
Posts
362
Reaction score
1,771
Katika maisha shule kunakuwa kuwa na changamoto mbalimbali hasa tuliosoma shule za St kayumba mm nakumbuka baada ya kumaliza shule ya sekondari .Nilibahatika kufaulu na kupangiwa kuendelea na masomo shule moja ya boys huko mikoa ya nyanda za juu kusini.Muda ulipowadia kufunguliwa shule kijana nilijiandaa kwa ajili ya kuripoti nakumbuka tulitumiwa form za maandalizi nikanunua vitu vyote pamoja na sare .Siku ya kufunguliwa ikawadia nikabeba tranka langu na vifaa vingine mzee tulienda wote wahuni wakanipokea vifaa vyangu na kuvipeleka bwenini mm nikabakia na mzee kwa ajili ya kukamilisha Mambo Fulani .Baada ya muda kwenda nikaenda bwenini kucheki vifaa vyote hakuna kumbe wahuni walionipokea walikwenda kuviuza mtaani mm sura sikuwashika godoro ,tranka na ndoo nikawa nimepoteza dah! Sio mm peke yangu niliyeibiwa wengi tuu wanaoripoti walikuwa wakiibiwa na wababe wa pale shule form five tulikuwa tukiitwa form one wa kiangazi .nikabaki nikilia tuu mzee akaninulia vitu vingine akaniambia uwe makini ukiibiwa Tena sitokunulia toka siku iyo nikawa mbabe Sana nikaacha unyonge .ebu na ww unakumbuka ubabe gani uliokutana nao shuleni hasa za bweni.
 
Mm nakumbuka tulipigwa mikasi siku moja kabla ya mahafali yetu



Tuongeze tangawizi na limau
 
Hahaha .. Nakumbuka nimereport day one, tukaambiwa Twende Prepo usiku. Jamaa sina hili wala lile nang’aa macho na kushangaa shangaa sina cha kusoma . Naona majamaa pembeni yangu wanadiscuss topics tena wanabishana na kusolve word problems ambazo sijawahi kusikia.. nilipanic sana na kujiona nimeshafail [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]. Huu ubabe wa kuwahi masomo ulinitesa nikakonda kabisa na kujiona sipo kundi moja na wenzangu [emoji28]


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Wakati nipo kidato cha sita Iyunga Tech Mbeya kuna siku sikuingia prepo nimelala bwenini (Mkwawa) mara nasikia wahuni wanakimbizana... Tulikua na mwalimu mmoja wa nidhamu mnoko haswaa Mr. Ambonise akikudaka suspension si jambo la mjadala ndio alikua anaendesha zoezi la kudaka waliolala mda huo akiwa na baadhi ya viongozi wa wanafunzi.
Niliposhtuka kitu nilichokifanya nikavaa viatu halafu nikamwaga materials yote ya kwenye tranka chini, kisha nikaanza kupanga moja baada ya lingine, mwamba kufika pale nilipo na bonge moja la fimbo kuuliza unafanya nini? Nikajibu kuna notes natafuta hapa nilikua darasani nimerejea kuzifuata....akanicheki kwa muda akaniacha na kuelekea upande mwengine wa bweni kwa makubaliano nikimaliza niende darasani, alivyoondoka tu nikarudi kulala.
 
Nilitoka shule ya kata (Kikwete kwa hili nitamtetea mpaka unipige ngumi) nikaenda shule flani kule Kilimanjaro. Kwanza nilichagua shule mwenyewe, nilichagua kwa kuzingatia shule iko jamii gani maana mimi kuna vitu siwezi vumilia na najua viko mazingira kadhaa hapa nchini.

Sijawahi faya maamuzi niiyofurahia kama hili jambo. Shule nilipokelewa na dogo mmoja alikuwa form III akanisubiri nitoke mapokezi akabeba mizigo yangu na kunipeleka dorm moja the zuri kwa kila kitu pale shule. Maisha ya kistaarabu kwa wanafunzi na wengi wa walimu, wakorofi hawakosi. Mkuu wa shule ni the best sijawahi ona: msikivu, ana msimamo, sio mbabe wala maamuzi ya kijinga. Tulimpenda wote hata wakorofi.

Nimetoka na marafiki kibao na still madogo kibao wananitafuta hadi sasa. Huwa nakariri sana watu na sibagui eti form six asiongee na form one, hiyo sina. Nilikuwa namiliki simu kiubishi na nilifanya sana transaction za madogo hasa nauli za likizoni. Nilikuwa kiongozi wa dini. Sijawahi jutia na huwa napamiss sana pale. Nitakuwa naenda sana na isitoshe K'njaro napakubali mno.

Nilikuwa natoka sana nje ya shule. Mitaa mingi nimeenda, sikuwa mhuni hata. Sikuwa maskini hata kidogo.
 
Wakati nipo kidato cha sita Iyunga Tech Mbeya kuna siku sikuingia prepo nimelala bwenini (Mkwawa) mara nasikia wahuni wanakimbizana... Tulikua na mwalimu mmoja wa nidhamu mnoko haswaa Mr. Ambonise akikudaka suspension si jambo la mjadala ndio alikua anaendesha zoezi la kudaka waliolala mda huo akiwa na baadhi ya viongozi wa wanafunzi.
Niliposhtuka kitu nilichokifanya nikavaa viatu halafu nikamwaga materials yote ya kwenye tranka chini, kisha nikaanza kupanga moja baada ya lingine, mwamba kufika pale nilipo na bonge moja la fimbo kuuliza unafanya nini? Nikajibu kuna notes natafuta hapa nilikua darasani nimerejea kuzifuata....akanicheki kwa muda akaniacha na kuelekea upande mwengine wa bweni kwa makubaliano nikimaliza niende darasani, alivyoondoka tu nikarudi kulala.
Tulikuwa tunaita ambuuuush ticha akija usiku. Ukisikia hivyo ukiwa dorm unakimbia. Wanafunzi pamoja na utani, kwenye hili swala hatukuwa tunataniana.
 
Back
Top Bottom