Unakumbuka Nini kuhusu maisha shule za bweni A level share kisa chako.

Unakumbuka Nini kuhusu maisha shule za bweni A level share kisa chako.

Katika maisha shule kunakuwa kuwa na changamoto mbalimbali hasa tuliosoma shule za St kayumba mm nakumbuka baada ya kumaliza shule ya sekondari .Nilibahatika kufaulu na kupangiwa kuendelea na masomo shule moja ya boys huko mikoa ya nyanda za juu kusini.Muda ulipowadia kufunguliwa shule kijana nilijiandaa kwa ajili ya kuripoti nakumbuka tulitumiwa form za maandalizi nikanunua vitu vyote pamoja na sare .Siku ya kufunguliwa ikawadia nikabeba tranka langu na vifaa vingine mzee tulienda wote wahuni wakanipokea vifaa vyangu na kuvipeleka bwenini mm nikabakia na mzee kwa ajili ya kukamilisha Mambo Fulani .Baada ya muda kwenda nikaenda bwenini kucheki vifaa vyote hakuna kumbe wahuni walionipokea walikwenda kuviuza mtaani mm sura sikuwashika godoro ,tranka na ndoo nikawa nimepoteza dah! Sio mm peke yangu niliyeibiwa wengi tuu wanaoripoti walikuwa wakiibiwa na wababe wa pale shule form five tulikuwa tukiitwa form one wa kiangazi .nikabaki nikilia tuu mzee akaninulia vitu vingine akaniambia uwe makini ukiibiwa Tena sitokunulia toka siku iyo nikawa mbabe Sana nikaacha unyonge .ebu na ww unakumbuka ubabe gani uliokutana nao shuleni hasa za bweni.
Kitanda cha juu akiwa kikojozi una wakati mgumu kitanda cha chini.
 
Advanced level student unaibiwa kiboya hivyo, wakati uko Olevel hukuwahi kusikia stori za shule za bweni? Ninesoma bweni Shule za Serikali miaka 6 sikuwahi kuibiwa
Mgeni ni mgeni tu kiongozi, mimi yangenikuta hayo sema tu nilibahatika kupangwa bweni la wezi.
hao wengine waliipata maana ukienda darasani ukirudi unakuta chaga zinakuangalia
 
Nilitoka shule ya kata (Kikwete kwa hili nitamtetea mpaka unipige ngumi) nikaenda shule flani kule Kilimanjaro. Kwanza nilichagua shule mwenyewe, nilichagua kwa kuzingatia shule iko jamii gani maana mimi kuna vitu siwezi vumilia na najua viko mazingira kadhaa hapa nchini.

Sijawahi faya maamuzi niiyofurahia kama hili jambo. Shule nilipokelewa na dogo mmoja alikuwa form III akanisubiri nitoke mapokezi akabeba mizigo yangu na kunipeleka dorm moja the zuri kwa kila kitu pale shule. Maisha ya kistaarabu kwa wanafunzi na wengi wa walimu, wakorofi hawakosi. Mkuu wa shule ni the best sijawahi ona: msikivu, ana msimamo, sio mbabe wala maamuzi ya kijinga. Tulimpenda wote hata wakorofi.

Nimetoka na marafiki kibao na still madogo kibao wananitafuta hadi sasa. Huwa nakariri sana watu na sibagui eti form six asiongee na form one, hiyo sina. Nilikuwa namiliki simu kiubishi na nilifanya sana transaction za madogo hasa nauli za likizoni. Nilikuwa kiongozi wa dini. Sijawahi jutia na huwa napamiss sana pale. Nitakuwa naenda sana na isitoshe K'njaro napakubali mno.

Nilikuwa natoka sana nje ya shule. Mitaa mingi nimeenda, sikuwa mhuni hata. Sikuwa maskini hata kidogo.
Sio moshi tech mkuu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakumbuka nilifika Kituo cha mabasi kwenye ule mji saa 11 jioni EAT kutoka Dar es salaam nilipolala kutoka mkoani kwetu. Nikiwa nimevaa shamba dress na tranka langu nisijue pakwenda, ghafla nikawaona wasichana wawili weupe wamevaa sare za shule wakaja kunisalimia na kuniomba wanisaidie kubeba mizigo na kuniongoza kwenda shule.
Baada ya kuwahoji niligundua walikuwa ni form one na ndio walikuwa wameruhusiwa wanarudi nyumbani Ila waliamua kunisaidia na kurudi tena shule.
Mbarikiwe sana H na mwenzako W.
Watu wa kusini niwakarimu sana. Kwa hili nawaheshimu sana.
 
Wakati nipo kidato cha sita Iyunga Tech Mbeya kuna siku sikuingia prepo nimelala bwenini (Mkwawa) mara nasikia wahuni wanakimbizana... Tulikua na mwalimu mmoja wa nidhamu mnoko haswaa Mr. Ambonise akikudaka suspension si jambo la mjadala ndio alikua anaendesha zoezi la kudaka waliolala mda huo akiwa na baadhi ya viongozi wa wanafunzi.
Niliposhtuka kitu nilichokifanya nikavaa viatu halafu nikamwaga materials yote ya kwenye tranka chini, kisha nikaanza kupanga moja baada ya lingine, mwamba kufika pale nilipo na bonge moja la fimbo kuuliza unafanya nini? Nikajibu kuna notes natafuta hapa nilikua darasani nimerejea kuzifuata....akanicheki kwa muda akaniacha na kuelekea upande mwengine wa bweni kwa makubaliano nikimaliza niende darasani, alivyoondoka tu nikarudi kulala.

Nimejificha sana darini ilimradi tu nisiingie darasani, usiku ni kulala au stori tu na kufungiwa kufuli moja kubwa sana kwa nje na ‘dom’ leader mtiifu... siku moja Maximo katudaka Amri Abeid pale chemba ya nje ikawa noma.

Msalimie Kyege na wazee wa kuvuna wanaovusha misosi.
 
Nimejificha sana darini ilimradi tu nisiingie darasani, usiku ni kulala au stori tu na kufungiwa kufuli moja kubwa sana kwa nje na ‘dom’ leader mtiifu... siku moja Maximo katudaka Amri Abeid pale chemba ya nje ikawa noma.

Msalimie Kyege na wazee wa kuvuna wanaovusha misosi.
Kyege aliondoka pale nadhani ilikua kati ya 2011/2012 labda kama alirejea tena
 
Katika maisha shule kunakuwa kuwa na changamoto mbalimbali hasa tuliosoma shule za St kayumba mm nakumbuka baada ya kumaliza shule ya sekondari .Nilibahatika kufaulu na kupangiwa kuendelea na masomo shule moja ya boys huko mikoa ya nyanda za juu kusini.Muda ulipowadia kufunguliwa shule kijana nilijiandaa kwa ajili ya kuripoti nakumbuka tulitumiwa form za maandalizi nikanunua vitu vyote pamoja na sare .Siku ya kufunguliwa ikawadia nikabeba tranka langu na vifaa vingine mzee tulienda wote wahuni wakanipokea vifaa vyangu na kuvipeleka bwenini mm nikabakia na mzee kwa ajili ya kukamilisha Mambo Fulani .Baada ya muda kwenda nikaenda bwenini kucheki vifaa vyote hakuna kumbe wahuni walionipokea walikwenda kuviuza mtaani mm sura sikuwashika godoro ,tranka na ndoo nikawa nimepoteza dah! Sio mm peke yangu niliyeibiwa wengi tuu wanaoripoti walikuwa wakiibiwa na wababe wa pale shule form five tulikuwa tukiitwa form one wa kiangazi .nikabaki nikilia tuu mzee akaninulia vitu vingine akaniambia uwe makini ukiibiwa Tena sitokunulia toka siku iyo nikawa mbabe Sana nikaacha unyonge .ebu na ww unakumbuka ubabe gani uliokutana nao shuleni hasa za bweni.
Sisi wa Zengo boys tuna Visa vingi sana sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Boarding bana dah ....
maisha ya kula kwa table dah, nikapangwa na wahuni full ubabe muda wa msosi[emoji23][emoji23][emoji23]
kumiliki illegal material....
Naingia prepo saa mbili nipe nusu saa ni sha horizontal [emoji23][emoji23][emoji23]
Mkuu

Daah kuna uhuni najutiaga Sana kwann niliufanya

Kulia kwenye table msosi tunachukua kwenye madishi dirishani kwa kutumia kadi

Aseeh Nakumbuka Wahuni Cku Ya ugali walikuwa Hawataki kuosha madishi sa ikifika Cku ya wali Nilikuwa naiba dishi naenda nalo bwenini.. Dah

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati nipo kidato cha sita Iyunga Tech Mbeya kuna siku sikuingia prepo nimelala bwenini (Mkwawa) mara nasikia wahuni wanakimbizana... Tulikua na mwalimu mmoja wa nidhamu mnoko haswaa Mr. Ambonise akikudaka suspension si jambo la mjadala ndio alikua anaendesha zoezi la kudaka waliolala mda huo akiwa na baadhi ya viongozi wa wanafunzi.
Niliposhtuka kitu nilichokifanya nikavaa viatu halafu nikamwaga materials yote ya kwenye tranka chini, kisha nikaanza kupanga moja baada ya lingine, mwamba kufika pale nilipo na bonge moja la fimbo kuuliza unafanya nini? Nikajibu kuna notes natafuta hapa nilikua darasani nimerejea kuzifuata....akanicheki kwa muda akaniacha na kuelekea upande mwengine wa bweni kwa makubaliano nikimaliza niende darasani, alivyoondoka tu nikarudi kulala.
Bazoka bafo wapo Iyunga??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kati ya vtu vilinishinda boarding bas ni prepo asee afu nashukuru master na mtaaluma wa hyo skuli hawakuwa wanoko na wala prepo haikuwa lazma. yaan dinner ilikuwa inaanza kugawiwa saa 12 jion then mnaingia kpindi cha dini mpaka saa 2. sasa mm ikishafika saa 2 plus ile shibe yaan n mwendo wa kupiga horizontal mpaka kesho yake........

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom