Unakumbuka Nini kuhusu maisha shule za bweni A level share kisa chako.

Unakumbuka Nini kuhusu maisha shule za bweni A level share kisa chako.

Kuogeshwa kwenye mto usiku.

Hiyo ilikuwa form 5. Nimetoka kusoma day O level, sijawahi experience life la boarding. Niliona shule chungu mnoo.

Shuleni pale palikuwa na mto usiokauka maji mwaka mzima. Wakulungwa/wajuba walikuwa wanakuja usiku wa manane ukiwa umelala, wanakubeba ivoivo ulivyolala, kama ulikuwa umelala uchi unaenda ivoivo. Wanakupeleka mtoni, wanakulazimisha uzame mzima mzima. Kisha wanakurudisha bwenini na kukuamrisha upande kitandani ivoivo.

Baada ya muda likatokea bonge moja la timbwili. Form 6 & Form 4 VS Form 5 & Form 3. Ilipigwa mechi kali mpaka FFU wakaja kutuliza ghasia.

Mwisho wa siku kuna wajuba walipeperushwa na shule hawakuimaliza. Hiyo ilikuwa kama laana maana mwaka mmoja nyuma kuna mwanafunzi mmoja wa shule jirani aliuawa shuleni hapo (Lyamungo vs Umbwe).
Unforgetable
 
Tulikuwa tunaita ambuuuush ticha akija usiku. Ukisikia hivyo ukiwa dorm unakimbia. Wanafunzi pamoja na utani, kwenye hili swala hatukuwa tunataniana.
[emoji851][emoji851][emoji851][emoji851][emoji851][emoji851]

Nimecheka kishenzi, kwamba mtataniana vyooote ila kwenye Ambush lazima heshima iwepo.
Unforgetable
 
Wavulana F6 2018 ifunda tech nadhani mnakumbuka vizuri kilicho tupata.

Our motto SKILLS AND EFFICIENCY
 
Hahaha .. Nakumbuka nimereport day one, tukaambiwa Twende Prepo usiku. Jamaa sina hili wala lile nang’aa macho na kushangaa shangaa sina cha kusoma . Naona majamaa pembeni yangu wanadiscuss topics tena wanabishana na kusolve word problems ambazo sijawahi kusikia.. nilipanic sana na kujiona nimeshafail [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]. Huu ubabe wa kuwahi masomo ulinitesa nikakonda kabisa na kujiona sipo kundi moja na wenzangu [emoji28]


Sent from my iPhone using JamiiForums
Hawa mafala wa ainahyo walinitesa Sana
Yani Cku ya kwanza kwenda class nakuta jamaa wanasolve trig Mara differentiation Mara integration aseeh jamaa wanabishana kinoma.. Nilijiona mjinga na nishafeli.. Niiwakariri wale jamaa na finally necta niliwaacha mbali Sana

Nakumbuka kuna siku nilikaa bwenini nikalia Sana.. Nikamkumbuka mama alivoniambiaga kuwa kuna Maisha magum duniani.. Ckuwahi kula marage ya wadudu.. Ugali mgumu wa Dona na kande la wadudu.. Mwanzoni nilikonda Sana.. Nilikuja nikazoea na nikatusua vizuri Sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika maisha shule kunakuwa kuwa na changamoto mbalimbali hasa tuliosoma shule za St kayumba mm nakumbuka baada ya kumaliza shule ya sekondari .Nilibahatika kufaulu na kupangiwa kuendelea na masomo shule moja ya boys huko mikoa ya nyanda za juu kusini.Muda ulipowadia kufunguliwa shule kijana nilijiandaa kwa ajili ya kuripoti nakumbuka tulitumiwa form za maandalizi nikanunua vitu vyote pamoja na sare .Siku ya kufunguliwa ikawadia nikabeba tranka langu na vifaa vingine mzee tulienda wote wahuni wakanipokea vifaa vyangu na kuvipeleka bwenini mm nikabakia na mzee kwa ajili ya kukamilisha Mambo Fulani .Baada ya muda kwenda nikaenda bwenini kucheki vifaa vyote hakuna kumbe wahuni walionipokea walikwenda kuviuza mtaani mm sura sikuwashika godoro ,tranka na ndoo nikawa nimepoteza dah! Sio mm peke yangu niliyeibiwa wengi tuu wanaoripoti walikuwa wakiibiwa na wababe wa pale shule form five tulikuwa tukiitwa form one wa kiangazi .nikabaki nikilia tuu mzee akaninulia vitu vingine akaniambia uwe makini ukiibiwa Tena sitokunulia toka siku iyo nikawa mbabe Sana nikaacha unyonge .ebu na ww unakumbuka ubabe gani uliokutana nao shuleni hasa za bweni.
Hii ni ifundaaaa
 
Kuiba mahindi ya walimu usiku na kuchemsha juu ya dari, mchana kugoma kula sababu ya chakula kibaya.
Tukarudishwa nyumbani shule nzima, tukakaa home mpaka tukajisahau kama sisi ni wanafunzi. Wakati tunarudi shule tunakutana na mock ya mkoa wale wasongo wamepiga mapindi wakapasua sisi wengi tuliojua tulikua likizo tukapata marks zinazokaribia umri wetu. Ila ilipofika necta mkeka ulipinduka hatari.
Msuli wa zima moto ulikua mtamu sana.
Mwaka uliofuatia madogo wakaendeleza mtindo wetu wa mahindi, wakachoma bweni.
 
Katika maisha shule kunakuwa kuwa na changamoto mbalimbali hasa tuliosoma shule za St kayumba mm nakumbuka baada ya kumaliza shule ya sekondari .Nilibahatika kufaulu na kupangiwa kuendelea na masomo shule moja ya boys huko mikoa ya nyanda za juu kusini.Muda ulipowadia kufunguliwa shule kijana nilijiandaa kwa ajili ya kuripoti nakumbuka tulitumiwa form za maandalizi nikanunua vitu vyote pamoja na sare .Siku ya kufunguliwa ikawadia nikabeba tranka langu na vifaa vingine mzee tulienda wote wahuni wakanipokea vifaa vyangu na kuvipeleka bwenini mm nikabakia na mzee kwa ajili ya kukamilisha Mambo Fulani .Baada ya muda kwenda nikaenda bwenini kucheki vifaa vyote hakuna kumbe wahuni walionipokea walikwenda kuviuza mtaani mm sura sikuwashika godoro ,tranka na ndoo nikawa nimepoteza dah! Sio mm peke yangu niliyeibiwa wengi tuu wanaoripoti walikuwa wakiibiwa na wababe wa pale shule form five tulikuwa tukiitwa form one wa kiangazi .nikabaki nikilia tuu mzee akaninulia vitu vingine akaniambia uwe makini ukiibiwa Tena sitokunulia toka siku iyo nikawa mbabe Sana nikaacha unyonge .ebu na ww unakumbuka ubabe gani uliokutana nao shuleni hasa za bweni.
Advanced level student unaibiwa kiboya hivyo, wakati uko Olevel hukuwahi kusikia stori za shule za bweni? Ninesoma bweni Shule za Serikali miaka 6 sikuwahi kuibiwa
 
Back
Top Bottom