Suleman Jr
JF-Expert Member
- Jun 28, 2022
- 341
- 525
Umeanza vizuri lakini umemaliza vibaya,Kuna kitu mleta mada haukijui.
Hivi Kuna Mwenye upendo kama Mungu!!
Mungu ana upendo lakini hachangamani na dhambi. Hiyo stori ya JB Mpiana ni stori inasoshabihiana na sharia na matakwa ya Kiislam.
Mwanamke akiachwa akaolewa akaachwa anaruhusiwa kuolewa Tena na yule mwanaume wake wa mwanzo. Hayo ni maelekezo ya Dini. Na Yana mantiki kubwa sana.
Lakini pia Kuna jambo hawalielewi kuwa haya makanisa yanayochipukia Sasa yanaharibu sana ndoa za watu wengi.
Wanawake wengi waliopo kwenye makanisa hayo Wana migogoro mikubwa ya Ndoa na wengi wamewaacha waume zao na kuwaita kuwa ni mapepo Kwa maelekezo ya hao manabii uchwara na Mitume feki.
Wengi wamekua wakiwaambia Wanawake kuwa mwanaume akikuzingua achana naye usivumilie mateso ukafa Kwa stress.
Chaa ajabu wao manabii feki walikua wanafikiri kuwa wanaume wenye migogoro ya Ndoa ni Kwa sababu hawana akili na wanaosababisha wake zao wachepuke ni Kwa sababu hawapendi na kujali wake zao. Sasa hili ni Fundisho kuwa hata Masanja alampenda sana mkewe lakini akachepuka na kuliwa na muumini wake wa karibu.
Jambo la pili ni kuwa Binadamu ana hulka ya kupenda kulipa kisasi. Au kuona Mungu akilipa kisasi Kisha Roho yake inaridhika na kufurahia kisasi kinapolipwa.
Masanja anafuraha kubwa sana na Hana kinyongo Kwa sababu Adui yake amelipwa kisasa. Amajinyonga na kufilia mbali . Jambo ambalo Kwa Masanja ni malipo ya maovu aliyoyafanya kuingilia ndoa yake .
Masanja Hana kinyongo Tena na Marehemu mana amepata malipo ya juu kabisa yaani kama ni mtu aliyemwibia mtu Mali yake ameshahukumiwa kunyongwa. Sasa Kwa Nini Masanja asifurahiye ushindi huo. Na kwake ni ushuhuda mkubwa kuwa yeyote arakayeingilia ndoa yake atakutana na malipo mabaya kwenye maisha yake.
MASANJA kama binadamu anafuraha ya kuangamia Kwa adui yake alihujumu ndoa yake.
Pili atakayebaki na awakati mgumu ni mkewe Masanja mana hataaminika Tena kama mama Chungaji. Sio mfano wa kuigwa.Amepoteza thamani yake mbele ya jamii.
Hakuna anayependa kuona mkewe anachepuka. Na kuchepuka sio jambo la kifahari hata kidogo. Kuliona kuwa ni jambo la kawaida ni kuipotosha jamii na kujenga kizazi kisicho na maadili.
Mshahara wa dhambi ni mauti ya kiroho au hata kimwili. Mke wa Masanja ajitafakari mana dhambi hiyo itamtafuna na imemuondolea thamani yake Kwa kiwango kikubwa .
Lakini pia Masanja Kuna wakati atakua na Mawazo Mengi sana kila atakapokumbuka tukio Hilo lililomdhalilisha Kwa kiwango kikubwa.
Ni tukio mabaya kwenye jamii. Hivyo watu wasijaribu kuyahalalisha .Yakemewe na yawe ni Fundisho. Wahenga walisema Mke wa mtu ni sumu lakini Mzee wa upako akaongeza kuwa mume wa mtu ni maziwa.
Katiba mambo ambayo ni halali kumwacha mke au mume ni zinaa. Hivyo hata wasipoachana Kwa nje lakini kiroho wamevunja agano waliloapa Kwa kutumia dini hizo hizo ambazo wanazihubiri na kufunga Ndoa. Masanja anatumia Biblia kupata umaarufu lakini Biblia hiyo hiyo inakataza Zinaa na Mwanamke mzinifu sio tu anatakiwa kuachwa Bali kupigwa mawe mpaka kufa.
Ina maana mzinifu hasamehewi?
YESU aliletewa mwanamke aliekamatwa akizini akaambiwa anatakiwa apigwe mawe hadi afe lkn akawajibu "yoyote ambae anahisi hana kosa basi achukue jiwe na ampige" wale waliomkamata walitokomea kusikojulikana.
Fahamu tu sisi upande wetu tumepewa nafasi ya kutubu kujutia makosa yetu, kama kwenu haipo poleni sana.
Ila mkuu mbona sijawahi waona mkipigana mawe kisa uzinzi? Au waislam hawazini?
Sent from my Infinix X624B using JamiiForums mobile app