Unamshauri nini kijana asiye na ajira ambaye yupo tu mtaani?

Unamshauri nini kijana asiye na ajira ambaye yupo tu mtaani?

Mkuu kwa sasa nafasi za kujitolea ni kama kuomba kazi tu nazo mpaka connection
Anaweza hata kujifunza fani yoyote nyingine mtaani itakayomuingizia kipato, zipo shughulu ambazo zinachukuliwa poa sana mtaani, lakn zinaingiza kipato kinachoweza kufaa kujikimu. Siyo lazima kuangalia zaidi ajira inayohitaji elimu ya darasani.
 
Shida ni kwamba kila kijana aliyehitimu anapenda kuajiriwa kazi za ofisini.....lakini kama atapata fursa ya kulima basi ajikite kwenye kilimo tena kwa jembe la mkono...baada ya miaka miwili/ mitatu hawezi kulia njaa, aende vijijini ajiunge na vijana wanao fyatua tofali za kawaida ndani ya miaka michache atasimama vizuri kwa miguu yake
 
Ndio hio ni huko bush uko unaozeshwa yaan mke unapewa ni wazee wanaokuchakulia tu mke wanakuozesha na plot unapewa maana huko bush kuna maeneo makubwa tu hayafanyiwi chochote na wanyama wa kufuga yaan mifugo unapewa, anza maisha sasa sio huku town nani atakupa hivyo vyote?

Huku town Issue ni kutunga ndoa ya uongo na ukweli upate mtaji watu watachangishana michango ya huku na kule tembeza kadi za harusi door to door sasa ile michango michango ndio mtaji wako wa kuendeshea maisha hapo bado haujahesabu zawadi za hapa na pale utakazopewa na ndugu, jamaa na marafiki

Chukulia kadi moja mtu mmoja achangie 50,000/- wakiwa wawili wachangie 70,000/-

Wakichangia watu 100 tu

100×50,000 = 5,000,000

Hapo bado kuna wale wa kujitolea kulipia ukumbi na wakulipia misosi na kumlipa MC huku 5M bado inapumua

Hilo nimepiga kadrio la chini

Baada ya hapo songa mbele ushapewa mtaji tayari unasubiri nini? Au bado haujaisoma akili yako?
Watu mnarahisha sana mambo...mtu umechoka nani anakuchangia hizo hela[emoji3]

Ili uchangiwe lazima na ww uwe na hela/mtaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna namna jamaa una Manipulate Sana Data zako unapoandika kuhusu pesa, kiwandani mishe nyingi amount per day ni 5000 mpaka 10,000 maximum hiyo ndiyo 90% ya viwanda ukiona mtu anapata 25K kiwandani basi hiyo kazi anayofanya ukipewa unakimbia sikuhiyohiyo.

Kuhusu Tech hakuna niliposema huitaji mtaji soma Hints zangu kwa umakini sana ukishindwa kwenye Tech kwa kipengere Cha mtaji sahau kabisa kuhusu kujiajiri hii Dunia kwa kigezo cha mtaji...Tech ndio sehemu inayotoa nafasi kuanza na mtaji mdogo zaidi.
Nipo Karibu na viwanda flani min Ni 5000 ila mambo ya kichanganya Ni 2500O per day Ila niliacha baada ya kuona sio tu ngumu Bali unsafe watu kukatika vidole Ni kawaida
 
Mimi nilikuwa na wazo la kubadili maji ya chumvi kuwa fresh water. Maana eneo nililopo ni maji ya chumvi. Na washika dau wangu ni watu wa saluni na migahawa. Changamoto nataka kutumia distilation kama njia ya kufanya hvyo, ubaya wa hii njia inakula nishati sana na pia malighafi ya kuandaa kamtambo hako kdogo ni changamoto. Ila kwa hesabu za kawaida hukosi ya kula per day.
Distilled water Ni pure water unaweza uza kiwandani kwenye maabala achana na hao watu wa saluni sijui mgahawa kwanza hayafai kwa chakula
 
Nchi imejaa wasomi hawana nyuma wala mbele.

Wazazi wamechoka kununulia kifurushi,

Bahati ilimwendea mmoja tu Majaliwa,
 
Mkuu huyo kijana mwambie aende akaombe kazi kwenye makampuni ya ulinzi makubwa mfano G4S au GARDA WORLD.

Mara nyingi kwa kijana ambaye hana connection, hizi kazi za ulinzi huweza kumexpose kijana au kumuweka kwenye platforms flani ambazo ni rahisi yeye kuonekana / kuonana na watu wengi wazito ambao ni ngumu kuonana nao in a normal way.

Mfano akishaajiriwa, anaweza kuwekwa kwenye malindo nyeti kama Mahoteli makubwa (SERENA, HYYAT ,SLIP WAY, CORAL BEACH, n.k) au ofisi za BALOZI mbalimbali mfano Us embassy, EUROPEAN UNION, TURKEY EMBASSY, n.k, au pia anaweza akapangiwa lindo la mtu binafsi mwenye pesa zake, au makampuni mbali mbali ambapo kiuhalisia yatampa EXPOSURE nzuri sana. Maeneo haya ni rahisi sana Mlinzi mwenye sifa za kitaaluma kupata kazi endapo zikitangazwa, kwanza ni rahisi kuaminika na kupewa kipaumbele kuliko mtu mwingine wa nje.

Kazi ya ulinzi ni kazi nzuri sana kwa kijana anayetaka kutafuta exposure na connection huku akiendelea kusubiri na kupambania ajira ya ndoto yake aliyosomea japo sometimes anaweza pia akajikuta amepata michongo mingine mikubwa out of profession yake.

NOTE
Mungu humsaidia anayejisaidia, usitegemee miujiza ikukute huku ukiwa unashinda ndani tu unafungua mahotpot ya vyakula na kulala kama mjamzito. Ulinzi ni kazi ngumu , akubali kudharaulika, kufubaa,,kukosa usingizi,,kurisk maisha yake (kuuza roho) na mengine mengi.
 
Nchi imejaa wasomi hawana nyuma wala mbele.

Wazazi wamechoka kununulia kifurushi,

Bahati ilimwendea mmoja tu Majaliwa,
Dah hali ya ajira ni ngumu mama.ila Mungu umpa mtu kwa wakat wake tuendelee kupambana.
 
Njoo dm, nikupe mchongo wa ajira. Wakala wa ajira serikalini na sekta binafsi
Screenshot_20221110-102039.jpg
 
Nadhani kila moja wetu anafahmu kuwa hali ya maisha now imekuwa ngumu hususani kwenye swala zima la kipato na matumizi yapo juu sana. mpaka inapelekea maisha yanakuwa magumu sana, kila mtaa utakao pita utakuna na bodaboda.

Siyo kazi mbaya ila ndio kazi ambayo vijana wengi wanaweza kuifanya kupata ridhiki zao.

Sasa leo mchana nilikaa na ndugu yangu yeye kamaliza chuo lakini yupo tu mtaani, kaniuliza hivi kama nikikuomba ushauri nifanye kazi ili niingize kipato utanishauri nifanye kazi gani ghafla ghafla nimekosa jibu la kumpa.

Enyi wana jamiiforums naomba tushirikiane katika kutoa mawazo ya idea za biashara zenye uitaji wa mtaji wa kuanzia laki 1 na nusu hadi laki 3 ambazo zinaweza kuwasaidia hawa vijana wasio na ajira kuingiza kipato

Karibuni kwenye mjadala
Ajifunze kuogelea
Ashinde maeneo ya maziwa...
Aombe neema kama ya majaliwa
Napita tu..asiombee ajali
 
Aende sokoni atoe aibu achague kitu kimoja auze weather ni matunda, dagaa au mboga za majaniii akikomaa mwezi mmoja hayo mawazo ya ujobless yataisha na uzuri mtaji wa sokoni unaanza hata na laki 2 tu inatosha
 
Back
Top Bottom