Unanishaurije kusafiri peke yangu safari ya km 1000

Nimeamini tunatofautiana au kuna mlima na kichuguu,mwanaume safari ya mwakani unaanza kuifikiria leo hadi unaianzishia makala?usiwe unafikiria kidogo hivyo hayo nimambo yakawaida sana,la utakua mshamba wa magari na kusafiri
 
Dar Masasi nilipiga gia mwezi uliopita. Siku ya mwisho pumzika vya kutosha then ondoka mapema sana kama saa kumi na moja ili usianZe kuchoshwa na foleni za Dar.

Ukiondoka mapema sana unajikuta ikifika labda saa mbili tayari upo Ikwiriri.

Njia hiyo beba chakula chako hotel ni tatizo. Hakikisha gari yako ipo vizuri njia hiyo haina magari mengi na sehemu kubwa ni pori
 
Sawa mkuu asante kwa ushauri hakika nitaufanyia kazi nilale njiani coz sijawahi tumbea umbali huo,,na spidi ntazngatia pia mkuu
Poa. Hakikisha umepiga chupa moja ya Azam/ Mo Energy au Redbull kabla ya safari na baada ya masaa manne hivi piga 'kichupa' kingine. Hii itakusaidia kukuondolea uchovu na usingizi pia.
 
We unahis pancha kwa hiyo gari ina tair peke yake matatizo yako mengi kwenye gari usitembee peke yako
 
Funga mziki mkubwa ndani ya gari, weka playlist ya nyimbo zilizochangamka kama za club zile na old school rap songs ili kusudi zikupe mizuka, achilia sauti ya wastani ila inayosheheni kwenye cabin.
Kwa msaada mcheki dicksound akufanyie namna. Hutochoka na safari utaiona fupi tu!!
 
1st time nilisafirisha trekta kutoka Dar kwenda Kisaki- Morogoro, nilitoka Dar saa 5 Usk nilifika saa 10jion bila ya kupmzka.. 2. 10/2017 Nilisafirisha Trekta nyngne Swaraj 855Fe kutoka Dar mpk Mlimba( kutoka ifakala mjini mpk mlimba ni masaa 6 kwa Noah) nilitumia Siku 3 na nilipumzk Masaa 8 tu nilipita mikumi SAA 2 usiku....! Kabla ya hapo nilizoea kuendsh 30km tu... Xo unawez ukiamua ila kama ni mdhaifu wa usingz.. Husitembee pk yako...
 
Huwa natumia njia moja nyepesi sana.
Nabeba chupa za kutosha za maji, kila saa nakunywa njiani, hiyo itanifanya nisimame mara kwa mara kupunguza maji na kujinyoosha kabla sijaendelea.
Kila baada ya 200 km nasimama kwa dk 10-15 hasa kwa safari ndefu sana.
Nikisikia usingizi nashusha vioo vya mbele vyote halafu naongeza mwendo kidogo nipigwe upepo. Otherwise nakutakia safari njema mkuu.
 

Saafi mimi nianze na kaswali kadogo tu, hizo 300km ulitembea na mtu? na je ulitumia masaa ma ngapi ku cover? na je ilikuwa wakati wa usiku au mchana?


safari ya Ruvuma nimeifanya maranyingi kwa private car hivyo nina mengi ya kukushirikisha.....):
 
Duuh mkuu sawa ila sijapata mtu sasa
Safari ndefu unaweza kuenda.. Kikubwa usikimbie kuwa na goals.. Utaenda wapi mpaka wapi kwa muda gani.. Huwa ndio nafanya hivyo.. Inanisaidia nisiende mbio au nisiende taratibu sana inaset uchovu mwingi.

Usitumie Ac.. Huwa naona haina haja kama unatembea zaidi ya 80km/h ukionanguvu inapungua kaa nyuma ya gari.jingine au hata Lori.. Nenda nalo taratibu.
 
[QUOTE="pipikijiti[/QUOTE]
Inawezekana kabisa kusafiri umbali huo peke yako ila unakuwa mpweke sana. Vizuri kuwa mtu pembeni lakini usitoe lift kwa mtu ambae humjui vizuri, kwakuwa akiwa mtu hamuendani kimaongezi hiyo safari itakuwa ndefu zaidi kimawazo.
 
Kabla ya kuanza safari pitia vituoni chukua abiria hata wawili watatu kwanza ni ulinzi tosha halafu kale ka hela wanakatoa unapunguza gharama za Mafuta. Hizo ndiyo zetu huku pande za usukumani kahama.
 
Dah! Umetoa ushauri wa muhimu sana!

Juzi nimesafiri kutoka Arusha kuja Dar usiku kuanzia saa 6 ili nikwepe matrafiki.

Nilipanga nisizidi kasi ya km 100 ili endapo ikitokea tatizo niweze kumudu gari.

Barabarani shida ni nyingi, kuna kugonga wanyama nk Hivyo ukiwa kasi sana utashangaa kumgonga Mbwa tu kunapindua gari lako.

Safari ilikuwa ndefu lakini nilifanikiwa kufika Dar salama kwenye majira ya saa 2 asubuhi.
 
Tecniq

Hakuna technique nzuri kwenye kuendesha gari hasa kwa safari ndefu kama kukaa nyuma ya gari jingine.

Hii ilinisaidia kuua kipande cha Same - Korogwe kwa muda mchache kuliko kawaida.

Safari mkiwa wawili watatu mnafuatana inapunguza uchovu na pia inakuhakikishia usalama na msaada endapo likitokea tatizo.
 
Juzi nimesafiri kutoka Arusha kuja Dar usiku kuanzia saa 6 ili nikwepe matrafiki.

Safari ilikuwa ndefu lakini nilifanikiwa kufika Dar salama kwenye majira ya saa 2 asubuhi.
Safii.. Hata ivyo kusafiri kwa masaa nane inaonekana ulikuwa unapepea...
 
[QUOTE="pipikijiti
Inawezekana kabisa kusafiri umbali huo peke yako ila unakuwa mpweke sana. Vizuri kuwa mtu pembeni lakini usitoe lift kwa mtu ambae humjui vizuri, kwakuwa akiwa mtu hamuendani kimaongezi hiyo safari itakuwa ndefu zaidi kimawazo.[/QUOTE]
Poapoa sugu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…