Unapoongoza elewa kuwa wewe ni kiongozi tu! Tabia za kufokeana Kama watoto peleka Kwa watoto wako nyumbani

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema Wakuu!

Kuna viongozi wakipewa dhamana wanarukwa sijui na akili, wanafoka foka, kufokeana watu wazima ni kudhalilishana tu.

Hakuna aliyekulazimisha uteua mtu, Kama mtu kaboronga fukuza kazi, sheria zingine zifuate.

Sio kupewa tuu uongozi unajifanya mkoloni ndani ya nchi, na kuwabagaza wasaidizi wako kama vile Wake zako.

Usilete mambo ya kijeshi kwenye uongozi hasa Kwa kizazi hiki.

Ukitaka ubabe na kufokeana nenda kaombe Cheo jeshini huko, ndipo kuna ubabe ubabe na kufuata amri. Tena nadhani haa jeshini kunataratibu zake.

Unakakuta kakijana kadogo tuu kanafokea watu wazima waliokazidi umri kisa kana uongozi.

Nyie Wazee wapumbavu, wajinga,
Sijui ninyi ni majizi, mafisadi, utadhani Yeye ndiye Jaji au hakimu aliyethibitisha hatia ya Msaidizi wake.

Tuheshimiane.
Huwezi mfokea mtu hadharani ili upate sifa Kwa watu, uonekane Mchapakazi na mwema.

Vijana wadogo, mnaoingia kwenye Siasa jihadharini na mambo ya kufokea watu ilhali mnatumikia Umma!

Ukitaka kufokea watu anzisha Kampuni yako, fokea Wafanyakazi wako,
OA na zaa watoto wafokee hao ndio halali yako.
Hata mke anayejielewa huwezi mfokea kipuuzi puuzo akakuvumilia.

Taratibu zipo, andika barua au sema sina kazi, Kama ni mwizi kesi ipelekwe mahakamani.

Lakini sio watu tutoe Kodi zetu ili utufanye Kama watoto wako, hiyo hapana! Umezoea kufoka kafoke huko kwenu!

Hii ni nchi, hili ni taifa! Sio jamii au kikundi Fulani cha watu! Au kitaasisi Fulani! Lazima viongozi wajue hilo.
Lazima wajue nchi hii inamakabila zaidi ya 120 na watu wa kila namna. Hivyo heshima kitu cha Bure!

Unapewa uongozi unataka kuleta mambo ya kwenu huko kwenye nchi,

Ukiongoza uwe na adabu na heshima ili uheshimiwe!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
 
Utafokewa tu kama kura aina nguvu ya kuamua nani akae madarakani na nani aondoke.
"Ukipewa" cheo wajibu wako unakuwa zaidi kwa yule aliyekupa cheo
Hapana!

Embu fikiria Taikon napewa kacheo Fulani alafu nakuja kumfokea Baba yako au mtu aliyelingana na Baba yako ambaye kanizidi Hadi Mimi umri.

Huko ndio kuvurugwa
 
Hapana!

Embu fikiria Taikon napewa kacheo Fulani alafu nakuja kumfokea Baba yako au mtu aliyelingana na Baba yako ambaye kanizidi Hadi Mimi umri.

Huko ndio kuvurugwa
Taikon ndio kazi zilivyo.

Shida yetu waafrika hatuwezi kujiongoza na kujisimamia,

Unakuta kazi zimelala,mzee hana time na wewe unapokea shit toka juu,sasa kila mtu ana namna yake ya kupokea pressure.
Ila heshima iwe pande zote inabidi pia wazee wafanye majukum yao kwa weledi.
 

Sio kwenye Siasa za Afrika ambazo mtu anakufokea Kwa lengo la kujipatia point kwako.

Mbona kina Mtaka hapo Dodoma hawafanyi hivyo, au kina Jokate
 
Dawa yao ni kuwaloga busha likae mdomoni washindwe kufoka-foka kama wana hip-hop
 
Mfokaji mmoja atiwe aibu ili wafokaji wengine waache

Embu fikiri, ati ninakuteua alafu nikipuyanga kidogo unanigeuza punch bag kunipiga ili kujikosha mbele za watu
Sijali heshima yako, watoto wako, Mkeo wala cha nini! Huo si ujuha huo.

Uungwana ni vitendo
 
Ninyi ndio watumishi pasua kichwa maofisini.
 
Embu fikiri, ati ninakuteua alafu nikipuyanga kidogo unanigeuza punch bag kunipiga ili kujikosha mbele za watu
Sijali heshima yako, watoto wako, Mkeo wala cha nini! Huo si ujuha huo.

Uungwana ni vitendo
Haiko sawa, wengi wa wafokaji wamepungukiwa na utimamu wa akili. Wakimbizwe Mirembe na waanzishiwe matibabu haraka sana
 
Una bahati hujafanya kazi chini yangu; ningekufokea na kazi ningekufukuza!

Wewe ndio unabahati Kwa kuepuka kupata hasara na kuku-trendisha Kwa aibu ambayo ungeipata kutoka kwangu.

Mimi huwezi kunioshea nikakuacha, majibu ungeyapata palepale ili iwe fundisho Kwa wengine wapuuzi wenye tabia Kama hiyo.

Heshimu watu uheshimiwe
 
Nami nina bahati ya ku deal na frustrated personnel kama wewe. Na Nina wanyooshaga kweri kweri. Na wewe ningelikunyoosha!!!
 
Nami nina bahati ya ku deal na frustrated personnel kama wewe. Na Nina wanyooshaga kweri kweri. Na wewe ningelikunyoosha!!!

Siku zote mshindi hutokea mwishoni!

Hiyo ndio Kauli nakuachia,
Wewe endelea kufokafoka siku ukutane na wanaume tutakunyoosha ili ujifunze kuwa na heshima.

Fokea mtoto na Mkeo nyumbani, na kwenye Kampuni zako lakini usilete ushamba wako kwenye nchi hasa Zama hizi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…