Unawafahamu watu waliofanikiwa kwa kuwatoa kafara watu wao wa karibu?

Unawafahamu watu waliofanikiwa kwa kuwatoa kafara watu wao wa karibu?

Utajiri unatokana na mipango na juhudi, hata uende kwa mwamposa kama hauna mipango na juhudi utaendelea kuwa maskini. Ndio maana humu Kuna watu wanasema walokole wengi ni maskini kwa sababu mtu anashinda kanisani anaacha kufanya kazi kwa bidii kutafuta maendeleo
 
Watu wanajidai hawafahamu haya mambo ndio maana wanakuja na nyuzi zao kujidai wanatafuta uhakika.
Wamuulize UMUGHAKA

Ukifuatilia story za kila familia duniani unaweza kusema ni za kutatanisha sana ila kiwango cha utajiri na umaarufu ndio unazifanya familia nyingine kuongelewa zaidi kuliko familia nyingine.
Unadhani kwanini?
 
Mimi namjua mmoja alikua rafiki wa mama yangu utajiri wake ni wa kutumia nyota za wafanyakazi wake
Ila ilipofika mwaka 2018 ikabidi amtoe mtoto wake na akafanya hivyo

Ashawahi kumshawishi mama yangu ajiunge huko mama akakimbia nduki na urafiki ukaisha.

Alikuja dar kama housegirl kutoka Upareni ila sasa hivi ni tajiri.
Duh! Aisee 🤔
 
Ila najiuliza swali Moja kwanini watu wengi ambao inasemekana wana utajiri wa kichawi, hawana utajiri mkubwa wa kumfikia bakhresa, mo dewji au hata Reginald Mengi 🤔 wengi utakuta Wana vighorofa viwili mjini, ndo utajiri wa kichawi huo ephen_
Hapo ndio utajua kwamba hakuna utajiri wa kishetani.

Maana watu wanaodai kuna utajiri wa kishetani ukiangalia huo utajiri wao bado ni wa kiwango cha chini sana.

Hawamfikii hata Mo Dewji, Bakhressa au Dangote.

Kama mtu anadai kuna utajiri wa kishetani, Kwa nini asiutumie kwa nguvu zake zote awazidi matajiri wakubwa duniani kama Elon musk, Jeff Bezos, Billgates, Warren Buffett na wengineo?

Utakuta mtu anadai kuna utajiri wa kishetani lakini maisha yake ni ya kimaskini halafu anakomaa tu kuna utajiri wa kishetani!!!

Kuutumia atajirike, hataki.

Unajua hawa waafrika hasa watanzania maskini wana mentality za kijinga sana.
 
Utajiri unatokana na mipango na juhudi, hata uende kwa mwamposa kama hauna mipango na juhudi utaendelea kuwa maskini. Ndio maana humu Kuna watu wanasema walokole wengi ni maskini kwa sababu mtu anashinda kanisani anaacha kufanya kazi kwa bidii kutafuta maendeleo
Upo sahihi Kbsa mkuu
 
Hapo ndio utajua kwamba hakuna utajiri wa kishetani.

Maana watu wanaodai kuna utajiri wa kishetani ukiangalia huo utajiri wao bado ni wa kiwango cha chini sana.

Hawamfikii hata Mo Dewji, Bakhressa au Dangote.

Kama mtu anadai kuna utajiri wa kishetani, Kwa nini asiutumie kwa nguvu zake zote awazidi matajiri wakubwa duniani kama Elon musk, Jeff Bezos, Billgates, Warren Buffett na wengineo?

Utakuta mtu anadai kuna utajiri wa kishetani lakini maisha yake ni ya kimaskini halafu anakomaa tu kuna utajiri wa kishetani!!!

Kuutumia atajirike, hataki.

Unajua hawa waafrika hasa watanzania maskini wana mentality za kijinga sana.
We jamaa bado unakazia msimamo wako tu kwamba Mungu Wala utajiri wa kishirikina havipo eeh😅
 
Mimi namjua mmoja alikua rafiki wa mama yangu utajiri wake ni wa kutumia nyota za wafanyakazi wake
Ila ilipofika mwaka 2018 ikabidi amtoe mtoto wake na akafanya hivyo

Ashawahi kumshawishi mama yangu ajiunge huko mama akakimbia nduki na urafiki ukaisha.

Alikuja dar kama housegirl kutoka Upareni ila sasa hivi ni tajiri.
Duh yani mtu unatafuta ajira ujikwamue kimaisha kazi unapata na nyota yako inachukuliwa. Hatari sana
 
Nakumbuka nipo mdogo Moshi huko kuna nyumba moja ina mtoto/kijana ambae akili zake sio nzuri, yule kijana ilikuwa kila ikifika jioni ya saa 12 analia kama ng'ombe na kweli kwao wanafanya biashara ya kuuza nyama mjini /Dar na unaambiwa walikuwa wanauza balaa.
Jioni ndio mida ya kufunga biashara/hesabu!!
😮😮😮
 
Ofisi za Freemasons kwa DSM ziko wapi ? Ukiachana na jengo la mason hall posta mwenye kujua anijuze ndugu zanguni
 
Ila najiuliza swali Moja kwanini watu wengi ambao inasemekana wana utajiri wa kichawi, hawana utajiri mkubwa wa kumfikia bakhresa, mo dewji au hata Reginald Mengi 🤔 wengi utakuta Wana vighorofa viwili mjini, ndo utajiri wa kichawi huo ephen_
mbona jibu jepesi sana hilo.
Ila ninaweza kukuuliza swali pia
Unahisi Iq zao, na creativity zinafanana? na muda walio initiate?
 
Namfahamu jamaa mmoja alikuwa tajiri sana enzi sisi tunakuwa jamaa alikuwa anatumia baiskeli tu kama usafiri wake binafsi ila alikuwa na magari mengi tu.

Ajabu alikuwa na hilux ya mizigo ila bidhaa za duka lake alikuwa anafuata yeye mwenyewe kwa baiskeli yake ila kwa wengine anakodishia hizo gari za kubeba mizigo.

Sisi tulizoea kumuita TAJIRI MCHAFU wananzengo walikuwa wanasema kamtoa sadaka mdogo wake na huyo mdogo mtu alikuwa chizi fresh anakaa hapo dukani kwa kaka yake tu na hakuna wakumtoa hapo.

Haya mambo yanawezekana ila nafikiri ni mateso sana.
Kuna watu wanabishia hiki kitu ila haya mambo yapo sana
 
We jamaa bado unakazia msimamo wako tu kwamba Mungu Wala utajiri wa kishirikina havipo eeh😅
Kama vipo nenda kavitumie kwa nguvu zako zote, Uwazidi matajiri wakubwa duniani kama Elon musk na Jeff Bezos.

Wewe si unadai na kuamini kuna utajiri wa namna hiyo, Mbona umeshindwa kuutumia au mbona huutumii ili utajirike?
 
Kuna watu wanabishia hiki kitu ila haya mambo yapo sana
Kama unajua yapo, mbona huyatumii?

Kama unajua mambo hayo yapo, Mbona umeshindwa kuyatumia kwa juhudi zako zote, Uwazidi matajiri wakubwa duniani kama Elon musk au angalau basi ufikie utajiri wa kina Bakhressa?

Mbona waafrika hawautumii huo uchawi wao kuwazidi wazungu?

Tumieni huo uchawi kujenga viwanda vikubwa, barabara za juu (fly overs), Airports, Ports, shule na hospitali na mlete maendeleo kwenye jamii zenu kwa kutumia huo uchawi.

Kama kweli huo uchawi wenu una nguvu na unafanya kazi kweli.
 
Waniulize Mimi,nimewahi kuishi kwenye utajiri wa nguvu za kishirikina na Nina Wajua watu wangu wa karibu ambao wanaishi na utajiri huo!

Lakini pia,binafsi hadi hivi Sasa Nina Wajua watu wawili (wataalamu) ambao wanatoa utajiri wa nguvu za Giza,mmoja yupo Zanzibar na Mwingine yupo Malawi!

Mkuu maisha yangu ni simulizi tosha,sema kwasababu ya wapumbavu wa hapa JF huwa naamua tu kukaa kimya maana ukibishana na mjinga yawezekana ukawa mjinga zaidi yake!

Nimewahi hadi kulala na maiti hapo Malawi ili nifanikiwe na nilifanikiwa sema ndo hivyo maisha yangu yote ya mafanikio wanawake ndo huwa kikwazo kwangu !

Mtu anakuja hapa anabisha hata hajawahi Kutembea popote zaidi ya kutoka Mbeya kuja Dar au kutoka Dar kwenda Arusha !

Sihitaji kuuliza Kwa mtu Mimi mwenyewe ndiye ushuhuda !

Kama watabisha ngoja waendelee kubisha but for now Sina muda wa kubishana na Abharisya!
Usishangae ukatafutwa PM na huyu huyu aliyekataa uwepo wa utajiri wa namna hii akataka umpe connection ya Malawi😀
 
Mojawapo ya story huwa nazisikia sana na mtu kuwatoa watoto wake au ndugu zake kafara ili afanikiwe katika biashara au siasa. Utoaji kafara huwa unaelezewa kwa mtu huyo aliyoetolewa kafara kufariki kwa kinachodhaniwa kifo cha utata au kupatawa matatizo ya akili(kichaa).

Unaweza kuonyeshwa kichaa fulani ukaambiwa huu ni mtambo wa kutengeneza pesa wa tajiri fulani au ndio chanzo cha mafanikio cha mwanasiasa fulani.

Unajuaje au unathibitishaje kwamba fulani amefanikiwa kwa sababu ya kafara ya mtoto, mzazi, mke au ndugu yake?
Ndugu yangu wa kifikia; mtoto wake wa kwanza ana utindio wa ubongo, na mtoto wake wa pili na wa mwisho alizaliwa mlemavu wa miguu ILA sikuwahi kusikia anahusishwa na imani za kafara ajabu alilaumiwa mke wake kwamba ana mikosi.

Naamini angekuwa na uchumi wa kutisha ama nafasi ya cheo basi hizi tuhuma zingemhusu moja kwa moja.

Japo sikatai haya mambo yapo.
 
Back
Top Bottom