Hiyo ni nyungu sio uchawi Wala nini.
Mimi na ndugu zangu wa ukoo yaani watoto wa baba mkubwa, mdogo, shangazi, wapwa na wajomba.
Kipindi hicho nilimaliza kidato Cha sita ila kaka zetu wamemaliza vyuo kikuu na wengine elimu mbalimbali na hakuna aliye na kazi.
Tukatakiwa turudi kijijini na tulifanya hivyo .
Babu yetu aliyafanya hayo yote usiku wa manane kipindi Cha Giza Totoro.
Nakumbuka maneno ya babu akisema yeye Hana kinyongo na Mizimu ya Ukoo Haina kinyongo twende tukapambane na tukalukishwa moto.
Asubuhi ikaanza pungo, hili nadhani kwa wazaramo na wandengereko wanalijua, nakumbuka ilivyofika zamu yake akasema anatenda kama ilivyo ada kama walivyo tenda Babu wa Babu yake.
Baada ya hapo tukaenda kufanya usafi makaburini na kaburi la mwanzilishi wa ukoo huku tukitamka kile tukitakacho na chale zikahusika huku akichinjwa mbuzi mweusi, mweupe na mwekundu.
Hivyo wajukuu tukapambane na tusiwe na hofu nasi zamu yetu itafikia.
Mimi nilikaa miezi mitatu tu nikawa nachagua kazi ila kaka zangu wote walipata kazi na dada zetu wa Ukoo.
Rest in peace Babu ndevu Sina Tena wa kumtania nikipata maokoto pindi niludipo.