"Ungekuwa Mzuri ungekuwa Umeolewa" kauli hii Wanawake wanapenda kuambiana inaukweli kiasi gani?

Kila mtu huoa au huolewa na wa level yake,

Hakuna Mwanamke akawa mbaya kwa wanaume wote,suala la kuoa au kuolewa ni uamuzi wa mtu binafsi na pia hua ni riziki inayotoka kwa Mungu.

Lakini MTU anaweza kuikataa riziki Kutoka Kwa Mungu.
Yaani unapewa riziki yako lakini hauitaki Kwa sababu huridhiki nayo.
Vipi Hilo?
 

😀😀

Sasa kizuri kikikosa Mtazamaji kitaendelea kuwa Kizuri? Yàani Ipi faîda ya Ûzuri ikiwa hakuna Mtazamaji?

Au ndîo ûzuri Usio na Tija?

NI Sawa na Mtu aambiwe anaakili lakini Akili Zake hazitumii Wala kutumika,
Au Mtu awe na Pesa lakini hakuna watumiaji au hazitumiki .
 
Mabishano ndo wanaume hawapendi Ila sio smartness .

😆😆

Challenge ni muhimu sana.

Darasani Mwalimu Kilaza Hapendi mwanafunzi anayemchallenge, ni kawaida waalimu Wakali wengi kuwa na uwezo mdogo katika kufundisha na kujua contents

Mwanamke huwa mbishi akishagundua uwezo wako mdogo au akitilia Mashaka uwezo wako.

Lakini Wakati mwingine Mwanamke hubisha ili Kupima Uelewa wako kuhusu kile anachokubishia.
Wanawake most of them wàpo hivyo hasa wale Smart
 
Umeona eeh raha ya uzuri watazamaji wawepo

Ila watz tunapenda kujiliwazia matatizo yetu kwa kutumia maisha ya wengine
 
Amina👊
 
Uzuri tabia ni vile hawa wakina delila wanazani sisi tunangalia sura na shepu wakati wa kuoa
 




Challenges muhimu ila usimchallange MTU Ila challenges mambo yake.

Sio unakaa unasema wanaume wafupi wabaya au wanawake wembamba wabaya hii itaonesha haupo smart.
 
Umeona eeh raha ya uzuri watazamaji wawepo

Ila watz tunapenda kujiliwazia matatizo yetu kwa kutumia maisha ya wengine

Labda awe miss world, au ûzuri wake unatumika kwèñye matangazo ya biashara, au air hostess, au tourhostess au receptionist katika maduka, hoteli au biashara, au video Vix sijui video queen.

Sasa hujaolewa, hufanyi biashara yoyote, ûzuri wako hautumiki popote unafikiri Hiko kichambo utakachopewa na Waja hakitakuwa na mantiki?

Uzuri lazima úwe na Tija.
Yani ukisikia kitu NI kizuri ujue kina mambo yafuatayo;
1. Kinafurahisha,
2. Kitamu
3.kina rahisisha mambo au Vitu na kina ufanisi.
 
Mimi kwa mtazamo wangu na kwa upembezi wa mambo nimejionea baadhi ya mambo.
1. Unaweza ukawa umevutiwa na Mwanamke ukahangaika mpaka ukapata mawasiliano yake mkaanza kuwasiliana vizuri mpaka kuanza kuitana majina yote mazuri lakini unakuta, Mwanamke anakuwa na mambo ya kuvunja moyo sana anaomba Vocha unamtumia bando la data na kifurushi hata kukupigia simu hapigi hata kukusalimia kwa ujumbe pia no ngumu nayo. Huwa inafadhaisha sana.

2. Anavaa anapendeza vizuri lakini kila siku anakwambia sijaoga na anataka ale chipsi 🤣🤣🤣

Mambo ni mengi sana kwahaya mawili tayari kwangu anakuwa ameshapoteza sifa ya kuwa Girlfriend kabisa.
 

Mwanamke WA aina hiyo anakuwa hajakupenda.
Wengi Kutumia Mbinu hizo kupunguza idadi ya waliofanya Application 😃
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…