Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza watumishi wa Halmashauri ya Wilaya Mlele wahamie mara moja kwenye nyumba 11 zilizokuwa za wajenzi wa Barabara ya Inyonga-Mlele na kukabidhiwa kwa halmashauri hiyo.
Watumishi ambao ameagiza wahamie kwenye nyumba hizo ni Afisa Usalama wa Wilaya (DSO), Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Mlele (OCD), Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele, Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mlele (DMO)pamoja na watumishi wengine wa Hospitali ya Wilaya.
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana (Desemba 13, 2022 )wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Mlele mkoani Katavi baada ya kujionea mwenyewe kuwa zimetelekezwa na zinaharibika kwa kukosa uangalizi. “Watumishi wanahangaika hawana makazi, nyumba zimeachwa nyasi zimeota hadi kwenye korido.
Watumishi wote wanaopaswa kuhamia katika nyumba hizi baada ya kumaliza mkutano huu kila mmoja aende kwenye yake na ahamie.
Mkurugenzi naomba orodha ya majina ya watakaohamia.”
Watumishi ambao ameagiza wahamie kwenye nyumba hizo ni Afisa Usalama wa Wilaya (DSO), Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Mlele (OCD), Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele, Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mlele (DMO)pamoja na watumishi wengine wa Hospitali ya Wilaya.
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana (Desemba 13, 2022 )wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Mlele mkoani Katavi baada ya kujionea mwenyewe kuwa zimetelekezwa na zinaharibika kwa kukosa uangalizi. “Watumishi wanahangaika hawana makazi, nyumba zimeachwa nyasi zimeota hadi kwenye korido.
Watumishi wote wanaopaswa kuhamia katika nyumba hizi baada ya kumaliza mkutano huu kila mmoja aende kwenye yake na ahamie.
Mkurugenzi naomba orodha ya majina ya watakaohamia.”