Dam55
JF-Expert Member
- Oct 8, 2015
- 5,641
- 11,958
Habari Kaka, mimi ni Mama wa watoto wawili, nimeolewa ndoa yangu ina miaka 7 sasa, mwkaa jana nilikorofishana na mume wangu, nilimfumania na dada wa kazi. KutoKana na kunidhalilisha nilichukua jukumu la kuondoka ili kumuacha, lakini alikuja kuomba msamaha nikamsamehe, lakini nilishindwa kusahau, nikiwa katika upweke huo nilijikuta naanzisha mahusiano na X wangu.
Mahusiano yaliendelea mpaka mwaka huu mwanzoni, mume wangu aligundua, nikamuambia kuwa nimemua kulipa kisasi kwakua nayeye alichepuka. Hicho kitu kilimuumiza sana mume wangu, akanifukuza na kusema kuwa hanitaki. Baada ya kuondoka kwa mume wangu nilibaki mwenyewe, nilienda kupangisha, X wangu hakuniacha, aliniambia kuwa nitafute pesa tufungue Biashara.
Nilikubali, nikatafuta pesa kwa kuchukua mkopo kazini tukafungua duka kubwa la spea, kwakua nilikua nakusoma nilisema kama tunafungua duka basi liwe duka la jina langu. Alikubali nikajua kuwa ananipenda, tulifungua duka, mimi nilichukua mkopo kazini, nikaweka milioni 15 na yeye akaweka milioni 15. Baada ya hapo kila kitu kilibaki jina langu, nikawa nasimamia mimi kila kitu.
Mke wake alijua na kuanza kunisumbua, mimi sikujali kwani kama ni ndoa ya kwangu ilishakufa. Tatizo Kaka lipo kwa huyu mwanaume, duka ni langu lakini sijui pesa zinaenda wapi? Yaani kitu kidogo anachukua pesa dukani, anasema kuwa atarudiasha lakini harudishi. Mwanzo nilimvumilia, lakini sasa hivi nimechoka, anajenga yeye na mke wake, wanakuja kuchukua vitu dukani kwetu ila kulipa inakua ngumu. Yaani duka la milioni 30 sasa hivi vitu vilivyobaki hata milioni 10 havifiki na zote kala yeye.
Nikikasirika ananiambia kuwa ataniacha, kaka nampenda, mume wangu ameshaniacha anaishi na mwanamke mwingine, nina watoto wawili naishi nao, mume wangu hahudumii watoto kwa chochote, nimehangaika ustawi wa jamii mpaka nimechoka, huyu mwanaume naye hahundumii watoto wangu, nina mimba yake ananiambia nikizaa wakwake ndiyo atahudumia, nimechaganyikiwa sana Kaka, naomba msaada wako, sitaki kumpoteza mimi nitakua mtu wa kuachwa mpaka lini?
Ingekuwa wewe ungemshauri nini mtu kama huyu?
Mahusiano yaliendelea mpaka mwaka huu mwanzoni, mume wangu aligundua, nikamuambia kuwa nimemua kulipa kisasi kwakua nayeye alichepuka. Hicho kitu kilimuumiza sana mume wangu, akanifukuza na kusema kuwa hanitaki. Baada ya kuondoka kwa mume wangu nilibaki mwenyewe, nilienda kupangisha, X wangu hakuniacha, aliniambia kuwa nitafute pesa tufungue Biashara.
Nilikubali, nikatafuta pesa kwa kuchukua mkopo kazini tukafungua duka kubwa la spea, kwakua nilikua nakusoma nilisema kama tunafungua duka basi liwe duka la jina langu. Alikubali nikajua kuwa ananipenda, tulifungua duka, mimi nilichukua mkopo kazini, nikaweka milioni 15 na yeye akaweka milioni 15. Baada ya hapo kila kitu kilibaki jina langu, nikawa nasimamia mimi kila kitu.
Mke wake alijua na kuanza kunisumbua, mimi sikujali kwani kama ni ndoa ya kwangu ilishakufa. Tatizo Kaka lipo kwa huyu mwanaume, duka ni langu lakini sijui pesa zinaenda wapi? Yaani kitu kidogo anachukua pesa dukani, anasema kuwa atarudiasha lakini harudishi. Mwanzo nilimvumilia, lakini sasa hivi nimechoka, anajenga yeye na mke wake, wanakuja kuchukua vitu dukani kwetu ila kulipa inakua ngumu. Yaani duka la milioni 30 sasa hivi vitu vilivyobaki hata milioni 10 havifiki na zote kala yeye.
Nikikasirika ananiambia kuwa ataniacha, kaka nampenda, mume wangu ameshaniacha anaishi na mwanamke mwingine, nina watoto wawili naishi nao, mume wangu hahudumii watoto kwa chochote, nimehangaika ustawi wa jamii mpaka nimechoka, huyu mwanaume naye hahundumii watoto wangu, nina mimba yake ananiambia nikizaa wakwake ndiyo atahudumia, nimechaganyikiwa sana Kaka, naomba msaada wako, sitaki kumpoteza mimi nitakua mtu wa kuachwa mpaka lini?
Ingekuwa wewe ungemshauri nini mtu kama huyu?