James Comey
JF-Expert Member
- May 14, 2017
- 8,759
- 14,831
Sasa unafikiri kipi kitaanzaTofautisha kurudi Kwa Yesu Kwa HUKUMU na kunyakuliwa Kwa WATAKATIFU duniani ilhali mambo mengine yakiendelea kama kawaida.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sasa unafikiri kipi kitaanzaTofautisha kurudi Kwa Yesu Kwa HUKUMU na kunyakuliwa Kwa WATAKATIFU duniani ilhali mambo mengine yakiendelea kama kawaida.
Unyakuo utokeapo, Kuna wengine hawatajua kabisa kilichotokea, na kitachoanza ni Unyakuo.Sasa unafikiri kipi kitaanza
Hakikisha wakati wa kulala unakula na kushibaSalaam,Shalom!!
Nalikuwa katika Roho, usiku, ndani ya nyumba, ghafula nikapata uwezo wa kuona nje mawinguni.
Naliona jeshi kubwa la Malaika na WATAKATIFU wakiongozwa na jemedari mkuu, Yesu Kristo, amevaa taji yenye kungaa sana kichwani mwake, mikononi alishika upanga ungaao sana, alipita mawinguni amepanda farasi mweupe, na farasi huyo alipita akikanyaga mawingu kama farasi apitapo Nchi kavu,Majeshi ya Malaika yalifuatana naye wakiwa pia wamepanda juu ya farasi weupe Kila Mmoja, na baada ya Mfalme Yesu kupita akiambatana na Majeshi ya Mbinguni, aligeuka na kunitizama huku usoni mwake akiwa ametabasamu.
Nilijaribu kutaka kuwaonyesha Walio karibu yangu Ili waangalie juu na kuona kinachotokea lakini sikuona aliyebahatika kuona nilichoona, nilitamani kumfuata huko aliko mawinguni Ili kufurahi na kuambatana naye lakini baada ya kunitizama, akageuka na kuendelea na msafara wa Majeshi ya Malaika na WATAKATIFU wake.
.......Mwisho wa taarifa......
Source: Niliyoyaona na kuyaandika, yapo katika vifungu hivi ndani ya BIBLIA.
(Waraka wa Yuda 1:14)
Na Henoko, mtu wa Saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, angalia Bwana alikuja pamoja na WATAKATIFU wake, maelfu elfu. Ili afanye HUKUMU juu ya watu wote.
Ufunuo wa Yohana 14:1-5,
1: Kisha nikaona na tazama huyo mwana kondoo, amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye Jina lake na Jina la baba yake limeandikwa katika VIPAJI vya NYUSO ZAO.
Ufunuo wa Yohana 19:11-16.
11: Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi weupe, na Yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa- Kweli, naye Kwa HAKI ahukumu na kufanya vita.
12:Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya KICHWA chake, vilemba vingi, naye ana Jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila Yeye mwenyewe.
13: Naye amevikwa vazi lililochovywa katika Damu, na Jina lake aitwa NENO la Mungu.
14: Na Majeshi yaliyo Mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.
15: Na upanga mkali hutoka kinywani mwake Ili awapige mataifa Kwa huo. Naye atawachunga Kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadgabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.
16. Naye ana Jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA.
Ikiwa unapenda kujitakasa Ili usiachwe pale WATAKATIFU watakaponyakuliwa, fuatisha Sala hii:
EE MUNGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO, NINAKUKIRI WEWE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU, ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA, NIPE UWEZO WA KUISHI MAISHA MATAKATIFU, DHAMBI ISINISHINDE, UOVU USINISHINDE, ULEVI USINISHINDE, UZINZI USINISHINDE, NINAOMBA HAYO KUPITIA JINA LA YESU KRISTO ALIYE BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU. AMEN.
Karibu katika familia ya Mungu 🙏
Msabato ukimwambia habari za Unyakuo hawezi kuelewa,Hakikisha wakati wa kulala unakula na kushiba
jibukwanza swali.halafu adamu hana baba na kama unasema anae tuambie mamaake ni naniNani baba wa Adam?