Unyama huu wanaoufanya Polisi utamgharimu Rais Samia

Unyama huu wanaoufanya Polisi utamgharimu Rais Samia

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari!

Miaka 5 hivi imepita tulikuwa tukikemea mambo fulani mtandaoni. Kitendo cha serikali yenye zaidi ya vyombo sita vya usalama na haki kujichukulia sheria mkononi.

Serikali ifuate procedure katika kila zoezi, kama sheria itamtia mtu hatia na kuhukumiwa kuuawa auawe, kama itamfunga jela afungwe kama itamwacha huru aachwe.

Sasa polisi wanafika mitaani na kukusanya vijana wasio na kazi, na wale wanaowashuku kuuza au kuvu bangi kisha kuwaua kinyama. Misiba ni mingi mitaani, inatia huruma. Hili jambo ni kinyume na haki za binadamu.

Kijana anashikwa ndani ya masaa 12 anakuwa ameshakatishwa uhai. Upelelezi wa kutosha umefanyika? Hili zoezi nina hakika limepoteza vijana wasio na hatia. Hebu wapelekeni mahakamani mkawaue baada ya mahakama kuwatia hatiani.

Rais Samia utakuwa na mwisho mbaya. Police wamegeuza Kitonga Dar kuwa machinjio ya binadamu. Hata familia zenu zina vijana wa hovyo, wangekuwa wanaishi uswahilini tungewaita panya road. Serikali (mzazi na mlezi mkuu) inakwepa jukumu lake la kuwalea watoto wake na badala yake inwaua.

NB: Mimi si mhalifu, ni raia safi kabisa, sijapoteza ndugu yangu kwa hii operation na wala sina ndugu mhalifu, ila nimeumia tu na haya yanayotokea. Misiba ni mingi, huzuni na vilio. Huku viunga vya Kitonga ambako wamekugeuza machinjio ndiko ninakoishi. Jana nilienda uswahilini Tandika na Buza ni huzuni.
 
Habari!
Miaka 5 hivi imepita tulikuwa tukikemea mambo fulani mtandaoni. Kitendo cha serikali yenye zaidi ya vyombo sita vya usalama na haki kujichukulia sheria mkononi.
Serikali ifuate procedure katika kila zoezi, kama sheria itamtia mtu hatia na kuhukumiwa kuuawa auawe, kama itamfunga jela
Wewe kama kijana unajua vizuri operation linaloendelea sasa ni kuwasaga 'panya road' halafu wewe bado unakaa maeneo hatarishi usiku mkubwa eti unavuta bang.

Polisi haiwezi kutofautisha kibaka na mvuta bangi endapo utakutwa usiku sehemu isiyoeleweka na ukaamriwa ujisalimishe kisha ukatoka nduki lazima risasi zikuhusu mkuu.

Siungi mkono mauaji ya aina yoyote yale ila kipindi hiki cha operation maalum tujihadhari sana na kuzurura usiku pasipo sababu inayoeleweka.
 
Wewe kama kijana unajua vizuri operation linaloendelea sasa ni kuwasaga 'panya road' halafu wewe bado unakaa maeneo hatarishi usiku mkubwa eti unavuta bang.

Polisi haiwezi kutofautisha kibaka na mvuta bangi endapo utakutwa usiku sehemu isiyoeleweka na ukaamriwa ujisalimishe kisha ukatoka nduki lazima risasi zikuhusu mkuu.

Siungi mkono mauaji ya aina yoyote yale ila kipindi hiki cha operation maalum tujihadhari sana na kuzurura usiku pasipo sababu inayoeleweka.

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Wewe huna info za kutosha juu ya hii operation ndio maana umeandika hivi.
 
Habari!
Miaka 5 hivi imepita tulikuwa tukikemea mambo fulani mtandaoni. Kitendo cha serikali yenye zaidi ya vyombo sita vya usalama na haki kujichukulia sheria mkononi.
Serikali ifuate procedure katika kila zoezi, kama sheria itamtia mtu hatia na kuhukumiwa kuuawa auawe, kama itamfunga jela afungwe kama itamwacha huru aachwe.
Sasa police wanafika mitaani na kukusanya vijana wasio na kazi, na wanavuta bangi kisha kuwaua kinyama.
Misiba ni mingi mitaani. Inatia huruma. Hili jambo ni kinyume na haki za binadamu.
Kijana anashikwa ndani ya masaa 12 anakuwa ameshakatishwa uhai,. Upelelezi wa kutosha umefanyika ?
Hili zoezi nina hakika limepoteza vijana wasio na hatia .
Hebu wapelekeni mahakamani mkawaue baada ya mahakama kuwatia hatiani.
RAIS SAMIA utakuwa na mwisho mbaya.
Police wamegeuza KITONGA Dar kuwa machinjio ya binadamu.
Hata familia zenu zina vijana wa hovyo wangekuwa wanaishi uswahilini tungewaita panya road.
Serikali (mzazi na mlezi mkuu) inakwepa jukumu lake la kuwalea watoto wake na badala yake inwaua.
🎶Ukisikia yala ujue imempata, alielenga ana shabaha hajafanya makosa🎶
Mleta mada nyimbo hii inakuhusu.
 
Habari!
Miaka 5 hivi imepita tulikuwa tukikemea mambo fulani mtandaoni. Kitendo cha serikali yenye zaidi ya vyombo sita vya usalama na haki kujichukulia sheria mkononi.
Serikali ifuate procedure katika kila zoezi, kama sheria itamtia mtu hatia na kuhukumiwa kuuawa auawe, kama itamfunga jela afungwe kama itamwacha huru aachwe.
Sasa police wanafika mitaani na kukusanya vijana wasio na kazi, na wanavuta bangi kisha kuwaua kinyama.
Misiba ni mingi mitaani. Inatia huruma. Hili jambo ni kinyume na haki za binadamu.
Kijana anashikwa ndani ya masaa 12 anakuwa ameshakatishwa uhai,. Upelelezi wa kutosha umefanyika ?
Hili zoezi nina hakika limepoteza vijana wasio na hatia .
Hebu wapelekeni mahakamani mkawaue baada ya mahakama kuwatia hatiani.
RAIS SAMIA utakuwa na mwisho mbaya.
Police wamegeuza KITONGA Dar kuwa machinjio ya binadamu.
Hata familia zenu zina vijana wa hovyo wangekuwa wanaishi uswahilini tungewaita panya road.
Serikali (mzazi na mlezi mkuu) inakwepa jukumu lake la kuwalea watoto wake na badala yake inwaua.
Hao unaowatetea polisi wanawajua vuzuri, wagonjwa sugu wanajana na madaktari. Polisi wameamua kuwaua sababu wanawajua, waambie waache kuvuta bangi usiku kwenye vichaka hawatauawa.
 
Narudia kushauri waacheni Polisi wafanye kazi yao.
Hawa watoto wenu wameua na kujeruhi watu vibaya sana.
Kaeni kwa kutulia....
Lazima mjue Serikali yoyote makini haitakubali...
Kwanza unasema wanavuta bangi...bangi inaruhusiwa kuvutwa kwa sheria ipi?..hapo hapo unaomba procedure ifuatwe....procedure ipi kwa wavuta bangi.
Katika hili Mungu wabariki PT.
 
HILI LA KUUA PANYA ROaD SIO SAHIHI.. kila mtu asikilizwe na ahukumiwe na sheria mahakamani. Mtu akifa unaweza kumpa hatia yeyote hata kama aliuliwa kwa makosa...
Ile tume ya kuangalia Jeshi letu ifanye kazi kwa haraka..
 
Habari!
Miaka 5 hivi imepita tulikuwa tukikemea mambo fulani mtandaoni. Kitendo cha serikali yenye zaidi ya vyombo sita vya usalama na haki kujichukulia sheria mkononi.
Serikali ifuate procedure katika kila zoezi, kama sheria itamtia mtu hatia na kuhukumiwa kuuawa auawe, kama itamfunga jela afungwe kama itamwacha huru aachwe.
Sasa police wanafika mitaani na kukusanya vijana wasio na kazi, na wanavuta bangi kisha kuwaua kinyama.
Misiba ni mingi mitaani. Inatia huruma. Hili jambo ni kinyume na haki za binadamu.
Kijana anashikwa ndani ya masaa 12 anakuwa ameshakatishwa uhai,. Upelelezi wa kutosha umefanyika ?
Hili zoezi nina hakika limepoteza vijana wasio na hatia .
Hebu wapelekeni mahakamani mkawaue baada ya mahakama kuwatia hatiani.
RAIS SAMIA utakuwa na mwisho mbaya.
Police wamegeuza KITONGA Dar kuwa machinjio ya binadamu.
Hata familia zenu zina vijana wa hovyo wangekuwa wanaishi uswahilini tungewaita panya road.
Serikali (mzazi na mlezi mkuu) inakwepa jukumu lake la kuwalea watoto wake na badala yake inwaua.
Tulisema humu, raia wakasema tunatetea panya road.

Vp watoto wa wakubwa masaki na oyster bay wale wabwia unga nao wameuwawa?
 
Katika kipindi hiki kama huna issue Acha kukaa vijiweni kaa kwenu!


Kwa matukio waliyokuwa wanafanya panyaroad naunga mkono ukikamatwa Tu Shaba iwe ni Halali yako.

Hakuna nchi ujambazi na wizi ulimalizwa Kwa watu kufungwa Acha kujidanganya. Ujambazi humalizwa Kwa kupigwa risasi. Waache police wafanye KAZI Yao.

Kama Una ndugu yako ni panya road mwambie atubu kinyume na hapo jiandaeni Jamii imfunze.

Huu muda unapoteza kuandika humu utumie kuwaasa ndugu zako panya road wajitafutie pesa Kwa njia Halali kinyume na hapo utaendelea kuleta lawama zako Kwa Jeshi la police.
 
Habari!
Miaka 5 hivi imepita tulikuwa tukikemea mambo fulani mtandaoni. Kitendo cha serikali yenye zaidi ya vyombo sita vya usalama na haki kujichukulia sheria mkononi.
Serikali ifuate procedure katika kila zoezi, kama sheria itamtia mtu hatia na kuhukumiwa kuuawa auawe, kama itamfunga jela afungwe kama itamwacha huru aachwe.
Sasa police wanafika mitaani na kukusanya vijana wasio na kazi, na wanavuta bangi kisha kuwaua kinyama.
Misiba ni mingi mitaani. Inatia huruma. Hili jambo ni kinyume na haki za binadamu.
Kijana anashikwa ndani ya masaa 12 anakuwa ameshakatishwa uhai,. Upelelezi wa kutosha umefanyika ?
Hili zoezi nina hakika limepoteza vijana wasio na hatia .
Hebu wapelekeni mahakamani mkawaue baada ya mahakama kuwatia hatiani.
RAIS SAMIA utakuwa na mwisho mbaya.
Police wamegeuza KITONGA Dar kuwa machinjio ya binadamu.
Hata familia zenu zina vijana wa hovyo wangekuwa wanaishi uswahilini tungewaita panya road.
Serikali (mzazi na mlezi mkuu) inakwepa jukumu lake la kuwalea watoto wake na badala yake inwaua.
Tangu lini POLISI wakakamilisha operation bila kuonea mtu?

Anyway tusubiri ushahidi, hizi zibaki kuwa TETESI.
 
Polisi huwa wanawafaham wahalifu sana tu ila haki za binadam ndo huwa zinawarudisha uraiani wahalifu ambao ni tishio sana, zamani wahalifu wa kutumia bunduki walikua wakipelekwa mahakamani wanatafuta mawakili wanachezesha wanatoka wanaendelea kushika bunduki, Arusha risasi zililia sana, Kigoma kila siku bus zilitekwa, kahama sheli zilivamiwa sana enzi hizo, Ila baadae police wakaanzisha operesheni kila mtumia bunduki wakimkamata utaskia kafa baada ya kujaribu kutoroka na sasa hivi hali ni shwari.

Kwahiyo hata hao panya rodi wameshakamatwa sana lakin wakipelekwa mahakamani wanaenda kufungwa kifungo cha nje miez 3 unamuona Yuko tu mtaani na alikamatwa na ushahidi wote baada ya muda wanarudi kupora na kuua watu tena, panya rodi hawajaanza leo hapo daslam na waasisi wanajulikana kabisa acha wafyekwe ili tuwe salama, hakuna kitu kinauma Kama unatafuta kwa jasho alafu mtu anakuja kukupora, kukusababishia ulemavu au kukuua kabisa ili tu akunyang'anye mali yako
 
Polisi huwa wanawafaham wahalifu sana tu ila haki za binadam ndo huwa zinawarudisha uraini wahalifu ambao ni tishio sana, zamani wahalifu wa kutumia bunduki walikua wakipelekwa mahakamani wanatafuta mawakili wanachezesha wanatoka wanaendelea kushika buduki, Arusha risasi zililia sana, Kigoma kila siku bus zilitekwa, kahama sheli zilivamiwa sana enzi hizo, Ila baadae police wakaanzisha operesheni kila mtumia bunduki wakimkata utaskia kafa baada ya kujaribu kutoroka na sasa hivi hali ni shwari.

Kwahiyo hata hao panya rodi wameshakamatwa sana lakin wakipelekwa mahakamani wanaenda kufungwa kifungo cha nje miez 3 unamuona Yuko tu mtaani na alikamatwa na ushahidi wote baada ya muda wanarudi kupora na kuua watu tena, panya rodi hawajaanza leo hapo daslam na waasisi wanajulikana kabisa acha wafyekwe ili tuwe salama, hakuna kitu kinauma Kama unatafuta kwa jasho alafu mtu anakuja kukupora, kukusababishia ulemavu au kukuua kabisa ili tu akunyang'anye mali yako
Ndio ndio Acha watangulizwe
 
Katika kipindi hiki kama huna issue Acha kukaa vijiweni kaa kwenu!


Kwa matukio waliyokuwa wanafanya panyaroad naunga mkono ukikamatwa Tu Shaba iwe ni Halali yako.

Hakuna nchi ujambazi na wizi ulimalizwa Kwa watu kufungwa Acha kujidanganya. Ujambazi humalizwa Kwa kupigwa risasi. Waache police wafanye KAZI Yao.

Kama Una ndugu yako ni panya road mwambie atubu kinyume na hapo jiandaeni Jamii imfunze.

Huu muda unapoteza kuandika humu utumie kuwaasa ndugu zako panya road wajitafutie pesa Kwa njia Halali kinyume na hapo utaendelea kuleta lawama zako Kwa Jeshi la police.
Ah kabisa....

Watoto hawasikiiii kuna watoto watukutu bila mkono wa chuma
Hawatuliiii
Eti umkamate ukimuweka ndani
Tu kesho kaachiwaaa

Ova
 
Back
Top Bottom