Unyama huu wanaoufanya Polisi utamgharimu Rais Samia

Unyama huu wanaoufanya Polisi utamgharimu Rais Samia

Ni kweli kabisa.
Ni mtu mjinga pekee atakayesema kuwa Wezi na panya road hawajulikani.

Tatizo hata wakikamatwa watatoka au kutolewa kimagendo,
Pale tuu Kariakoo unaweza ibiwa simu, ukamkamata mwizi ukampeleka kituo cha msimbazi na kithibitisho alafu kesho yake ukamkuta mwizi yuleyule nje.

Panyaroad wanafahamika, ukikamatwa ukiwa na panyaroad hayo ni makosa yako,
Wewe unajua kundi hili ni wezi alafu unatembea nao Kama sio kutafuta watu lawama ni nini?
Kwa hiyo bw Robert, ukikutwa na na panya road, adhabu yako ni kifo?
Huwa nasoma makala zako nakuona kama ni mtu mbobevu,
Kumbe unashabikikia uuwaji wa watuhumiwa,?
Mahakama zifutwe ili police watoe hukumu kwa watuhumiwa,
 
Habari!
Miaka 5 hivi imepita tulikuwa tukikemea mambo fulani mtandaoni. Kitendo cha serikali yenye zaidi ya vyombo sita vya usalama na haki kujichukulia sheria mkononi.

Serikali ifuate procedure katika kila zoezi, kama sheria itamtia mtu hatia na kuhukumiwa kuuawa auawe, kama itamfunga jela afungwe kama itamwacha huru aachwe.

Sasa polisi wanafika mitaani na kukusanya vijana wasio na kazi, na wanavuta bangi kisha kuwaua kinyama. Misiba ni mingi mitaani, inatia huruma. Hili jambo ni kinyume na haki za binadamu.

Kijana anashikwa ndani ya masaa 12 anakuwa ameshakatishwa uhai. Upelelezi wa kutosha umefanyika? Hili zoezi nina hakika limepoteza vijana wasio na hatia. Hebu wapelekeni mahakamani mkawaue baada ya mahakama kuwatia hatiani.

Rais Samia utakuwa na mwisho mbaya. Police wamegeuza Kitonga Dar kuwa machinjio ya binadamu. Hata familia zenu zina vijana wa hovyo, wangekuwa wanaishi uswahilini tungewaita panya road. Serikali (mzazi na mlezi mkuu) inakwepa jukumu lake la kuwalea watoto wake na badala yake inwaua.

NB: Mimi si mhalifu, ni raia safi kabisa, sijapoteza ndugu yangu kwa hii operation na wala sina ndugu mhalifu, ila nimeumia tu na haya yanayotokea. Misiba ni mingi, huzuni na vilio. Huku viunga vya Kitonga ambako wamekugeuza machinjio ndiko ninakoishi. Jana nilienda uswahilini Tandika na Buza ni huzuni.
wakati panya road wameua raia raia wasio na hatia, hukuwaambia kwamba wanakiuka haki za binadamu. Leo wao wameuawa ni kukiuka haki za binadamu.

Achana na hiyo ajenda. Kama unajali haki za binadamu, waambie panya road waache kupora na kuwaua raia wema, ni kinyume cha haki za binadamu.

Kama huwezi, nyamaza.
 
Kwa hiyo bw Robert, ukikutwa na na panya road, adhabu yako ni kifo?
Huwa nasoma makala zako nakuona kama ni mtu mbobevu,
Kumbe unashabikikia uuwaji wa watuhumiwa,?
Mahakama zifutwe ili police watoe hukumu kwa watuhumiwa,
utakuwa ni mharifu ww sio bure , watu wanateseka kisa hao panyaroad ww unawatetea wanaowatunza hao panyaroad , ungekuwa krb ningekutoa shing , nmepitia mikasa ya hao panya road ni mashetani
 
Wewe huna info za kutosha juu ya hii operation ndio maana umeandika hivi.
ww una info gan kushinda tuliopo maeneo yenye mikasa mingi , utakuwa mpumbav kushabikia mtu kukaa maeneo hatarish au krb na watu hatarish wkt anajua dar ipo kweny hali gan ss hv
 
Kuua siyo ishu nzuri, wawakamate na kuwapeleka Mahakamani wakienda jela wakafanyishwe kazi ngumu maisha wapewe kesi za uhaini tu (Treason)
uwe unauliza sio kuwaona waliopo kweny field wajinga
 
Hao unaowatetea polisi wanawajua vuzuri, wagonjwa sugu wanajana na madaktari. Polisi wameamua kuwaua sababu wanawajua, waambie waache kuvuta bangi usiku kwenye vichaka hawatauawa.
ww ni panyaroad , mm sio wa njano ila sina ujinga wako huo wa kusapoti uhalifu kisa siipend serikali
 
Hawa wanaowatetea panya road natamani siku wakutane nao watalelewa. Me wamempora simu shangazi yangu, mama mtu mzima wa miaka 70 wamempiga na bapa za panga alfajiri tu asieee .


Sasa nadhani watu hawajui ubaya wa hawa vijana hadi wakutane nao kwenye eneo la tukio.
Watu wanazungumzia utawala wa sheria, ni jambo zuri sana lakini kama tukisema tuufuate kama ulivyo hali haitokuwa nzuri.
Watu wanashindwa kujua kuwa mtu anaweza kuwa jambazi na polisi wakamshika kwenye tukio lakini ushahidi usijitosheleze na akaachiwa.

Kuna mmoja nilimwambia asubiri wamvamie kwake,wamuibie, wamlawiti yeye na wabake mke wake mbele ya watoto wake ndio atakuja hapa kuzungumzia haki za binadamu kwa wahalifu washenzi.
 
HILI LA KUUA PANYA ROaD SIO SAHIHI.. kila mtu asikilizwe na ahukumiwe na sheria mahakamani. Mtu akifa unaweza kumpa hatia yeyote hata kama aliuliwa kwa makosa...
Ile tume ya kuangalia Jeshi letu ifanye kazi kwa haraka..
ukikutana na panyaroad utarud hapa kusema wapelekwe kwenye sheria
 
Wewe kama kijana unajua vizuri operation linaloendelea sasa ni kuwasaga 'panya road' halafu wewe bado unakaa maeneo hatarishi usiku mkubwa eti unavuta bang.

Polisi haiwezi kutofautisha kibaka na mvuta bangi endapo utakutwa usiku sehemu isiyoeleweka na ukaamriwa ujisalimishe kisha ukatoka nduki lazima risasi zikuhusu mkuu.

Siungi mkono mauaji ya aina yoyote yale ila kipindi hiki cha operation maalum tujihadhari sana na kuzurura usiku pasipo sababu inayoeleweka.

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Nakazia[emoji109]
 
Walisha waambia muwakanye vijana wenu mkaona wanawatania full kulitukana jeshi la polisi sijui wamekuwa wazembe sasa wameacha uzembe wanafanya kazi tulia dawa hiwaingie

Sent from my Nokia G10 using JamiiForums mobile app
ASILIMIA kubwa wanaotetea hawa wahuni Ni wanufaika wao.

Either wazazi,ndugu,wanunuzi, n.k
 
Kwa hiyo bw Robert, ukikutwa na na panya road, adhabu yako ni kifo?
Huwa nasoma makala zako nakuona kama ni mtu mbobevu,
Kumbe unashabikikia uuwaji wa watuhumiwa,?
Mahakama zifutwe ili police watoe hukumu kwa watuhumiwa,

Hakuna sehemu nimesema wauawe,
Ingawaje hao Vijana ukicheza nao Kwa kuwabembeleza wanaweza kukutoa roho kiutani utani.

Nimeshashuhudia matukio kama matatu ya hao panyaroad, najua vile wanavyo react wanapokutana na Polisi.

Kama watashindwa kujisalimisha Kwa polisi alafu wanawashambulia polisi ili wakimbie unategemea nini kitatokea?

Sishauri watu wauawe na polisi bila kufuata sheria lakini nafahamu zipo Ajali katika Kazi pale polisi wanapokabiliana na hao Vijana.

Polisi lazima wazingatie sheria,
Lakini kuna wakati wahalifu hutumia udhaifu wa sheria hiyohiyo kuwadhuru Polisi,

Wale waliouawa bila Shaka ni kwaajili ya kuwaogopesha Panyaroad wengine ndio maana Hali itatulia Kwa Muda.
Lakini amini usiamini wezi na panyaroad wa mtaani hawaogopi mahabusu.
Mbona kila wakati wanapelekwa na kutolewa,

Maeneo Kama Banana, airport, vingunguti, mpaka unatokea Buguruni wapo Vijana wahuni wanakamatwa kila leo Kwa matukio ya kihuni hata kabla haya ya panyaroad ya juzi.
Tatizo ni kuwa hawaogopi jela kwani wanatolewaga wanachoogopa ni kifo tuu.

Ukiwatishia kuwakamata kwao sio tatizo, Ila ukiwatishia Uhai wao hapo lazima wapoe.

Approach iliyotumiwa na Jeshi la polisi kuanza Kwa kuua Wale sita ilikuwa nzuri, ili kuwatisha panyaroad, na wametishika.
Lakini kama wangeanza na kukamata Kwanza ninakuhakikishia bado matukio yangekuwa yanaendelea Kwa baadhi ya Maeneo.
 
Polisi huwa wanawafaham wahalifu sana tu ila haki za binadam ndo huwa zinawarudisha uraiani wahalifu ambao ni tishio sana, zamani wahalifu wa kutumia bunduki walikua wakipelekwa mahakamani wanatafuta mawakili wanachezesha wanatoka wanaendelea kushika bunduki, Arusha risasi zililia sana, Kigoma kila siku bus zilitekwa, kahama sheli zilivamiwa sana enzi hizo, Ila baadae police wakaanzisha operesheni kila mtumia bunduki wakimkamata utaskia kafa baada ya kujaribu kutoroka na sasa hivi hali ni shwari.

Kwahiyo hata hao panya rodi wameshakamatwa sana lakin wakipelekwa mahakamani wanaenda kufungwa kifungo cha nje miez 3 unamuona Yuko tu mtaani na alikamatwa na ushahidi wote baada ya muda wanarudi kupora na kuua watu tena, panya rodi hawajaanza leo hapo daslam na waasisi wanajulikana kabisa acha wafyekwe ili tuwe salama, hakuna kitu kinauma Kama unatafuta kwa jasho alafu mtu anakuja kukupora, kukusababishia ulemavu au kukuua kabisa ili tu akunyang'anye mali yako
Umeandika vizur sn,
Hawa panya road ifikie hatua waylfyekwe tu
 
Tangu lini POLISI wakakamilisha operation bila kuonea mtu?

Anyway tusubiri ushahidi, hizi zibaki kuwa TETESI.
mpumbav huyo , vijana wengi wanauliwa ni wale wanaokaidi kusimama wanapoamriwa kusimama , mm nmekutana na polisi sio chini ya mara 5 mida ya saa 5 usk kwa wiki hiz mbili , ila sijawai pigwa wala kusumbuliwa , wanaouliwa wengi ni vibaka na panyaroad ambao tyr wanajijua ni wakosaji
 
Tangu lini POLISI wakakamilisha operation bila kuonea mtu?

Anyway tusubiri ushahidi, hizi zibaki kuwa TETESI.
mpumbav huyo , vijana wengi wanauliwa ni wale wanaokaidi kusimama wanapoamriwa kusimama , mm nmekutana na polisi sio chini ya mara 5 mida ya saa 5 usk kwa wiki hiz mbili , ila sijawai pigwa wala kusumbuliwa , wanaouliwa wengi ni vibaka na panyaroad ambao tyr wanajijua ni wakosaji
 
Wewe huna info za kutosha juu ya hii operation ndio maana umeandika hivi.
Kwa maelezo ya hapo juu nawaunga mkono polisi, labda ungesema vijana wanakamatwa majumbani kwao wakiwa wamelala..
 
Cha muhimu vijana ni kuepuka makundi
Sheria gani imemkataza kijana asijumuike na wenzake.

Siyo kila kijiwecha vijana ni wahalifu.

Kuna vita isiyoisha baina ya vijana na grown up fools.

Vijana wanahitaji maongozi na fursa. Endeleeni kukwapua mali za umma na kusababisha dropouts wanaogeuka wahalifu baada ya kupoteza matumaini.

Kuna siku yaja vijana wataturudi sisi tunaojifanya hatukuwahi kuwa vijana kabla
 
Tatizo na madogo nao wanafanya uhalifu at impunity level wanakata watu panga za USO kubaka na unyama mwingine WA kiboya
Ila approach inayotumika na police Tanzania si Sawa kazi ya police ni kuapprehend criminals na kuwaleta kwenye mahakamani kujibu kesi zao na hukumu kutolewa na mahakama , hii prejudicial killings and jungle justice tendency ni recipe for disaster inaweza tumika kama tool ya kuwaumiza na kuwakandamiza watu wengine ,nadhani tuliona mambo ya ovyo na unyama WA kutisha uliofanyika awamu iliyopita Chini ya magufuli na genge lake la akina sabaya ,Makonda ,mnyeti na washenzi wengine ,death squads za kuwinda , kutesa ,kuteka , kuua na kubambikizia kesi Kwa wapinzani na watu wengine wanaotofautiana na viongozi Kwa namna moja au nyingine .

Hii inayofanywa na police haifai ni approach mbaya Sana , nini Maana ya kuwa na mahakama ? Nini Maana ya kuwa na justice system , police waongezewe trainings na resources za kuchunguza uhalifu na kubaini wahalifu ,hasa issues kama forensics NK ili kazi ziwe zinafanyika Kwa ufasaha zaidi na si kubahatisha na kufanya witch hunts
 
Back
Top Bottom