Uongo mkubwa zaidi kutokea dunia - The biggest scam in the world

Uongo mkubwa zaidi kutokea dunia - The biggest scam in the world

Logical non sequitur fallacy

Naona hunielewi hata.

Unayonijibu hata hayahusiani kabisa na nlichokuuluza

Swali hili linaonesha limekuchemsha.

Narudia mara ya tatu:

Mungu mjuzi wa yote, kwanini anawapa watu mtihani ilihali anajua hata majibu ya mtihani huo!?
Nikujibu mara ngapi sasa...

Jibu nitakuwa narudia kama kawaida👉kwa vile binadamu ana akili na anaweza kutatua mitihani hiyo maana Mungu yeye ndio kampa akili so anajua uwezo wa binadam.
 
Aliileta kiarabu vipi Tena wakati huko juu umesema mitume kuanzia Adam Musa, Hud walikuwa waislamu wote. Wao walisoma kuran ipi nyingine ustaadh!?
Ona ulivyo kilaza, hivi unasomwa ninacho kiandika ?

Qur'an ni kitabu alichopewa Mtume ambaye alikuwa anaongea Kiarabu.

Hao mitume wengine walipewa ujumbe wao kwa lugha zao.

Ongeza umakini kijana.
 
Je, kitendo cha kumchoma moto mtoto wako kama adhabu kitatafsiriwa na jamii kama cha upendo?
Ndugu na jamaa zako watakuona kama baba mwenye upendo au vinginevyo?

Vipi jirani yako angefanya kitendo kama hicho. Je, utaamini ukiambiwa jirani huyo alikua ni mtu mwenye upendo sana kwa mtoto wake??
Kiislamu mwenye kuchoma ni Allah, mwanadamu ni haramu kuadhibu au kuwa kitu kwa kukichoma.

Uwe unasoma ninacho kiandika, hili nililielezea huko nyuma.
 
Thibitisha kwamba Allah huyo ni chanzo cha kila kitu.
Nithibitishe mara ngapi ?

Hivi unajua ya kuwa hakuna kitu chochote chenye ushahidi mkubwa na WA wazi kuzidi uwepo wa Allah ? Yaani hata uwepo wako wewe ushahidi wake sio mkubwa Wala wa wazi kuzidi ushahidi wa uwepo wa Allah.

Ndio maana hamjawahi kuthibitisha kutokuwepo kwake.

Ukiona mbingu, Ardhi, uwepo wako wewe vyote ni ushahidi wa kuwepo kwa Allah.

Niliweka andiko huko nyuma kuthibitisha uwepo wake.
 
Infropreneur na Smotor hebu tulijadli suala hili la kuwepo ama kutokuwepo kwa MUNGU kimantiki.

Mleta mada Mayu na nyie ni lazima tukubaliane kwamba hoja ya Mungu kwamba yupo ama hayupo ni lazima ianzie kwenye hoja ya kuumbwa kwa ulimwengu.
Kwanza, kwa nini unadhani ulimwengu uliumbwa?

Kwa nini umeweza kuamini Mungu usiyemjua Hana muumbaji, Lakini unataka ulimwengu uwe na muumbaji?
Wapinga Mungu husema kwamba dunia imeibuka tu toka kusikojulikana mamilioni kadhaa ya miaka iliyopita.
Dunia haina chanzo,

Kama kila kitu kilichopo lazima kiwe na chanzo, Basi hata Mungu na yeye lazima awe na chanzo. Mungu huyo Hawezi kutokea tu from nothing.

Kanuni ni kwamba, 👇

Kama kila kitu kilichopo lazima kiwe na chanzo, Basi hata
"Chanzo cha chanzo" na chenyewe lazima kiwe na chanzo chake na
"Chanzo cha, chanzo chake" lazima kiwe na chanzo.

Ili muundo ule ule wa
"ULAZIMA KUWEPO CHANZO" uonekane na ufuatwe kwa vitu vyote, Kusiwepo kitu chochote kitakacho kwenda kinyume na ulazima huu wa
"kuwepo chanzo" kwa kujitokeza chenyewe tu pasipo chanzo.

Nadhani una nielewa.

Hivyo SI LAZIMA kwamba, Dunia lazima iwe na Chanzo.

Ila kama "ulazima" huo lazima uwepo kwamba
"lazima vitu vyote vilivyomo viwe na chanzo" Basi hata Mungu hawezi kwenda kinyume na ulazima huo, Na yeye lazima awe na chanzo.


Lakini kabla hatujaenda mbali sana jee nyie akili zenu zinawatuma kwamba ulimwengu ulianzaje na ni kwa nini nyie mmetokeza kuwa binadamu na siyo Ng'ombe!!
Ulimwengu hauja anza, upo tu na hauna mwanzo wala mwisho.

Kama kila kitu lazima kiwe na mwanzo, Basi na wewe unapaswa kuonesha mwanzo wa Mungu.

Ili muundo ule ule wa
"ULAZIMA KUWEPO CHANZO" ufuatwe.

Kama unaweza kuamini Mungu usiyemjua Hana chanzo, Basi hata Ulimwengu si lazima uwe na chanzo.

Nadhani hapa logic imekamilika.
 
Allah katika ubora wake

Yaani katoto kakifa kachanga kwenye shuruba ya kansa au taunami na bado anakasubiria hadi siku ya kiama anakapa tena mtihani kakifeli moto unakahusu
Huyu ndio Mungu mwenye upendo wote?

Kuamini ujinga huu inabidi ujitoe ufahamu
Kwako wewe upendo ni nini ? Isiwe mnatafsiri upendo kwenu nyinyi ndio ubwege na ufala.
 
Qurani hata miaka 1500 haijafikisha, hiyo 50,000 umeitoa wapi?
Ona mlivyo wajinga hata kuunganisha hoja mnashindwa, shida yenu ni kusoma mkaelewa.

Nimeongelea kalamu ilishaandika makadirio miaka elfu 50 kabla ya kuumbwa kwa mbingu na ardhi, wewe unakuja kuongelea Qur'aan. Hili linaingiaje hapo ?
 
Allah katika ubora wake

Yaani katoto kakifa kachanga kwenye shuruba ya kansa au taunami na bado anakasubiria hadi siku ya kiama anakapa tena mtihani kakifeli moto unakahusu
Huyu ndio Mungu mwenye upendo wote?

Kuamini ujinga huu inabidi ujitoe ufahamu
[emoji23][emoji23] ani hakuachi salama
 
N
Ndugu Maisha ya Dunia ni ya Kupita tu, wewe kuachwa mzima mpaka dkk hii usifurahie sana, maana yake ni kwamba Una Jukumu zito nyuma yako La Kutekeleza Lengo la wewe kuletwa hapa Duniani

Sasa Huruma yako kwa mtoto aliyezaliwa akiwa na Changamoto hali ya kwamba wewe mtu mzima na Uko sawa basi hakika mtoto huyo Akifa yeye anakuwa wa kwanza kuenda katika Pepo kwani Mwenyezi Mungu alimpatia Changamoto na yeye ndiye anayejua ni Kwanini amefanya hivyo!

Furahia kuwa Hai na kuwa na Afya Njema Kabisa, but you Got to Know you have Task to Accomplish bro
Una hubiri
Hakuna aliye niacha mzima
Hakuna pepo
Hakuna mwenyeziMungu
 
Ona mlivyo wajinga hata kuunganisha hoja mnashindwa, shida yenu ni kusoma mkaelewa.

Nimeongelea kalamu ilishaandika makadirio miaka elfu 50 kabla ya kuumbwa kwa mbingu na ardhi, wewe unakuja kuongelea Qur'aan. Hili linaingiaje hapo ?
Miaka 50.000 kabla ya kuumbwa mbingu na ardhi? dunia ina miaka zaidi ya billioni 13, nani aliandika au binadamu gani anajua historia ya zaidi ya miaka billioni 13, endeleeni kula matango pori mliyoletewa na mabeberu na wafanyabiashara za utumwa
 
Unajaribu kusema nini mkuu?

Mimi kutokua na lakufanya kuna uhusiano gani na kuwepo kwa Mungu?

Niliaminishwa kuhusu mungu wa upendo wote ndio nikaanza kujiuliza why aruhusu haya maswahibu kwa vitoto vichanga visivyo na hatia?
mkuu naomba unisamehe kama nitakuwa nauliza mambo yako ya undani sana
bila shaka wewe ni msomi si ndivyo?
 
😂😂😂Panapotokea majanga katika madhara kuna ishu ya kuokolewa na kujiokoa vyote ni uwezo wa binadamu katika kupambania mitihani ya kidunia.


Sio kila janga watakufa wote ,ndio maana kule turkey yule dogo alikutww siku kadhaa mbele kweny kifusi kwa kawaida hakupangiwa kufa kabisa ..

Sio kila janga litaathiri na kuua kila mtu ndio maana kuna idadi na wengine wanapona.
Je hao wanao kufa hawaku jaliwa uwezo na hiyo Akili ya kujiokoa na Mungu?
 
Je hao wanao kufa hawaku jaliwa uwezo na hiyo Akili ya kujiokoa na Mungu?
Mbona watu wanakufa daily ni kifo chao tu kimepangwa ,kila mtu atakufa kwa style yake ...

Hata uwe mzima unaweza kufa ghafla tu.

Unaweza kuwa na akili ya kujiokoa na ukafa kwani wavuvi wanakufa daily na wanajua kuogelea..
 
kama Mungu hayupo, ni nani aliumba dunia na viumbe hai vyake.

Binadamu hajui mambo mambo mengi sana yakiwemo hayo uliyoandika

Lakini kutokujua sio kichaka cha kumfichia Mungu ambaye hayupo

Kuna mambo mengi sana binadamu alikua hayajui lakini sasa anayajua na ndani yake hakuna uthibitisho wa Mungu
 
Mbona watu wanakufa daily ni kifo chao tu kimepangwa ,kila mtu atakufa kwa style yake ...

Hata uwe mzima unaweza kufa ghafla tu.

Unaweza kuwa na akili ya kujiokoa na ukafa kwani wavuvi wanakufa daily na wanajua kuogelea..
Basi Akili unayosema tumepewa na huyo Mungu ya kupambana na mitihani ya kidunia ni DHAIFU sana na haina maana yeyote wala msaada wowote kwa binadamu.
 
Back
Top Bottom