Upande wa pili wa usalama wa Taifa ukoje?

Upande wa pili wa usalama wa Taifa ukoje?

Kuna janki mmoja alikuwa anasoma Chuo cha SAUT anasuka dread alikuwa boss wa usalama tena mkubwa tu aliletwa pale maalum jamaa alikuwa anaongea kikongo kuliko wakongo wenyewe.
Mwanza uyo mwana yupogo anatembelea V8 baadhi ya sehemu anajulikana kama mganga wa kienyeji.
 
TISS ni moja ya kazi complex sana.
watu wanakuwa inspired na movie za kijasusi lakin in reality hizo kazi ni ngumu.
unaweza usiishi kwa uhuru mpaka unastaafu.
uzalendo wa hali ya juu na kujitolea sana kwenye hii kazi vinahitajika
Movie za kijasusi zina matukio magumu kuliko ujasusi wenyewe, kama ingekuwa uhalisia uko vile majasusi wengi wangekufa. Rej. Mission Impossible n.k
 
Vijana wanapenda sana hiyo kazi ya TISS lakini hawaijui vizuri,Kuwa TISS hauishi kwa amani,inabidi 24 hrs uwe Clean,24hrs monitored,ukifanya jambo ambalo linaweza kuhatarisha majukumu yako wanakula KICHWA,Tutakukuta Kwenye Kisima Umekufa au Mtaroni umepigwa risasi au kupigwa Polonium 210 ufe taratibu....Achaneni na mawazo ya kuwa TISS ndio deal,Enzi za nyuma walikuwa wanatumia kivuli cha TISS kula rushwa ila sasa wanapigika tu maana Ngosha na yeye ana watu wake wanaangalia mienendo yao hivyo nao wanaogopa...TISS tunakaa nao mitaani yaani nanga inapaa full kupigika.
Kuna mmoja babake mkubwa aliwahi kuwa mkuu wa kitengo pale kijitonyama alivyotoka masomoni babake akampenyeza sehemu pale mjini kwenye kishirika cha serikali jamaa kila siku yeye ni kuchange magari na anatembea na bastora full mashauzi nowdays katupwa huko mbeya nimemkuta juzi na mark2 box kajichokeaaaaa.nikamkumbusha zile misele akaishia kusema wewe acha tuu. Ngosha alivyoingia kapandikiza watu wake ka kanda ya ziwa tu huko wengine tupa kule.
 
Kuna demu nilikuwa napiga ila yuko vizuri kimaisha na alikuwa anafanya kazi posta ofisi sijui kumbe ni katiss aise kilichokuwa kuwa kinanikera nikupenda kuongea na simu mida ya jioni kwa muda mrefu sanaa halafu akiwa pekee.yake basi hiyo tabia ikawa inanikera banaa nikamwambia anachekacheka basi ananipoza maisha yanaendelea ssiku moja tumelala nikajifanya nimelala kumbe namcheki akaingiza password za simu nikazinakili.kumbe mwaka wKe wa kuzailiwa siku moja anaenda kuoga nikaifungua simu daa pekupekua maagizo kibao maa taariifa za ajabu ajabu mengine wanawasiliana kwa code...kwa mfano kuna moja nilikuta sms inasema wasilian na kobe akupe mguu wa kuku kesho na kazi sehemu. Hhheee nikakausha nikawa napeleleZa.mengine siyaeliwi kutoka na lugha zao basi siku nilimwambia na ndo siku alinitumia sms ya kuachana namii nami kwakuwa nilikuwa napiga kisela nikajisemea powa mpaka sijamuona sijui yuko wPi. Hii sio kazi kabisaa.
 
Movie za kijasusi zina matukio magumu kuliko ujasusi wenyewe, kama ingekuwa uhalisia uko vile majasusi wengi wangekufa. Rej. Mission Impossible n.k
Movie za kisajusi nyingi zina potray fantasy. but not the reality.
people thinks kuwa spy.. unakuwa na access to all toys and the goverment is on your side everyday... well not the case. its not the reality
 
Linaweza kuwa swali lisiloeleweka haraka, Labda nianze na simulizi kwanza

Mwaka 1979 Tanzania iliingia kwenye vita na Uganda maarufu kama vita ya KAGERA. Mwaka 1995 nilikutana na mzee Mkumbi(marehemu) mmoja wa watu ambao walikaribia kabisa kupigana vita hiyo. Miongoni mwa mambo aliyonisimulia ni kuwa yeye alirudia eneo la mwisho ambalo angetoka hapo ilikuwa ni moja kwa moja anaingia uwanja wa vita. Anasema alifurahi sana kwani akiwa kwenye eneo la mwisho ambalo daktari alikuwa anawapima afya ndipo alinusurika, kilichomnusuru ni kukutana na daktari ambaye alikuwa ndugu yake, akamuokoa kwa kueleza kuwa afya yake si mzuri.

Binafsi ingawa sikusema nilimshangaa sana huyu mzee kwa sababu alichokifurahia ni kukwepa majukumu yake ya msingi kama Mwanajeshi, hata huyo daktari kwangu bado hakuwa Mzalendo alitaka mtoto wa nani afe na wa nani abaki? Na hawa ndio wale ambao ni wengi wanaajiriwa kwenye majeshi yetu kwa njia za upendeleo lakini je tumeangalia nini athari yake?

Kuna hii idara maarufu ambayo wengi wanatamani kuajiriwa ambayo ni usalama wa Taifa, Licha ya mshahara na marupurupu yake upande wa pili wa idara hii ukoje(side effect yake ni ipi?) Kuna jamaa waliibuka kwa ahadi za kuajiri watu kwenye Idara hiyo ambapo walikuwa wanahongwa Mil 1 na kuendelea ili kuwapatia watu kazi kwenye Idara hiyo, Hivi ni kweli watu wanaoingia kwa mtindo huo watayaweza hayo majukumu? Au kazi yenyewe ni ile ya kupita kurekodi tu watu wanaomkosoa Rais kwenye vijiwe vya kahawa? Hakuna majukumu ambayo yanamtaka mtu kujitoa ambayo yanaweza kumfanya mtu akwepe kutimiza wajibu wake kama yule mzee aliyekwepa kwenda kupambana Uganda?

NAULIZA TU.
shughuli yoyote ya serikali inahitaji uzalendo, kazi kubwa ya TISS ni analysis.
 
Kuna mmoja babake mkubwa aliwahi kuwa mkuu wa kitengo pale kijitonyama alivyotoka masomoni babake akampenyeza sehemu pale mjini kwenye kishirika cha serikali jamaa kila siku yeye ni kuchange magari na anatembea na bastora full mashauzi nowdays katupwa huko mbeya nimemkuta juzi na mark2 box kajichokeaaaaa.nikamkumbusha zile misele akaishia kusema wewe acha tuu. Ngosha alivyoingia kapandikiza watu wake ka kanda ya ziwa tu huko wengine tupa kule.

Ni kweli wanaokula ni NYOKA walio kwenye system ya ngosha ,wale wa zamani nanga inapaa!!
 
huu ni UONGO kwann wakuue ?

hakuna jwtz yenye nidhamu na ufanisi bila TISS
Sijui kwanini hii nchi huwa inaona JWTZ ni moja ya chombo kama vile kimeshushwa kutoka mbinguni.

Bora umueleze ukweli ili ujinga uondoke.

Licha ya Jeshi kuwa na Military Inteligenc ila hakuna sehemu popote pale ambapo hakuna TISS ktk hivi vyombo.

Mbona polisi wana Inteligenc yao na bado pia TISS wapo humohumo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
umekalili bro

kila taasisi ya serkali ina dawati maalum la watu wa tiss na sio kila tiss ni mchomaji wengine wapo ajiri ya ushauri

mfano mkuu wa misitu kigoma yupo karibu saana na watu wa tiss katika harakati zake za kupambana na ujangiri na huwa wanampa full support

pia majuzi tu hapa TPA Kigoma imepigwa bilion 8 watu wa tiss from makao makuu wakaja na sasa bado wapo tunaishi nao(kuna uchunguzi unaendelea)
Mueleze huyo ili akuelewe. Huwezi kuwazuia TISS popote wanapopahitaji.

Kambi za Jeshi zina ofisi kabisa ya Usalama wa Taifa.

Ofisi ya mkuu wa wilaya bado pia zina ofisi ya usalama wa Taifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtaani kwetu wanaitwa wa Mchichani. Ni kazi tu kama kazi zingine, zina mazuri na mabaya sema ndo hivyo wabongo tunayo hulka ya kuabuse nafasi flani flani, mbuzi anakula kwa urefu wa kamba yake
 
Back
Top Bottom