UPDATE: Watumishi waliomwagiana Maji ya Dripu wakisherehekea 'Birthday' wasimamishwa Kazi

UPDATE: Watumishi waliomwagiana Maji ya Dripu wakisherehekea 'Birthday' wasimamishwa Kazi

View attachment 2832151
=============


View attachment 2832152
Serikali iemanza kufanya uchunguzi kuhusu video inayosambaa mtandoni ikiwaonyesha watoa huduma za afya wakisherehekea siku ya kuzaliwa kwa kumwagiana majitiba maarufu ‘dripu’.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumapili, Desemba 3, 2023 Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Tumaini Nagu amesema bado video hizo hazina uhalisia na eneo linalotajwa, hivyo wanashirikiana na waganga wakuu wa maeneo husika kujiridhisha.

“Nimeiona asubuhi hii tunafuatilia, inaonekana kama hicho kituo kilichoandikwa pengine si chenyewe, lakini hatujapata uhakika vizuri,” amesema.'

Profesa Nagu amesema wanafuatilia kupitia Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita na Mganga Mkuu wa Manispaa ya Geita, lakini bado hawana uhahika kama ni kituo cha Serikali au cha binafsi.

“Tumeona picha za watu, lakini tunafuatilia kuona ni kituo gani, inawezekana pia si jina la kituo kilichoandikwa, tukishafuatilia tutatoa majibu mpaka tupate ukweli wa tukio lenyewe,” amesema Profesa Nagu.

Katika video hiyo iliyokuwa na maelezo kuwa ni watumishi wa afya katika kituo cha afya Nyankumbu, walionekana wanatumia maji ya kutibia wagonjwa (dripu) kwa sherehe yao ya kuzaliwa.

Hata hivyo, maoni ya watu mbalimbali katika mtandao wa kijamii wa Instagram yalijikita kwa Wizara ya Afya kutolea ufafanuzi jambo hilo, wakitaka ichukue hatua na kama kuna uvunjifu wa maadili ya utumishi wa afya, uwajibikaji uwepo.

“Watanzania wanakosa dawa na vifaa tiba huko kwenye vituo vya afya vijijini, lakini wengine wanafanyia birthday?” amehoji Amos James.

“Unatumia mali ya Serikali iliyogharimu mabilioni ambayo kule Tanga mama mjamzito alipoteza uhai kwa kukosa tu pesa ya huduma ya upasuaji, huduma ambayo huenda angeipata bila kulipa chochote,” amesema Abdul Salaam.

Fahamu kuhusu dripu

Mfamasia na Mkufunzi wa Shule ya Famasia wa Chuo Kikuu Muhimbili (Muhas), David Myemba amesema majitiba yanayotumika kumwekea mgonjwa kupitia mishipa ya damu kawaida nusu lita huuzwa Sh2,000 japokuwa inategemea na ujazo husika kama ni lita moja ni zaidi ya hapo.

Alipoulizwa iwapo kuna madhara yoyote ambayo mtu anaweza kuyapata akitumia ndivyo sivyo, Mnyemba amesema hakuna madhara, isipokuwa kama mtu atakunywa mengi anaweza kuharisha.

“Ukinywa mengi unaweza kuharisha, lakini kuna mengine hayana madhara yoyote, ukinywa yenye sukari nyingi inapandisha sukari ghafla na kuna mengine yana madini mengi akitumia anaweza kupata madhara.

“Kwa kunywa hayana madhara, lakini hayatakuwa na faida ya moja kwa moja. Majitiba yanatakiwa kutumika kwa kuingiza moja kwa moja kweye mishipa ya damu, kwani hata ukinywa hayakati kiu kirahisi kama maji ya kawaida,” amesema Mnyemba.

MWANANCHI
Nilijua tu hawa watakuwa wanawake kwani wapenda sana kufanya vijisherehe uchwara....hawataki kupitwa na sherehe yoyote. Tatizo ni hawo wanaume wsliojichomeka humo kwenye sherehe. Hawa wanaume yafaa wachukuliwe hatua maradufu zaidi.
 
View attachment 2832151
=============


View attachment 2832152
Serikali iemanza kufanya uchunguzi kuhusu video inayosambaa mtandoni ikiwaonyesha watoa huduma za afya wakisherehekea siku ya kuzaliwa kwa kumwagiana majitiba maarufu ‘dripu’.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumapili, Desemba 3, 2023 Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Tumaini Nagu amesema bado video hizo hazina uhalisia na eneo linalotajwa, hivyo wanashirikiana na waganga wakuu wa maeneo husika kujiridhisha.

“Nimeiona asubuhi hii tunafuatilia, inaonekana kama hicho kituo kilichoandikwa pengine si chenyewe, lakini hatujapata uhakika vizuri,” amesema.'

Profesa Nagu amesema wanafuatilia kupitia Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita na Mganga Mkuu wa Manispaa ya Geita, lakini bado hawana uhahika kama ni kituo cha Serikali au cha binafsi.

“Tumeona picha za watu, lakini tunafuatilia kuona ni kituo gani, inawezekana pia si jina la kituo kilichoandikwa, tukishafuatilia tutatoa majibu mpaka tupate ukweli wa tukio lenyewe,” amesema Profesa Nagu.

Katika video hiyo iliyokuwa na maelezo kuwa ni watumishi wa afya katika kituo cha afya Nyankumbu, walionekana wanatumia maji ya kutibia wagonjwa (dripu) kwa sherehe yao ya kuzaliwa.

Hata hivyo, maoni ya watu mbalimbali katika mtandao wa kijamii wa Instagram yalijikita kwa Wizara ya Afya kutolea ufafanuzi jambo hilo, wakitaka ichukue hatua na kama kuna uvunjifu wa maadili ya utumishi wa afya, uwajibikaji uwepo.

“Watanzania wanakosa dawa na vifaa tiba huko kwenye vituo vya afya vijijini, lakini wengine wanafanyia birthday?” amehoji Amos James.

“Unatumia mali ya Serikali iliyogharimu mabilioni ambayo kule Tanga mama mjamzito alipoteza uhai kwa kukosa tu pesa ya huduma ya upasuaji, huduma ambayo huenda angeipata bila kulipa chochote,” amesema Abdul Salaam.

Fahamu kuhusu dripu

Mfamasia na Mkufunzi wa Shule ya Famasia wa Chuo Kikuu Muhimbili (Muhas), David Myemba amesema majitiba yanayotumika kumwekea mgonjwa kupitia mishipa ya damu kawaida nusu lita huuzwa Sh2,000 japokuwa inategemea na ujazo husika kama ni lita moja ni zaidi ya hapo.

Alipoulizwa iwapo kuna madhara yoyote ambayo mtu anaweza kuyapata akitumia ndivyo sivyo, Mnyemba amesema hakuna madhara, isipokuwa kama mtu atakunywa mengi anaweza kuharisha.

“Ukinywa mengi unaweza kuharisha, lakini kuna mengine hayana madhara yoyote, ukinywa yenye sukari nyingi inapandisha sukari ghafla na kuna mengine yana madini mengi akitumia anaweza kupata madhara.

“Kwa kunywa hayana madhara, lakini hayatakuwa na faida ya moja kwa moja. Majitiba yanatakiwa kutumika kwa kuingiza moja kwa moja kweye mishipa ya damu, kwani hata ukinywa hayakati kiu kirahisi kama maji ya kawaida,” amesema Mnyemba.

MWANANCHI
Kwanza kabisa siyo kama nawatetea kwa picha iliyopo hapo juu, ila twende mbele turudi nyuma. Tuna uhakika gani kama hiyo ni drip au walitumia chupa ambayo ilishatumika kujaza maji? Tusiwe wepesi sana wa kutamka kosa bila ya kuwepo uthibitisho. Miaka ya hivi karibuni watumishi wa umma wamekuwa wakichambuliwa kuwa na makosa bila kupata ushahidi wa kutosha. Unakuta mtumishi katenda kazi yake inavyotakiwa lakini unakuja sikia ooh afukuzwe,asimamishe, ashitakiwe bila kuwepo uthibitisho wa kosa. Nimekuwa nikifatilia sana nisikiapo watumishi wa umma lakini asilimia kubwa huwa tunawaonea sana kuanza sema wafukuzwe bila kuwepo ushahidi wa kosa. Sasa kama hapa ingependeza ufanyike ushahidi ili ijulikane ni kweli wametenda kosa ndiyo hatua stahiki zichukuliwe.. Kuna mtumishi mmoja iliwahi tokea kaletewa pesa na ndugu yake akamlipie ada kama kawa kuna mtu akapiga picha na kusambaza kuwa anapokea rushwa cha ajabu pesa jamaa alipokea akawa anahesabu bila kificho. Fikiria alivyomchafua mtu yule.Hawa ni madaktari siamini sana kama kwa taaluma yao tena wakuijirekodi kuwa wametumia drip kufanya hivi tuache uchunguzi uthibitishe.
 
Back
Top Bottom