Updated List: Haya ndio makabila yenye wasomi zaidi Tanzania

Updated List: Haya ndio makabila yenye wasomi zaidi Tanzania

Si kweli,pitia sensa ya watu kwenye mikoa ya wasukuma,tufanye wakazi wote humo wasukuma,wanafika 20m!?..20m ni mikoa minne iliyosheheni Kama dar...simiyu,shinyang,geita,mwanza hazifikishi watu 20m
Nimerekebisha ni milioni 10 na ushehe, nilikosea ku type

katika kila watz 6 kuna msukuma 1
 
Sema bn wachaga wapo smart sana kwenye kubebana unaweza Kuta padre mchaga wa shirika flan akapewa chance ya kusaidia vijana kumi jimboni mwake, akawachukua wachaga wenzake hata ambao hawajui mlango wa kanisa 😄
Sijui wanalalamika nini watu wa makabila mengine kila kitu kiko wazi ukipata chansi shika mkono nduguzo.....

😂😂😂😂😂🙌🙌🙌ishara na sala muhimu wanazijua hivyo hawatomuanguasha kama kuna interview.
 
Si kweli,pitia sensa ya watu kwenye mikoa ya wasukuma,tufanye wakazi wote humo wasukuma,wanafika 20m!?..20m ni mikoa minne iliyosheheni Kama dar...simiyu,shinyang,geita,mwanza hazifikishi watu 20m
Umesahau
Tabora,
Katavi,
Rukwa,
Morogoro,
Mbeya


Wamesambaa karibu kila kona ya nchi leta hiyo taarifa yako ya sensa.

Wasukuma ndio kabila kubwa Tanzania.
 
Sema bn wachaga wapo smart sana kwenye kubebana unaweza Kuta padre mchaga wa shirika flan akapewa chance ya kusaidia vijana kumi jimboni mwake, akawachukua wachaga wenzake hata ambao hawajui mlango wa kanisa [emoji1]
Kwa kweli, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wakerewe na wajita wameingiliana sana,

Wamatengo ni jamii ndogo hio ila ndio ya pili kuwa na percent kubwa ya kuelimika kwa mikoa ya kusini nyuma ya Wanyaki.

Wakurya wameelimika hasa hawa wa dsm, wengi wazazi wao wapo majeshini uwezo wa ada upo.

waha bado sana mkuu, labda kwa biashara wapo nyuma ya mkinga
Wamatengo wako nyuma ya wanyakyusa kwa ukandaa huu wa juu kusini.
 
Umesahau
Tabora,
Katavi,
Rukwa,
Morogoro,
Mbeya


Wamesambaa karibu kila kona ya nchi leta hiyo taarifa yako ya sensa.

Wasukuma ndio kabila kubwa Tanzania.
Hao waliosambaa wafidie na makabila mengine wanaoishi mwanza,simiyu,geita,shinyanga..tufanye hiyo mikoa yao wote ni wasukuma,hawafiki 20m,tabora Ina watu 3m+, majority wanyamwezi,moro wangapi?
 
1. Wachaga - Kama kawaida yao sio watu wa kujisifia iwe ni biashara, maendeleo ya vijini kwao, n.k. Kiufupi hawa suala la elimu wapo Mbali tangu enzi za ukoloni, Mkoa wa Kilimanjaro ni mdogo ila ndio unaongoza kwa shule nyingi hasa maeneo ya uchagani, Kitu cha ziada ambacho wengi hawakijui ni kwamba wana mwamko wa shule za kimataifa na hata miji wanayoishi ya Moshi na Arusha kuna shule hizi nyingi kama St Constatine, Braeburn, INternational school of Moshi, Kennedy house, n.k. Kwenye shule hizi watoto utaowakuta kutoka Tz ni wachache ila majority huwa ni wachaga kwasababu ya mwamko, sio suala la mzazi kuwa na pesa tu, na hata zile nafasi za udhamini wanazijaza wao, Shule hizi ni tofauti kabisa na hizi za Necta, huku ukisoma kuna guarantee kubwa kusoma vyuo bora duniani, Walimu bora wa kimataifa, connections nzito, n.k.

2. Wahaya - Yes, Ni nani asiewajua watu hawa waliowekewa kizuizi na Nyerere kwa alama za kufaulu darasa la saba ? Hawa watu wanaipenda shule jamani, Shida ni kwamba kuna changamoto za kiuchumi mkoani Kagera, wapo wengi wanaotamanigi kuendelea na shule na uwezo upo ila inawalazimu waendelee na maisha mengine,

3. Wanyakyusa - Ughonile, Nimeishi nao so nawajua vizuri hawa kina Mwakyusa, Mwakatobe, Mwakyembe, Bukuku, n.k., wazazi wa kinyakyusa hasa wamama wanaasa sana watoto wasome, wapo tayari kujinyima kwa lolote mtoto asome shule nzuri, Nakumbuka nikiwa Mbeya mtu anaweza kuresit form 4 hata mara 3 kutafuta credit, hawana jambo dogo kwenye elimu !! kuhusu uwezo darasani wanao wa kawaida ila wapo wachache nishawai kutana nao ni ma genius, Kwa sasa Mbeya ndio mkoa inaoongoza kwa vyuo ukiitoa Dsm, Kuba shule za kiingereza 4 za serikali za msingi, Shule za Sekondari zipo nyingi

4. Wasukuma - Wingi wao unawabeba nao waweze kuonekana, kuna wasukuma milioni 10 na ushehe hapa Tz, katika kila watanzania 6 kuna msukuma 1, Tatizo la kuwa chini kielimu ni kwamba huko mikoa ya Simiyu, Geita, Shinyanga, n.k shule ni changamoto ila Mwanza wamejitahidi,

5. Wakerewe / Wajita - (Hapa nitaomba mnisahishe hivi wakerewe na wajita ni kabila moja ? ) Anyway nachojua Wakerewe wapo visiwa vya ukerewe, Wajita wapo ukerewe na mkoa wa Mara, Ukerewe ndio wilaya inayoongoza kwa phd, Jimbo kama musoma vijijini huko ni kawaida wagombea wote kuwakuta wana phd, hawapo namba moja kwasababu wanaosoma wanafika mbali sana kielimu ila wanaopata access ya elimu bado wachache.

Bonus....

Wapare, Wakurya, wamasai wa Meru, Wangoni wa wilaya ya Tunduru (Wamatengo) n.k. huku changamoto ni access ya elimu ila angalau nao si haba.
Mngoni usimkabidhi Wife hatofika salama,..ila pesa zinafika🤭🤭
 
Kwahyo sisi wakinga,wahehe mnatuchukuliaje kielimu lakini😅😅😅
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nitegemee connection JF? nilishavuka hizo level
Si ndo watu wanavotishianaga humu ooh! Ukiomba msaada watu wanapitia threads na michango yako humu! Yaan niache kutetea nyeto & kupinga ndoa kisa kupata connection 🤣🤣🤣asaalaleeeee!
 
1. Wachaga - Kama kawaida yao sio watu wa kujisifia iwe ni biashara, maendeleo ya vijini kwao, n.k. Kiufupi hawa suala la elimu wapo Mbali tangu enzi za ukoloni, Mkoa wa Kilimanjaro ni mdogo ila ndio unaongoza kwa shule nyingi hasa maeneo ya uchagani, Kitu cha ziada ambacho wengi hawakijui ni kwamba wana mwamko wa shule za kimataifa na hata miji wanayoishi ya Moshi na Arusha kuna shule hizi nyingi kama St Constatine, Braeburn, INternational school of Moshi, Kennedy house, n.k. Kwenye shule hizi watoto utaowakuta kutoka Tz ni wachache ila majority huwa ni wachaga kwasababu ya mwamko, sio suala la mzazi kuwa na pesa tu, na hata zile nafasi za udhamini wanazijaza wao, Shule hizi ni tofauti kabisa na hizi za Necta, huku ukisoma kuna guarantee kubwa kusoma vyuo bora duniani, Walimu bora wa kimataifa, connections nzito, n.k.

2. Wahaya - Yes, Ni nani asiewajua watu hawa waliowekewa kizuizi na Nyerere kwa alama za kufaulu darasa la saba ? Hawa watu wanaipenda shule jamani, Shida ni kwamba kuna changamoto za kiuchumi mkoani Kagera, wapo wengi wanaotamanigi kuendelea na shule na uwezo upo ila inawalazimu waendelee na maisha mengine,

3. Wanyakyusa - Ughonile, Nimeishi nao so nawajua vizuri hawa kina Mwakyusa, Mwakatobe, Mwakyembe, Bukuku, n.k., wazazi wa kinyakyusa hasa wamama wanaasa sana watoto wasome, wapo tayari kujinyima kwa lolote mtoto asome shule nzuri, Nakumbuka nikiwa Mbeya mtu anaweza kuresit form 4 hata mara 3 kutafuta credit, hawana jambo dogo kwenye elimu !! kuhusu uwezo darasani wanao wa kawaida ila wapo wachache nishawai kutana nao ni ma genius, Kwa sasa Mbeya ndio mkoa inaoongoza kwa vyuo ukiitoa Dsm, Kuba shule za kiingereza 4 za serikali za msingi, Shule za Sekondari zipo nyingi

4. Wasukuma - Wingi wao kuwa 16% katika population ya nchi ndio unawabeba zaidi waweze kuonekana ila kwa asilimia ya wasomi ndani yao bado ni wachache sana walioelimika, Tatizo la kuwa chini kielimu ni kwamba huko mikoa yao walipojazana kama Simiyu, Geita, Shinyanga, n.k shule ni hazipewi kipaumbele, wasomi wengi hutokaa Mwanza,

5. Wakerewe / Wajita - (Hapa nitaomba mnisahishe hivi wakerewe na wajita ni kabila moja ? ) Anyway nachojua Wakerewe wapo visiwa vya ukerewe, Wajita wapo ukerewe na mkoa wa Mara, Ukerewe ndio wilaya inayoongoza kwa phd, Jimbo kama musoma vijijini huko ni kawaida wagombea wote kuwakuta wana phd, hawapo namba moja kwasababu wanaosoma wanafika mbali sana kielimu ila wanaopata access ya elimu bado wachache.

Bonus....

Wapare, Wakurya, wamasai wa Meru, Wamatengo wa Ruvuma, n.k. huku changamoto ni access ya elimu ila angalau nao si haba.
Pia kuna kabila dogo la Wamwera toka Lindi, Ruangwa na Nachingwea.....hawa nao wamesoma sana na si kabila la maringo hata akisoma hapendi kujionyesha kama Muhaya kwa kujifanya anaongea Kiingereza kibovu ili watu wajuwe kakariri lugha za watu, wataongea Kiingereza tu kama itabidi afanye hivyo.
 
Back
Top Bottom