Elections 2015 Updates: Mchakato na Matokeo ya kura za maoni ya Ubunge CCM nchini kote

Elections 2015 Updates: Mchakato na Matokeo ya kura za maoni ya Ubunge CCM nchini kote

kumetokea hali ya sinto fahamu huko tarime baada ya kukamatwa kwa kura zaidi ya elfu 20000 zilizo onyesha jina la nyangwine, ni matumaini yangu kua ccm inaelekea kudondoka katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu kutoka na kutojiamini na wanachama wao. Ni jambo lakushangaza katika jamii kwa watia nia wa ccm kwa ngazi mbali mbali kukamatwa na rushwa. Hii ni dalili tosha la anguko la ccm mwaka huu.
 
Uchaguzi umeharishwa hadi kesho baada ya kukamatwa kwa karatasi zenye majina ya Nyambari na Gaudensia zilizotikiwa kwa majimbo ya Tarime mjini na Vijijini. Ni elfu ishirini 20,000 Invisible

Chanzo:ITV
 
Last edited by a moderator:
Hehehehe kawaida iyo ndani ya chichiem
 
Duuu...huku ni kina muganyizi tuuu ...
hapa kuna kitu tofauti nimejifunza
maana sijaona hapo kina
Simba Mpunda (kutoka songea)
Mushi Kileo (wachaga)
Mwakatumbula Mwakyambiki (wanyakyusa)
Kikoti Kufakunoga (wahehe)
Ngosha N'gwanangwa (wasukuma)
Sanga Chengula (wakinga) n.k
hiyo ni baadhi tu ya mifano niliyoitoa ....wadau mnaweza toa zaidi.

Unataka kusemaje.........mbona umeongea VIRAI.....elezea kidogo walau iwe KISHAZI ila kisiwe tegemezi. Soma vizuri majina ya wagombea wa KYERWA kisha useme kuhusu huyo chacha. Pia zungumzia neutral names ambazo umeshindwa kuzi attach.... na utumbo wako utueleze unawafahamu vipi.
 
Kutoka Mkoani Kagera nakuletea LIVE UPDATES ikiwemo na matokeo kadri nitakavyoyapata.

Historia kidogo
Mkoa wa Kagera una majimbo tisa ya uchaguzi ambapo wabunge wawili tu wametangaza kung’atuka ambao ni Deogratias Ntukamazina wa Jimbo la Ngara na Bw Esutace Katagira wa jimbo la Kyelwa.

Saa 12:02 Adhuhuri
Hizi ni baadhi ya picha kutoka vituo mbalimbali katika kata zilizoko manispaa ya Bukoba.
wengine kutoka vyama tofauti na CCM.


View attachment 272870

View attachment 272871

View attachment 272872

Saa 10:38 Asubuhi
.Wanachama wa CCM wanaendelea na upigaji kura ingawa katika maeneo mbalimbali ya kata ya Kanyigo wilyani Missenyi wasimamizi wanalalamikia kuwepo kadi za ccm ambazo hazipo katika kitabu cha orodha ya wanachama

.Kata ya Nshambya Bukoba Mjini na maeneo mengine ya mji wa Bukoba zoezi linaendelea ingawa kuna wanachama wachache sana katika vituo.

.Mgombea mmoja katika jimbo la Bukoba(jina lake nitalitaja baada ya kupiga kura)jana aligoma kusaini makubaliano ya kutaka kila mgombea kukubaliana na matokeo na kuwa tayari kumuunga mkono atakayepitishwa .

.Wilayani Karagwe wanachama bado hawaamini macho wao kukuta wagombea wawili maarufu Gosbert Blandes(mbunge wa sasa) na Karimu Amri ambao walidaiwa kujitoa majina yao hayamo katika orodha ya wanaotakiwa kupigiwa kura.Hivyo hao wanachama siyo wagombea,baadhi ya akina mama wamegoma kupiga kura baadhi ya maeneo kwa kukosekana wagomea hao.

Wagombea kwa kila Jimbo

Bukoba Mjini:
Wagombea ni
1:Balozi Khamis Kagasheki,
2:Bw.George Rubaiyuka,
3:Bw. Josephat Kaijage,
4:Bi.Elieth Projestus
5: Dr.Anathory Amani,
6:Bw.Philbert Katabazi,
7:Bw.Mujuni Katarahiya
8: Bi.Celestina Rwezaura.

BukobaVijijini
Wagombea ni
1:Bw.Jasson Rweikiza ,
2:Bw. Nazir Karamagi
3:BW.Nelson Itagasa.

Muleba Kaskazini
Wagombea ni
1: Charles Mwijage
2: Bw.Ambrose Nshala.

Muleba Kusini
Wagombea ni
1😛rofesa Anna Tibaijuka,
2😀r Adam Nyaruhuma,
3:Bw.Stivin Tumaini,
4:Bw.Flavius Kahyoza,
5:Mhandisi Buruani Rubanzibwa,
6:Muhaji Bushako
7:Kaino Mendesi
8: Bw. Erick.

Jimbo la Ngara
Wagombea ni
1:Syprian Gwassa,
2😀r Philemon Rugumiliza,
3:Bi.Helen Adrian n
4:Bw.Wilbald Ede
5: Bw.Alex Gashaza,
6:Bw.Jelard Muhile,
7:Johakim Nchunda ,
8:Bw.Issa Samma
9: Bw.Ladslaus Bambanza.

Jimbo la Nkenge
Wagombea
1:Asumpta Mshama,
2😀iodorous Kamala,
3😀r Mazima,
4:Bw Frolent Kyombo,
5:Bw Julius Rugemalira
6:Bw......

Jimbo la Kyerwa
Wagombea ni .Innocent Seba Bilakwate,Stephano Edward Katemba
3.Lameck Chacha Ng’ang’a
4.Norbeth Kobwino
5.Sinsibath Kashunju Runyogote
6.Pancrace Shwekelela
7.Awaam Ahamada Ngalinda

Jimbo la Karagwe.
1.Mwalimu Dagobati Deogratias
2.Audax Christian Rukonge
3.Innocent Luga Bashungwa
4.Gosbert Begumisa Blandes
5.Alfred Rujwahuka
6.Amoni Chakushemeire Eustad
7.Karimu Amri

ahaaaaa loh huyu mtoto norbeth kobwino aliwa lini? Kafufukia wap? Loh kumbe na mm siku moja ntakuwa mbunge loh, norbeth wewe katafte uzoefu yo too young to this loh.

Mkuu ukipata pic ya norbeth kobwino mtoto wa mwl kobwino niwekee nione kama alikua loh. Shule moja alimaliza la 7 nikiwa std 3 and since then sijawai mwona loh
 
Leo ni August 1,2015 Wanachama wa chama cha Mapinduzi (CCM) nchi nzima wanakusanyika katika maeneo ya matawi yao kuchagua mgombea mmoja atakayeshindana na wagombea wengine kutoka vyama tofauti na CCM.

Mchakato wa kampeini katika mkoa huu zimetawaliwa na vituko,udhalilishaji kwa baadhi wa wagombea hivyo hata upigaji kura za maoni utakuwa hivo hivyo,hii ndiyo sababu inatufanya tufuatilie live kura hizi.

Updates...






😱😱
 
Hivi huyu Mwinyi siyo tamaa ya MADARAKA, yaani wao wakiona Unguja kimenuka wanakuja kufanya FUJO bara, huu ni upuuzi unatakiwa kuwa defined kwenye katiba

Wanadhani majina yatawabeba, wamuche Dr bana teh teh teh
 
Wandugu vipi Habari ya Zungu na kijana mbishi Mrisho Gambo???? Mwenye update Jaman pande hizo!
 
Updates za uchaguzi jimbo la Kongwa kwa mheshimiwa Ndugai, matokeo katika baadhi ya vituo mheshimiwa ambaye alituhumiwa kumpga mgombea mwenzake ameshnda kwa kura nyngi sana dhidi ya wagombea wenzake
 
MWAKYEMBE AWABWAGA MWAKALINGA, LOWASSA NA KYELA FM KWA KISHINDO
Na Malikira S.

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mbunge wa Kyela aliyemaliza muda wake, Dk. Harrison Mwakyembe, amewabwaga kwa kishindo kikubwa wahasimu wake wa kisiasa kwenye kura za maoni zilizofanyika wilayani Kyela leo.

Muda wa saa kumi jioni ulipotimu wa kukamilisha upigaji kura, Mwakyembe alikuwa tayari anaongoza kwenye vituo karibu vyote kwa zaidi ya asilimia 75, akiwaacha kwa mbali wagombea ubunge wenzake 9 akiwemo George Mwakalinga anayeishi Uingereza na kuitumia redio yake, Kyela FM, kinyume na taratibu kwa kujitangaza kwa wiki mbili mfululizo kuwa chaguo bora na kumkandia Dk. Mwakyembe kuwa hafai.

Mwakalinga, mhandisi aliyekosa kabisa haiba ya uanasiasa kutokana na uongeaji wake wa taratibu usio na mvuto na hasira kali za papo kwa papo, anadaiwa kuwa karibu na Edward Lowassa, mwanasiasa mkongwe nchini aliyehamia CHADEMA kutoka CCM hivi majuzi, kutokana na kaka yake Mwakalinga kuoa Monduli.

Pamoja na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) kumtahadharisha asiitumie kisiasa redio yake aliyoisajili kama redio ya jamii kwa kukejeli, kutukana na kudhalilisha wengine, Mwakalinga kwa kushirikiana na wanasiasa wenzake wanane walioungana naye kumkabili Mwakyembe, ameendelea kuitumia Kyela FM kumshambulia Dk. Mwakyembe na kuwasihi wananchi wasimpe kura.

Mwakalinga kwa kushirikiana na aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kyela, Gabriel Kipija, mwanasiasa mchanga anayefundisha Chuo cha Uhasibu Mbeya, John Mwaipopo na mkandarasi anayetuhumiwa kuchelewesha miradi mitatu ya barabara wilayani Kyela, Vincent Mwamakimbula, wamekuwa wakiwalipa fedha wafuasi wa CHADEMA kumfanyia fujo Dk. Mwakyembe kwenye mikutano ya kujinadi kwa nia ya kumvunja moyo.

Dk. Mwakyembe kama ilivyo kwa wanasiasa wazoefu, hakuteteleka na aliendelea kuelezea utekelezaji wa Ilani za Uchaguzi za CCM za 2005 na 2010 na kuwathibitishia wananchi Kyela kuwa wilaya yao imepiga hatua kubwa ya maendeleo.

Idadi kubwa ya wananchi Kyela hawajafurahishwa na udhaifu wa TCRA wa kushindwa kusimamia sheria zake, hivyo kuiacha Kyela FM ikivuruga mchakato wa kidemokrasia ndani ya CCM kwa zaidi ya wiki mbili.

Taarifa tulizopokea toka kwa mawakala wa vituo karibu vyote wilayani Kyela zinaonyesha Mwakyembe akiwa mbele ya wagombea wengine na huenda akapata zaidi ya asimilia 75 ya kura zote.
 
Uchaguzi wa kura za maoni kupitia CCM katika jimbo la Tarime Mjini na Vijijini umeahirishwa hadi kesho baada ya kukamatwa kura feki Zimekamatwa Kura feki zaidi ya elfu 20 zikiwa zimewekewa alama ya NDIO kwa majina ya wagombea Nyambare Nyangwine na Gaudencia Kabaka.
 
Back
Top Bottom