Upepo kisiasa umebadilika, Lissu aongezewe ulinzi

Upepo kisiasa umebadilika, Lissu aongezewe ulinzi

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Siyo siri tena kuwa tangia kurejea nchini kwa mwanasiasa TAL, hali ya kisiasa nchini imebadilika kabisa.

Haipo shaka kuwa huyu ndiye mwanasiasa anayefuatiliwa zaidi kwa sasa hapa nchini na makundi yote. Humo wamo wafuasi wa chama chake na hata wafuasi wa vyama hasimu, chawa na viongozi wao bila kuwasahau watanzania wengine.

Tathmini ya kawaida mitaani na kwenye mitandao inaonyesha hivyo. Kwa hakika haihitajiki TWAWEZA kuthibitisha hilo.

Wapo ambao kwenye kujitoa kimasomaso wametaka kumkejeli na hata kutaka kukejeli kushambuliwa kwake Dodoma. Wapo ambao wana wivu kama ule wa Six, wenye hata kutamani wao wangekuwa huyu mwamba. Wapo wenye kuchukizwa na popularity yake. Wapo wenye kujidhania kuwa ni bora zaidi kwanini iwe huyu, nk nk.

Zaidi sana wapo waliomfyatulia risasi na hata wale wenye lao jambo, walioliratibu shambulizi zima kule Dodoma.

"Yapo pia mataifa hasimu yanayotuzunguka ambayo yanaweza kupenda kuukaanga mbuyu."

Kwa hakika itakuwa kujidanganya sana kudhani kuwa eti hali ni shwari bin sawia.

"TAL na CHADEMA chonde chonde, uinzi unasibu uhalisia."
 
Taifa adui kwa Tanzania ni lipi ?

Kwa mfano ikitokea TL akauwawa unahisi kuna kitu chochote kitatokea tofauti na mazishi?

Taifa lolote lililowahi kututishia kwenda vitani nasi haliwezi kuwa taifa rafiki. Vita si jambo dogo.

Huyu ndugu aliwahi kutishiwa kuuwawa, aliwahi kushambuliwa kuuwawa na amekwisha nusurika kuuwawa.

Kwanini tusijipange kuona yuko hai badala ya kujipanga kwa mazishi?
 
Siyo siri tena kuwa tangia kurejea nchini kwa mwanasiasa TAL, hali ya kisiasa nchini imebadilika kabisa.

Haipo shaka kuwa huyu ndiye mwanasiasa anayefuatiliwa zaidi kwa sasa hapa nchini na makundi yote. Humo wamo wafuasi wa chama chake na hata wafuasi wa vyama hasimu...
Naunga mkono hoja kwa asilimia zaidi ya 100; isipokuwa tu nyongeza ni kwamba mimi nina dhana kuwa TL anaweza akawa anafuatiliwa na kundi tofauti na lile la wanasiasa, ukizingatia yale ambayo tayari yameshawahi kumtokea huko nyuma.

Akipewa ulinzi, itakuwa imewasaidia Serikali kuepuka uwezekano wa kuja kuchonganishwa naye tena kwa mara nyingine huko mbele ya safari.

Good idea
 
Naunga mkono hoja kwa asilimia zaidi ya 100; isipokuwa tu nyongeza ni kwamba mimi nina dhana kuwa TL anaweza akawa anafuatiliwa na kundi tofauti na lile la wanasiasa, ukizingatia yale ambayo tayari yameshawahi kumtokea huko nyuma. Akipewa ulinzi, itakuwa imewasaidia Serikali kuepuka uwezekano wa kuja kuchonganishwa naye tena kwa mara nyingine huko mbele ya safari.
Good idea

Ninakubaliana na wewe 💯%.

Kuongezea hapo, zingatia kina Jilala, Mtambuka na wenzao vinara wa kuandika habari za Lissu, nyuzi kama hizi ni mwendo wa kupita kimya kimya.
 
Siyo siri tena kuwa tangia kurejea nchini kwa mwanasiasa TAL, hali ya kisiasa nchini imebadilika kabisa...
Hakika Tundu Lissu, ndiye Nelson Mandela wa nchi hii, hivi sasa

Kupitia mateso aliyoyapata Kwa kupigwa risasi 16, mchana kweupe, bila hata mtuhumiwa hata mmoja kukamatwa Ili ahojiwe.

Huyu ndiye ninayemtabiri kuwa the next President of our country
 
Naunga mkono hoja kwa asilimia zaidi ya 100; isipokuwa tu nyongeza ni kwamba mimi nina dhana kuwa TL anaweza akawa anafuatiliwa na kundi tofauti na lile la wanasiasa, ukizingatia yale ambayo tayari yameshawahi kumtokea huko nyuma. Akipewa ulinzi, itakuwa imewasaidia Serikali kuepuka uwezekano wa kuja kuchonganishwa naye tena kwa mara nyingine huko mbele ya safari.
Good idea
Una akili kubwa. Vilaza hatakuelewa kamwe
 
Lissu Kapotea tayari!!! Tunahadaana tu humu mitandaoni!!

Kwa alama zote hizo za msisitizo, inaonekana uko na makasiriko sana na huyu ndugu aliye kipenzi cha wengi.

Ni kutokana na mwendelezo wa makasiriko ya watu kama wewe, ni vyema mapema sana ya ka "serve as a wake up call" akapatiwa ulinzi sahihi.

Aliwaudhi nini Lissu watu kama nyie?

FoVixEVWAAAou0r.jpeg
 
Hivi wale makomandoo waliokuwa wanamlinda Mbowe, na wengine wakamlinda Lissu wakati ule wa kampeni hawapo?

Kama wapo, unataka waongezwe wengine na chama chake, au serikali nayo itie mkono wako?

Kama ulinzi anaopewa na chama chake unaonekana hautoshi, basi vyema apewe ulinzi na serikali, ni kuongea na mama mwenye nchi tu.
 
Hivi wale makomandoo waliokuwa wanamlinda Mbowe, na wengine wakamlinda Lissu wakati ule wa kampeni hawapo...

Kwa hali ilivyo huyu bwana ni mtu anayefuatiliwa zaidi hapa nchini kuliko wote. Beberu akiita HVT - High Valued Target.

Kuna watu hawalali wanamfuatilia huyu bwana iwe ni kwenye Space, tweets, mahojiano, mikutano, safari nk.

Makomando wale na walinzi wa Chadema hakuna shaka kuwa wanafanya kazi nzuri. Lakini ni wazi kuwa haitoshi.

Kwenye jamii zilizoendelea ulinzi na usalama wa watu hutegemeana na hali halisi ilivyo na yaweza badilika kila wakati.

"Kiuhalisia ulinzi huwa hauombwi bali wenye dhamana hupaswa kuwajibika kutokana na "threat level" kwa mtu na mazingira, inayotofautiana baina ya mtu na mtu."

Ninadhani pamoja na walinzi wa Chadema, assurance na facilitation ya serikali kwenye kuhakikisha huyu bwana yuko salama ni muhimu sana.

TAL mwenyewe na CHADEMA wenyewe ni muhimu wakajiridhisha kuwa usalama wa kutosha upo.

Si vyema kupuuza lolote. Lolote kinaweza kutokea. Hii ikiwa ni kutokea kwa maadui wote wa ndani na hata nje.

Tahadhali ni kabla ya hatari.
 
Back
Top Bottom