Upepo wa kisiasa nchini hausomeki, kuna nini?

Upepo wa kisiasa nchini hausomeki, kuna nini?

Mimi hii point ya uchaguzi hainiingii akilini sana kwa sababu siuoni upinzani wenye nguvu, nje ya chama na ndani ya chama.

Ama labda nipate ufafanuzi zaidi kutoka kwako namna hofu hiyo ya uchaguzi inavyoweza hata kuhatarisha usalama wa maisha ya watu kwa kiasi kikubwa namna hii!
Upinzani upo ndani na sio nje. Nguvu ya vijana wawili waliowekwa pembeni juzi Kati inachangia pia.
 
Katika kipindi hiki kifupi kama miezi mitatu hadi sita, upepo wa kisiasa hausomeki. Matukio tunayoyaona mengine si tu siyo ya Kitanzania lakini yanakinzana na hata mila, utamaduni, umoja wetu kitaifa na hata imani yetu.

Mengine ni aibu hata kuyasema maana ni laana kwa Taifa letu. Viongozi kwa sana wako kimya, kimya kizito. Kuna nini?
  • Watoto wadogo wanabakwa na kulawitiwa.
  • Watu wanauwawa kama majuzi Mohammed Kibao wa Tanga.
  • Watu wanatekwa na kutupwa maporini
Wakati huo huo mikeka ya teuzi na tengua ni kila baada ya mwezi mmoja. Sasa inaelekea gundi inayotuunganisha Watanzania inazidi kuwa nyepesi.

Mwalimu alisema ili tuendelee, tunahitaji vitu vinne; Watu, Ardhi, Siasa safi na Uongozi bora!

Tunakosea wapi?
Tunakosea hapo kwenye CCM!
 
Bora hata mtangulizi wake alivuka kuingia awamu ya pili kidogo. Yeye hatoboi mbali ya hiki kiporo alichomalizia.

By 2026 kama atakuwa hai basi atakuwa busy akisimulia hadithi za alfu leila ulela kwa wajukuu zake Kizimkazi.
watu hawamtaki kabisa
 
Tulikosea kwenye duplication ya siasa safi na uongozi bora, ni kitu kile kile, mtaji una miss hapo, ili kuendana na theory ya Adam Smith ya Land, labor, capital na entrepreneurship, kosa la Nyerere ni moja tuu kusema fedha sii msingi, fedha ni matokeo, kiukweli fedha ni msingi sana!, and in fact, fedha ndio kila kitu!, inahamisha watu na milima!. Twigwa wawili jike na dume, wameibwa kutoka Serengeti na watu wenye fedha, wakawapeleka Dubai kwenye zoo, leo watu wanamiminika zaidi kuwaangalia twiga wa Dubai, kuliko wale wa Serengeti!.
P
The most important resource for development is not money, but people. They only need to be empowered and enabled. Ni nukuu toka kwa mwana sosholojia nimemsahau jina.
 
Zunguka kote lakini mkirudi tuandike katiba mpya ndo dawa pekee iliyobaki kama tunataka kuendelea kuwa taifa Moja

Vinginevyo ni kuendelea kujlilisha upepo kuwa mambo yatajiset yenyewe

Ccm wanaamini watutumia udanganyifu utekaji, mauaji, ufisadi na ugaidi kuendelea kutawala
Lakini mbinu hizi xinaenda kushindwa

Njia pekee ya kuzuia nchi isimeguke vipande vipande ni kuleta katiba mpya yenye serikali za shirikisho
Mtake mistake


Wakati ccm wako bize kuteka na kuua wapinzani wakidhani ndo adui wa taifa je. Wamechungulia kuaona hatari ya kumeguka kwa nchi??
Katiba inapoleta kigugumizi kwa kiongozi kuwashughulikia wahalifu NDANI ya serikali basi katiba hiyo ni mufilisi.
 
Katika kipindi hiki kifupi kama miezi mitatu hadi sita, upepo wa kisiasa hausomeki. Matukio tunayoyaona mengine si tu siyo ya Kitanzania lakini yanakinzana na hata mila, utamaduni, umoja wetu kitaifa na hata imani yetu.

Mengine ni aibu hata kuyasema maana ni laana kwa Taifa letu. Viongozi kwa sana wako kimya, kimya kizito. Kuna nini?
  • Watoto wadogo wanabakwa na kulawitiwa.
  • Watu wanauwawa kama majuzi Mohammed Kibao wa Tanga.
  • Watu wanatekwa na kutupwa maporini
Wakati huo huo mikeka ya teuzi na tengua ni kila baada ya mwezi mmoja. Sasa inaelekea gundi inayotuunganisha Watanzania inazidi kuwa nyepesi.

Mwalimu alisema ili tuendelee, tunahitaji vitu vinne; Watu, Ardhi, Siasa safi na Uongozi bora!

Tunakosea wapi?


View: https://www.facebook.com/chechetimes/videos/534875735776176/?mibextid=rS40aB7S9Ucbxw6v

CHADEMA kuna hili nalo mkalitazame.

Unabii inazidi kutimia.
 
Back
Top Bottom