LGE2024 Upigaji Kura Kata ya Itumbili Magu ulivyokuwa, Waziri Dkt. Stergomena ni mmoja kati ya walioshiriki

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) tarehe 27 Novemba 2024 amepiga Kura ya kuwachagua Viongozi wa Serikali za Mitaa katika Mtaa wa Unyamwezini Kata ya Itumbili, Magu mkoani Mwanza.

Mara baada ya kupiga Kura, Dkt. Stergomena Tax, amesema ameridhishwa na hali iliyopo kituoni hapo ambapo alisema “Natoa wito kwa Wananchi wenzangu kufika kwenye Vituo vilivyoandaliwa ili waweze kupiga Kura na kutumia haki yetu ya kikatiba na kuwachagua viongozi ambao tunaona tumeridhika nao.”

Naye Mkuu wa Wilaya Magu, Joshua Nasari amewahakikishia Wananchi Usalama katika vituo vyote wilayani hapo.

Naye Afisa Msimamizi Kata ya Itumbili, Bi. Lina Amata ameeleza kuwa, zoezi la upigaji kura limeenda vizuri na hakuna changamoto yoyote iliyojitokeza.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…