Upinzani acheni kumu-underrate Makonda, mnapotezwa , Jamaa anaitangaza CCM kwelikweli, hatangazi Mtu!

Mleta mada yuko sahihi, kama tunakubaliana asilimia kubwa ya watanzania ni wajinga, wale wanaodanganyika kwa tshirts za CCM wakati wa kampeni, na kama Makonda ndio anazunguka kuwadanganya hao wajinga kwa kuongea na mawaziri, wapinzani wasidharau anachofanya makonda.

- Ni kama kitu cha kijinga kwa mwerevu, lakini kwa mjinga, ni kitu cha ajabu sana.

Hata kama CCM huiba kura, lakini kwa sasa panahitajika nguvu ya kwenda na Makonda step by step, huyu anaonekana kabisa amekuja kuifanya ile kazi ambayo Chongolo na Kinana iliwashinda, na mpaka sasa, anaifanya vyema, zitafutwe mbinu za kukabiliana nae, hata kama anachosema ni uongo, ukirudiwa sana hugeuka kweli.
 
Tathimini inaonyesha kuwa watu wengi walio vilaza na wale wenye vyeti feki ndiyo wanakunwa sana na uchapakazi wa Makonda na matumaini makubwa kwake.
 
Ujinga na umasikini ni kitu kibaya sana,unaitàmgaza CCM yenye miaka zaidi ya 50 ,kwani Kuna chama kingine kilisha ongoza?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…