Uchaguzi 2020 Upinzani kujitoa kushiriki Uchaguzi Mkuu 2020 siyo uoga wala ujinga, kitakuwa ni kitendo cha ushujaa na uzalendo

Sawa kabisa!
 
Wapinzani wetu nao wanataka vyeo hata kwa njia haramu. Hapo ndipo tutasubiri sana kuleta mabadiliko ya kweli
 
Kwa huzuni sana, lengo la CCM ni kuwafanya wapinzani wakuu hao wasusie uchaguzi. Ndio lengo kuu maana kina lipumba watabaki na itahesabika vyama 14 vimeshiriki uchaguzi.
 
Niseme ukweli, japo mchungu, kuwa upinzani tulionao hauwezi kujitoa maana wapinzani wengi nao wanapigania vyeo si mabadiliko. Wanasema siasa inalipa! Wako tayari kushiriki uchaguzi wanaouita uchafuzi, batili na haramu ilimradi waambulie udiwani, ubunge na kura za urais za kuongezea ruzuku za vyama vyao. Wengi (si wote) wanagombea maslahi yao binafsi, si maslahi ya umma!

Mara kadhaa nimewahi kuwashauri kwamba tupiganie tume huru kwanza, katiba mpya kwanza, wagombea huru kwanza na mifumo mingine mipya kwanza ndiposa tuingie kwenye uchaguzi, lakini wapi. Ni dhahiri kuwa bila uwanja sawa wa kisiasa, bila kuwa na refa (tume huru) asiyeegemea upande wowote ni kushiriki kwa hiari uchafuzi, ubatili na uharamu. Wasilalamike!

Kenya na Malawi walimwengua rais aliyepitishwa na tume za upendeleo kwasababu walibadili mifumo ya uchaguzi na kuruhusu matokeo kuhojiwa mahakamani. Lakini wapinzani wetu wanataka vyeo kwanza na marupurupu yake!

Nawaomba baada ya uchaguzi wakae kimya, wasilalamikie dosari zozote zitakazojitokeza, maana wamekubali kushiriki uchaguzi chini ya tume na mifumo mingine wanayodai batili na haramu. Ukikubali kushiriki kula chakula unachojua kina sumu na haramu, usilalamike utakapoanza kuharisha!
 
Usiwapotoshe mkuu, itakula kwao chief
 
Nasema itakuwa ni ushujaa na kutanguliza maslahi ya taifa, itakuwa ni njia pekee sahihi na muafaka ya kuonesha kutokubaliana na uchaguzi huu batili uliojaa hila, fitina na nia ovu.
Too late, halafu itawagharimu sana. Na itakuwa salama kwa nchi maana vyama vingine ndiyo hivyo vimekuwa na makando makando yakuwa na mkono wa beberu nyuma yake.
 
Nafikiri mngechukua njia ingine ya kumshauri na kupunguza yale mlokuwa mwazungumza dhidi yake majukwaani nina imani kungekuwa na suluhu.

Ndo maana akaamua kama hali itakuwa hivyo basi hakuna siasa...
Ndio ni maoni yako, lakini ni ya kishoga!.
 
Sasa mtu anafika bei unakuja kulete propaganda huku.watu wameshaakuwa wajesiriamali wanaachia nafasi kwa kisingezio mara hoo nimeenguliwa
 
Sasa hicho ni nini? Constructive ideas anazokubali jiwe ni kusifu na kuabudu tu, hujaunga mkono juhudi no matter lugha gani umetumia utashughulikiwa.

Umesahau figisu walizofanyiwa KKKT baada ya ule waraka wao? Wakaambiwa hawajasajili katiba etc. Ule waraka ulikuwa siyo constructive?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…