Upinzani Tanzania msirudie kosa walilofanya wenzenu wa Namibia

Upinzani Tanzania msirudie kosa walilofanya wenzenu wa Namibia

Namibia ipo kwenye uchaguzi kwa Sasa. Uchaguzi huu ulikuwa ni mgumu Kwa chama tawala Cha SWAPO ila vyama vya upinzani baadala ya kuungana vikaamua kila mmoja kupambana pekee yake mwisho wa siku SWAPO inaongoza kwa matokeo ya Sasa kwa Asilimia 48 ya kura za urais mpaka Sasa. Vyama vya upinzani vina kura Asilimia 52 ila vimegawana baina yao.

Hivyo basi, Kama vyama vya upinzani vitashiriki mwaka 2025, vianze kutengeneza umoja kwa Sasa ili visigawane kura, bila kuungana CCM itazidi kuwaonea na mwisho wa siku mtabaki kulalamika na hakuna atakayewasikiliza.

Zito na Mbowe hawawezi kuungana maana zito kwa mbowe ni msaliti.

Vinginevyo Chadema ichague viongozi wengine wenye sura mpya ,mawazo tofauti na mtizamo tofauti .
Vyama vingine kwa mfano vinaamini Chadema ni chama cha Wachagga. Sasa uta wa aunganisha vipi hapo ?

Ni ama pawe na mabadiliko ndani ya vyama au vibaki kuwa vyama vya upinzani milele.

Hakuna mtanzania anaweza kukubali chama kilichochafuliwa kuwa ni cha kikabilza kiingie madarakani . Usalama na haki ya wote itakua mashakani.


Lakini pia Mbowe akitafakari kubwa anataka kujenga Taifa bora la Kesho lenye demokrasia ya kweli na ya mfano au anataka kuwa kama CCM kutlinda kwa nguvu zote hata kwa kuua misingi ya kidemokrasia .
Tofauti ya CCM na chadema ni ipi maana vyama vyote vinaua demokrasia ya ndani kwa utetezi kuwa ni kulinda chama kisife mikonii mwao . Huu ni upumbavu wa Nchi za kiafrika . Vyama hata vikifa lakini upinzani wa hoja udumu ndilo jambo la msingi .
Kenya hakuna KANU na maisha ya amani yanaendelea . Kenya wangengangana kulinda KANU wangepoteza maisha ya watu wengi na bila shaka leo nchi ingekuwa kwenye vita kubwa.

Mtu anayengangana kulinda chama kingine nyume na demokrasia kiuhalisia mtu huyo ana ukabila,Udini na ubinafsi .
Siku pakikosekana vyama vingine CCM watatawala kwa kuegemea ukabila ili kupata uungwaji mkono .
Siku ukabila ukaisha watatawala kwa kutumia Udini ili kupata uungwaji mkono . Hapo ndipo amani itakapotoweka maana kila mmoja atajijengea kwa misingi itakayombeba kwa wakati huo.
Demokrasia ni muhimu kuanzia ndani ya vyama .
Madudu yanayofanyika ndani ya CCM na figisu na vitisho kwa sasa vimeegemea kwenye Udini sana yote ni kwa sababu ya kuona chama ndicho kila kitu hata Mwenyezi Mungu na sheria za nchi hazifuatwi.

Kwa sasa kuna watu wa dini fulani ni waoga hata kujipambanua kama ni Chadema kwa namna wanavyotushwa kuwa awamu ya dini fulani waiunge mkono hata kama wanakosea .
Chama ni mafalsafa tu kwenye makaratasi jambo la msingi ni kuwa na kiongozi bora anayelinda na kufuata katiba ya nchi .
Bila shaka Tundu Lisu anafaa kurejesha utawala wa sheria unaosimamia haki .
RIP . Ally Kibao.
 
Nadhani Kuna wimbi la mabadiliko linakuja, SA tuliona, Botswana, Msumbiji na Sasa Namibia. Nadhani kwa Tanzania CCM imejikita kwenye vyombo vya Dola kiasi kwamba ni vigumu kukiondoa.
Upo sahihi...ni vyama vya Upinzani Tz kuja na mikakati mipya na yenye tija ili kuing'oa CCM..Hakuna linaloshindikana
 
Inaonekana humu JF kuna watu wa kitengo wengi wamo na mission ya kuwapa Wabongo matumaini hewa ya kuamini ktk uchaguzi ambao haupo!, kama njia ya kuwazubaisha hivi waswiwaze njia za hatari
 
Watanzania ni misukule inayotembea
Hata ukiwachapa kisha badae ukwapa t-shirt na kuwawekea nyimbo za diamond na Simba na yanga watakubali tu

Watanzania ni changamoto pia.
 
Ulichokiandika wala hakiakisi ukweli wa siasa za vyama vingi hapa nchini.
Kama hujui tu, fahamu haya;

1. Huenda 90% ya vyama vya upinzani vilivyopo hapa Tanzania kwa sasa ni matawi ya CCM. Vinaimba na kucheza kila mdundo unaopigwa na CCM. Chama makini cha upinzani kinawezaje kuweka muungano na vyama vingine vya upinzani vya style hiyo?

2. Huenda 90% ya vyama vya upinzani vilivyopo sasa hapa Tanzania haviko hai. Hazina wanachama, viongozi, ofisi, harakati, agenda wala ushawishi. Ni uchafu tu.

Haina shida hata hivyo Asilimia 10 vyaweza kufungana. Naongelea vyama vyenye nguvu vya upinzani amabavyo havizidi vinne.
 
Kiukweli kabisa chama kikipata ushindi chini ya 50% inatakiwa kuwe na runoff election.

Uchaguzi uende ngwe ya pili. Vyama viwili au vitatu vilivyopata kura nyingi vichuane tena mpaka kimoja kipate zaidi ya 50%, hiyo ndiyo iwe mandate.

La sivyo, chama kinachoongoza kwa kura chini ya 50% kiunde serikali ya mseto kwa kushirikiana na vyama vingine, kwa kutafuta mandate ya kupata zaidi ya 50% ya kura.

Kweli kabisa mkuu
 
Ukawa 2015?
Mambo yaliharibika walipomleta the late ENL!

Sasa hivi wasilete mgeni. Wakifanya huo ujinga ndio watapotea moja Kwa moja na hakuna mwananchi atakaye wasikiliza.
 
Namibia ipo kwenye uchaguzi kwa Sasa. Uchaguzi huu ulikuwa ni mgumu Kwa chama tawala Cha SWAPO ila vyama vya upinzani baadala ya kuungana vikaamua kila mmoja kupambana pekee yake mwisho wa siku SWAPO inaongoza kwa matokeo ya Sasa kwa Asilimia 48 ya kura za urais mpaka Sasa. Vyama vya upinzani vina kura Asilimia 52 ila vimegawana baina yao.

Hivyo basi, Kama vyama vya upinzani vitashiriki mwaka 2025, vianze kutengeneza umoja kwa Sasa ili visigawane kura, bila kuungana CCM itazidi kuwaonea na mwisho wa siku mtabaki kulalamika na hakuna atakayewasikiliza.
Tatzo hawa upinzan wa tz kama TLP kile cha mzee wa ubwabwa nk hamna vyama pale ni kupotezana maboya tu. Kingine tamaa na usaliti ndani kwa ndani kwa wapinzani wa hapa kwetu. Hawana mshikamano dhabiti. Mwisho kurubuniwa
 
Ila hizi lawama zenu huwa sizielewi, nani kasema hao wanaoshabikia mpira na muziki hawafuatilii ama kijihusisha na siasa?

Itisha tamasha la muziki halafu itisha mkutano wa siasa uone wapi watu wataenda. Ndio maana CCM kwa kulijua Hilo huwa wanaleta wasanii.
 
Siku ukienda kwenye vituo vya kupigia kura na ukawaona watu wanaojitokeza kupiga kura ni watu wa namna gani utachoka mpaka mkia.

Vijana ambao ndio wenye fikra za kimapinduzi wapo nyuma ya keyboard wanapress battons tu, kwenye kupiga kura hawaonekani.

Kweli kabisa. Wanahitaji kuhamasisha.
 
Ilikuwepo UKAWA ambapo wapinzani wote walishirikiana na CHADEMA. Too bad sahizi walio strong ni ACT na CHADEMA ila wote wenyeviti wake ni kama mapandikizi ya CCM. Hamna upinzani imara, watu wanafocus na Ruzuku tu.
Namibia ipo kwenye uchaguzi kwa Sasa. Uchaguzi huu ulikuwa ni mgumu Kwa chama tawala Cha SWAPO ila vyama vya upinzani baadala ya kuungana vikaamua kila mmoja kupambana pekee yake mwisho wa siku SWAPO inaongoza kwa matokeo ya Sasa kwa Asilimia 48 ya kura za urais mpaka Sasa. Vyama vya upinzani vina kura Asilimia 52 ila vimegawana baina yao.

Hivyo basi, Kama vyama vya upinzani vitashiriki mwaka 2025, vianze kutengeneza umoja kwa Sasa ili visigawane kura, bila kuungana CCM itazidi kuwaonea na mwisho wa siku mtabaki kulalamika na hakuna atakayewasikiliza.
 
Hapa weka vizuri. Upinzani una asilimia 52? Sasa inakuaje SWAPO iongozee? Katiba ya Namibia mshindi apate zaidi ya asilimia 50. Sema kura za wapinzani mmoja mmoja zikiunganishwa zinafika asilimia 52. Yaani kama vile uokote zaa mzee wa Ubwabwa, CDM, ACT, CUF nk...🙏🙏🙏

Mkuu umesoma vizuri?. Hicho unachosema ndicho nilichoandika. Kwamba mpaka Sasa Kwa kura zilizohesabiwa SWAPO Wana Asilimia 48 na vyama vingine vya upinzani Asilimia 52 vikigawanywa baina yao.
 
Bongo hata viungane vyama vyote vya upinzani mshindi hapatikani kwa kura bali kwa kutangazwa. Hivi titaacha lini kuwa na matumaini hewa?

Ila vikiungana na kuachiana base na kuweka mipango ya kulinda kura hata ccm. Wakiiba itafika sehemu watachoka.
 
Huko walikojikita ndo kubaya kwao. Ni bora waache demokrasia ifuate mkondo wake hata wakija kushindwa wataweza kurudi tena. Lakini Kwa sasa wakiondoka hawarudi tena

Kweli kabisa
 
Back
Top Bottom