Uchaguzi 2020 Upinzani wasizuie wabunge wao kwenda kuapa na kuhudhuria Bunge

Uchaguzi 2020 Upinzani wasizuie wabunge wao kwenda kuapa na kuhudhuria Bunge

Kuwapeleka maanake umekubali UHUNI uliyofanya lazima wa protest. Hao wabinge wa Upinzani hawakupatikana kwa kura bali walichofanya CCM ni gelesha kuhalalisha WIZI waliofanya. Wameona aibu kuwa 100% Ushindani kama ule mpk mzee baba alipiga magoti ndo fake zile kama vile. Watu wanavinyongo japo wako kimya
Wenye vinyongo ni wanyama na kuku wa cdm, na sio watu huru wa JMT. Imeisha hiyoooooooooooo
 
Zitto kafaidi ubunge kwa miaka 15 kwa kutumia tume hiihii, leo kwakuwa hayumo basi uchaguzi ni batili na waliochaguliwa wasiende bungeni, jamani tuache usanii. Ninamuomba Mh. Spika ajae awalinde hawa mbuzi wa kafara kwenye ubunge wao ili nao wafaidi matunda ya Tume, jitihada zao na rasilimali zao walizopoteza wakati wa kampeni.
Kumbe kulitumimikia bunge ni kufaidi?
 
Wameshahudhuria tayari wa CUF , Chadema na ACT wazalendo
 
Yaani vyama vya upinzani vifanye jitiada zoote za kuimarisha demokrasia alafu siku ya mwisho chama tawala kinakuja kubaka demokrasia kwa kutengeneza matokea ya chaguzi kinacho yajua chenyewe, tena kwa mitutu ya bunduki na
toa ushihidi. Mimi nina ushahidi wa mambo yafuatayo ambao ninaweza kuudhibisha nikitakiwa kudhibitisha:

1. Siku ya kupiga kura nilikuta watu wachache sana kituoni, nilitumia dk 5 tu kupiga kura pamoja kwamba nilikwenda saa4 asubuhi. Hii ina maana kuwa watu hawakwenda kupiga kura.
2. Niliwaona wajumbe wa CCM wakipita nyumba kwa nyumba kuwahimiza wanachama wao kwenda kujiandikisha daftari la kupiga kura na kwenda kupiga kura siku ya kupiga kura, na hii ilifanyika nchi nzima.

3. Siku majina ya wapiga kura yalipobandikwa niliwaona wajumbe wakihakiki majina ya wanachama wao kama yapo kwenye orodha na kuwarahisishia kufahamu kituo watakacho kwenda kupigia kura.

Vitu kama hivi sikuviona kwa wapinzani, inawezekana kura ziliibwa lakini kama CCM wangekuwa na njia rahisi hivyo ya kupata kura basi wasingezunguuka nchi nzima kupiga kampeni, wazingetumia wasanii wengi kupiga kampeni, Rais Magufuli asingelezimika kupiga magoti kuomba kura na wajumbe wao wasinge hangaika kupita nyumba kwa nyumba kuomba kura.

Lazima tuambiane ukweli kama tunataka kupona. Viongozi wa upinzani ni wapiga dili, wangechaguliwa wao kwenye ubunge kelele zisingekuwa nyingi sana.
 
Mbona kama mnawa lazimisha si mlitaka kuwa peke yenu lakini
Unafahamu hao wabunge walitumia hela ngapi kwenye kampeni? chama kitawarudishia? je, wasipohudhuria vikao katiba itabadilishwa?
 
Nakubaliana asilimia 100 kwamba waende bungeni ni haki yao
Wabunge 19 ni wengi saana katika iboresha
Nakumbuka bunge la 2011
Walikua wanasaidia kwa kiwango kikubwa alikua mnyika, mdee, zito, wenje na wengine
Walikua hawafiki 10 lakini bunge lilikua la moto!
Waende na wachangie hoja..
Mabadiliko yoyote yale hayaletwi na viongozi pekee. Sisi wananchi wa kawaida tuna nafasi pia. Tujiulize (ukiwemo wewe mtoa hoja), tumefanya nini katika kuchochea mabadiliko zaidi ya kupiga kura na kulalamikia viongozi wa upinzani? Hata hivyo, napendekeza wabunge hawa wa upinzani waende bungeni wakale hela hizo na ikiwezekana wasichangie chochote ili wasionekane wakwamishaji wa maendeleo.
 
Kwani lazima wawe wa CHADEMA?
si wachukue vyama vingine??

atakayeapishwa tunamvua uanachama, anapoteza sifa ya kuwa mbunge, tunasimamia misimamo yetu
 
Unafurahia mateso wanayofanyiwa wapinzani hapa nchini?
Hii nchi tuliyo wachiwa na baba wa taifa likiwa moja lililoshikamana leo hii mnaligawa vipande vipande kisa siasa!
Baba wa Taifa ndiye chanzo cha tatizo kwa kutuachia katiba ya aina hii, usimtaje kabisa unapoongelea masuala ya demokrasia nchini.
 
Kwani lazima wawe wa CHADEMA?
si wachukue vyama vingine??

atakayeapishwa tunamvua uanachama, anapoteza sifa ya kuwa mbunge, tunasimamia misimamo yetu
Unasahau hata Zitto alipofukuzwa na chadema aliendelea na ubunge wake hadi mwisho? atakuwa mbunge wa mahakama.

Lazima wabunge hao 19 watoke chadema kwa mujibu wa katiba na kanuni za uchaguzi. Chama kilichopata kura kwa kiasi fulani.
 
toa ushihidi. Mimi nina ushahidi wa mambo yafuatayo ambao ninaweza kuudhibisha nikitakiwa kudhibitisha:

1. Siku ya kupiga kura nilikuta watu wachache sana kituoni, nilitumia dk 5 tu kupiga kura pamoja kwamba nilikwenda saa4 asubuhi. Hii ina maana kuwa watu hawakwenda kupiga kura.
2. Niliwaona wajumbe wa CCM wakipita nyumba kwa nyumba kuwahimiza wanachama wao kwenda kujiandikisha daftari la kupiga kura na kwenda kupiga kura siku ya kupiga kura, na hii ilifanyika nchi nzima.

3. Siku majina ya wapiga kura yalipobandikwa niliwaona wajumbe wakihakiki majina ya wanachama wao kama yapo kwenye orodha na kuwarahisishia kufahamu kituo watakacho kwenda kupigia kura.

Vitu kama hivi sikuviona kwa wapinzani, inawezekana kura ziliibwa lakini kama CCM wangekuwa na njia rahisi hivyo ya kupata kura basi wasingezunguuka nchi nzima kupiga kampeni, wazingetumia wasanii wengi kupiga kampeni, Rais Magufuli asingelezimika kupiga magoti kuomba kura na wajumbe wao wasinge hangaika kupita nyumba kwa nyumba kuomba kura.

Lazima tuambiane ukweli kama tunataka kupona. Viongozi wa upinzani ni wapiga dili, wangechaguliwa wao kwenye ubunge kelele zisingekuwa nyingi sana.
vituo hewa kibao kila kona ya nchi, kula feki kila mahali, kula tulizo piga yalikuwa maigizo ma sarakasi tuu
 
Wacha wabunge wa wapinzani washiriki vikao vya bunge lijalo, na ikiwezekana wapeleke majina ya watu wa ubunge wa viti maalumu. Maana kuhudhuria au kutokuhudhuria hakusaidii kuimarisha demokrasia wala vyama vya upinzani wala kubadilisha siasa za Tanzania.

CUF walifanya hivyo mara nyingi bila kuzaa matunda yoyote. Wabunge wa upinzani wamekuwa wakisusia vikao vya bunge mara kadhaa lakini sikuona walichofanikisha sanasana kujinufaisha wao wenyewe kiuchumi.

Itakuwa ni kuwanyima fursa wabunge wa upinzani waliochaguliwa kama tutasema wasihuhudhurie pia bunge. Hata wakisusia hawana uzito wowote wa kubalidisha mambo zaidi ya kuwakosesha fursa yao ya kiuchumi, kisiana na kijamii.

Vyama vijipange upya kwa 2025 kwa kufanya yafuatayo:
1. Kueneza vyama vyao hadi vitongojini.

2. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanajiandikisha kwa wingi kwenye daftari la kupiga kura wakati utakapowadia.

3. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanakwenda kupiga kura wote siku ya kupiga kura.

4. Wahakikishe kuwa wakati wa kujaza fomu za kugombea kuna watu maalumu wanaohakiki ujazaji na urudishwaji wa fomu hizo kwa usahihi.

5. Hakikisheni kuwa kuanzia sasa na kabla ya 2025 mnapata muafaka kuhusu Tume Huru ya uchaguzi na wasimamizi wake. Kama mkishindwa kuipata Tume huru ya uchaguzi tafadhali sana msiwasumbue na kuwarubuni wananchi kwa kuwapa matumaini ya uongo. Tunafahamu kuwa wanasiasa wanawatumia wananchi kama mtaji wao wa kuichumi wa kuwafikisha kwenye posho, mshahara, magari makubwa na kiinua mgongo bungeni na wapenzi wao wa viti maalum na kujipatia ruzuku. Na hii ndiyo maana walikuwa wakishiriki chaguzi za vyama vingi bila kujali Tume imekaakaaje.

Wanasema Tume ni mbaya kila siku lakini Tume hiyohiyo ilikuwa ikiwatangaza kushinda Ubunge. Naishukuru sana Tume safari hii kwa kuacha kuwatangaza hawa jamaa ili waufahamu ukubwa wa shughuli.

Tuwaache waliotangazwa kushinda nao wakafaidi kama vile nyie mlivyofaidi kwa miaka 10 kwa kutumia Tume ya aina hiihii.

Nitawashangaa wale walioshinda kama watasikiliza porojo za kuwaambia wasiende kupata mpunga bungeni, hata 2015 malalamiko yalikuwa hayohayo kwa Tume lakini walikwenda bunge kilafi pamoja na malalamiko ya Lowassa kuibiwa kura.

Kwakuwa wao safari hii wametemwa basi wanataka walioshinda wasiende bungeni. Huu ni utoto.

Hakuna haja ya kushiriki bunge ambalo wamesgasema uchaguzi wake uligubikwa na ukiukwaji wa kanuni na sheria za uchaguzi. Kama wameshasema huo uchaguzi haukuwa huru na wakatoa witu uchaguzi urudiwe kwanini sasa waingie huko bungeni tena
 
Kama wangechaguliwa Mbowe, Sugu na Msigwa bado wangekatazwa kwenda bungeni?

Wangekatazwa kwa wizi ule wa kule kupatikana mtaani zikiwa kwenye mabegi hata angeshinda nani huo haukuwa uchaguzi tuseme ukweli bila kumung’unya maneno
 
Unasahau hata Zitto alipofukuzwa na chadema aliendelea na ubunge wake hadi mwisho? atakuwa mbunge wa mahakama.

Lazima wabunge hao 19 watoke chadema kwa mujibu wa katiba na kanuni za uchaguzi. Chama kilichopata kura kwa kiasi fulani.
Good ila anapoteza sifa ya kuongoza Kamati za bunge,

unajua kwanini CCM wanang'ang'ania wabunge wa upinzani??
 
Baba wa Taifa ndiye chanzo cha tatizo kwa kutuachia katiba ya aina hii, usimtaje kabisa unapoongelea masuala ya demokrasia nchini.
Tatizo lako ni kutoangalia na kuelewa nini kimeandikwa
 
Zitto kafaidi ubunge kwa miaka 15 kwa kutumia tume hiihii, leo kwakuwa hayumo basi uchaguzi ni batili na waliochaguliwa wasiende bungeni, jamani tuache usanii. Ninamuomba Mh. Spika ajae awalinde hawa mbuzi wa kafara kwenye ubunge wao ili nao wafaidi matunda ya Tume, jitihada zao na rasilimali zao walizopoteza wakati wa kampeni.

Hiyo hoja haina mantiki yoyote ile awamu hii serikali imeingilia moja kwa moja maamuzi ya tume ikiwa ni tangu kuchapishwa kwa ballot papers hadi sasa inaonekana ballot paper zilichapishwa kienyeji sana ndo maana zilikuwa zimezagaa mitaani kwenye mabegi haijulikani kampuni gani ilichapisha hata zile kula zilizopatikana polisi hawajatwambia upelezi wao umeonesha zilizoka wapi zile. Hii ni kasoro kubwa sana katika uchaguzi huu ambayo haijawahi tokea chaguzi za nyumba.
 
Wacha wabunge wa wapinzani washiriki vikao vya bunge lijalo, na ikiwezekana wapeleke majina ya watu wa ubunge wa viti maalumu. Maana kuhudhuria au kutokuhudhuria hakusaidii kuimarisha demokrasia wala vyama vya upinzani wala kubadilisha siasa za Tanzania.

CUF walifanya hivyo mara nyingi bila kuzaa matunda yoyote. Wabunge wa upinzani wamekuwa wakisusia vikao vya bunge mara kadhaa lakini sikuona walichofanikisha sanasana kujinufaisha wao wenyewe kiuchumi.

Itakuwa ni kuwanyima fursa wabunge wa upinzani waliochaguliwa kama tutasema wasihuhudhurie pia bunge. Hata wakisusia hawana uzito wowote wa kubalidisha mambo zaidi ya kuwakosesha fursa yao ya kiuchumi, kisiana na kijamii.

Vyama vijipange upya kwa 2025 kwa kufanya yafuatayo:
1. Kueneza vyama vyao hadi vitongojini.

2. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanajiandikisha kwa wingi kwenye daftari la kupiga kura wakati utakapowadia.

3. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanakwenda kupiga kura wote siku ya kupiga kura.

4. Wahakikishe kuwa wakati wa kujaza fomu za kugombea kuna watu maalumu wanaohakiki ujazaji na urudishwaji wa fomu hizo kwa usahihi.

5. Hakikisheni kuwa kuanzia sasa na kabla ya 2025 mnapata muafaka kuhusu Tume Huru ya uchaguzi na wasimamizi wake. Kama mkishindwa kuipata Tume huru ya uchaguzi tafadhali sana msiwasumbue na kuwarubuni wananchi kwa kuwapa matumaini ya uongo. Tunafahamu kuwa wanasiasa wanawatumia wananchi kama mtaji wao wa kuichumi wa kuwafikisha kwenye posho, mshahara, magari makubwa na kiinua mgongo bungeni na wapenzi wao wa viti maalum na kujipatia ruzuku. Na hii ndiyo maana walikuwa wakishiriki chaguzi za vyama vingi bila kujali Tume imekaakaaje.

Wanasema Tume ni mbaya kila siku lakini Tume hiyohiyo ilikuwa ikiwatangaza kushinda Ubunge. Naishukuru sana Tume safari hii kwa kuacha kuwatangaza hawa jamaa ili waufahamu ukubwa wa shughuli.

Tuwaache waliotangazwa kushinda nao wakafaidi kama vile nyie mlivyofaidi kwa miaka 10 kwa kutumia Tume ya aina hiihii.

Nitawashangaa wale walioshinda kama watasikiliza porojo za kuwaambia wasiende kupata mpunga bungeni, hata 2015 malalamiko yalikuwa hayohayo kwa Tume lakini walikwenda bunge kilafi pamoja na malalamiko ya Lowassa kuibiwa kura.

Kwakuwa wao safari hii wametemwa basi wanataka walioshinda wasiende bungeni. Huu ni utoto.
Ningekuelewa kama ungesema watafute pesa za kuwanunulia mawakala AK47 na Grenade za kujilinda wakati wanasimamia zoezi la kuhesabu kura vituoni.
 
Back
Top Bottom