Uchaguzi 2020 Upinzani wasizuie wabunge wao kwenda kuapa na kuhudhuria Bunge

Uchaguzi 2020 Upinzani wasizuie wabunge wao kwenda kuapa na kuhudhuria Bunge

"Wacha wabunge wa wapinzani washiriki vikao vya bunge lijalo, na ikiwezekana wapeleke majina ya watu wa ubunge wa viti maalumu. Maana kuhudhuria au kutokuhudhuria hakusaidii kuimarisha demokrasia wala vyama vya upinzani wala kubadilisha siasa za Tanzania...."
Kama ndivyo hivyo kwamba kuhudhuria na kutohudhuria hakusaidii, basi waache wachague kutohudhuria. Hoja yako ya Chadema kuwaruhusu wabunge wake kuhudhuria umeihitimisha vibaya. Hata hivyo majina ya viti maalum yanatokana na kura za wabunge katika uchaguzi ambao Chadema walishasema uchaguzi haukuwa wa haki, kwa hiyo wakiteua wabunge wa viti maalum watakuwa wamekubali matokeo ya uchaguzi waliousema kuwa haukuwa wa haki.
 
Watanzania tunapaswa kujiuliza, hivi demokrasia ya vyama vingi ni kwa ajili ya vyama vya siasa au kwa ajili ya Watanzania? Wakati mwingine ukisoma maoni ya Mtanzania utafikiri vyama vya upinzani vinapigania mambo yao tu.
 
wabunge waupinzani hawatakiwi sasa waende wakafanye nini,hizo nafasi jazazeni ,au ccm mmeisha,wapo wale wajumbe kibao wasombeni wajalizie hizo nafasi ili mutimize lengo la kuwepo kijani na manjano tupu humo bungeni,nawashangaa mnahangaika.
 
Ningekuelewa kama ungesema watafute pesa za kuwanunulia mawakala AK47 na Grenade za kujilinda wakati wanasimamia zoezi la kuhesabu kura vituoni.
Wakala ndo nini bhana we, kama mbunge mwenye mshahara amekubali kuunga juhudi sembuse wakala!!!
 
wabunge waupinzani hawatakiwi sasa waende wakafanye nini,hizo nafasi jazazeni ,au ccm mmeisha,wapo wale wajumbe kibao wasombeni wajalizie hizo nafasi ili mutimize lengo la kuwepo kijani na manjano tupu humo bungeni,nawashangaa mnahangaika.
Unasema hayo kwakuwa sio mbowe, sugu, zitto au msigwa waliotangazwa, wale jamaa wasingekubali pesa ya bunge iwapite, Hii hoja ya tume tume tume mbona ni ya muda mrefu, sio ya leo. Ilishampata mgombea Mrema, Lipumba, Slaa, Maalim, Lowassa, Mghwila, lakini mara zote hizo wabunge wa chadema na ACT waliingia bungeni, kwanini kwa Lissu wabunge wasiingie bungeni?
 
Kama ndivyo hivyo kwamba kuhudhuria na kutohudhuria hakusaidii, basi waache wachague kutohudhuria. Hoja yako ya Chadema kuwaruhusu wabunge wake kuhudhuria umeihitimisha vibaya. Hata hivyo majina ya viti maalum yanatokana na kura za wabunge katika uchaguzi ambao Chadema walishasema uchaguzi haukuwa wa haki, kwa hiyo wakiteua wabunge wa viti maalum watakuwa wamekubali matokeo ya uchaguzi waliousema kuwa haukuwa wa haki.
Ninasema wabunge waende bungeni kwasababu zifuatazo:
1. Chaguzi zote za vyama vingi wapinzani walikuwa na malalamiko lakini hawajawahi kuacha kuingia bungeni wale waliobahatika kutangazwa kushinda majimbo na wale wa viti maalum.

2. Wabunge watapata kipato cha kuinua maisha yao na wapendwa wao kama watashiriki vikao

3. Vyama vya upinzani vitapata first hand information kutoka bungeni kupitia hawa wabunge watakaoshiriki vikao

4. Wabunge hao watakuwa na nguvu za kiuchumi 2025 kumudu kujiingiza kwenye kinyanganyilo

5. Chama kitapata ruzuki ya kuendeshea ofisi za chama

6. Wabunge hao wataweza kurejesha pesa walizokopa kuendeshea kampeni za uchaguzi

7. Wananchi waliowachagua wanastahili kuheshimiwa uwamuzi wao wa kuwakilishwa na huyo mbunge.
 
Wacha wabunge wa wapinzani washiriki vikao vya bunge lijalo, na ikiwezekana wapeleke majina ya watu wa ubunge wa viti maalumu. Maana kuhudhuria au kutokuhudhuria hakusaidii kuimarisha demokrasia wala vyama vya upinzani wala kubadilisha siasa za Tanzania.

CUF walifanya hivyo mara nyingi bila kuzaa matunda yoyote. Wabunge wa upinzani wamekuwa wakisusia vikao vya bunge mara kadhaa lakini sikuona walichofanikisha sanasana kujinufaisha wao wenyewe kiuchumi.

Itakuwa ni kuwanyima fursa wabunge wa upinzani waliochaguliwa kama tutasema wasihuhudhurie pia bunge. Hata wakisusia hawana uzito wowote wa kubalidisha mambo zaidi ya kuwakosesha fursa yao ya kiuchumi, kisiana na kijamii.

Vyama vijipange upya kwa 2025 kwa kufanya yafuatayo:
1. Kueneza vyama vyao hadi vitongojini.

2. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanajiandikisha kwa wingi kwenye daftari la kupiga kura wakati utakapowadia.

3. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanakwenda kupiga kura wote siku ya kupiga kura.

4. Wahakikishe kuwa wakati wa kujaza fomu za kugombea kuna watu maalumu wanaohakiki ujazaji na urudishwaji wa fomu hizo kwa usahihi.

5. Hakikisheni kuwa kuanzia sasa na kabla ya 2025 mnapata muafaka kuhusu Tume Huru ya uchaguzi na wasimamizi wake. Kama mkishindwa kuipata Tume huru ya uchaguzi tafadhali sana msiwasumbue na kuwarubuni wananchi kwa kuwapa matumaini ya uongo. Tunafahamu kuwa wanasiasa wanawatumia wananchi kama mtaji wao wa kuichumi wa kuwafikisha kwenye posho, mshahara, magari makubwa na kiinua mgongo bungeni na wapenzi wao wa viti maalum na kujipatia ruzuku. Na hii ndiyo maana walikuwa wakishiriki chaguzi za vyama vingi bila kujali Tume imekaakaaje.

Wanasema Tume ni mbaya kila siku lakini Tume hiyohiyo ilikuwa ikiwatangaza kushinda Ubunge. Naishukuru sana Tume safari hii kwa kuacha kuwatangaza hawa jamaa ili waufahamu ukubwa wa shughuli.

Tuwaache waliotangazwa kushinda nao wakafaidi kama vile nyie mlivyofaidi kwa miaka 10 kwa kutumia Tume ya aina hiihii.

Nitawashangaa wale walioshinda kama watasikiliza porojo za kuwaambia wasiende kupata mpunga bungeni, hata 2015 malalamiko yalikuwa hayohayo kwa Tume lakini walikwenda bunge kilafi pamoja na malalamiko ya Lowassa kuibiwa kura.

Kwakuwa wao safari hii wametemwa basi wanataka walioshinda wasiende bungeni. Huu ni utoto.
Maoni mengine yanafurahisha kama yajayo. Unaambiwa anayekulipa mshahara posho gari nyumba ndiye umsikilize anataka nini, pia hakuna mikutano ya vyama visivyokuwa na serikali alafu wewe unaeneza ukuaji wa vyama!!!!!!!!!!!!!! 🙄🙄
 
Watanzania tunapaswa kujiuliza, hivi demokrasia ya vyama vingi ni kwa ajili ya vyama vya siasa au kwa ajili ya Watanzania? Wakati mwingine ukisoma maoni ya Mtanzania utafikiri vyama vya upinzani vinapigania mambo yao tu.
Uko sahihi mkuu hapo. Ukiangalia sana wanasiasa huwa wanawatumia watanzania kujipatia pesa ila hawana nia ya dhati. Ndio maana ni rahisi kusikia mbunge anakwenda kuunga juhudi. Ndiyo maana utakuta kiongozi wa siasa anakamatwa au kupigwa lakini hakuna wananchi wanaochukua hatua. Kiongozi atataunwa mpaka anakwisha lakini wananchi hawachui hatua wanaendelea na mishe zao za maisha kama kawaida. Kama kweli wanasiasa wangekuwa wanayasema yale ya wananchi ya ukweli hasahasa wasingekuwa na haja ya kuwaambia watu kuwa nitawaingiza watu barabarani. Hao watu wangejiingiza barabarani wao wenyewe kama hiyo kero ingekuwa kweli inawahusu wao.

Wanasiasa wanawatumia wananchi kama farasi kuwapeleka bungeni wakapate kibarua kinono tu basi, ndio maana unawakuta akina Mbowe, Sugu, Msigwa, Zitto, Prof Jay, Mdee, Mnyika nk walikuwa wakiingia bungeni hata kama wanadai tume sio huru kwa miaka yote hii, na wengine walikuwa wakihama vyama bila kujali wale waliowapigia kura watajisikiaje.
 
Maoni mengine yanafurahisha kama yajayo. Unaambiwa anayekulipa mshahara posho gari nyumba ndiye umsikilize anataka nini, pia hakuna mikutano ya vyama visivyokuwa na serikali alafu wewe unaeneza ukuaji wa vyama!!!!!!!!!!!!!! 🙄🙄
Kwa miaka 5 vyama vya siasa vilipigwa marufuku kufanya siasa, kwahiyo mimi nilidhani mwaka huu na kipindi hiki cha kuruhusiwa kwa siasa wapinzani wangefanyakazi za kuvijenga vyama vyao kwa uchaguzi wa 2025 zaidi kuliko kushinda uchaguzi wa 2020. Nilitaraji wapinzani wangefahamu kuwa baada ya uchaguzi kupita siasa zitasimama tena hadi 2025, hivyo wangefanya kazi za kufungua matawi hadi kwenye vitongoji badala ya kujikita kwenye kuomba kura kwa watu ambao hawana uhakika kama walijiandikisha kwenye daftari la wapiga kura na watapiga kura.

Inamaana kuwa kama Lissu angeshinda uchaguzi hii miradi ya reli, bwawa la umeme, kuhamia dodoma, meli, ndege, nk yote angeachana nayo kabisaaa. Huu ungekuwa upuuzi kwetu kwa kiwango cha lami. Maana sijawahikumsikia Lissu kwenye kampeni zake akisema atamalizia miradi hii ambayo tayari imeshatafuna hela zetu nyingi. Mimi hata kama simpendi JPM lakini napenda bwawa, dodoma iwe mji mkuu, reli ya kisasa, elimu bure, ndege, tembo wetu wasiuawe ovyo hata ikibidi kwa kuwaua hadharani wanaoua tembo. Sasa cdm walikuwa hawasemi kuhusu mambo hayo hata kidogo kwenye kampeni zao zaidi ya kulalamikia kila jambo hata yale mazuri.
 
Wacha wabunge wa wapinzani washiriki vikao vya bunge lijalo, na ikiwezekana wapeleke majina ya watu wa ubunge wa viti maalumu. Maana kuhudhuria au kutokuhudhuria hakusaidii kuimarisha demokrasia wala vyama vya upinzani wala kubadilisha siasa za Tanzania.

CUF walifanya hivyo mara nyingi bila kuzaa matunda yoyote. Wabunge wa upinzani wamekuwa wakisusia vikao vya bunge mara kadhaa lakini sikuona walichofanikisha sanasana kujinufaisha wao wenyewe kiuchumi.

Itakuwa ni kuwanyima fursa wabunge wa upinzani waliochaguliwa kama tutasema wasihuhudhurie pia bunge. Hata wakisusia hawana uzito wowote wa kubalidisha mambo zaidi ya kuwakosesha fursa yao ya kiuchumi, kisiana na kijamii.

Vyama vijipange upya kwa 2025 kwa kufanya yafuatayo:
1. Kueneza vyama vyao hadi vitongojini.

2. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanajiandikisha kwa wingi kwenye daftari la kupiga kura wakati utakapowadia.

3. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanakwenda kupiga kura wote siku ya kupiga kura.

4. Wahakikishe kuwa wakati wa kujaza fomu za kugombea kuna watu maalumu wanaohakiki ujazaji na urudishwaji wa fomu hizo kwa usahihi.

5. Hakikisheni kuwa kuanzia sasa na kabla ya 2025 mnapata muafaka kuhusu Tume Huru ya uchaguzi na wasimamizi wake. Kama mkishindwa kuipata Tume huru ya uchaguzi tafadhali sana msiwasumbue na kuwarubuni wananchi kwa kuwapa matumaini ya uongo. Tunafahamu kuwa wanasiasa wanawatumia wananchi kama mtaji wao wa kuichumi wa kuwafikisha kwenye posho, mshahara, magari makubwa na kiinua mgongo bungeni na wapenzi wao wa viti maalum na kujipatia ruzuku. Na hii ndiyo maana walikuwa wakishiriki chaguzi za vyama vingi bila kujali Tume imekaakaaje.

Wanasema Tume ni mbaya kila siku lakini Tume hiyohiyo ilikuwa ikiwatangaza kushinda Ubunge. Naishukuru sana Tume safari hii kwa kuacha kuwatangaza hawa jamaa ili waufahamu ukubwa wa shughuli.

Tuwaache waliotangazwa kushinda nao wakafaidi kama vile nyie mlivyofaidi kwa miaka 10 kwa kutumia Tume ya aina hiihii.

Nitawashangaa wale walioshinda kama watasikiliza porojo za kuwaambia wasiende kupata mpunga bungeni, hata 2015 malalamiko yalikuwa hayohayo kwa Tume lakini walikwenda bunge kilafi pamoja na malalamiko ya Lowassa kuibiwa kura.

Kwakuwa wao safari hii wametemwa basi wanataka walioshinda wasiende bungeni. Huu ni utoto.
Wengine wameshaapishwa huku

IMG-20201109-WA0024.jpg
 
Hao ni watu waoga, shida yao sio diwani huyo, wafanye utafiti wa kina. Wameondoa uhai wa wasiokuwa na hatia.
Ni kweli kama lile jeshi lilikwenda kuuwa watu 13 kule pemba pamoja na kurmjeruhi mama wa miaka 75 kwa mabomu waliyorusha nyumbani kwake
 
Kwa miaka 5 vyama vya siasa vilipigwa marufuku kufanya siasa, kwahiyo mimi nilidhani mwaka huu na kipindi hiki cha kuruhusiwa kwa siasa wapinzani wangefanyakazi za kuvijenga vyama vyao kwa uchaguzi wa 2025 zaidi kuliko kushinda uchaguzi wa 2020. Nilitaraji wapinzani wangefahamu kuwa baada ya uchaguzi kupita siasa zitasimama tena hadi 2025, hivyo wangefanya kazi za kufungua matawi hadi kwenye vitongoji badala ya kujikita kwenye kuomba kura kwa watu ambao hawana uhakika kama walijiandikisha kwenye daftari la wapiga kura na watapiga kura.

Inamaana kuwa kama Lissu angeshinda uchaguzi hii miradi ya reli, bwawa la umeme, kuhamia dodoma, meli, ndege, nk yote angeachana nayo kabisaaa. Huu ungekuwa upuuzi kwetu kwa kiwango cha lami. Maana sijawahikumsikia Lissu kwenye kampeni zake akisema atamalizia miradi hii ambayo tayari imeshatafuna hela zetu nyingi. Mimi hata kama simpendi JPM lakini napenda bwawa, dodoma iwe mji mkuu, reli ya kisasa, elimu bure, ndege, tembo wetu wasiuawe ovyo hata ikibidi kwa kuwaua hadharani wanaoua tembo. Sasa cdm walikuwa hawasemi kuhusu mambo hayo hata kidogo kwenye kampeni zao zaidi ya kulalamikia kila jambo hata yale mazuri.
Very interesting to go through contradictory phrases.
Wangapi walizuiwa kufanya kampeini japo kilikuwa kipindi cha kampeini?? Ukiona sheria rasmi ya kuruhusu vyama kufanya siasa inapuuzwa mchana kweupe na vyombo vyetu vya dora vinasimamia hilo, usitegemee mbingu ishuke au ardhi iwe mbingu. Mwenye masikio na asikie pia mwenye macho na aone.
Nikutakie siku njema kabisa.
 
Very interesting to go through contradictory phrases.
Wangapi walizuiwa kufanya kampeini japo kilikuwa kipindi cha kampeini?? Ukiona sheria rasmi ya kuruhusu vyama kufanya siasa inapuuzwa mchana kweupe na vyombo vyetu vya dora vinasimamia hilo, usitegemee mbingu ishuke au ardhi iwe mbingu. Mwenye masikio na asikie pia mwenye macho na aone.
Nikutakie siku njema kabisa.
Baada ya Trump kudai uchaguzi haukuwa huru na haki, unadhani wapinzani Afrika watasema nini? Kama Tume ya uchaguzi ya Marekani inalalamikiwa, je, Tume za uchaguzi za Afrika zitanusurikaje na lawama?. Viongozi wa Afrika wamepata pa kuficha nyuso zao zenye masizi.

Marehemu Christopher Mtikila alikuwa anajuwa namna ya kujenga hoja zilizowagusa wananchi moja kwa moja kiasi cha kuwafanya waingie barabarani wao wenyewe bila kuingizwa barabarani na kiongozi kama walivyotaka iwe hawa akina pangu pakavu.

Ninachosema mimi ni kwamba inawezekana kweli wapinzani wetu wanayo hoja za uchaguzi, lakini je, walikuwa na takwimu za watu wao wangapi walijiandikisha kwenye daftari za wapiga kura, na wangapi walienda kuwapigia kura? CCM wenzao angalau walikuwa na takwimu hizo kuhusu wanachama wao.
 
Baada ya Trump kudai uchaguzi haukuwa huru na haki, unadhani wapinzani Afrika watasema nini? Kama Tume ya uchaguzi ya Marekani inalalamikiwa, je, Tume za uchaguzi za Afrika zitanusurikaje na lawama?. Viongozi wa Afrika wamepata pa kuficha nyuso zao zenye masizi.

Marehemu Christopher Mtikila alikuwa anajuwa namna ya kujenga hoja zilizowagusa wananchi moja kwa moja kiasi cha kuwafanya waingie barabarani wao wenyewe bila kuingizwa barabarani na kiongozi kama walivyotaka iwe hawa akina pangu pakavu.

Ninachosema mimi ni kwamba inawezekana kweli wapinzani wetu wanayo hoja za uchaguzi, lakini je, walikuwa na takwimu za watu wao wangapi walijiandikisha kwenye daftari za wapiga kura, na wangapi walienda kuwapigia kura? CCM wenzao angalau walikuwa na takwimu hizo kuhusu wanachama wao.
Ukishavamia talling centers and head and zonal / regional offices za vyama ukanyang`anya computers and other critical docs what do you expect?????
Malengo ya watawala wacha yatimizwe na wote tuseme AMINA.
Karibu lunch mkuu
 
Kama viongozi wa upinzani wanatoroka nchi na wengine wamejifisha ubalozini, je, ni wananchi wangapi wanaweza kufanya hivyo? Wanawadanganya wananchi walalahoi eti tutaingia barabarani, mbona wao wamesepa?
Soma historia viongozi wengi wameishi uamishoni mfano Ayatollah khemein kiungoz wa Iran alishaishi uamishoni, rais Emerson nangagwa wa Zimbabwe alishaishi uamishoni kumkimbia Mugabe,

Kipindi Cha miaka ya 80's viongozi wengi wa nchi za kiafrika walifanyia harakati zao wakiwa Tanzania, means walikua wanaishi uamishoni Tanzania jifunze kusoma historia
 
Soma historia viongozi wengi wameishi uamishoni mfano Ayatollah khemein kiungoz wa Iran alishaishi uamishoni, rais Emerson nangagwa wa Zimbabwe alishaishi uamishoni kumkimbia Mugabe,

Kipindi Cha miaka ya 80's viongozi wengi wa nchi za kiafrika walifanyia harakati zao wakiwa Tanzania, means walikua wanaishi uamishoni Tanzania jifunze kusoma historia
Nadhani Tanzania ni tofauti kidogo, Osca Kambona na Abdulraham Babu walijaribu wakaambulia patupu. Ingawa hata Gadaff na Saadam hawakuamini kilichowatokea.
 
Wacha wabunge wa wapinzani washiriki vikao vya bunge lijalo, na ikiwezekana wapeleke majina ya watu wa ubunge wa viti maalumu. Maana kuhudhuria au kutokuhudhuria hakusaidii kuimarisha demokrasia wala vyama vya upinzani wala kubadilisha siasa za Tanzania.

CUF walifanya hivyo mara nyingi bila kuzaa matunda yoyote. Wabunge wa upinzani wamekuwa wakisusia vikao vya bunge mara kadhaa lakini sikuona walichofanikisha sanasana kujinufaisha wao wenyewe kiuchumi.

Itakuwa ni kuwanyima fursa wabunge wa upinzani waliochaguliwa kama tutasema wasihuhudhurie pia bunge. Hata wakisusia hawana uzito wowote wa kubalidisha mambo zaidi ya kuwakosesha fursa yao ya kiuchumi, kisiana na kijamii.

Vyama vijipange upya kwa 2025 kwa kufanya yafuatayo:
1. Kueneza vyama vyao hadi vitongojini.

2. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanajiandikisha kwa wingi kwenye daftari la kupiga kura wakati utakapowadia.

3. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanakwenda kupiga kura wote siku ya kupiga kura.

4. Wahakikishe kuwa wakati wa kujaza fomu za kugombea kuna watu maalumu wanaohakiki ujazaji na urudishwaji wa fomu hizo kwa usahihi.

5. Hakikisheni kuwa kuanzia sasa na kabla ya 2025 mnapata muafaka kuhusu Tume Huru ya uchaguzi na wasimamizi wake. Kama mkishindwa kuipata Tume huru ya uchaguzi tafadhali sana msiwasumbue na kuwarubuni wananchi kwa kuwapa matumaini ya uongo. Tunafahamu kuwa wanasiasa wanawatumia wananchi kama mtaji wao wa kuichumi wa kuwafikisha kwenye posho, mshahara, magari makubwa na kiinua mgongo bungeni na wapenzi wao wa viti maalum na kujipatia ruzuku. Na hii ndiyo maana walikuwa wakishiriki chaguzi za vyama vingi bila kujali Tume imekaakaaje.

Wanasema Tume ni mbaya kila siku lakini Tume hiyohiyo ilikuwa ikiwatangaza kushinda Ubunge. Naishukuru sana Tume safari hii kwa kuacha kuwatangaza hawa jamaa ili waufahamu ukubwa wa shughuli.

Tuwaache waliotangazwa kushinda nao wakafaidi kama vile nyie mlivyofaidi kwa miaka 10 kwa kutumia Tume ya aina hiihii.

Nitawashangaa wale walioshinda kama watasikiliza porojo za kuwaambia wasiende kupata mpunga bungeni, hata 2015 malalamiko yalikuwa hayohayo kwa Tume lakini walikwenda bunge kilafi pamoja na malalamiko ya Lowassa kuibiwa kura.

Kwakuwa wao safari hii wametemwa basi wanataka walioshinda wasiende bungeni. Huu ni utoto.


Unaongelea bunge lipi ?? au hili lilowekwa na Jeshi la Mabeyo na Security ya Diwani pamoja na Polisi ya Sirro wakisaidiwa na majeshi ya kukodi kutoka BURUNDI ???
 
Back
Top Bottom