Upoteaji wa majina ya asili ya Waafrika

Ndo manabii wa siku hizi wanawadanganya,
 
hongera sana kwa uzi huu mzuri. Hili jambo huwa nalifikiria sana aisee. Yaani tumepoteza identity yetu kabisa. Na hili kwa kiasi kikubwa linachagizwa na dini za kigeni tulizoletewa. Mfano, Kwa wakristo wanakwambia kabisa mtoto wakati wa kubatizwa apewe jina la kikristo, hapa wanakuwa washakulimit kutumia jina lako la asili kwa kisingizio cha dini. Kwani tujiulize, huwezi kuwa mkristo au muislam na ukatumia jina lako la asili.? Je jina lako ndo tiketi ya kuiona pepo?
Mbona west africans ni waumini wa hizi dini tulizoletewa na wengi wao wanatumia majina yao ya asili?

Pili, haya majina yanachagizwa na ulimbukeni wa wazazi ambao wanadhani jina la kizungu ni superior kwa jina kiafrica. Wapo radhi kulikejeli na kulicheka jina la asili na kulitukuza jina la kigeni. Huu ni upotokaji wa kiwango kikubwa sana. Yaani mtu yuko proud kuitwa jina la muarabu au mzungu ila asiitwe jina ala asili yake!

Hivi wazungu/ waarabu tuliwa jiuliza huwa wanatufikiriaje wakisikia tunajiita majina yao?
 

Watoto wangu nimewapa majina ya kiafrika tu. Na hapa niliamua kuwa mbabe kidogo. Wake zangu nimewakataza kuwapa watoto majina sijui za kikristu au kizungu.

Huwa nawapa wake zangu nafasi ya kuchagua majina ila kwa maelekezo na sharti moja tu, lazima majina yawe ya kiafrika la sivyo natumia turufu yangu kutoa jina na hakuna mjadala katika hilo.

Pia nimekataa, hakuna mwanangu kuniita sijui daddy, mimi ni baba. Full stop.

Lugha pia za asili na kiswahili ndo nawafundisha watoto. Kiingereza wanajifunzia shuleni.

Huu ni msimamo wangu kama binadamu ninayejitambua.
 
Je wewe unajina la Asili? Unalionea fahari au unalionea haya?
Master wazungu wametuletea system yakijinga sana na kwa kweli wametuweza kw asilimia zote kwakuwa hata milima ,maziwa,mbuga za wanyama walibatiza wao ,angalia mlima kilimanjaro,tizama olduvai george,chekshia ziwa victoria ,geukia amboni tanga,
Haya njoo kwenye vitu vya asili angalia hata kuku wameleta chotara,ng'ombe ,nguruwe,mbuzi,mbegu za mazao zote ,miti ya muda mfupi,angalia hata lugha sasa uzungu ndio ujanja........yote wamegeuza na kuleta uzungu hybrid,,,,wametung'oa mazima yote kwa yote tuwaombee Maasai waendelee na utamaduni wa asili uliobaki wakiafrika japo watatoweka nao au kubadlishwa mojakwamoja,utashangaa watoto wanaozaliwa sasa wakiitwa Putin,Zulensky na mengineyo.....tumekwisha
 
Baada ya wa marekani weusi kuacha majina ya asili na kuanza kutumia ya kizungu ilibidi 🆔 card zao zianze kutaja na rangi ya mwenye hiyo 🆔 kama huyo John McCain ni black au Caucasian
 
Wasukuma na wamasai kwa hili wamejitahidi ila wachaga na wahaya wanaongoza kuita watoto ,majina ya kizungu
 
Ongezea pia mtu mweusi anaitwa Abdoul razack majid au fatma masoud
 
Kuna haja kama taifa kuliangalia hili swala kwa ssa mpaka mtu ataje mpaka jina la 3 ndipo utagundua ni mtu wa sehemu gani mfano mimi ...NOEL ANTHONY KIMWERY kupitia jina langu la 3 ndipo utagundua ...aaahh kumbe [emoji12]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…