Miss Kyenda, ni wanadamu wachache sana wanaokubali mabadiliko, haijalishi mabadiliko gani, ya aina yoyote ile..
Lakini pia ukiangalia katika mapinduzi ya jambo lolote lile duniani ni lazima pawepo na “sacrifice”. Ukiangalia historia ya mambo duniani, hakuna ukombozi uliowahi kutokea pasi na kuwa na wahanga.
JPM anaonekana ni mwiba mchungu, lakini ipo siku atafananishwa na lile jiwe kuu la pembeni walilolikataa waashi.
Nasema haya kwa maana kwamba Watanzania kama tunataka mabadiliko na kufikia maendeleo ya kweli, hatuna budi kukubali baadhi yetu kama sio wote kuwa sadaka kwa manufaa ya kizazi kijacho.
Hakuna nchi iliyowahi kuendelea hapa duniani bila ya kuwepo wahanga, watu waliopambana na hata kufa kwa ajili ya ukombozi wa nchi zao( haijalishi iwe ni kwa njia ya vita ama amani)
Mimi naichukulia hali hii tunayopitia kama taifa kuwa ndio “sacrifice” yetu kwa ajili ya mustakabali mwema wa Taifa hili. Naikumbuka historia ya safari ya wana Israel jangwani kuelekea nchi ya ahadi, mapinduzi ya viwanda Ulaya na Marekani kuelekea maendeleo, China na Asia katika ujenzi wa nchi zao, n.k. Ni safari zilizokuwa na taabu na machungu mengi lakini mwisho wa siku walizifikia ahadi na ndoto zao. Na hata sasa vizazi vyao vinakula mema ya nchi zao lakini vinawakumbuka majemedari hao walioumia/kufa kwa ajili ya kizazi kilichopo.
Watanzania tukubali tu, hatuwezi (kama kweli tunataka maendeleo) kuyafikia pasipo kuwa na watu watakaojitoa na hata kufa kwa ajili ya wengine.
Mimi ni mtumishi wa serikali na hata hili la 25% linanigusa na kuniumiza lakini najifariji kwamba hii ndio sacrifice yenyewe ili watoto na wajukuu zangu waje waikute Tanzania ya maziwa na asali huko siku za usoni.
Lakini pia hata maandiko yanatuambia kuwa safari ya mbinguni sio nyepesi, ni yenye tabu na mapito magumu na kwamba watakaostahimili mpaka mwisho ndio watavikwa taji ya uzima.