Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Habari za muda mabibi na mabwana!

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza nawashauri wanachama wenzangu na wananchi kwa ujumla. Mwaka 2020 tusipoteze tena kama ilivyotokea mwaka 2015. Haya yote ni kwa sababu hatukutulia vizuri katika mchujo wa kumpata kiongozi bora.

Karibuni kwa maoni yenu.

====
Hafai
 
Leo Wapinzani Na Baadhi Ya Vegetables Narrative Wanasema Membe Anafaa Kugombea Nafasi Ya Urais Na Kusahau Kua CCM Ni Ile Ile Na Katiba Ya Nchi Ni Ile Ile.

Tatizo Hapa Hawezi Kua Mtu Tatizo Linaweza Kua Ni Katiba Pamoja Na Mfumo Mzima,Wapinzani lieni Na Katiba Mengine Yaacheni.
kwa sasa shida ni Jiwe
 
Hapo BM hajaongea wanaweweseka,je akisimama jukwaani itakuwaje!!
 
Kwenye nchi ya kaanani iliyo jaa viwanda
Dah... How? Kwa staili yenu hii? Kama JK alishindwa....EL asingeweza hata kujaribu...BM ndiyo hataweza kujaribu kabisaaaa[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Watumishi fanyeni hujuma indirect dhidi ya serikali hii onevu kwenu ni miaka 3 hakuna ongezeko la mishahara na maslahi yenu yanazidi kukandamizwa.
 
Na hili jua la Dar nenda kwa mangi pata juice ya Ceres sina neno nitalipa kabisa........ yaan tungeweza kuondokana na huyu mtu hata maisha ya watu wangekuwa marefu... maana na mpango wa kuua mpk wazee wetu
Tangu lini kutangaza nia likawa kosa. Tunaelekea wap?
 
Watumishi fanyeni hujuma indirect dhidi ya serikali hii onevu kwenu ni miaka 3 hakuna ongezeko la mishahara na maslahi yenu yanazidi kukandamizwa.

Unajitahidi sana kushawishi yasiyowezekana
Hayata timia....
Punguza stress na safari ya bariiiidiii..!
 
Akisimama Membe Lowasa au Lisu anachukua nchi mapema hata kabla kura kuhesabiwa. Akishinda tujiandae na vita visivyo lazima kati yetu na Rwanda na baada ya kuipiga Rwanda ataipiga Malawi. Membe ni Mbabe sana na hatupo tayari kwa hasara.
Mbabe kumzidi jiwe?
 
Wakuu Salaam.

Kiongozi yeyote ktk kuhakikisha mambo yake yanaenda vizuri huwa ni lazima ahakikishe ktk safu yake ya maamuzi na utendaji kwa asilimia zaidi ya 90 ana watu ambao ni watiifu kwake na wako tayari kuyabeba mawazo na maono yake siku zote.

Kwa muktadha huo huo ni imani yangu kuwa hata ndani ya CCM chini ya Mwenyekiti wake Mh. Rais Magufuli hali ni hiyo hiyo na ni vigumu sana kuwa na agenda inayotishia ustawi wa Mwenyekiti halafu utegemee agenda hiyo ikapita, hilo haliwezekani.

Kwa siku za karibuni wako watu wenye ndoto ya kutaka kuona Mstaafu B. Membe akishika hatamu ya uongozi wa nchi hii mwaka 2020 kwa tiketi ya CCM, kwa kujiaminisha kuwa eti wanaweza fanikisha uasi dhidi ya mwenyekiti wao, hili jambo haliwezi kufanikiwa na si ajabu baadhi ya watu wakapigwa permanent ban ktk chama.

Hivi kwa nini wasiwe majasiri na watoke ndani ya CCM na kuanzisha chama chao ili waweze kumsimamisha mgombea wanayemtaka na ambaye wanaamini watanzania watampokea na kumpa nafasi ya kuongoza, mbona majirani zetu kenya walifanya hivyo na baadhi yao wakafanikiwa yuko Rais Mstaafu Mwai Kibaki, Rais wa sasa Uhuru, William Ruto na R. Odinga anayeendelea kupambana.

Tofauti na hapo hizi blah blah za mitandaoni hazitasaidia chochote na mabadiliko pekee ya 2020 Inshallah Mungu akituweka hai ni Dr. Hussein Ally Hassan Mwinyi atakayeshika hatamu Zanzibar huku JPM na Mama Samia ngoma inogile.
Ni wachache sana wanaweza kuukubali huu ukweli. Hasa kwa siasa zetu hizi za mahaba.....
 
Mexene et al., naomba nipigwe ban ya mwaka.kunamijitu inakera mnoo mpaka watamani kuyapiga risas za ubongo.....endeleeni kushangilia hivyo hivyo, mpaka pale atakapoanza kuuwa watu wake wa karibu akihisi wanamuhujumu ndiyo akili zitawakaa saw a.
Mlipo ambiwa hakuna aliye salama ,mnadhan utani. Vyombo vya habari kwapani, bunge kwapani,mahakama kwapani , upinzani kwapani, anaanza na dini kuzitia kwapani maana uchunguzi wa kakobe tumeusikia.
Ule mwisho bado, mpaka atakapo anza kuuwa watu wa chama chake na washauri wake wa karibu ,ndiyo ule utakao kuwa wakati ulio tabiriwa.....endeleeni kushangilia , imbeni mapambio yotee, tukaneni wanaomkosoa woteee, wakati unakuja kila mtu atalia ,kuomboleza na kusaga meno na hakutakuwa na kimbilio.......
Kwa ujinga huu uliouandika ni kweli unastahili ban ya mwaka, nguchiro wewee
 
Tanzania ya "Shamba la Bibi " ilianzia kwenye CCM shamba la bibi na Upinzani shamba la bibi, kwa ujumla vyote vilizaa matunda ya Ufisadi, wizi, uhuni, utapeli, ukosefu wa maadili na kustawisha shamba la bibi kwa muonekano wa kitonga na kufanya maisha ya wajukuu wa bibi kuwa mepesi sana, kiasi cha kumiliki visima vya mafuta, vitalu katika mbuga zetu, biashara za magendo na kujiita wenye Shamba na kusema wao ndio watengeneza "Mabwana Shamba".

Shamba la bibi lililea na kusomesha wajukuu ambao baadae waligeuka wezi na kuiba katika shamba hilo hilo la bibi, Wajukuu hao wasomi waliliingiza Shamba la bibi kwenye mikataba feki, mibovu na ya kibeberu kwa faida ya matumbo yao, uhuni katika vitengo walivyopewa wakiaminiwa kwa maslahi ya Umma.

Ifike mahali tuseme imetosha, tumechoka kuwa shamba la bibi,tuwakemee watu kama Zitto anayesema anautaka urais ili watu wale bata.

Zitto anataka kuturudisha kwenye Tanzania ya "Shamba la bibi "ambapo baadhi ya watu walipewa dhamana na Serikali katika nyadhifa mbalimbali wakakosa maadili ya uongozi kwa makusudi ama kwa bahati mbaya na wakasababisha uzembe ambao umeligharimu Taifa.

Hasara kubwa ambayo watanzania wameipata ni kupoteza fedha nyingi ambazo zingeweza kuisaidia Serikali kuboresha maisha ya watanzania katika nyanja mbalimbali za kielimu.

Fedha ambazo zimepotezwa na Wajukuu katika "shamba la bibi" leo hii zingeweza kusaidia kuinua maendeleo katika nyanja mbalimbali za kielimu, afya na kiuchumi kwa lengo la kusogeza karibu maendeleo kwa wananchi katika maeneo mbalimbali hususani maeneo ya vijijini.

Juhudi kubwa zinazoonyeshwa na Rais John Magufuli kupigania na kuzilinda rasilimali za nchi ambayo ilikuwa "Shamba la bibi" kwa maslahi ya Taifa ni jambo ambalo litasaidia kuchangia kwa kasi harakati za kimaendeleo.

Kwa jicho la kifalsafa na kwa uwanda mpana na mrabaha wa kibeuzi inatupa fasiri yakinifu kuwa CCM isipokuwa safi, basi hata taifa hili litanuka kwa uchafu na utakatifu hautakuwapo Lumumba hata Magogoni, kwa maana upigaji wa wajukuu wasomi waliotuingiza kwenye mikataba mibovu,utaendelea kuliumiza taifa hata pale atakapopatika wa kuisafisha Lumumba na kuifanya safi na nyeupe kama karatasi.

Ni kwa msingi huo, nathubutu kumpongeza Rais John Magufuli kwa kuamua kusafisha nyumba yake (CCM), kwani huku ndiko tunakopata viongozi wa kisiasa wanaokwenda kushika madaraka Serikalini.

Namuona Membe katika mlingayo wa kuhusianisha falsafa ya Lowassa pale makundi mbalimbali ya watu yalipojitokeza kwenda kumshawishi agombee urais akiratibu kundi la bodaboda,Mama ntilie,Mashehe na Wachungaji na kundi la 4u Movement, Kwa fasiri jadidi Membe anakopi ya Lowassa na kutaka kuwafanya Watanzania ni majuha kwa kutaka kuirudisha Tanzania ya "Shamba la bibi " Kwa ufupi Malumbano, misigano na mitafaruku yote ni kupata suluhu ya kufanya maisha bora na kula bata kama atakavyo Zitto na kuifanya Tanzania kama imefika kilele cha mafanikio ilihali tumefunikwa na wimbi la umasikini.

Kiini na kitako cha kutoa cha gumzo hili ni kukumbusha tulipotoka kwa maana anayesahau historia basi hajui aendapo, Nakumbusha enzi za watu kutamba kwa kusema "hii nchi tumeiweka mfukoni" unanijua Mimi ilihali wasijue wanayemtambia kuwa ni yule mzee aliyejenga reli ya kati kwa fimbo na kwa malipo ya thumuni.

Nimejitahidi kuumba fikra kwa ufupisho ili kukidhi matakwa ya hadhira ya jamii.

Ni rahisi kutamba upo juu ya Chama,lakini ni vigumu na inachukua miongo na falsafa ngumu sana kumpata "Mao Zedong wa Taifa la China ama Julius Nyerere wa Taifa la Tanzania" mumpatapo mpeni ushirikiano kama wachina walivyompa ushirikiano Mao Zedong na kukifuma upya chama na Taifa na sasa wachina wanatembea kifua mbele duniani.

Kikundi cha watu wachache ndani ya CCM,Chadema,ACT wanaotaka kuirudisha nchi yetu kuwa Tanzania ile ya Shamba la Bibi kamwe tutawapinga na hatutaruhusu wamhujumu rais wetu Mzalendo wala kuihujumu Tanzania iwe ndani ama nje ya nchi, Tunahitaji Magufuli wengi kuanzia ngazi ya shina, mtaa, Kata, Wilaya na Mkoa ili kuweza kuitengeneza upya Tanzania kutoka Tanzania iliyokuwa "Shamba la bibi".

Niwatakie tafakuri jadidi na ubeuzi mwema wa gumzo hili na kuwapiga Vita wale wote wanaotaka kuturudisha kwenye ile iliyokuwa Tanzania ya Shamba la Bibi.
 
Membe oyeeee [emoji106][emoji106]

Membe safii [emoji106][emoji106][emoji106][emoji106]

[emoji41]
 
Back
Top Bottom