Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Habari za Jumapili waungwana

Uchaguzi mkuu wa Urais, wabunge na madiwani unatarajiwa kufanyika 2020 hapa nchini. Ni kiasi cha kama miaka miwili tu ijayo

Kwa mtazamo wangu huu ndio muda muafaka kwa wale wote wanaotaka kugombea hasa nafasi ya Urais wawe ndani ya Chama tawala au Upinzani wajitokeze mapema na kutangaza nia zao za kuomba ridhaa ya vyama vyao kugombea nafasi hiyo

Kwa kufanya hivyo watakua wanatutendea haki Watanzania kwa sababu tutakua na muda wa kutosha kuwapima uwezo wao wa kila nyanja

Miaka miwili ya kumsoma mtu mwenye nia ya kua Rais wa nchi yetu inatosha kabisa kufahamu utimamu wa afya yake ya akili, uwezo wake wa kiuongozi, uwelewa wake wa masuala muhimu ya ndani na nje ya nchi, kuchimba historia yake, uadilifu wake kuanzia ngazi ya familia na uzalendo alionao kwa nchi.

Itatupa pia nafasi ya kumpima uwezo na utayari wake wa kuunganisha nchi hii ambayo inamchanganyiko wa matabaka mbalimbali ya kijamii. Pia itatupa fursa ya kumjua mtia nia anauelewa gani kuhusu dunia ilivyo, uchumi unaendeshwaje na kama anatambua kinaga ubaga changamoto zainazoikabili dunia yetu na mikakati yake ya kuivusha salama nchi yetu katikati ya changamoto hizo

Huu ndio utaratibu uliopo katika nchi hasa zilizoendelea. Ni utaratibu ambao unahakikisha kua Rais ajae anakua ni mtu mwenye uwezo hasa wa kua kiongozi wa nchi na sio kituko

Tatizo tulilonalo kwenye nchi yetu ni kwamba tunataka surprises za dakika za mwisho. Tena tatizo hili lipo kwa vyama vyote vya siasa. Wanatuletea tu wagombea huku wanatuona Watanzania ni mazwazwa, tutamchagua tu hata watuwekee jiwe ilimradi chama kimempitisha! Utamaduni wa kuteua wagombea kama bahati nasibu ipo siku utatugharimu kama Taifa!!! Tutakuja kumpata Rais wa ajabu haijawahi kutokea, atakaekua ni aibu na fedheha kwa Taifa

Binafsi sijamsikia Bernard Membe akitangaza nia ya kugombea Urais lakini yalipoletwa madai kama anayo nia hiyo yametokea maoni tofauti ambapo watu wengine wanamuunga mkono na wengine wakimpinga na hata kumkashifu na mwenyewe hajakubali wala kukataa madai hayo

Kwa mtazamo wangu kama kweli Bwana Membe anayo nia ya kugombea nadhani kafanya jambo zuri sana. Huu mjadala unaoendelea kumuhusu naona kama ni mjadala wenye afya sana ambao unaweza kutuonyesha uwezo na mapungufu ya Membe ili wananchi wamjue na waamue

Badala ya kusema hana haki ya kugombea(kwa utamaduni wa CCM?) mjadala ungejikita katika kuchambua uwezo wake na mapungufu yake na kama hafai basi mapungufu yake yasemwe waziwazi na kama anafaa basi isiwe nongwa kwa yeye kutia nia ya kugombea

Ningependa na watu wote wenye nia hiyo kutokea vyama vyote wangefanya hivyo na wao ili watupe fursa na muda wa kutosha wapiga kura wa kuweza kuwachambua na kuwajua na isije kua tena mambo ya kushangazana dakika za mwisho
2020 ni Membe
 
"Wana jamvi tuliochoshwa na huu utawala wa mtawala wa nchi ile hebu tuimbe haka kanyimbo hadi asikie aelewe kuwa hatuutaki uongozi wake na matendo yake"

Nimepita kijiwe cha wana CCM kindakindaki nimesikia wakiimba na kuelezana. Kweli wamemchoka!
Membe kweli... Kwelikweli.... apo jiwe atakuwa anaisi kujikojolea
 
Naomba niwarejeshe katika mifano kadhaa mwaka 2013 Zitto Kabwe,Prof. Kitila Mkumbo na wenzao Samson Mwigamba walifukuzwa uanachama Chadema.

Kamati kuu ya chama hicho ilitangaza hadharani kuwa Zitto na wenzake walikuwa wameandaa mpango wa kumuondoa mwenyekiti wa wakati huo madarakani bila kufuata taratibu za chama na kwamba walitaka kumpindua Mbowe.

Kwa tafsiri ya haraka ni kuwa japo ilikuwa ni haki ya kikatiba kwa Zitto kugombea nafasi ndani ya chama hicho lakini kufanya kampeni,vikao na mikakati ya ushindani ndani ya chama ilihali kipenga hakijapulizwa lilikuwa ni kosa lililowafukuza.

Lakini ikumbukwe kuwa iwapo tuhuma hizi dhidi ya Membe ni za uongo au zimepikwa na baadhi ya watu ndani au nje ya chama ,suala hili lisiposhughulikiwa kwa busara na maamuzi magumu litaendeleza mpasuko na kukoleza mgogoro ndani ya chama. Lakini chama kikijidhihirisha kuwa kuna mwanachama wao mmoja au kundi Fulani linalopanga kuendesha vikao na mikakati ya urais kabla ya kipenga ,ni wakati muafaka wa kuchukua maamuzi magumu dhidi yao kulingana na taratibu .

Kuutaka urais ni haki ya kikatiba ya Membe ila kosa linaweza kuwa kuendesha kampeni na kupanga mikakati ya ushindani ndani ya chama kabla ya kipenga.
Katika hilo hawezi kukwepa lawama iwapo ni kweli,maana katibu mkuu wa CCM kama mtendaji mkuu wa cham ana wajibu wa kusimamia katiba na taratibu za chama.

Kwa uelewa wangu,katiba na kanuni za CCM zikisimamiwa ipasavyo BM anaweza akajikuta anapoteza vyote.
 
Alishasema atazamisha nusu ya chama kwa siku moja siku wakiimba huo wimbo
Sasa, matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno
Ngoja tuone sisi ni wazeee wa "hands off eyes on" until Oktober 2020
 
CCM mfumo ni uleule..
Zimbabwe wametoa Moga wa ZANU na kumweka Mnangagwa wa ZANU..
Ni upuuzi uleule..
Wananchi hawamtamani hata mwaka bado.
 
In a real sense when you start a battle you need to know and understand your anemy's strength strength and weakness. But for this case I am 100% sure that you either dont understand your enemy or you are underestimating your enemy.
 
Membe kweli... Kwelikweli.... apo jiwe atakuwa anaisi kujikojolea
8CAF2E60-94EB-42C3-809B-CA6D225E8074.jpeg
 
Hivi tutaacha lini kufuata mkumbo
Kufuata mkumbo ni kawaida ya maisha ya mwanadamu. Amezalwa uchi wa mnyama lakini akaparamia nguo kwa kufuata mkumbo tu, alikuwa ananyonya maziwa lakini akalazimishwa afuate mkumbo na kuanza kula ugali, amezaliwa na bikra yake lakini akafuata mkumbo wa vishawishi ikavunjwa.
Kufuata mkumbo hakutaisha mpaka kiama. Twende na Membe
 
Mnaimbaimba huku ila come 2020, CCM inakuja kumpitisha Jiwe kwa 100%. Akili za wana CCM wanazijua wenyewe
 
Back
Top Bottom