Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Membe ndio angeharibu zaidi....hii nchi ingekuwa kama Zimbabwe au Venezuela mkuu
...go for Magufuri over Membe mkuu
 
Kwani katiba ya chama chao cha kijani inasemaje?
Huyu aliyeko madarakani si mpaka amalize miaka 10 au?
Au kuna mabadiliko.
 
 
Viongozi wetu wa taifa hili wamebarikiwa na wameweza kutufikisha hadi hapa tulipo, kuanzia Nyererr, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na inshallah 2020 ningependa nafasi iende kwa Membe

Ni mtu mwelewa, diplomatic, jasiri, mwenye hekima na alieelimika.

Namkubali Raisi wetu wa sasa ambae ni mchapa kazi, ila tu binafsi namwelewa zaidi Membe.

Inshallah Bernard Member utakuwa raisi 2020


Ikiwa nimefanya uchochezi wa aina yoyote unaoenda kinyume na katiba na sheria za nchi hii nawaombeni mnijulishe
 
Kwahiyo ukimwelewa wewe maanake watz wote million 59 tumemkubali????? Akili za watz mungu ingilia kati uwiiii
 
Tunataka Rais KIJANA!
Tupo pamoja kwenye hili. Nnasikitika sana kuona watu wanawapigia promo watu wazee waje kuwa marais. Tukubali tukatae ili nchi yetu isonge mbele zaidi tuachane na hawa wagombea wazee watatuchelewesha sana. Maana wengi wao mitizamo yao ni tofauti sana na speed ya mabadiliko ya mambo inayoendelea kwa sasa duniani
 
Nataka nijue kitu kimoja..je haiwezekani mkutano mkuu wa ccm kumkataa rais aliyeboronga na kumwachie mwingine agombee?Maana huyu jiwe hafai hata kwa bure!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…