Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Cha ajabu analalamika urais ni mgumu sana ila bado anampango wa kugombea tena 2020. Kama mambo ni magumu apishe wenye pumzi wapige kazi. Analalamika chai ya moto halafu anaendelea kunywa

Hapo sasa!! Cha ajabu watanzania watampa tena kazi mtu aliyelalamika ameshindwa kazi
 
Hapo sasa!! Cha ajabu watanzania watampa tena kazi mtu aliyelalamika ameshindwa kazi
Wakati wa kampeni alikua mpole, mnyenyekevu anaongea kwa uchungu kama mwanamke anayekaribia kujifungua kumbe ni bazazi la kutupwa. Leo wakurugenzi wa halmashauri wote ni makada tena wenye tishio la kutomtangaza mpinzani kuwa mshindi jamaa katuharibia sana nchi yetu kabakia kujisifia tumenunua ndege kwa mpigo tukidai alete utaratibu wa manunuzi anageuka mbogo
 
Jasusi mbobezi na mwanadiplomasia aliyetukuka rais ajaye kabla 2020 ndugu Bernard Kamillus Membe kama angekuwa leo rais Swala la kuuwawa Khashoggi angeingilia kati na kutuliza mambo kwa njia ya upatanishi na diplomasia.

Akiwa waziri wa mambo ya nje awamu ya 4 Membe aliweza kuiweka karibu sana Tanzania na mataifa ya uturuki na Saudi Arabia.

Pia Membe angekuwa rais angeenda mbali zaidi kwa kuwaleta karibu Saudi Arabia na Qatar kwa kuwafanya ku "extend an olive branch" katika mustakabali mzima wa mashariki ya kati.

Chini ni picha Rais Membe akimwaga balozi wa Saudi Arabia aliyemaliza muda wake ndugu Hani Abdullah alipokuwa waziri wa mambo ya nje awamu ya 4

View attachment 914182
[emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38] watu mna utani na jiwe"chini ni picha ya Rais Membe" daaaadeki mnatafuta balaaaa
 
[emoji23] [emoji23] mie St Kayumba ila hicho kiinglishi duh! Nimekielewa[emoji23]
 
Hahahaha..

Kwa muda mfupi tu nimewaelewa wanaopiga hii kampeni..hahahaha

Ni kitengo cha propaganda cha Magu..

Hahahaha....
 
Hebu acheeni utani nyie. Hivi ni nani anayewatuma kuandika haya?

Kabla hatujaenda huko mbali sijui Saudia na Uturuki, tujiulize kipindi akiwa waziri alifanya nini?

Ni kipi cha kujivunia alicho kifanya huyo Membe hata kumtamani awe Rais leo?

Yaani ni bora Mwigulu au Nyalandu mara kumi kuliko Membe. Huyu bwana Membe alibebwa na Jakaya, huo ndio ukweli.

Ingawa Lowassa anatuhuma"hewa" za ufisadi (maana hakuna aliyefanikiwa kuthibitisha ufisadi wake sio mahakama mpya za mafisadi zilizoanzishwa) ila bora mara ishirini zaidi ya Membe.

Watanzania ni nani aliyewaloga? Kila kitu bendera fuata upepo, watu wa maslahi na kupinga kweli kisa takrima ya buku kumi!

Tunatakiwa ku-brainstorm na kujadiliana kwa kina juu ya nani anapaswa kuwa Rais. Urais ni taasisi sio sawa na kuuza genge sokoni.


TUAMKE WATANZANIA, TUIPENDE NCHI KWA KUWA WAZALENDO WASIOKUWA WAOGA NA WANAOHADAIWA NA VIRUSHWA UCHWARA HATA KUSHABIKIA WATU WANAOUTAKA URAIS KWA MASLAHI BINAFSI/MTANDAO WAO.

Kwa sasa Rais ni Magufuli tuliheshimu hilo.
 
Watanzania upumbavu mtaacha lini?

Hivi hamuoni kabisa hii kama ni move ya kupoteza ishu ya mo?
 
Watanzania upumbavu mtaacha lini?

Hivi hamuoni kabisa hili kama ni move ya kupoteza ishu ya mo?
 
Back
Top Bottom