Mods naomba msinichanganye Thread yangu na hizo thread ambazo rasmi naona ziko kimkakati zaidi, na kama mtanichanganya basi nitawaona au nitalazimika kuamini kwamba nanyi ni sehemu ya mkakati huo.
Leo na siku chache nyuma kumeanza kuwa na thread nyiingi humu zikimhusisha Bernard membe aliyeukosa urais 2015 akigombea ndani ya watia nia ndani ya CCM.
Wanaoweka thread zao humu ni watu ambao avatar zao zinajirudia rudia. (Jambo linalotia shaka na kutuaminisha kuwa huu ni mkakati.)
Mimi sitaki kurefusha stori bali nauliza yafuatayo .
;kama membe ni mwanadiplomasia mahiri (kulingana na wanamkakati hawa).
Mbona hatusikii akiitwa hata kwenye utatuzi au usuluhishi wa migogoro mbalimbali ya kidiplomasia duniani, mzee mahiga amekuwa muda wote akilipaisha jina la nchi hii kwa kuitwa mara nyingi na kukabidhiwa majukumu makubwa ya kidiplomasia ikiwemo IGAD kabla ya kuteuliwa kuwa waziri wa mambo ya nje aliko sasa hivi.na pia mzee Mkapa na Kikwete pia, ambako mpaka sasa mzee mkapa ni msuluhishi wa mgogoro wa burundi.
Tusisahau pia mama Aisha kigoda yeye alihudumu katika nafasi kubwa kabisa katika UN.
Pia tusisahau mama Getruda mogela na mama Anna tibaijuka waliohudumu sehemu mbalimbali katika UN HABITAT na jumuia ya madola.
Lakini huyu membe pamoja na kuhudumu mambo ya nje kwa muda mrefu, tangu alipotoka katika nafasi hiyo ni kama amesahaulika ndani na nje ya nchi.
Je mnaoibuka kimkakati sasa hivi na mkionekana rasmi kuja na staili ile ile ya kimtandao mnaweza kutuambia ni lini alijisafisha na kashfa ya fedha za Ghaddafi?(ambayo huenda Jumuia za kimataifa zinalitambua na kujiweka kando nae).
Na je kama yeye ni mwanadiplomasia mahiri,zaidi ya kutumia muda mwingi kujiandalia mazingira ya kuusaka urais, ni lipi alilotufanyia nchi hii kama waziri wa mambo ya nje, ambalo inaweza kumpa legacy kwa wananchi wazalendo wa nchi hii?
Na hivyo kutulazimisha kumuamini kwa hilo?
Na mwisho kabisa...ni kwa nini sasa ambapo kuna mgogoro wa bei ya zao la korosho huko mikoa ya kusini.
Angalizo:
Hii inaweza kutufanya wananchi tulazimike kumuamini vizuri musiba na Tamko lake juu ya majina Yale. Namnukuu nusiba.
1.subash Patel.
2.Abdulahman kinrana
2.Nape nnauye.
3.Tundu lissu.
4.Zitto zubery kabwe.
5.mlowola.
6.Yussuph makamba.
7.Aikael mbowe.
8.Massoud kipanya.
9.Said michael(cartoonist)
10:Rostam Aziz.
Na wengine wanne majina nimeyasahau lakini clip ipo YouTube.
CCM INA TARATIBU ZAKE ZA KUWAPATA WAGOMBEA WA CHAGUZI MBALIMBALI. kila muda unapowadia lakini hii ya mitandaoni sasa hivi tena ikichagizwa na Avatar za Chadema tunaowajua humu JF, hakika si bure!
Msituvurugie nchi yetu na kasi yetu mpya ya maendeleo. Mnapaswa kukemewa kama ukoma!
Walaaniwe wale woote waliokaa miaka zaidi ya 18 iliopita na kujiundia kundi la wanamtandao, maana umetuharibia nchi mpaka sasa inatusumbua kuirudisha kwenye mstari.
Kama huyu membe hakufaa kwa wana ccm kumchagua kwa wakati ule, ni sabuni gani kaogea hadi atufae kwa sasa!
Ahsanteni. Naomba kuwakilisha na tujadiliane kwa hoja si matusi.