Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Usichokijua ni kwamba hiyo Miliion 50 kwa kila kijiji ilikuwepo kwenye Ilani ya Uchaguzi 2015 sa sijui kama angekuwa Membe ndiye mgombea angefuta hicho kipengere ama vipi! Jibu unalo mwenyewe.

Watanzania walitaka mabadiliko, Sasa jiulize mabadiliko waliyoyataka Watanzania wakati awamu ya nne inatoka madarakani tungepata kitu cha tofauti kama Membe angekuwa Rais? Unamuona Membe akiwa na utofauti kati yake na Membe?

Mabadiliko ya Kweli ypo kwa JPM. Tulizoea kuiba sasa fanya kazi kihalali upate mshahara wako wa halali. Membe angekuwa Rais wala asingeweza kuajili kila Mwananchi wa Tanzania. Membe anekuwa Rais labda angekodi Ndege sio kununua katu, SGR mradi angepewa Mchina tena kwa mkopo wa riba ya hatari, Meli ziwa Victoria! Sidhani Mradi wa maji Rufiji asingewaza hilo! namuombea JPM amalize salama kwenye awamu zake zote 2 alafu tutarudi tena hapa kufanya tathimini.
Yawezeka wewe ndo ulizoea kuiba ila sisi tuliokuwa tuishi kwa juhudi zetu na halili mvua na jua letu. Mfano tu kwa mkulima wa mahindi auze debe shilingi 3000 kisa jamaa alifunga mipaka 2017 kisiasa.

Hivi kwanini waajiriwa mnahisi kila anaepitia wakati mgumu sasa alikuwa mwizi that's very cheap politics.
 
Membe ni mwana diplomasia hata Tundu Lissu angekaa nae meza moja wakayazubngumza
Angetafuta njia za kukabiliana na upinza si biashara ya nunua nunua rudia uchaguzi.
Hizi story za Membe sizielewi, mbona abrupt kama uyoga. What's behind this
 
Yawezeka wewe ndo ulizoea kuiba ila sisi tuliokuwa tuishi kwa juhudi zetu na halili mvua na jua letu. Mfano tu kwa mkulima wa mahindi auze debe shilingi 3000 kisa jamaa alifunga mipaka 2017 kisiasa.

Hivi kwanini waajiriwa mnahisi kila anaepitia wakati mgumu sasa alikuwa mwizi that's very cheap politics.
Alifunga mipaka kisiasa..! aibu sana hii kwa mtu mwelevu kama wewe kuliona hili? nchi ngapi zinafunga mipaka yao kwasaabu za kujitosheleza ndani kwanza?
 
Wakuu samahani kwa kuwa outdated
Hivi Membe kafanya nini hasa?! Maana naona ghafla ana trend kila kona ya mtandao
Naomba msaada wa maelezo mafupi wa alichofanya au hata link nisome walau nipate mwanga

Usiulize Unga mkono tu, Membe 2020..
 
Naona kama mnajifurahisha, yaani naona kama Maigizo, watu na akili zenu mnakaa mnadanganyana Membe anaenda kuchukua nchi 2020.

Mimi na akili zangu za kuvukia barabara nauliza ATAPITIA NJIA GANI?

Ndani ya CCM , Mwenyekiti ndiye mgombea urais na ndiye mwenye sauti ya mwisho ,

Kupitia Upinzani ,ndio kabisa hawezi kushinda , Tuliona kwa LOWASSA,.
Labda kama ana hela za kuchezea,

Kupitia Uhaini, hapa atadakwa mapema sana..

NAWAULIZA NYIE MLIOKULA HELA ZAKE NA KUTUMWA MITANDAONI , MNAJUA ATAKUWA RAIS KWA NJIA GANI?

Mtuambie, sio mnasumbua mitandaoni lakini hamtuambii atapitia njia gani , ya golgotha au kaanani,

JIWE ameshajizatiti ana JESHI, TISS, UHAMIHAJI, POLIS , TUME YA UCHAGUZI,N.K

MEMBE ana nini? Au anataka kuliwa hela zake kama Lowassa?
Mkuu unayoongea wewe ni maneno ya kawaida mno tena ni maneno ya kitoto.
Unaongea as if unaijua kesho,wewe unaweza kutuambia nini kitatokea 2020?
Kwa mtu mwenye hekima atakujibu kuwa hiyo ni siri ya Mungu,lakini wewe tayari unajua eti kwa Sababu tu Magufuli ana TISS,jeshi na vyombo vyote vya dola.
Tambua kuwa Magufuli siyo Mungu,na si TISS wote wanampenda,na ndani ya CCM pia hapendwi kabisa, amejaribu kujitengenezea mtandao wake ndani ya CCM, utambue kuwa hadi sasa hivi CCM iko vipandevipande kwa Sababu yake.
Kwa hiyo lolote linaweza kutokea 2020,hakuna ajuaye hiyo ni siri ya Mungu.
 
Ana wananchi wenye machungu na kupoteza kazi zao, machungu ya kudhalilishwa, machungu ya kubomolewa nyumba zao, machungu ya kutukanwa vilaza, machungu ya kutoona local chanel, machungu ya kutoona bunge live, machungu ya kupigiwa shangazi zao, machungu ya gharama za maisha kuwa juu, machungu ya sukari kugoma kushuka bei. Huku mtaani wanamachungu sana. We acha tu mzee
Kwani lowassa hakuwa na hao watu?
 
Hakuna Rais mswahili tena nchi hii milele. Bora mzoee kukomaa. Nchi ina raslimali kibao ila tunakuwa wa hovyo tunsshindwa na vi nchi kama Rwanda? Never again.
Hakuna maendeleo bila maumivu.
 
Kuna watu tukisema Membe aongoze nchi 2020 wanabeza
Wengine wanatuita sisi ni vibaraka Wa Membe kitu ambacho sio cha kweli, Mimi sio kibaraka Wa Membe wala mheshimiwa Membe Mimi hanijui

Kitu ninachoamini ndicho nitaendelea kuamini, kwa sasa watanzania tumebadilika japo tume ya uchaguzi na vyombo vya Dora ndio hawataki kubadilika wanaturudisha nyuma

Ile kanuni ya kwamba Raisi lazima atawale miaka kumi imepitwa na wakati
Tukikupa miaka mitano ikakushinda basi kaa pembeni waachie wengine wanaoweza

Kwa miaka mitatu tu hii mambo yanaenda kombo

Vijana hawana ajira, tangu nchi kupata Uhuru awamu hii ya tano ndio awamu ambayo vijana wengi wamerandaranda mitaani bila ajira hata zile ajira za ualimu, nursing, udaktari hazipo tena

Ndani ya miaka hii mitatu watu wamefukuzwa kazi hovyo hovyo wamekua tegemezi, watu wamerudishwa kwenye Lindi la umaskini, watumishi Wa umma hawajapanda madaraja wala kuongezwa mishahara, kila siku uhakiki uchwara usio na kikomo

Ndani ya miaka mitatu ahadi zimeshindwa kutekelezeka zimebaki ni ahadi hewa, milioni hamsini kila kijiji imekua longolongo tu, ajira kwa vijana kama mnavyojionea mwenyewe,

Ndani ya miaka mitatu tumeshuhudia kauli za kibabe zisizo na mashiko kwa wananchi na viongozi wengine, wananchi wananangwa, viongozi wanatishwatishwa hovyo hovyo kama watoto wadogo

Kwa miaka hii mitatu tumeshuhudia mtu mmoja kuwa one man show, kila kitu anataka awe fonti fedi sijajua ni kupenda sifa au ni nini

Ndani ya awamu hii ndio tumeshuhudia taifa linaingia kwenye gharama za mauchaguzi uchwara yasiyo na tija kodi za wananchi zinachezewa, wananchi tumefanywa wajinga kupindukia,

Kwahayo machache yapo mengine mengi japo yapo na mambo mazuri yaliyofanyika lakini tunasema asante na yatosha sasa

2020 yafaa kwenda na mtu mwingine naye ni Bernard Membe

Bernard Membe unafaa kutuongpza
Iwe mvua liwe jua tutakua nyuma yako

Hatuwezi tena kuwasapoti watu wasio na shukrani

2020 Twende na BENARD MEMBE✔

#MEMBE_FOR_PRESIDENT2020
Ndugu Mleta maada inaonekana kabisa hujui historian ya nchi hii, na aliyekutuma naye hakukupa data. Kwa taarifa tu Tanzania kutoajili mwaka 1986 -1990 kulikuwa na Structural Adjustment Program (SAP) maelefu ya Watanzania walifutwa kazi na ajira zilisimamishwa kabisa Fact.

Membe aliogombea akashindwa therefore akae pembeni mpaka 2025. Amekuwa waziri kipindi chote cha KJ alifanyia nini Tanzania.
 
January makamba anaweza kuwa tishio kwenu ufipa kwa ccm makamba wakimuondoa chama ndio kinazidi kuimarika badala ya kunyong'onyea
 
Mikwara tu..Ghadafi na JK nani alikuwa na nguvu...Ghadafi kafia kwenye mtaro
Gaddafi hakupambana na mtu mmoja au wawili alishindana na mataifa makubwa wakiwemo wananchi wake
Sasa hii vita ya urais huoni ni nyepesi sana
 
Majanga haya. Leo vijana wa bavicha niwakumpigia debe mwana CCM tena kuwa raisi wa nchi hii kweli? Naapa nakukata tamaa ya kurudi kwenye chama cha upinzani.
Hii ni hatari sana
Nyie wenyewe mmewanunua mkawajaza huko Lumumba.. Unafikiri ukifuga kunguru anageuka kuwa kuku? Sasa wanacheza kote kote. Tulieni dawa iingie.. M4P!
 
Back
Top Bottom