Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Uchaguzi 2020 Urais 2020, CCM twende na Benard Membe. Mwanadiplomasia nguli wa kuivusha Tanzania

Habari za muda mabibi na mabwana!

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza nawashauri wanachama wenzangu na wananchi kwa ujumla. Mwaka 2020 tusipoteze tena kama ilivyotokea mwaka 2015. Haya yote ni kwa sababu hatukutulia vizuri katika mchujo wa kumpata kiongozi bora.

Karibuni kwa maoni yenu.
Si mwingine bali ni yeye mwanadiplomasia mbobezi Cammilius
Mpole mnyenyekevu mtaalam aliyebobea Jasusi
Ana huruma utu uungwana na hana visasi
Hawezi kuonea watu, kuwateka au kuwapiga risasi
Toka Mtukula, Pemba, Kigoma, Ruvuma hadi kule Masasi
Ni Bernard Cammilius atakuza uchumi kwa kasi

Chukua fomu baba muda ukifika nchi upewe
Tumechoka sisi kugeuzwa kuku kuonewa na mwewe
Nchi hii haina tena wa kuiokoa tunakukabidhi mikoba wewe
Tumekandamizwa sana, kubebeshwa zigo la jiwe
Cammilius baba huko uliko ubarikiwe
Tia nia kiongozi, tusonge mbele madhalimu waingiwe kiwewe

Tusamehe 2015 hatukujua ni kipi kitajiri huko mbele
Tukacheza makida, bila kujua tukapiga vigelegele
Sasa tumeshajua kuwa uongozi bora si uwezo wa kufoka na kupiga kelele
bali ni hekima uungwana, kufikiri na si ndulele
Tuliodhani ni wakombozi wanatuletea mambo ya kale
Wanabana kila kona, kila uhuru ili kinyonge watutawale
Taifa la Kambarage eti leo wanatugeuza misukule?
Hapana, Mzee baba kamata fomu tulale nao mbele kwa mbele

Washa moto Cammilius mzee baba tutafanya taifa letu jema tena
Walipoharibu rekebisha, mapya leta, Jamhuri iweze kufana
Sisi ni watu wazima, hawawezi kutugeuza wana
Kututia hofu ndani ya nchi yetu wenyewe, kutugeuza watwana
Watu wanatekwa, watu wanapotezwa, watu wanaokotwa kwenye viroba, mambo ya ajabu sana
Tunataka uhuru wetu, Uchumi, Elimu bora, afya njema, haki ktk nchi hayo ndo mambo ya maana

Tangaza nia kiongozi 2020 tusonge
Tumechoka sisi kugeuzwa wanyonge

N.B
MWANA JF KAMA NA WEWE UNAWEZA KUANDIKA MISTARI TUPIA HAPA
 
ASANTE.
Mkuu vitu vingine unapaswa utafakari sana. Hivi unadhani kwamba Raisi Magufuli kama Mwenyekiti wa CCM atajiweka kwenye mazingira ya CCM kuteua mgombea wa CCM mbadala wake? HUyu Magufuli ninayemfahamu au mwingine? Au hujaona tayari ameshajiwekea mazingira kwamba hilo lisiwezekane hata kidogo?
 
Kiongozi wangu mpendwa, mzalendo namba moja amekuwa akilalamika mara nyingi juu ya uzito wa jukumu la kuongoza taifa. Imefika kipindi alijuta kwanini alibeep. Naamini yeye mwenyewe anatamani kupumzika na atafanya hivyo hapo 2020 japo wengi tutatamani aendelee ila kwakuwa ana maamuzi yake binafsi ni vyema tuheshimu mawazo yake pia. Kwa jinsi tunavyompenda, apumzike tu kwakweli amefanya mengi mazito.
 
kwakweli siipendi CCM lakini pogba simpendi zaidi" Naomba hili suala la membe liwe kweli na ikibidi afaulu katika hili azimio lake"... ccm mlitukosea heshima sana kumpatia nchi huyu mkaanga sumu
Hakuna kitu kizuri kama kuwa na rafiki ambae mnafanana kwa hobby,interest,hisia,chaguzi,vilabu vya michezo na mambo mengine kama hayo.kwa kifupi Mkuu hearly,hii post yako mimi sio tu nimeipenda bali pia nitaitunza kama sala yangu siku ya kupiga kura ya serikali za mitaa,diwani,mbunge na hata rais.Nitayatumia maneno ya post hii kufanya maamuzi muhimu sana ya kuchagua bila kujali kama nitakaye mchagua atatangazwa mshindi ama la.
 
Kafanye utafiti then urudi.Usiongee kitu usichokijua. Bajeti ya jk kwa mwaka ilikua kwenye billion 300+ kwa jpm ni 400+.Sijui ka hili unalijua. Ushawah sikia migomo chuo kikuu kama enzi hizo?
Maandano ya jk yalitawanywa kwa maji ya kuwasha, wakati kichaa anatawanya kwa risasi za moto je ni nani aweza kusogeza pua kwny maandamano yanayotawanywa kwa risasi za moto?
 
Kama mnamuona anafaa mwambieni anzishe chama chake au ahamie CHADEMA ili mumchague 2020
Ila sisi bado tunamuhitaji JPM aendelee kuwanyoosha mafisadi
Wee unaongea Kama nani eti aanzishe chama chake ???? Humu humu. Hahami mtu na kampeni zinaendelea wee Kama hutaki hama wewe.
 
Sio Davids ni Davies
😳
Screenshot_2018-10-29-11-07-36.png
 
Ni jambo la kushitua mno kwamba wafuasi wa Chadema sasa wamegeuka kuwa wafuasi kindaki ndaki wa Bernard Membe na muda wote hakauki midomoni mwao.!

Ikumbukwe Bernard Membe ni mwana ccm lakini anapata mahaba makubwa kutoka chadema kuliko hata kutoka ccm!
Kwa sasa ikitokea Bernard Membe nagombea urais na Freeman Mbowe ,Bavicha wote watamchagua Bernard Membe na kumtosa Mbowe!

Membe kukosa urais inawauma mno Chadema kuliko hata Membe mwenyewe inavyomuuma!

Swali la kujiuliza ,ni nini kimewatokea Bavicha hadi wakawa wafuasi wa kada wa ccm na kuacha viongozi wao wa Chadema?
 
Back
Top Bottom