Urusi, China, Iran na Saudi Arabia zaanza maandalizi ya kuachana na matumizi ya Dola ya Marekani

Urusi, China, Iran na Saudi Arabia zaanza maandalizi ya kuachana na matumizi ya Dola ya Marekani

Matajiri walitoka wapi si kwa biashara tu za kila siku ogopa sana nguvu ya soko
Watarudi wenyew kwenye Dola na Euro ao ni vile wanajitekenya tu mnyama ata habari hana, zaidi ya nchi 50 ulimwenguni tena mataifa yenye nguvu zaidi duniani yako upande wa Dola na Euro itakuwa hizo nchi zinazochechemea
 
Hamna kitu hapo, sasa China biashara zake na nchi za magharibi ambayo ndio kubwa zaidi atafanyaje.

Hata hivyo kumezuka tena wimbi la makampuni ya Marekani kuanza kuondoka tena China, yanafanya "Disinvestment from the communist state."
Mkuu achana na mchina kabisa kwenye swala la business na ubinafsi, ni kama wanaiona kesho. Ukiona mchina karuhusu kampuni ya nje kuwekeza kwao hasa za manufacturing baada ya muda flani lazima nao wanaanzisha business inayofanya biashara sawa na kuzalisha bidhaa kama hii ya muwekezaji na wote wanaofunga biashara zao na kuondoka China wengi unakuta tayari wana rival wa kichina anaezalisha bidhaa kama yake na anaiuza kwa bei ndogo so huyu invester hawezi kushindana sokoni.
 
Hayo makampuni yanaondoka kwa sababu za kisiasa kwa sababu wanahofia kuinuka kwa China kiuchumi na kuwa miongoni mwa mataifa yenye nguvu na ushawishi duniani.

Wanasiasa wa nchi za Magharibi wanawashawishi wamiliki wahamishe viwanda vyao wakidhani watairudisha China nyuma

Ila kiuchumi, kimiundombinu, logistic, kiusalama, stable currency, nishati ya uhakika na soko la uhakika China bado ndo sehemu bora zaidi kwa uwekezaji pale Asia na duniani kuliko hayo mataifa ambayo wanahamishia makampuni yao kama Vietnam, India, Malaysia, Singapore n.k

Pia baadhi ya makampuni yanahama kwa sababu wanakabili ushindani mkali kutoka kwa makampuni na viwanda vya ndani

Jiulize kwa nini serikali ya Marekani imeshindwa kumsawishi Elon Musk akiondoe kiwanda chake cha magari ya Tesla pale Shanghai? Anajua changamoto yake akihama China

"Makampuni yana hama kwasababu ya ushawishi wa na wanasiasa, JIULIZE NI KWANI SERIKALI YA MAREKANI IMESHINDWA KUMSHAWISHI ELON MUSK AKIONDOE KIWANDA CHAKE CHA MAGARI PALE Shang?
Anajua changamoto yake akihama China".

Hiyo ni koment ya mtu mmoja ila ni kama vile kichwani wako wawili wanabishana.JF RAHA SANA🤣🤣
 
"Makampuni yana hama kwasababu ya ushawishi wa na wanasiasa, JIULIZE NI KWANI SERIKALI YA MAREKANI IMESHINDWA KUMSHAWISHI ELON MUSK AKIONDOE KIWANDA CHAKE CHA MAGARI PALE Shang?
Anajua changamoto yake akihama China".

Hiyo ni koment ya mtu mmoja ila ni kama vile kichwani wako wawili wanabishana.JF RAHA SANA🤣🤣
Legeza fuvu hilo uelewe
 
wote wanaofunga biashara zao na kuondoka China wengi unakuta tayari wana rival wa kichina anaezalisha bidhaa kama yake na anaiuza kwa bei ndogo so huyu invester hawezi kushindana sokoni
💯🤝

Niliwaambia hawa jamaa pale juu mojawapo ya sababu ya kuhamisha viwanda ni ushindani mkubwa kutoka kwa viwanda vya ndani
 
JF ina tatizo naandika napost comment inafutika. Narudia kwa ufupi.

China haina demokrasia utawala wake ni chama kimoja, haijawahi kuwa na free general election hata moja, katiba yake haijatengamaa mwaka huu Xi kajibadilisha na kuchaguliwa tena kwa 100% hivi, wakati huo kamfunga Waziri wa Sheria aliyekuwa anapinga kuongezewa muda (kuna wanaJF walidhani ni uwajibikaji wa serikali). Central Bank yao sio independent kuna muda inaamuliwa ifanye devaluation ya RMB wakati $ inakuwa valued na soko. Nchi yao inaongozwa na chama CCP, jeshi na serikali vikiwa kitu kimoja wakati nchi zinazoaminika zinaongozwa na serikali, bunge, mahakama vikiwa independent.
Nchi kama hiyo ni risk kuhifadhi hela kwa sarafu yake. Ushawahi ona oligarchy wa Urusi katunza hela kwenye RMB au benki za China? Si wanatunza Switzerland na kwingine.

China itafanikiwa kufanyia biashara sarafu yake kwa kiasi fulani ila sio sarafu yake kuwa reserve ya nchi nyingine. Kwanza China inakwepa sarafu yake kupatikana sana duniani (kuna athari zinaambatana na fedha yako kuwa widely available).
Huwezi waambia Brazil wadundulize hela waweke akiba kwa sarafu ya China, kesho China wakiibuka wanaona biashara inawapiga chenga wanapunguza thamani ya sarafu, umeweka bilioni 500 zinakuwa bilioni 400 bila sababu za msingi. Au Brazil inatukana China ghafla Xi Jingpin akisema wafungie hawa, hakuna kenge pale CCP anagoma. Bora uko Marekani bunge huru linapitia au benki inaweza goma ikafungua kesi kwenye mahakama huru.

Kuna EU inafanya biashara sana na China, kuna Japan, India na South Korea ni maasimu wa asili wa China na wapo top 10 ya uchumi duniani, bado kuna Marekani yenyewe. Hizi hutoziona zinaitumia RMB, hapo tushaondoa nchi 4 za uhakika kati ya 10 ambazo 6 nyingine karibia ziko EU kina France, UK, Germany, etc. Hapo China anabaki na uhakika wa Russia ambayo ni ya 8 kwa transactions za kibiashara, wakati Marekani ndio ya kwanza kwake.

Na bado Biden mayaimayai yupo, hakai term nyingine huyu. Akija Rais aggressive kama walivyokuwa kina Reagan mtakuja gundua Marekani ina nguvu sana kiuchumi ikiamua. China bado bado tupo na status quo ileile
Good narration
 
Basi kila mahali uwe unaandika na kuzungumza Jamuhuri ya Muungaji wa Tanzania badala ya Tanzania tu.
Acha kupoteza muda.
Nimeuliza ulichoa andika. Japan na Turkey hazipo kwenye maandishi yako.

Official name ndicho kiwakilichi kikuu na wala sio maneno ya kuokoteza yasiyo leta maana yoyote ile ya kueleweka.
 
Back
Top Bottom