Urusi walalamika kuhusu uwepo wa wanajeshi wa Marekani wanaoelekeza namna ya matumizi ya HIMARS

Urusi walalamika kuhusu uwepo wa wanajeshi wa Marekani wanaoelekeza namna ya matumizi ya HIMARS

Mkuu, naomba nikuulize, hivi taifa la Ukraine halikuwahi kuangukia na kufuata sera za urusi?
Kama taifa la Ukraine liliwahi kuwa mfuasi mwaminifu wa sera za urusi, marekani na mataifa ya magharibi yalifanyaje Ili kuirudisha Ukraine ifuate sera za magharibi??
Je marekani na washirika wake waliivamia Ukraine wakiilazimisha ifuate sera za magharibi??..,bila shaka hapana,
Je marekani na washirika wake waliwezaje kuifanya Ukraine awe mfuasi mwaminifu wa sera za magharibi? .., jibu utakalolipata hapa ni USHAWISHI.,kwa nini urusi haamini katika USHAWISHI na badala yake anaona matumizi ya nguvu pekee ndo njia ya kutimiza malengo yake?
Dunia ya Leo haiitaji matumizi ya nguvu Bali USHAWISHI tu,ukishindwa kunishawishi Ili nifuate sera zako,basi kubali maumivu tu,
Mwanamke mwenyewe anaitaji ushawishi Ili uweze kumpata sembuse taifa[emoji848]
Well said, nimekuelewa vizuri, shukrani - kusema kweli pale Ukraine hapakutimika ushawishi hata kidogo,kilicho fanyika pale kilitokana na vyombo vya kijasusi vya magharibi kujipenyeza nchini Ukraine pamoja na NGO za uongo na kweli hao ndio walitumika ku-fund vijana na kuchochea colour revolution,wakawapa mafunzo na kuwalipa snippers wa kulenga shabaha na kuuwa watu - in short creating chaos/turmoil ili nchi hisitawalike, kama unakumbuka hata seneta wa Merikani marehemu McCain na Nulad walikuwa wanafunga safari ya zaidi 3000Km kutoka Merikani kuja Ukraine kuja kuchochea vurugu hizo nchini Ukraine -why Ukraine?? Kilicho fanyika pale ni mapinduzi kuiondoa madarakani Serikali halali iliyo chaguliwa kidemokrasia na sio ushawishi.

Cha ajabu jaribio kama hilo lilipo fanyika mjini Washington DC pale Bungeni, waandamanaji wakilalama kwamba Trump ndiye alishinda kura kwa hiyo ndiye alipashwa kuwa Rais na sio Biden,je,kama wabunge wa Urusi wangefunga safari kuja Merikani kuwaunga mkono waandamanaji,je, Serikali ya Merikani ingesemaje?? Labda tuanzie hapo.
 
umeandika pumba sn yaan bajeti ya Urusi ni mara mbili ya USA hlf atumie 5% ya nguvu yake kupambana na nchi inayosaidiwa na USA na west
Daaaa[emoji2] defence budget US Ni $700b+ Russia ni$69+nb
 
Maana kwamba HIMARS ni too advanced kutumika na wanajeshi wa Ukraine wenyewe bila kuwa na waelekezaji, ni zana ambazo zimesababisha majanga makubwa sana kwa Urusi na kubadilisha mkondo.

Mpaka sasa zimetumika kulipua maghala 50 za silaha za Warusi pamoja na maangamizi mengine, Warusi wanazisaka usiku na mchana, wamezikalia vikao, wamezijadili na kuzilaani ila bado muziki ule ule, na Marekani tayari wanaongeza zingine.

Kuna madude aina nyingi bado Marekani hawajawapa Ukraine, na tayari Urusi wamejichokea, hizi HIMARS ni chombezo tu la kujaribisha uwanja, binafsi hata sikua nafahamu kuna silaha aina hii ya HIMARS.
======================

INTERACTIVE-HIMARS.png



Ukraine said it has used US-supplied HIMARS rocket systems to destroy 50 Russian ammunition depots since receiving the weapons last month, while Russia has claimed its forces destroyed a HIMARS ammunition depot in Ukraine’s Khmelnytskyi region.

Moscow has previously said it has destroyed several of the high mobility artillery rocket systems (HIMARS) supplied to Ukraine by the West, in claims denied by Kyiv.
On Monday, Ukraine’s defence minister Oleksiy Reznikov underlined the growing impact that the HIMARS appear to be having as Ukraine tries to repel Russia’s invasion.

“This cuts their [Russian] logistical chains and takes away their ability to conduct active fighting and cover our armed forces with heavy shelling,” Reznikov said in comments on national television.

Reznikov’s remarks could not be independently verified. Russia did not immediately comment on the claims.

Reznikov said Ukrainian artillery crews had conducted “precise” attacks on several bridges. He gave no details but was apparently referring to three river crossings in the Russian-occupied Kherson region, which local occupation authorities say were attacked by HIMARS over the past week.


Reznikov also said Ukraine had received three Gepard anti-aircraft armoured fighting vehicles, the first of 15 expected, and that Kyiv was expecting to take delivery of several dozen Leopard tanks.

Russia meanwhile says it has destroyed several HIMARS, though Ukraine has denied this. In the latest such report, Russia’s defence ministry said on Monday its forces had destroyed an ammunition depot for HIMARS in the Khmelnytskyi region in western Ukraine.

Ukrainian officials have said repeatedly that Western supplies of weapons are critical to Ukraine’s military effort, and underlined the importance of the HIMARS because of Russia’s artillery supremacy in terms of numbers and ammunition.

HIMARS are a high-tech, lightweight rocket launcher that is wheel-mounted, giving it more agility and manoeuvrability on the battlefield.
Each unit can carry six GPS-guided rockets, which can be reloaded in about a minute with only a small crew.

Analysts say the system has a longer range and is more precise than the Soviet-era artillery that Ukraine had in its arsenal.
Russia has criticised the United States in particular for providing Ukraine with instructors to help Ukrainian forces use HIMARS.
Russia, which invaded Ukraine on February 24, has captured a chunk of territory in southern Ukraine and used its artillery supremacy in the east to make gradual territorial gains.



Cha kushangaza haijasaidia kurudisha maeneo yaliyochukuliwa.
 
Ni kweli, ndio maana walikuwa wamekubaliana na Russia ku-implement makubaliano yao ya Minsk kwa ajili ya kuleta amani baina ya Mataifa yao, sasa ni kitu gani kilicho kuja kutokea baadae? Serikali ya Zelensky wakawa wanavuta vuta miguu -mara leo waseme hili kesho lile wakajenga jeuri na viburi kutokana na ushauri wa mataifa ya magharibi notably Merikani, kwa kifupi hawakutaka makubaliano hayo yatekelezwe ili mwisho wa siku Urusi ilazimike kuingia vitani na Ukraine na hicho ndicho Merikani ilikuwa inakitafuta kwa muda mrefu kupata mwanya wa kihujumu Urusi kwa kutumia watu/taifa lingine sio USA moja kwa moja.

Ukisoma kiundani historia ya foreign policy/plan za Merikani za muda mrefu kuhusu taifa la Ukraine ndio utajuwa ni kwa nini Biden na maneocon wenzake wamelivalia njuga suala la Ukraine, wako radhi hata taifa lao likumbwe na mdololo wa kiuchumi watu wakose ajira ili mradi watimize/tekeleze malengo yao ya siri ya muda mrefu/miaka mingi yenye lengo la kuitumia Ukraine kama stepping stone ya kuihujumu Urusi kiuchumi na kuidhoofisha kijeshi kwa kupitia njia ya ku-fund na kutoa silaha kwa Ukraine ili ipigane a proxy war kwa niaba ya Merikani.

Mkitaka kujuwa undani wa mikakati ya muda mrefu ya Merikani kutaka kuitumia Ukraine kuihujumu Urusi mpaka kuisambaratisha kabisa ili ibaki na vinchi vidogo vidogo ambavyo multinationals ya taifa la Merikani yaje ku-plunder vast natural resources za Urusi - ni hilo tu,lakini hapa watazuga eti wanajali sana Ukraine na raia wake ,demokrasia na human rights -ulaghai mtupu.Mkitaka kujuwa undani wa kwa nini vita ya Ukraine inavaliwa njuga hasa hasa na Merikani, tafuteni kitabu kilicho andikwa na Prof. Zbigniew Brzezinski title ya kitabu ni: "The Grand Chessboard" kinazungumzia masuala ya Eurasia,lakini msikilizeni kwa umakini anazungumzia nini kuhusu taifa la Ukraine.

Watu hawajui tu, lakini ukweli wa mambo vita hii imechochewa na Merikani yenyewe kwa kushirikiana na NATO, hata Papa alizungumzia ukweli huo - Marekani walimshikiza Zelensky hasikubaliane na Urusi kuhusu Minsk accord, huku NATO ikiendeleza mazoezi ya kijeshi mipakani mwa Urusi, kibaya zaidi NATO hawataki kusikiliza concerns za Urusi kuhusu hakikisho la usalama wa Taifa lao kutoka kwa viongozi wa NATO, huku Merikani ikimwambia Zelensky asogeze majeshi yake na silaha kali ili wavamie majimbo ya mashariki mwa Ukraine yenye wakazi wengi wenye asili ya Urusi, vile vile na kuivamia Crimea nia hasa kuwauuwa kwa wingi Waukraine wenye asili ya Urusi, kwa bahati nzuri Warusi walipewa fununu za mpango huo ndio maana Warusi waka wawahi jeshi la Ukraine kwa execute a pre emptive strike, katika operation hii Warusi wako justified kabisa. Watu hawajui tu, lakini kuanzia 2014 mpaka sasa jeshi la Zelensky lilisha wapiga risasi na mabom Waukraine wenye asili ya Urusi zaidi 14,000 wakapoteza maisha, yaani Zelensky anarudia makosa yale yale kwa kumuiga Hitler's "final solution" operation aliyo wahi kuitumia kuwamaliza wayahudi kwenye gasi chambers wakati wa WW2.

Cha ajabu mauuaji hayo ya Waukraine 14,000 wenye asili ya Urusi hatujawahi kusikia hata siku moja USA na media zake zikikemea mauuaji hayo, masaa yote kumsema sema vibaya Putin!!
Inawezekana umesoma vitu vingi ila kuviunganisha upate hoja ndio tatizo lilipo. Ilibidi ueleze sababu za hao Waukraine wenye asili ya Urusi kuuwa ni zipi. Kwa kifupi ni kuwa, Urusi haiamini kama ni taifa huru, ndio maana hata hii vita ilipokuwa inaanza Mandonga (Putin)alisema anataka kusahihisha makosa ya kihistoria (kuirudisha Ukraine kuwa sehemu ya Urusi).
Ikumbukwe kwenye 2014 Urusi iliitwaa Crimea kwa nguvu kutoka Ukraine. Ili kuendeleza mipango yake miovu, akapandikiza mamluki kwenye majimbo ya Donesk na Luhansk ambayo yana raia wengi wanaoongea Kirusi. Mamluki hawa wamekuwa wakipewa Mafunzo na silaha kutoka Urusi ili wapambane na Serikali ya Kyiv kwa ajili ya kujitenga.
Hakuna taifa ambalo linaweza kuruhusu baadhi ya maeneo yake kujitangazia uhuru kienyeji namna hii. Urusi mwenyewe alitumia vita wale Chenchen walipotaka kujitenga kutoka Urusi, Nigeria iliwahi kupigana vita vya Biafra kwa ajili hii, mtiti wa Catalan tuliuona.
Hawa waasi wanaozungumza Kirusi ndio walikuwa wanauawa kutokea 2017 kutokana na uasi wao. Ati Urusi alienda kuwalinda waasi dhidi ya Serikali halali ili uasi ukamilike vizuri. Mandonga aache janjajanja zake.
 
Leo Pekee kuna Mji Umepigwa chakari ni maghala ya hizo Himars aliyanunu tajiri mmoja wa Ukraine nae kajumlishwa anaitwa Vadatusrsky....
 
Nikiikumbuka asikari wa parachute walivyokuwa wanatua kama mvua pale Kyiv na hatimaye wakafyekwa wote [emoji848][emoji848]..,alafu anatokea mtu anakwambia kuwa urusi hakuwa na lengo la kuiteka Kyiv Wala kuipindua serikali ya zelensiky [emoji848]..,bila aibu mtu anakwambia kuwa urusi aliondoka pale Kyiv kwa makubaliano maalum [emoji848]..,nawaangalia nasema hiiiiiii! Baghosha..,all in All urusi anavuna alichopanda, operesheni ya saa 72 imegeuka vita ya mda mrefu [emoji848]
Video please
 
Sijasema kwamba HIMARS hizifanyi kazi ninacho sema mimi ni kwamba uwezo wa GPS Guided Rockets hizo ni highly exaggerated na Mrusi atazipatia dawa muda si mrefu kuanzia sasa, hilo la kwanza; la pili: HIMARS zimewahi kutumika huko Syria na Wamerikani wenyewe na Waasi waliokuwa wanampinga majeshi ya Assad -sasa swali ni, je, zilishia wapi au zilisaidia nini katika efforts za waasi na Merikani za kutaka kumuondoa Assad madarakani (Regime change) hazikusaidia kitu ndio maana mpaka sasa Assad bado yupo madarakani.

Kitu kingine, HIMARS vile zilitumiwa sana na majeshi ya Marekani huko Afghanistan lakini hazikuleta mabadiriko yoyote kwenye mwenendo mzima wa vita nchini Afghanistani bado ma Mullahs waliwafanya marafiki zako wakatimua mbio kuliko Kip Keino na Ben Gipcho, oh yes, the Talibans scared a living daylights out of them Gringos - strange, don't you think?

Mifano hiyo michache ndio inifanya niamini kwamba contrary na adithi za Abunwasi zilizo jaa kwenye mitandao ya kijamii Dunia nzima HIMARS haziwezi kuwa a game changer kwenye vita hii ya Ukraine,Urusi bado itashinda to, come rain or shine na kikubwa zaidi ataendelea kuteka maeneo mengine ya Ukraine. Zelensky hasikubali kuendelea kudanganywa na Biden, akubali kukaa meza moja na Putin wasitishe vita na watekeleze maazimio ya Minsk - Ukraine hawezi kushindana na Super power washauri wa Uncle SAM wasikupotoshe wao wanashabikia vita hii ili wauze silaha wanatamani hata viendelee zaidi ya miaka kumi ili wapige hela ndefu, hawajali chochote kuhusu Ukraine wala raia wake, sijui kama Zelensky analitambuwa hilo naona yuko busy anapigwa picha akiwa na mkewe kwa ajili ya cover la Vogue Magazine hana habari kwamba nchi yake hipo vitani!!
Kulinganisha US kutumia HIMARS Afghanistan na Ukraine kutumia HIMERS dhidi ya Urusi ni vitu viwili tofauti. Hizi HIMERS kwa kiasi kikubwa naona zinalenga military infrastructures na kuziharibu. Taleban kwa kiasi kikubwa hawakuwa na military hardware za kushambulia, wala walikuwa walikuwa hawapigani conventional war, walikuwa na bunduki na wanashambulia kwa kuvizia na kurudi majumbani. Hapo HIMERS haziwezi kuwa na matokeo makubwa.
Kwa vita ya Ukraine, Urusi ana vifaa vingi na vikubwa vya kijeshi pamoja na miundombinu wezeshi. Hivyo matokeo ya HIMERS yataonekana vizuri tofauti na huko Afghanistan.
 
Ni suala la muda tu - HIMARS hutazisikia tena, kumbukeni Drones za Utruki huko Ukraine zilivyo shughurikiwa na air defense system za Russia hivyo Drone hizo siku hizi hazitambi tena - mwarobaini wa HIMARS bado huko jikoni unachemka muda si mrefu zitakumbwa na kisago cha nguvu, pia mamuluki wa Kimerikani wanao tumiwa kuzifyatua nao watapelekwa jehanamu watake wasitake.

Kumbukeni kwamba Urusi kitu ingine kabisa omba uwasikie kwenye radio tu, watu hawajui kwamba nguvu ya Urusi ya kijeshi inayo tumika kwenye operation hii nchini Ukraine ni asili mia 5% ya nguvu halisi ya Russian miIitary - kama Putin ange hamua kufanya kweli, saa hizi tungelikuwa tunazungumza mengine kabisa kuhusu Taifa la Ukraine.

Zelensky hasijifanye kichwa ngumu, atumie hekima na busara afanye mazungumzo na Putin ili kusitisha vita atekeleze makubaliono yao ya Minski hasikubali ushauri mbovu anaopewa na Biden na wapambe wake wachumia tumbo.

Zelensky akumbuke kwamba hata apate misaada lukuki kutoka magharibi hataweza kushinda vita hii, badala yake Taifa lake litazidi kuharibiwa vibaya sana na raia wengi kupoteza maisha, vile vile majirani zake wana mpango wa kuimega Ukraine vipande vipande: mashariki itamegwa na Urusi na actually wamekwisha anza mchakato wa kutwaa majimbo yote ya mashariki ,majimbo ya magharibi Poland na Romania ziko mbioni kuyamega, mwisho wa siku Ukraine itabakiwa na jimbo la Kiev tu, basi.
HIMARS ni zao la zamani sana, sio la New Millenium ni la 20th century ila laisumbua systems za 21st century
 
Package ya msaada inayofuata ya $280mil kutoka USA ina siraha za high and very advanced technology nyingi. Wa Ukraine wengi wapo Marekani wakipata maujuzi ya kuzitumia
Si hivyo tu, bali silaha advanced lazima wamarekani wawepo ili kuzuia kuuzwa kwa Urusi
 
Yaani hata mimi nakuunga mkono,Urusi ilitakiwa within 7 days iwe tayari imemaliza vita .Vita ikichykua muda mrefu adui anakusomal na hata kama ni nunda atakushinda tuu kwa sababy umejiaminin sana.
UK asingekubali Ukraine kudondoka, ndo maana alikuwa wa kwanza kabisa kupeleka silaha
 
Kwanini umeongea pumba leo mkuu au so wewe?., ata Russia akija kupata plan ya kuzuia HIMARS za Marekani maelfu mangapi ya askari wake watakuwa wamekufa., unadhan putin ataendelea kutojali askari wake kuuliwa? ndio mana saiv amepoa na kutafuta namna yoyote vita iishe.

America ni wanyama wa dunia ukitoa hizo HIMARS wataleta kubwa yake pia mwache putini akurupuke na silaha zake za kizamani, saiv tunaelezwa anaomba msaada wa silaha kutoka Iran
Kiuhalisia Marekani ana uzoefu sana, yeye vitani haendi jaribisha, anaenda piga
 
Kulinganisha US kutumia HIMARS Afghanistan na Ukraine kutumia HIMERS dhidi ya Urusi ni vitu viwili tofauti. Hizi HIMERS kwa kiasi kikubwa naona zinalenga military infrastructures na kuziharibu. Taleban kwa kiasi kikubwa hawakuwa na military hardware za kushambulia, wala walikuwa walikuwa hawapigani conventional war, walikuwa na bunduki na wanashambulia kwa kuvizia na kurudi majumbani. Hapo HIMERS haziwezi kuwa na matokeo makubwa.
Kwa vita ya Ukraine, Urusi ana vifaa vingi na vikubwa vya kijeshi pamoja na miundombinu wezeshi. Hivyo matokeo ya HIMERS yataonekana vizuri tofauti na huko Afghanistan.
Afu mwambie Taliban walikuwa wanatumia raia kama kinga
 
Hizo zote ni propaganda, tulishaona nia ovu za Russia kwa majirani zake kuanzia Georgia mpaka hapo Ukraine, acheni kuibebesha uchafu Marekani.
Mkuu hizi akili sijui pro russia huwa wanatoa wapi nadhani hata Putin akiwasikia atashangaa.

Wakati hii the so called operation inaanza walivyoanza ku mobilize vikosi walisema wako kwenye mazoezi US akaiambia dunia kwamba russia ana mpango wa kuivamia Ukraine ajabu wakapinga hawana nia hiyo siju kadhaa wanaingiza jeshi ukraine western allies wote walijua ndio basi Putin kashachukua ukraine yote to their suprise wakagundua kumbe ukrainians hawako tayari kuchukuliwa kirahisi na wana morali ya kupambana ndio kama unakumbuka support ilianza kutolewa baadae mpaka watu humi wakawa wanasema US anaogopa kumpa silaha ukraine.

Ajabu mrusi wa sokomatola anasema western ndio walitaka vita. Kama kawaida mambo yameanza kuwa magumu anabebeshwa mzigo US ambae ana support tu wakati walionza kuvamia nchi ni wao.
 
Mkuu, naomba nikuulize, hivi taifa la Ukraine halikuwahi kuangukia na kufuata sera za urusi?
Kama taifa la Ukraine liliwahi kuwa mfuasi mwaminifu wa sera za urusi, marekani na mataifa ya magharibi yalifanyaje Ili kuirudisha Ukraine ifuate sera za magharibi??
Je marekani na washirika wake waliivamia Ukraine wakiilazimisha ifuate sera za magharibi??..,bila shaka hapana,
Je marekani na washirika wake waliwezaje kuifanya Ukraine awe mfuasi mwaminifu wa sera za magharibi? .., jibu utakalolipata hapa ni USHAWISHI.,kwa nini urusi haamini katika USHAWISHI na badala yake anaona matumizi ya nguvu pekee ndo njia ya kutimiza malengo yake?
Dunia ya Leo haiitaji matumizi ya nguvu Bali USHAWISHI tu,ukishindwa kunishawishi Ili nifuate sera zako,basi kubali maumivu tu,
Mwanamke mwenyewe anaitaji ushawishi Ili uweze kumpata sembuse taifa[emoji848]
Atakuwa amekuelewa,
 
Back
Top Bottom