Urusi yapendekeza makao makuu ya UN yaondolewe Marekani na kuhamishiwa nchi nyingine

Urusi yapendekeza makao makuu ya UN yaondolewe Marekani na kuhamishiwa nchi nyingine

HERY HERNHO

Senior Member
Joined
Mar 4, 2022
Posts
110
Reaction score
458
4bv75dc7f163281m87d_800C450.jpg


Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema pendekezo la kuhamisha makao makuu ya Umoja wa Mataifa kutoka New York hadi nchi nyingine ni wazo zuri na linafaa kuzingatiwa.

Sergei Lavrov, ambaye yuko mjini New York, amewaambia waandishi wa habari kando ya mkutano usio rasmi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa: "Itakuwa vyema sana ikiwa Umoja wa Mataifa utahamisha makao yake makuu kutoka New York na kuupeleka mahali pengine popote".

Kuhusiana na suala hilo, Dmitry Peskov, msemaji wa Ikulu ya Kremlin, amesema wazo la kubadilisha makao makuu ya Umoja wa Mataifa kutoka New York hadi nchi nyingine linaweza kutathminiwa.

Akizungumzia tatizo la utoaji viza linalosababishwa na Marekani kwa jumbe za kidiplomasia na timu za vyombo vya habari vya nchi mbalimbali, msemaji huyo wa Kremlin amesema: Russia haiko peke yake katika tatizo la utoaji wa viza unaokwamishwa na Marekani ikiwa ni mwenyeji katika Umoja wa Mataifa.

Kuhusu hatua ya kutowapatia viza waandishi wa habari wa Russia wanaokusudia kwenda kufanya kazi katika Umoja wa Mataifa, Peskov amesisitiza kwa kusema: "hili ni suala linalohitaji majadiliano mazito na nchi ambazo, nazo pia zinalalamikia vikali suala hili".

Kabla ya hapo, waziri wa mambo ya nje wa Russia Sergei Lavrov aliielezea kuwa ni ujinga hatua ya Marekani ya kukataa kutoa viza kwa waandishi wa habari wa Russia.
 
Yupo sahihi kabisa, waandishi walikuwa waende kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa na sio Marekani. Sasa kisa Umoja upo Marekani basi wanajichukulia sheria mkononi bila kufuata taratibu za Umoja wa Mataifa. Zikiamishwa itatuliza kelele za USA, ingawa Marekani anaweza kuweka pingamizi maana nikama kumnyang'anya madaraka aliyojipa dhidi ya mataifa mengine.
 
Yupo sahihi kabisa, waandishi walikuwa waende kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa na sio Marekani. Sasa kisa Umoja upo Marekani basi wanajichukulia sheria mkononi bila kufuata taratibu za Umoja wa Mataifa. Zikiamishwa itatuliza kelele za USA, ingawa Marekani anaweza kuweka pingamizi maana nikama kumnyang'anya madaraka aliyojipa dhidi ya mataifa mengine.
Yupo sahihi ila kuhamisha makao makuu haitomkomoa Marekani. World Health Organisation makao makuu ni Geneva ila mchangiaji na mwenye maamuzi makubwa ni Marekani, World Trade Organization nayo HQ ni Geneva ila dunia inatumia $ kama reserve na transactions nyingi zinafanyika kwa hiyo sarafu, Food and Agriculture Organization ina HQ Rome, Italy ila sijawahi sikia hata siku moja Italy wanakaririwa wakiongea lolote kuhusu chakula duniani. Wala hutowaona wanachangia au kujihusisha na chakula, wala sio wazalishaji wakubwa.
 
Tanzania kwa kuwa ni nchi ya Amani Duniani sidhani kama tunaweza kukosa kuingiza kwenye 10 bora ya mataifa yatakayopendekezwa kuwa makao makuu ya UN.

Haya tena, wanadiplomasia wa kitanzania uwanja ni wenu sasa kuhakikisha UN inahamia Dodoma.... Russia wameisha fungua Pandora Box ☑️🎁
 
..catch ni money 💰 🤑 💸!,USA inachangia almost 35%ya kuendesha hii UN!,itahamishiwa nchi gani itakayokua na uwezo to bankrolls UN?,tujiulize Tanzania tunadaiwa kiasi gani cha michango yetu kule SADC, AU, na UN, then tujadili hoja hii kisayansi
 
View attachment 2599432

Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema pendekezo la kuhamisha makao makuu ya Umoja wa Mataifa kutoka New York hadi nchi nyingine ni wazo zuri na linafaa kuzingatiwa.

Sergei Lavrov, ambaye yuko mjini New York, amewaambia waandishi wa habari kando ya mkutano usio rasmi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa: "Itakuwa vyema sana ikiwa Umoja wa Mataifa utahamisha makao yake makuu kutoka New York na kuupeleka mahali pengine popote".

Kuhusiana na suala hilo, Dmitry Peskov, msemaji wa Ikulu ya Kremlin, amesema wazo la kubadilisha makao makuu ya Umoja wa Mataifa kutoka New York hadi nchi nyingine linaweza kutathminiwa.

Akizungumzia tatizo la utoaji viza linalosababishwa na Marekani kwa jumbe za kidiplomasia na timu za vyombo vya habari vya nchi mbalimbali, msemaji huyo wa Kremlin amesema: Russia haiko peke yake katika tatizo la utoaji wa viza unaokwamishwa na Marekani ikiwa ni mwenyeji katika Umoja wa Mataifa.

Kuhusu hatua ya kutowapatia viza waandishi wa habari wa Russia wanaokusudia kwenda kufanya kazi katika Umoja wa Mataifa, Peskov amesisitiza kwa kusema: "hili ni suala linalohitaji majadiliano mazito na nchi ambazo, nazo pia zinalalamikia vikali suala hili".

Kabla ya hapo, waziri wa mambo ya nje wa Russia Sergei Lavrov aliielezea kuwa ni ujinga hatua ya Marekani ya kukataa kutoa viza kwa waandishi wa habari wa Russia.
Wayakete Arusha.

Hatufungamani na mbabe yeyote
 
View attachment 2599432

Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema pendekezo la kuhamisha makao makuu ya Umoja wa Mataifa kutoka New York hadi nchi nyingine ni wazo zuri na linafaa kuzingatiwa.

Sergei Lavrov, ambaye yuko mjini New York, amewaambia waandishi wa habari kando ya mkutano usio rasmi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa: "Itakuwa vyema sana ikiwa Umoja wa Mataifa utahamisha makao yake makuu kutoka New York na kuupeleka mahali pengine popote".

Kuhusiana na suala hilo, Dmitry Peskov, msemaji wa Ikulu ya Kremlin, amesema wazo la kubadilisha makao makuu ya Umoja wa Mataifa kutoka New York hadi nchi nyingine linaweza kutathminiwa.

Akizungumzia tatizo la utoaji viza linalosababishwa na Marekani kwa jumbe za kidiplomasia na timu za vyombo vya habari vya nchi mbalimbali, msemaji huyo wa Kremlin amesema: Russia haiko peke yake katika tatizo la utoaji wa viza unaokwamishwa na Marekani ikiwa ni mwenyeji katika Umoja wa Mataifa.

Kuhusu hatua ya kutowapatia viza waandishi wa habari wa Russia wanaokusudia kwenda kufanya kazi katika Umoja wa Mataifa, Peskov amesisitiza kwa kusema: "hili ni suala linalohitaji majadiliano mazito na nchi ambazo, nazo pia zinalalamikia vikali suala hili".

Kabla ya hapo, waziri wa mambo ya nje wa Russia Sergei Lavrov aliielezea kuwa ni ujinga hatua ya Marekani ya kukataa kutoa viza kwa waandishi wa habari wa Russia.
Hahaha..
Wanapeleka mashushushu kama journalists wanataka waruhusiwe?!!!

Halafu yaweza kuwa kisasi maana Russia bado wanamshikilia mwandishi wa US kwa shutuma za kumbambikizia...

"Russian officials are upset that United States visas haven't been issued to Russian reporters amid ongoing efforts by the U.S. to push for the release of Evan Gershkovich, a journalist with The Wall Street Journal who was detained by Russia's Federal Security Service (FSB) at the end of March over espionage allegations..."
 
Back
Top Bottom