Usajili wa ‘Kanisa la Neema’ uchunguzwe

Usajili wa ‘Kanisa la Neema’ uchunguzwe

Siandiki ili kupinga uanzishwaji wa makanisa, naandika jambo ambalo kama halitashughulikiwa mapema, kuna siku litaleta matatizo, tena yawezekana yakawa matatizo makubwa sana.

KANISA LA NEEMA la mume wake na grace zoazoa vipodozi, limekuwa kero, linatukana na kupotosha Biblia na amekuwa akigombana na wachungaji wote Tanzania, sema tu kwasababu hawaji hewani kuongea, ila kuna kitu kinafukuta ndani kwa ndani ambacho kinatakiwa kupewa dawa urgently.

Tanzania kuna uhuru wa kuabudu, as long as umefuata sheria na miongozo iliyowekwa. Jambo hili limekuwa limechukuliwa kama uchochoro kwa matapeli wengi kukusanya watu ili aidha kujipatia utajiri kutoka kwao, au kwa malengo yao yoyote wayajuayo kwa kigezo kwamba Serikali haitakiwi kuingilia kati.

Majority ya victims, ni wanawake na watu masikini na wasiosoma...those people who have been stricken with problems na wanaenda kwao kama njia ya kutafuta msaada, badala yake wao wanatake advatage kuwafanya kitega uchumi.

USHAURI WANGU KWA SERIKALI
1. Kanisa la Kibwetele lilianza hivihivi, mwisho wa siku aliua watu zaidi ya 100 Uganda

2. Tuhakikishe Makanisa yanafunguliwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria. asiyefuata huo utaratibu, ashughulikiwe.

3. hata yale makanisa ambayo tayari yameshapewa vibali, yachunguzwe kuona kama wanacomply.

4. Viongozi wengine wa dini kwenye kamati zao wahusishwe katika kila kada. mfn. Wapentecost wanao umoja wao, waprotestant wengine wanao umoja wao, katholic etc, kama mtu hayupo kwenye aina hizo zote za Makanisa, basi aeleze yeye kanisa lake ni la aina gani ili asije kuleta migogoro isiyo ya lazima.

5. Kuna uzembe na rushwa nyingi sana zinafanyika kwenye ofisi ya usajili wa haya makanisa. mfn. haiji kichwani Nabii Suguye, amekuwa na kanisa miaka kadhaa yote hiyo, hadi ameanza kuomba nywele za utosini, kucha kidole kidogo n.k ilikuwa bado kidogo aagize walete nywele za sehemu za siri manake alishaanza kufundisha namna ya kufanya ngono madhabahuni. hapo ndio wakashtuka, muda wote huo kumbe kanisa lake halikuwa na usajili. INAKUWAJE MIAKA YOTE HIYO MTU ANAOPERATE KANISA BILA USAJILI?

6. kuna kanisa moja linaitwa KANISA LA NEEMA, ni la mzee wa Neema. huyu ni mme wake yule grace zoazoa anayetengeneza sabuni na vipodozi bila kuwa na elimu yeyote ya kemikali. Wakristo karibia wote Tanzania wamekuwa wakimlalamikia huyu mtu kwasababu mahubiri yake yote, ni kupindua Biblia hadi haijulikani kama yeye ni Mkristo au wa dini gani. amefungua pia tv, na anayo night club kama kanisa. ni wazi yeye anasema sio mpentecost, sio mkatoliki, sio wa dhehemu lolote, SASA HATUJUI AMEJISAJILI KWENU KAMA NANI. mtu huyu anakwaza ukristo, ana potosha mengi ambayo tunaogopa kuna siku isijetokea watu wasio na Mungu moyoni wakamdhuru, na pia anakosesha sana amani katikati ya watu kwasababu ya mafundisho yake. tunaomba chunguzwe ili kuona kama ana elimu yeyote ya dini, ametumwa na nani manake hadi anamiliki television ya TOP PLUS anagarimia vipi n.k. ni ushauri tu.

7. Tunaomba Serikali pamoja na kuwapa vibali/usajili, iwaangalie kwa jicho la karibu hao mitume na manabii wa kisasa, hao wanaouza mafuta, maji nk. wanafanya biashara kama biashara zingine tu kwa Jina la dini. iangalie usajili wao, hao kina mwamposa, ngurumo ya upako wanaogawa pesa hata hazijulikani zinatoka wapi, mzee wa upako na wengine wengi. HIVI KWELI HAWA WAMESAJILIWA?

8. kama Nabii Suguye, mzee wa ibada za nywele na kucha, amefungiwa kanisa hadi arekebishe usajili wake, ni kwali kwamba hao mitume wengine ambao ni contraversual wamesajili makanisa yao? au kwasababu wana pesa kama kina mwamposa?.

9. kama suguye aliexist miaka yote hiyo, tunajuaje kama hawapo wengine ambao anaamka tu asubuhi anaanzisha kanisa na kukusanya hela kwa maskini? bila hata kupitia serikalini.

Mambo haya nimeandika wengine wanaweza kufikiri nina bifu nao, sina, ila ni alart tu kwa serikali, isijekuja kushtuka shuka kukiwa kumekucha.

Wasalaam!

Yule jamaa ana mafundisho mabaya sana. Halafu anaona wengine wajinga na kuwadharau. Mtu unasemaje kwamba. Hakuna dhambi, dhambi ilishamalizwa?. Anaipinga Biblia waziwazi na kusema kuna kitabu kingine kitakuja huko mbeleni .

Sasa si ajitoe kwenye ukristo aanzishe dhehebu lake nje ya ukristo au dini yake. Mtu anafundisha mambo tofauti na ukristo na kuwaona wasiokubaliana naye ni wajinga. Ninachoshukuru pamoja na kelele zake zote , wakristo hawana muda naye kama walivyompuuza Mfalme Zumaridi.
 
imagine leo mtu anasimama anaasema, BIBLIA NI KITABU TU kama vitabu vingine. anachukua kil akilicho kwenye Biblia, anageuza kuongea kinyume chake na anasambaza kwa tv. haya mambo yanakwaza sana Wakristo, kupita kiasi. hadi wamemtungia jina kuwa anaitwa MPINGA KRISTO. lakini serikali bado tu inamwangalia mtu aliyejifanya anamhubiri Kristo lakini anahubiri upinga Kristo.
Mimi sijaona kosa lake otherwise kama mnataka yale yale ya kanisa katoliki kupinga wale wote waliokuwa wanataka kufundisha tofauti na walichokuwa wanafundisha wao.
Hata zumaridi walimwonea tu. Maana yeye hakuna sehemu aliwahi sema ni mkristo.
 
Pale Kongowe Mbagala Mpakani mwa Dar na Mkuranga Pana she'll pembeni Pana Kanisa na Msikiti vimedumu kwa miaka mingi sana bila mgogoro wowote! So long sio ardhi ya Msikiti kanisa linatumia au Msikiti unatumia ardhi ya kanisa hakuna tatizo wewe ndio una tatizo!

Ukifika KAMATA makutano ya barabara ya Nyerere na Ile ya chang'ombe kama unaenda mjini kabla ya daraja upande wa kulia Pana Kanisa na Msikiti na vimetenganishwa na ukuta tu miaka mingi sana sana na hukujawahi kutokea mgogoro au mtafaruku.

Msikiti wa Kichangani na kanisa la kilutheri magomeni vimetenganishwa na morogoro road na Wala hakuna shida Ibada unaendelea huku na kule bila shida.

Huku mitaani tumewekeana mipaka wakristo na waislamu Wala hakuna shida!
Maofisini na sehemu za mikusanyiko tunakaa pamoja bila shida yoyote na kubwa zaidi tunazikana kama ndugu!

Kuna Sehemu Moja Huko Rombo Kilimanjaro waislamu walitoa sehemu ya eneo lao Ili pajengwe kanisa katoliki na likajengwa!

Punguza chuki kama hakuna chochote mnaingiliana au kuhitilafiana wakati wa Ibada !
Asalam
kwa kifupi, kama msikini na kanisa vinakaa pamoja na hakuna shida, sio taabu. wala hakuna mwenye chuki na uislam au ukristo kwenye hili. rudi kwenye mada, makanisa ambayo hata mlevi akiwaona anaona wazi kabisa kwamba ni wapigaji, wanawatapeli raia, serikali ikae kimya? au wewe ni mmojawapo. kuna siku watakuja kukuomba unyoe mavvuzi uwapelekee wakuombee na jinsi mlivyoshikwa akili, utapeleka.
 
Mimi sijaona kosa lake otherwise kama mnataka yale yale ya kanisa katoliki kupinga wale wote waliokuwa wanataka kufundisha tofauti na walichokuwa wanafundisha wao.
Hata zumaridi walimwonea tu. Maana yeye hakuna sehemu aliwahi sema ni mkristo.
huoni kosa kwasababu unasali kwake, umeshashikwa masikio. hujielewi. mtu anayetukana ukristo, mtu anayetukana biblia, na anajiita ni mchungaji, kweli huoni kosa? hujui kuna wananchi wengine akili zao sio nzuri kuna siku wanaweza kumshughulikia? wewe kama kiongozi mfano, unachukua hatua gani kuzuia madhara ya mbeleni?

pia, unajua kama amesajili kanisa? kama hajasajili hapo hakuna kosa? kwahiyo hata zumaridi matendo kama yale ni ya kikanisa? akili zenu zote mmewapa mitume mmebaki makopo.
 
kwa kifupi, kama msikini na kanisa vinakaa pamoja na hakuna shida, sio taabu. wala hakuna mwenye chuki na uislam au ukristo kwenye hili. rudi kwenye mada, makanisa ambayo hata mlevi akiwaona anaona wazi kabisa kwamba ni wapigaji, wanawatapeli raia, serikali ikae kimya? au wewe ni mmojawapo. kuna siku watakuja kukuomba unyoe mavvuzi uwapelekee wakuombee na jinsi mlivyoshikwa akili, utapeleka.
Hata kuna watu wengine wanaona mwamposa mpigaji, wakatoliki na sadaka zao wapigaji.
Kwa hiyo kama mtazamo wa watu fulani ndio utahukumu kanisa fulani basi bila shaka yote yatafungwa.
 
huoni kosa kwasababu unasali kwake, umeshashikwa masikio. hujielewi. mtu anayetukana ukristo, mtu anayetukana biblia, na anajiita ni mchungaji, kweli huoni kosa? hujui kuna wananchi wengine akili zao sio nzuri kuna siku wanaweza kumshughulikia? wewe kama kiongozi mfano, unachukua hatua gani kuzuia madhara ya mbeleni?

pia, unajua kama amesajili kanisa? kama hajasajili hapo hakuna kosa? kwahiyo hata zumaridi matendo kama yale ni ya kikanisa? akili zenu zote mmewapa mitume mmebaki makopo.
Mimi sisali kwake kwanza nimemsoma kwenye thread hii.
As long as hajaua anafundisha maono yake fresh tu. Otherwise makanisa yaliyotangulia hapa nayo yangesema haya makanisa ya kuja yasiwepo mwanzo yanapotosha mafundisho.
 
imagine leo mtu anasimama anaasema, BIBLIA NI KITABU TU kama vitabu vingine. anachukua kil akilicho kwenye Biblia, anageuza kuongea kinyume chake na anasambaza kwa tv. haya mambo yanakwaza sana Wakristo, kupita kiasi. hadi wamemtungia jina kuwa anaitwa MPINGA KRISTO. lakini serikali bado tu inamwangalia mtu aliyejifanya anamhubiri Kristo lakini anahubiri upinga Kristo.

Yule anatakiwa akatazwe kutumia Biblia atumie kitabu chake. Mtu amekaa kuikosoa Biblia kila saa. Ila nachoshukuru watu hawana time naye, wamempuuza amebaki kudanganya wasiojitambua. Unajiita mkristo halafu unadai hakuna dhambi duniani, hivyo watu wazini wabake nk.
 
Yule jamaa ana mafundisho mabaya sana. Halafu anaona wengine wajinga na kuwadharau. Mtu unasemaje kwamba. Hakuna dhambi, dhambi ilishamalizwa?. Anaipinga Biblia waziwazi na kusema kuna kitabu kingine kitakuja huko mbeleni .

Sasa si ajitoe kwenye ukristo aanzishe dhehebu lake nje ya ukristo au dini yake. Mtu anafundisha mambo tofauti na ukristo na kuwaona wasiokubaliana naye ni wajinga. Ninachoshukuru pamoja na kelele zake zote , wakristo hawana muda naye kama walivyompuuza Mfalme Zumaridi.
anatakiwa asiwe amejisajili kama mkristo, kwasababu matendo yake yote yanapinga ukristo na yanakwaza ukristo na wakristo wote. swali ni je, aliposajili kanisa lake, kama kweli amesajili, alijisajili kama Mkristo? wa dhehebu gani, au anaanzisha dhehebu jipa n.k. shida ni kwamba, ofisi ya usajili kuna watu wazembe kupita kiasi kuna siku hapa yatatokea ya kibwetele na tutabaki midomo wazi. serikali kwanza ianze kuwajibisha watendaji pale kwenye usajili, iweke wale walio makini wanaosajili kanisa na kuanza kulifuatilia kama linaendana na minajili iliyoomba usajili.
 
kwa kifupi, kama msikini na kanisa vinakaa pamoja na hakuna shida, sio taabu. wala hakuna mwenye chuki na uislam au ukristo kwenye hili. rudi kwenye mada, makanisa ambayo hata mlevi akiwaona anaona wazi kabisa kwamba ni wapigaji, wanawatapeli raia, serikali ikae kimya? au wewe ni mmojawapo. kuna siku watakuja kukuomba unyoe mavvuzi uwapelekee wakuombee na jinsi mlivyoshikwa akili, utapeleka.
Hahahaaa Mimi huyu? Nimerespond kwenye mfano WAKO wa ifakara na lawama zako juu ya wizara ya ardhi!
Kuhusu makanisa uchwara kwakweli labda wizara ya mambo ya Ndani ikae tena upya na kupitia sheria na kanuni za usajili wa hivyo' vikundi mana sio makanisa kanisa Lina hadhi yake kitaasisi, kiundeshaji HATA publicity! Naungana na Wewé lazima tuoitie Sheria upya Ili kuweka baadhi ya mambo Sawa asante
 
Hata kuna watu wengine wanaona mwamposa mpigaji, wakatoliki na sadaka zao wapigaji.
Kwa hiyo kama mtazamo wa watu fulani ndio utahukumu kanisa fulani basi bila shaka yote yatafungwa.
basi, kama wewe ni muumini wake, tuanzie tu hapo, mtume wako amelisajili hilo kanisa? au ndo kama vile shamba la bibi unafanya chocote unachopenda kufanya kama vile hakuna serikali.

wakatoliki au wengine hao wote uliowataja, hawajawahi kuukashifu ukristo, na bado wakajiita wakristo.

kama nabii suguye amefungiwa pamoja na uwepo wa waumini 4000, huyo ambaye waumini hata 100 hana, anategemea tv kuumiza mioyo ya wakristo, wanasubiri nini kumfyekelea mbali?
 
Yule anatakiwa akatazwe kutumia Biblia atumie kitabu chake. Mtu amekaa kuikosoa Biblia kila saa. Ila nachoshukuru watu hawana time naye, wamempuuza amebaki kudanganya wasiojitambua. Unajiita mkristo halafu unadai hakuna dhambi duniani, hivyo watu wazini wabake nk.
na wizara ya mambo ya ndani/ usajili imekaa kimya tu. mtu anajiita mkristo halafu anakosoa ukristo, sasa anahubiri kwa mujibu wa usajili wake au la?
 
Utapeli upo kila kona hata huko unako sali kuna utapeli pia,achakuteseka na watu mind your our business.

Waumini wakianza kuyakimbia makanisa yenu yaliyopoa kiroho na kwenda kwenye makanisa yenye upako sadaka zenu zina pungua na kuanzisha bifu. Hizo conflict of interest baina yenu pambaneni nazo wenyewe.

Usihamishe mada. Umeelewa anachokiongelea? Mind your business kwenye mambo ya imani. Mtu anasema hakuna dhambi duniani, wewe zini ulishasamehewa is that appropriate.

Ukristo unaanguka kutokana na watu kujifanya hayawahusu mpaka serikali iingilie kati. Watu wanafanya mambo ya hovyo utasema you mind your own business. Juzi hapa Nandy kafunga ndoa mbele ya kanisa huku ana mimba kubwa ila ukiuliza unaambiwa mind your business.

Uislamu unakuwa kwa sababu watu hawatoralete ujinga kwenye imani. Ukifanya ujinga unachukuliwa hatua au kuomba radhi. Huku kwenye ukristo ni shida kila mtu anajiamulia anavyotaka.
 
kwa kifupi, kama msikini na kanisa vinakaa pamoja na hakuna shida, sio taabu. wala hakuna mwenye chuki na uislam au ukristo kwenye hili. rudi kwenye mada, makanisa ambayo hata mlevi akiwaona anaona wazi kabisa kwamba ni wapigaji, wanawatapeli raia, serikali ikae kimya? au wewe ni mmojawapo. kuna siku watakuja kukuomba unyoe mavvuzi uwapelekee wakuombee na jinsi mlivyoshikwa akili, utapeleka.
pima upana wa hilo barabala kutoka msikiti ulipo mpaka kanisa lilipo usiongee kujifurahisha kuishi karibu na kanisa la kirokole ni kazi kuvumilia vilio hivio na mziki sio lazima pia kwa nini mkuu wa wilaya hataki kutusikiza kwani kuna ulazima ganikati ya msikiti na kanisa kuwa sehemu 1 uliwai kuona kanisa la loma na kirokole wanatengenishwa ukuta
 
basi, kama wewe ni muumini wake, tuanzie tu hapo, mtume wako amelisajili hilo kanisa? au ndo kama vile shamba la bibi unafanya chocote unachopenda kufanya kama vile hakuna serikali.

wakatoliki au wengine hao wote uliowataja, hawajawahi kuukashifu ukristo, na bado wakajiita wakristo.

kama nabii suguye amefungiwa pamoja na uwepo wa waumini 4000, huyo ambaye waumini hata 100 hana, anategemea tv kuumiza mioyo ya wakristo, wanasubiri nini kumfyekelea mbali?
Akili yako inafurahisha.
Kwa hiyo mimi nikiwa against na mtazamo wako basi nasali kwa huyo jamaa.
We ni nani kujua nini sawa na nini si sawa?
Yani kwa mawazo yako basi lingebaki kanisa katoliki pekee duniani maana mengine yote yalikuwa against it na kwa mtazamo wake hayakuwa sawa.
Mwache jamaa apige pesa mbona akina ngwajima, mwamposa wanapiga pesa kwa bible hiyo hiyo tu
 
Mimi sisali kwake kwanza nimemsoma kwenye thread hii.
As long as hajaua anafundisha maono yake fresh tu. Otherwise makanisa yaliyotangulia hapa nayo yangesema haya makanisa ya kuja yasiwepo mwanzo yanapotosha mafundisho.
unasubiri auwe kama alivyouwa kibwetele ndio uone kuwa anachofanay sio sahihi?
 
pima upana wa hilo barabala kutoka msikiti ulipo mpaka kanisa lilipo usiongee kujifurahisha kuishi karibu na kanisa la kirokole ni kazi kuvumilia vilio hivio na mziki sio lazima pia kwa nini mkuu wa wilaya hataki kutusikiza kwani kuna ulazima ganikati ya msikiti na kanisa kuwa sehemu 1 uliwai kuona kanisa la loma na kirokole wanatengenishwa ukuta
basi, kama mnaona mpo karibu sana, aliyetangulia kujenga ndio abaki, aliyekuja baadaye ampishe mwenzake. kwani waliotoa vibali mjenge hawakuona hilo? au watu walijijengea tu?
 
wewe hujielewi,ni zombie wake. ngoja nikupishe tu.
Wewe ndio hujielewi unajifanya unapanga kipi sawa kipi si sawa. Kama wanafuta wafute makanisa yote maana yanawafanya watu wanakuwa mazombie otherwise waache tu watu wajipgie pesa bila double standards
 
Mwenye kanisa, elimu ya chini ni degree ya Theology kutoka chuo kinachotambulika, ikiwezekana na somo la falsafa. Tuige mfano wa Rwanda.

Kweli kabisa. Sio sasa hivi kila mtu anajiita nabii. Anafungua kibanda anaanza maunabii yake yasiyokuwa na kichwa wala miguu. Tujifunze kwa wenzetu waislamu huwezi kuswalisha mpaka umepata mafunzo ya Quran au kwa wakatoliki ambao ili uwe padri lazima usomee muda mfrefu.

Mtu unaamka asubuhi unajiita nabii Econonist , huna elimu unadanganya watu kuhusu maono. Maoni bila kuijua Biblia utaangusha watu kama walivyofanya akina Kibwetere.
 
Back
Top Bottom