Usajili wa ‘Kanisa la Neema’ uchunguzwe

Usajili wa ‘Kanisa la Neema’ uchunguzwe

Kweli kabisa. Sio sasa hivi kila mtu anajiita nabii. Anafungua kibanda anaanza maunabii yake yasiyokuwa na kichwa wala miguu. Tujifunze kwa wenzetu waislamu huwezi kuswalisha mpaka umepata mafunzo ya Quran au kwa wakatoliki ambao ili uwe padri lazima usomee muda mfrefu.

Mtu unaamka asubuhi unajiita nabii Econonist , huna elimu unadanganya watu kuhusu maono. Maoni bila kuijua Biblia utaangusha watu kama walivyofanya akina Kibwetere.
halafu wewe unatembelea v8, waumini hata pa kulala hawana na wanakuletea sadaka. na bado unawashika masikio. basi, uchukue sadaka na ufundishe mafundisho ya kweli, shida ni pale unaanza kuwaomba mara walete kucha, mara nywele za utosi (baadaye watakuja na vuzi), mara wakuuzie mafuta, mara wakuuzie chumvi pesa wanaweka mfukoni. hao ni matapeli tu serikali iingilie kati iwaokoe raia wake wanaumizwa.
 
Ni wivu tuu.

Wivu au kasema kweli?. Haya mambo ya kusema ndio yamefanya watu wanyamaze mpaka serikali imebidi kuingilia kati kutokana na kauli kama zako. Huku Zumaridi anajiita mungu, huku Nabii fulani anajiita malaika huku Mzee wa neema anadai hakuna dhambi na kule Suguye anadai njoo na nywele za utosini kesho atasema njoo na kinyesi.

Tusiunge mkono huu ujinga ipo siku litatokea janga ana hatutaweza kulizuia.
 
pima upana wa hilo barabala kutoka msikiti ulipo mpaka kanisa lilipo usiongee kujifurahisha kuishi karibu na kanisa la kirokole ni kazi kuvumilia vilio hivio na mziki sio lazima pia kwa nini mkuu wa wilaya hataki kutusikiza kwani kuna ulazima ganikati ya msikiti na kanisa kuwa sehemu 1 uliwai kuona kanisa la loma na kirokole wanatengenishwa ukuta
Usipaniki twende taratibu
Uandishi wako unanifanya nishindwe kukujibu kwa Hoja mujarabu!
1. Barabara ya Morogoro unayoiona Leo haikua hivyo' miaka kadhaa iliyopita ilikua two ways only. Na hizo nyumba za Ibada zilikuepo.

2. Nimekutolea mfano wa hapo KAMATA na pale kongowe mbona hujarespond kwamba ni wrong au right! Badala ya kulalamika na kusema naandika kwa kujifurahisha nakupa mifano hai! Unachotakiwa kufanya ni kupendekeza kwa msajili na wizara ya mambo ya Ndani kwamba waje na masharti ya usajili Pamoja na vibali vya ujenzi kwamba angalau kuwe na Miata mia Moja Kati ya eneo la kanisa na kanisa au kanisa na msikiti! Utaeleweka.

3. Nitaweza kukutajia panapo kanisa la kilokole na la Kiroma na sio kiloma yaliyopo sehemu Moja! Tafuta muda nenda pale mbezi mwisho utakuta Anglican Church wamepakana na Adventists na on the other side Pana kanisa la kilokole tena mawili and upande mwingine Kuna Roman Catholic church st Peter Claver! Kifupi ni eneo la makanisa ya madhehebu anuwai!
 
Wivu au kasema kweli?. Haya mambo ya kusema ndio yamefanya watu wanyamaze mpaka serikali imebidi kuingilia kati kutokana na kauli kama zako. Huku Zumaridi anajiita mungu, huku Nabii fulani anajiita malaika huku Mzee wa neema anadai hakuna dhambi na kule Suguye anadai njoo na nywele za utosini kesho atasema njoo na kinyesi.

Tusiunge mkono huu ujinga ipo siku litatokea janga ana hatutaweza kulizuia.
kuna manabii wameshapiga picha wakatengeneza chupi za wanawake hapahapa duniani, mwanamke akiwa na shida ya uzazi, wanamwambia nunua chupi yenye sura yangu utapata mtoto. hivyo ni kweli, siku mtu akisema anaumwa tumbo ili aombewe wanaweza kusema akalete kinyesi. kama ana shida ya uzazi wataasema akelete zile nywele za kule, wanafanya chochote watakacho kwa jina la uhuru wa kuabudu.

mimi nilifungulia tv yake jana, anasema BIBLIA NI KITABU CHA KAWAIDA KAMA VITABU VINGINE TU. hiyo ni moja, anaongea machukizo mengi ambayo yanaamsha hisia lakini unasema basi kwasababu mimi ni mkristo sitakiwi kujichukulia sheria mkononi ila kiukweli anaamsha hisia za hasira na ule mdomo wake wa kilevi.
 
PETER NYAGA mwenye tv ya urejesho, ana kanisa tabata pia, ni mkenya, tv yake ameunganisha tz na kenya, na watu michango/sadaka huwa wanatoa toka ncho zote mbili. huyu ndio ana upako wa VIP ana kila kitu kulingana na namna ulivyolipa pesa. mkenya kaja kupiga pesa tz na tunamwangalia tu kwa jina la uhuru wa kuabudu. kuna kengine huko morogoro nilikasikia kameenda sijui kwenye mlima gani, Nabii Joshua, kale kalikuwa Tanga. kanasema kameona kuna chemchemi kule morogoro watu waende yale maji ni ya uponyaji. na serikali inaangalia tu. hivi hapo unahitaji elimu au kipimo gano kujua kuwa huyu ni tapeli au la?
 
hamkatazwi kufungua makanisa hayo ya ajabu, hoja yangu ipo kwenye usajili, muwe mmefuata taratibu. hata kibwetele alikuwa na waumini ila serikali ya uganda ilipolalaa ilikuja kufukua tu maiti. mwenye akili ameshaona hili jambo ninaloongea kama la mantiki au la, na ni kwaajili ya kuokoa watu masikini wanaodanganywa na kutapeliwa, nabii anachorwa hadi tatoo, nabii anaendesha gari ya mil.300 kwa sadaka za mtua mbaye amekopa nauli aje kanisani. kumbe pamoja na yote hayo, hajasajili wala nini iyo cult yake. si bore msajili tu ili mjulikane kisheria?

Acha mentality za kimasikini na wivu wa kike,kwahiyo ulitaka hao manabii na mitume wawe masikini watembelee yeboyebo na suruali zilizotoboka matakoni ndio ufurahie?

Get a job acha wivu wa kike.
 
"Waumini wakianza kuyakimbia makanisa yenu yaliyopoa kiroho na kwenda kwenye makanisa yenye upako sadaka zenu zina pungua na kuanzisha bifu. Hizo conflict of interest baina yenu pambaneni nazo wenyewe." [emoji3][emoji3]

Wengi ya hawa manabii na wachungaji huwa wana bifu zao na kuchongeana kwingi kwa sababu ya sadaka za waumini,wana vita baina yao yote hii ni sadaka za waumini wanagombania.

Unadhani kwanini mzee wa upako alikua ana msemo wa watashindana lakini hawata shinda
 
anatakiwa asiwe amejisajili kama mkristo, kwasababu matendo yake yote yanapinga ukristo na yanakwaza ukristo na wakristo wote. swali ni je, aliposajili kanisa lake, kama kweli amesajili, alijisajili kama Mkristo? wa dhehebu gani, au anaanzisha dhehebu jipa n.k. shida ni kwamba, ofisi ya usajili kuna watu wazembe kupita kiasi kuna siku hapa yatatokea ya kibwetele na tutabaki midomo wazi. serikali kwanza ianze kuwajibisha watendaji pale kwenye usajili, iweke wale walio makini wanaosajili kanisa na kuanza kulifuatilia kama linaendana na minajili iliyoomba usajili.
Unashangaa dhehebu!! Watu wanajiita mitume kabisa .
 
Acha mentality za kimasikini na wivu wa kike,kwahiyo ulitaka hao manabii na mitume wawe masikini watembelee yeboyebo na suruali zilizotoboka matakoni ndio ufurahie?

Get a job acha wivu wa kike.
setikari yenyewe inayaogopa mkanisa wnaogopa kulogwa
 
PETER NYAGA mwenye tv ya urejesho, ana kanisa tabata pia, ni mkenya, tv yake ameunganisha tz na kenya, na watu michango/sadaka huwa wanatoa toka ncho zote mbili. huyu ndio ana upako wa VIP ana kila kitu kulingana na namna ulivyolipa pesa. mkenya kaja kupiga pesa tz na tunamwangalia tu kwa jina la uhuru wa kuabudu. kuna kengine huko morogoro nilikasikia kameenda sijui kwenye mlima gani, Nabii Joshua, kale kalikuwa Tanga. kanasema kameona kuna chemchemi kule morogoro watu waende yale maji ni ya uponyaji. na serikali inaangalia tu. hivi hapo unahitaji elimu au kipimo gano kujua kuwa huyu ni tapeli au la?
Iyo dini ni upumbavu mtupu na wanaofuata ni makondoo akili hawana hata .

Yaani hayo masharti ni ya waganga kabisa sema wao wanavaa suti sijui uje na kucha, mara kitambaa cheupe ..Majitu Haina akili ya kudadavua mambo kwamba hao ni waganga kisa wanavaa suti na hapo nyuma Kuna disco na pombe watu wanakunywa huko kweny kanisa.
 
makanisa ni haki yake kuwepo tatizo kelele vilio miziki mchana kutwa na usiku kucha watu hatulali wala atupumziki majumbani mwetu serikali sijui inaogopa nini kwa haya makanisa kuyapiga faini ya uchafuzi wa mzingira

jambo baya kabisa ni kuruhusu makanisa ni misikitu kuwa sehemu 1 kisa heti waisilamu na wakirito wana vumiliana hakuna uvumilivu hapa kuna siku sirikali itavuna inacho kipanda

mfano ifakara watu waaridhi wameruhusu kujengwa kanisa karibu na msikiti wa muhajirina kinachotenganisha baina ya msikiti na kanisa ni mita 5

mkuu wawilaya kaambiwa akufatilia kapuuza mkuu wamkoa nae kapuuza serikali za mitaa ndio kabisa kelele mtindo 1 msikiti huo umekuwepo miaka 25 iliopita mkuu wawilaya anawaogopa wachungaji na mkuu wa mkoa morogoro nae anawaogopa wanaona bora watu wauane kuliko kukata mzizi wa fitina

wanawadharau sana waisilam kisa hawana uwezo wa kuweka wakili tunsema hivi mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya watabue kuwa hata sisi waisilamu tunahaki nchii kwa sababu kodi tunalipa kama wakirito wanavio lipa kodi hiyo ndio inayo walipa mishahara na hayo magali wanayo tembelea na malipo yao baada ya kusitafu iweje wetudharau wawe upande wa kanisa?

Imamu Ebu punguza hasira,andika vzr ueleweke.
 
Yule jamaa ana mafundisho mabaya sana. Halafu anaona wengine wajinga na kuwadharau. Mtu unasemaje kwamba. Hakuna dhambi, dhambi ilishamalizwa?. Anaipinga Biblia waziwazi na kusema kuna kitabu kingine kitakuja huko mbeleni .

Sasa si ajitoe kwenye ukristo aanzishe dhehebu lake nje ya ukristo au dini yake. Mtu anafundisha mambo tofauti na ukristo na kuwaona wasiokubaliana naye ni wajinga. Ninachoshukuru pamoja na kelele zake zote , wakristo hawana muda naye kama walivyompuuza Mfalme Zumaridi.

Jamaa namuelewa sana nikirudi dsm nitanza kusali pale mana ameruhusu ndoa ya wake wengi safi sana hapa kanipata
 
Siandiki ili kupinga uanzishwaji wa makanisa, naandika jambo ambalo kama halitashughulikiwa mapema, kuna siku litaleta matatizo, tena yawezekana yakawa matatizo makubwa sana.

KANISA LA NEEMA la mume wake na grace zoazoa vipodozi, limekuwa kero, linatukana na kupotosha Biblia na amekuwa akigombana na wachungaji wote Tanzania, sema tu kwasababu hawaji hewani kuongea, ila kuna kitu kinafukuta ndani kwa ndani ambacho kinatakiwa kupewa dawa urgently.

Tanzania kuna uhuru wa kuabudu, as long as umefuata sheria na miongozo iliyowekwa. Jambo hili limekuwa limechukuliwa kama uchochoro kwa matapeli wengi kukusanya watu ili aidha kujipatia utajiri kutoka kwao, au kwa malengo yao yoyote wayajuayo kwa kigezo kwamba Serikali haitakiwi kuingilia kati.

Majority ya victims, ni wanawake na watu masikini na wasiosoma...those people who have been stricken with problems na wanaenda kwao kama njia ya kutafuta msaada, badala yake wao wanatake advatage kuwafanya kitega uchumi.

USHAURI WANGU KWA SERIKALI
1. Kanisa la Kibwetele lilianza hivihivi, mwisho wa siku aliua watu zaidi ya 100 Uganda

2. Tuhakikishe Makanisa yanafunguliwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria. asiyefuata huo utaratibu, ashughulikiwe.

3. hata yale makanisa ambayo tayari yameshapewa vibali, yachunguzwe kuona kama wanacomply.

4. Viongozi wengine wa dini kwenye kamati zao wahusishwe katika kila kada. mfn. Wapentecost wanao umoja wao, waprotestant wengine wanao umoja wao, katholic etc, kama mtu hayupo kwenye aina hizo zote za Makanisa, basi aeleze yeye kanisa lake ni la aina gani ili asije kuleta migogoro isiyo ya lazima.

5. Kuna uzembe na rushwa nyingi sana zinafanyika kwenye ofisi ya usajili wa haya makanisa. mfn. haiji kichwani Nabii Suguye, amekuwa na kanisa miaka kadhaa yote hiyo, hadi ameanza kuomba nywele za utosini, kucha kidole kidogo n.k ilikuwa bado kidogo aagize walete nywele za sehemu za siri manake alishaanza kufundisha namna ya kufanya ngono madhabahuni. hapo ndio wakashtuka, muda wote huo kumbe kanisa lake halikuwa na usajili. INAKUWAJE MIAKA YOTE HIYO MTU ANAOPERATE KANISA BILA USAJILI?

6. kuna kanisa moja linaitwa KANISA LA NEEMA, ni la mzee wa Neema. huyu ni mme wake yule grace zoazoa anayetengeneza sabuni na vipodozi bila kuwa na elimu yeyote ya kemikali. Wakristo karibia wote Tanzania wamekuwa wakimlalamikia huyu mtu kwasababu mahubiri yake yote, ni kupindua Biblia hadi haijulikani kama yeye ni Mkristo au wa dini gani. amefungua pia tv, na anayo night club kama kanisa. ni wazi yeye anasema sio mpentecost, sio mkatoliki, sio wa dhehemu lolote, SASA HATUJUI AMEJISAJILI KWENU KAMA NANI. mtu huyu anakwaza ukristo, ana potosha mengi ambayo tunaogopa kuna siku isijetokea watu wasio na Mungu moyoni wakamdhuru, na pia anakosesha sana amani katikati ya watu kwasababu ya mafundisho yake. tunaomba chunguzwe ili kuona kama ana elimu yeyote ya dini, ametumwa na nani manake hadi anamiliki television ya TOP PLUS anagarimia vipi n.k. ni ushauri tu.

7. Tunaomba Serikali pamoja na kuwapa vibali/usajili, iwaangalie kwa jicho la karibu hao mitume na manabii wa kisasa, hao wanaouza mafuta, maji nk. wanafanya biashara kama biashara zingine tu kwa Jina la dini. iangalie usajili wao, hao kina mwamposa, ngurumo ya upako wanaogawa pesa hata hazijulikani zinatoka wapi, mzee wa upako na wengine wengi. HIVI KWELI HAWA WAMESAJILIWA?

8. kama Nabii Suguye, mzee wa ibada za nywele na kucha, amefungiwa kanisa hadi arekebishe usajili wake, ni kwali kwamba hao mitume wengine ambao ni contraversual wamesajili makanisa yao? au kwasababu wana pesa kama kina mwamposa?.

9. kama suguye aliexist miaka yote hiyo, tunajuaje kama hawapo wengine ambao anaamka tu asubuhi anaanzisha kanisa na kukusanya hela kwa maskini? bila hata kupitia serikalini.

Mambo haya nimeandika wengine wanaweza kufikiri nina bifu nao, sina, ila ni alart tu kwa serikali, isijekuja kushtuka shuka kukiwa kumekucha.

Wasalaam!
Haujawa specific ni nini hasa katika biblia kinachopotoshwa na kinapelekea madhara gani jumuishi na mtambuka kwa nchi,jamii na mtu mmoja mmoja. Weka bayana kero zianishwe hapa umepopoma tu kiholela
 
Usihamishe mada. Umeelewa anachokiongelea? Mind your business kwenye mambo ya imani. Mtu anasema hakuna dhambi duniani, wewe zini ulishasamehewa is that appropriate.

Ukristo unaanguka kutokana na watu kujifanya hayawahusu mpaka serikali iingilie kati. Watu wanafanya mambo ya hovyo utasema you mind your own business. Juzi hapa Nandy kafunga ndoa mbele ya kanisa huku ana mimba kubwa ila ukiuliza unaambiwa mind your business.

Uislamu unakuwa kwa sababu watu hawatoralete ujinga kwenye imani. Ukifanya ujinga unachukuliwa hatua au kuomba radhi. Huku kwenye ukristo ni shida kila mtu anajiamulia anavyotaka.

Usihukumu usije kuhukumiwa,acheni magugu yaote pamoja na ngano yatapepetwa siku ya mavuno.
 
Hata Mimi nilipoona kanisa lina night club. Nikapata maswali.
Night clubs na Ukristo wapi wapi.
Pana mmoja aliwahi shauri eti kuwepo na disco la Kikristo.
 
Siandiki ili kupinga uanzishwaji wa makanisa, naandika jambo ambalo kama halitashughulikiwa mapema, kuna siku litaleta matatizo, tena yawezekana yakawa matatizo makubwa sana.

KANISA LA NEEMA la mume wake na grace zoazoa vipodozi, limekuwa kero, linatukana na kupotosha Biblia na amekuwa akigombana na wachungaji wote Tanzania, sema tu kwasababu hawaji hewani kuongea, ila kuna kitu kinafukuta ndani kwa ndani ambacho kinatakiwa kupewa dawa urgently.

Tanzania kuna uhuru wa kuabudu, as long as umefuata sheria na miongozo iliyowekwa. Jambo hili limekuwa limechukuliwa kama uchochoro kwa matapeli wengi kukusanya watu ili aidha kujipatia utajiri kutoka kwao, au kwa malengo yao yoyote wayajuayo kwa kigezo kwamba Serikali haitakiwi kuingilia kati.

Majority ya victims, ni wanawake na watu masikini na wasiosoma...those people who have been stricken with problems na wanaenda kwao kama njia ya kutafuta msaada, badala yake wao wanatake advatage kuwafanya kitega uchumi.

USHAURI WANGU KWA SERIKALI
1. Kanisa la Kibwetele lilianza hivihivi, mwisho wa siku aliua watu zaidi ya 100 Uganda

2. Tuhakikishe Makanisa yanafunguliwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria. asiyefuata huo utaratibu, ashughulikiwe.

3. hata yale makanisa ambayo tayari yameshapewa vibali, yachunguzwe kuona kama wanacomply.

4. Viongozi wengine wa dini kwenye kamati zao wahusishwe katika kila kada. mfn. Wapentecost wanao umoja wao, waprotestant wengine wanao umoja wao, katholic etc, kama mtu hayupo kwenye aina hizo zote za Makanisa, basi aeleze yeye kanisa lake ni la aina gani ili asije kuleta migogoro isiyo ya lazima.

5. Kuna uzembe na rushwa nyingi sana zinafanyika kwenye ofisi ya usajili wa haya makanisa. mfn. haiji kichwani Nabii Suguye, amekuwa na kanisa miaka kadhaa yote hiyo, hadi ameanza kuomba nywele za utosini, kucha kidole kidogo n.k ilikuwa bado kidogo aagize walete nywele za sehemu za siri manake alishaanza kufundisha namna ya kufanya ngono madhabahuni. hapo ndio wakashtuka, muda wote huo kumbe kanisa lake halikuwa na usajili. INAKUWAJE MIAKA YOTE HIYO MTU ANAOPERATE KANISA BILA USAJILI?

6. kuna kanisa moja linaitwa KANISA LA NEEMA, ni la mzee wa Neema. huyu ni mme wake yule grace zoazoa anayetengeneza sabuni na vipodozi bila kuwa na elimu yeyote ya kemikali. Wakristo karibia wote Tanzania wamekuwa wakimlalamikia huyu mtu kwasababu mahubiri yake yote, ni kupindua Biblia hadi haijulikani kama yeye ni Mkristo au wa dini gani. amefungua pia tv, na anayo night club kama kanisa. ni wazi yeye anasema sio mpentecost, sio mkatoliki, sio wa dhehemu lolote, SASA HATUJUI AMEJISAJILI KWENU KAMA NANI. mtu huyu anakwaza ukristo, ana potosha mengi ambayo tunaogopa kuna siku isijetokea watu wasio na Mungu moyoni wakamdhuru, na pia anakosesha sana amani katikati ya watu kwasababu ya mafundisho yake. tunaomba chunguzwe ili kuona kama ana elimu yeyote ya dini, ametumwa na nani manake hadi anamiliki television ya TOP PLUS anagarimia vipi n.k. ni ushauri tu.

7. Tunaomba Serikali pamoja na kuwapa vibali/usajili, iwaangalie kwa jicho la karibu hao mitume na manabii wa kisasa, hao wanaouza mafuta, maji nk. wanafanya biashara kama biashara zingine tu kwa Jina la dini. iangalie usajili wao, hao kina mwamposa, ngurumo ya upako wanaogawa pesa hata hazijulikani zinatoka wapi, mzee wa upako na wengine wengi. HIVI KWELI HAWA WAMESAJILIWA?

8. kama Nabii Suguye, mzee wa ibada za nywele na kucha, amefungiwa kanisa hadi arekebishe usajili wake, ni kwali kwamba hao mitume wengine ambao ni contraversual wamesajili makanisa yao? au kwasababu wana pesa kama kina mwamposa?.

9. kama suguye aliexist miaka yote hiyo, tunajuaje kama hawapo wengine ambao anaamka tu asubuhi anaanzisha kanisa na kukusanya hela kwa maskini? bila hata kupitia serikalini.

Mambo haya nimeandika wengine wanaweza kufikiri nina bifu nao, sina, ila ni alart tu kwa serikali, isijekuja kushtuka shuka kukiwa kumekucha.

Wasalaam!
Hii nchi ni kama shamba la bibi.
Kiukweli zama za leo kila kitu kimefunguliwa pasipo hata kuzingatia taratibu. Wapo baadhi wanapotosha na hakina anayejali.

Na si tu kwenye masuala ya imani hata kwenye mambo mengine ya kijamii, hakuna maadili. Wanamuzikinwanimba jukwaani wakiwa nusu uchi na nyimbo hazina maadili ya kitanzania!
 
Hata Mimi nilipoona kanisa lina night club. Nikapata maswali.
Night clubs na Ukristo wapi wapi.
Pana mmoja aliwahi shauri eti kuwepo na disco la Kikristo.
Mi nadhani hawa watu wakalipiwe vikali ili ikibidi watumie dini zao halisi wasijisingizie Ukristo. Ukristo hauko hivyo. Na kama ni mpinga Kristo basi mtu ajitanabaishe kabisa kuwa ni dini ya upinga Kristo or whatever atakavyoamua kujiita mwenyewe, na aruhusiwe kuendesha ibada zake kwa mujibu wa hiyo imani yake. Inakera sana kuona Ukristo unafanywa shamba la bibi kila mtu anajiamulia tu atakavyo! Hata kama ni uhuru jamani hapana, hizi issue zimekuwa too much aisee!
 
Back
Top Bottom