Ushahidi CHADEMA inatumiwa na TICTS kukwamisha uboreshaji wa bandari

hoja mfu
 
Mkuu umesema vizuri na asante kwa kuleta vifungu vya biblia, inayogusa kote kote kama msumemo
Matthew 7:1-5
[1]Judge not, that ye be not judged.
Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi.

[2]Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa.

[3]
Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii?

[4]Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?

[5]Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako. Kutweza Kitakatifu
 
Huwa wanasoma vitabu vya dini na kuvielewa hao zaidi ya kuvinajisi wanapoapa hadharani kuwa walaghai na wezi?
Shoka ipo chini ya mti.[emoji123][emoji106]
IMEANDIKWA!
[emoji116][emoji116]
Matthew 3:8-10
[8]Basi zaeni matunda yapasayo toba;

[9]wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto.

[10]Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
 
wananchi wamefuata upepo, ila tunaanza kutoboa tanga kama hivi
Tuo neutral na huu mchezo tutafaidi, sema serkali imekataa kutumia vyombo kujua ukweli.
Mfano.
1. Hili la TICTIS na CDM lingemlikwa ili siasa isiingie kwenye vitu muhimu na huu ni UHAINI
2. DP WORLD issue yake ni terms za Mkataba sio kuwa hawahitajiki au mtu asiwekeze. Wananchi wanaangalia maslahi ya mkataba sio uaraabu wa uhindi. Na watetezi wa mkataba kila mmoja anaibuka na aina yake ya kutetea. Hili linaleta wasiwasi. Kwanini swali moka majibu tofauti kutoka source moja ya wasemaji?
3. Vyama vya siasa ccm na cdm wasidhani hili ni kalata yao ya kujipatia umaarufu, mfano cdm tinawajua wameluwa wapingaji wa kila awamu wala hakuna walipongeza , zaidi walishangaza kusema tukivunja mikataba tunashitakiwa MIGA na hawakuona bora tushtakiwe kuliko kunyonywa. Ma ccm wao wanadhani wana hati miliki ya rasilimali za taifa na hata raia wote kitendo cha UCHAWA ni dalili ya kujitoa ufahamu wala reasoning imewatoka hao si WAZALENDO KABISA.
Mwisho ule mkataba uwe wazi na win win, na wanasiasa wasitufanye sisi wajinga, wanajikaanga kwa mafuta yao
 
Point[emoji4][emoji106]
 
Sijui kwa wengine, lakini mie nimechoshwa na makala hizi za kipumbavu zinazoletwa kila uchao ambazo hazijibu hoja bali propaganda na hisia tuu za kijinga.
Hivi nani kakataa wawekezaji wa bandari? Watu wanahoji mkataba huu nyie mnajizima data.
Ndio maana Kenya hawakubaliani na serikali yao inayojifanya haitaki kusikia watu wanataka nini, na tetesi zilizopo Nairobi na miji mikuu mingine ni kuwa kama hali itaendelea basi jeshi laweza kuingilia kati.
Jee hawa CCM wanataka tufike huko? Na jee tukifika huko na wakajikuta hawako madarakani watauweza mtiti wa sheria zitakazo wabana kwa makosa yao?
Maana hivi ni nani katika CCM anaweza kujikuta hana hatia ya rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, ubadhilifu au ufisadi?
Nafikiri tunafikia hapo mwishoni.
 
Nani aliwatuma msaini mkataba fyongo?
Kila mkiharibu mnajificha kwenye kichaka Cha chadema wanatumiwa, jibuni hoja zilizoko mezani la hamwezi nyamazeni au muachane na DPW. Maana hata mjinga akikaa kimya huonekana ana busara.
 
Una risiti ya deposit za pesa kwenda upinzani kutoka TICTS? Kama huna. tuaminije bandiko lako?
 
Mserekali huyu[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji106]
Your browser is not able to display this video.
 
Huku mnazunguka tu, hoja zijibiwe kama ifuatavyo: Mkataba huu ukomo wake lini? Mkataba huu kama ni mzuri kwa Nini bandari za Zanzibar hazimo? Mkataba huu ni wa bandari ya Dar es Salaam tu au bandari zote za baharini, maziwa na nchi kavu? IBARA 4 (2) inayosema iwapo Tanzania inapotaka kuweka mwekezaji mwingine maeneo mengine ya bandari inatakiwa iende Dubai kuomba ridhaa, Dubai wakikataa kutoa idhini ndio basi, je, nchi huru ikaombe ridhaa Dubai Tena kwa mali zake? Jibuni maswali yenye utata, msizunguke.
 
Wanaanza kuumbuka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…