Ushauri: Awamu Moja Kwa Mbunge inatosha kabisa, wananchi tunahitaji changamoto mpya.

Hahaaa!! Siyo mwananchi wa nchi hii. Mwananchi atakuambia siwezi kuacha kumpa Zungu kura yangu nikampe Mrema (mfano tu).
Hiyo Iko ndani ya uwezo wetu kabisa wananchi.

Wabunge wote waliopo tunaweza kuhakikisha wote hawarudi bungeni.
 
Ule umate mate wanao chukua wale matapeli ukipunguzwa kidogo tuu pesheni ikapunguzwa kwenye kulipwa wasumbuliwe kama walimu na wafanyakazi wengine wanavyo sumbuliwa na kwa kikokotoo kipya watajikata wenyewe taratibu watabaki wenye moyo wa kufanya kilicho wapeleka pale mjengoni
 
Nilishauri humu mshahara wa mbunge usizidi 5ml,

Hili likifanyika, wataingia bungeni watu serious pekee.
 
Mna hoja nzuri ila wakupitisha hayo ndo watakuwa waathirika na mawazo yenu hivyo ni ngumu sana mawazo yenu kupewa baraka hz.
 
Je bunge lina umuhimu gani kwanini tusitengeneze bunge dogo la Kikanda

Mfano mbunge wa kaskazini ,mbunge wa pwani n.k

Sioni mantiki yakuwa na wabunge wengi ambao hawana uwezo wa kuisaidia nchi.

Then ubunge iwe kazi MTU anaomba na anafanya interview utumishi na awe angalau Ana elimu ya diploma
 
Hii Iko ndani ya uwezo wetu wananchi,

Tuamue Kwa pamoja kuwa, mbunge Yeyote aliyekuwa bunge lililopita, asirudi bungeni.

Hawa watu wamebariki bandari zetu kupewa wageni.
Nani wakupitisha sheria hiyo. Mkiambiwa ingieni barabarani muandamane mnakua wabinafsi. Acha tunyooshwe hadi kiama.
 
Nilishauri humu mshahara wa mbunge usizidi 5ml,

Hili likifanyika, wataingia bungeni watu serious pekee.
Serikali inapoteza pesa nyingi sana kuwahudumia wale matapeli wanaovaa suti ambapo hizo pesa zingefanya mambo mengi ya maana kabisa yamejazana tuu mle ndani na hakuna jambo la msingi wanalo fanya zaidi ya kuimba mapambio ya kumsifia mama yao
 
Hawewezi kukuelewa hawa ccm. Kwa mfano nje ya siasa:-
1. Jenista Mhagama, Margret Sitta na mama Salma Kikwete ni walimu wa mwandiko darasa la kwanza.
2. Msukuma na Maganga ni watekaji wa mabasi.
3. Simbachawene na Lusinde ni makondakta wa daladala.
4. Ongezea na wewe
 
hiyo ni kuzuia, kuminya na kunyima watu uhuru na haki ya kuchagua viongozi wawatakao, lakini pia ni kutatiza haki, ndoto na vipaji hususani kwa vijana bila sababu za msingi, sizizo na maana wala mashiko, ispokua hisia dhaifu na potofu sana za kisiasa....

je,
unafahamu umri unaoruhusiwa kwa mgombea nafasi ubunge kikatiba Tanzania?
na umri wa kugombea urais je, unafahamu?

na ikiwa unafahamu,

mathalani mwaka ujao wa uchaguzi ndio una umri wa miaka 21, na umechguliwa kua mbunge. baada ya miaka mitano utakua umestaafu na umri gani?

na utaruhusiwa kufanya nini tena na hiyo katiba yako, na hali ya kua umeamua kufanya kazi ya siasa na pengine ndio taaluma iliyosomea kwa muda mrefu na kwa gharama kubwa?

hakuna haja kutengeneza bomu la wana mapinduzi ya kisiasa kinyemela namna hiyo....

hata hivyo, bado ukomo wa mbunge na hata raisi, ni miaka mitano tu kikatiba, tangu mfumo wa vyama vingi kuanzishwa nchini Tanzania, hilo nalo hujui
 
Umeambiwa kuwa ubunge ni ajira ya kudumu kwamba mtu akimaliza ubunge akiwa na miaka 29 hawezi fanya mambo mengine?

Miaka 5 ni ukomo kikatiba Kwa nafasi Si mtu.

Tunataka uwepo ukomo wa kugombea kama ilivyo katika nafasi ya Rais.
 
Mitano inatosha,

Kukosa ukomo Kwa nafasi za kisiasa, kunaua uthubutu na ndoto za vijana, na watu wenye uwezo.
nadhani tatizo lako ni kutokua na uelewa wala ufahamu wa kutosha kuhusu ukomo wa kiutawala kwa viongozi wa kisiasa mathalani wenyeviti serikali za mitaa, madiwani, wabunge na hata raisi....

mbona liko bayana sana? hata kwenye vyama vya kisiasa tu, ukicheki katiba zao utagundua, zote zina ukomo wa kipindi maalumu watu kuongoza
 
Naona tukiwapa awamu moja tutapigwa tuchakae, mbunge anaweza asifanye chochote jimboni kwake akijua hana cha kupoteza maana anajua kabisa muhula ukiisha hatorudi tena kugombea.
 
Kwenye Rasimu aliyosimamia Judge Warioba tulipendekeza ukomo wa kutogombea.

Tulipendekeza pia kuwa, uwepo namna ya kuwafuta KAZI wabunge wenye viburi aina ya Mwigulu
 
Naona tukiwapa awamu moja tutapigwa tuchakae, mbunge anaweza asifanye chochote jimboni kwake akijua hana cha kupoteza maana anajua kabisa muhula ukiisha hatorudi tena kugombea.
Ukomo huo uendani na possibility ya kufukuzwa KAZI ikiwa atakiuka mkataba aliosaini na wananchi.

Tuwasainishe mikataba, na tuwafukuze KAZI ikibidi hata kabla ya kwisha miaka mitano.
 
Umeambiwa kuwa ubunge ni ajira ya kudumu kwamba mtu akimaliza ubunge akiwa na miaka 29 hawezi fanya mambo mengine?

Miaka 5 ni ukomo kikatiba Kwa nafasi Si mtu.

Tunataka uwepo ukomo wa kugombea kama ilivyo katika nafasi ya Rais.
mawazo na mtazamo dhaifu sana,

hata babu yako warioba aliwahi kutaka kuja na wazo na mtazamo dhaifu kama wako, wananchi tukamwambia hilo wazo lako unaweza kulitumia mahali pengine sio Tanzania...

chungulia vizuri pendekezo la wananchi kuhusu unachotaka kulazimisha kwenye rasimu ya babu warioba itaelewa vizuri na itakusaidia sana liongeza uelewa na ufahamu juu ya mambo haya

leo unamzuia aliesomea siasa asifanye siasa kikatiba, kesho utaelekea kumzuia mwalimu au daktari nae awe na ukomo wa kufanya ualimu au udaktari wake, hutaishia hapo dhambi hii itaendelea kwa wakulima, wafugaji n.k na kwamba waache wanachokifanya wapishe wengine kikatiba
 
Kwenye Rasimu aliyosimamia Judge Warioba tulipendekeza ukomo wa kutogombea.

Tulipendekeza pia kuwa, uwepo namna ya kuwafuta KAZI wabunge wenye viburi aina ya Mwigulu
acha upotoshaji,
hembu weka cha babu warioba linganisha na hoja yako
 
Si ubaguzi huo,

Mbona Urais una ukomo, iweje ubunge usiwe na ukomo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…