Ushauri: Iundwe Kamati huru kubaini chanzo cha nyufa JNHP maana kuna harufu ya uhujumu uchumi

Kwamba aliyekuwa waziri wa Nishati, kabla ya Biteko alikuwa akijinadi na Maharage kuwa wao Wana team Bora ya Project magagement.

Uchunguzi makini wa HAKI unahitajika.

Vijijini watu hawana pesa ya kuhudumia watoto wao bima za AFYA, wasikie Bwawa lao walilokopewa Lina nyufa na hakijakamilika!!!
 
Mwenda zake kafanyaje?mbona Flyover ya Ubungo haina nyufa?
Hapa January ndiyo muhusika Mkuu na Bodi yake ya TANESCO iliyojaa Bankers badala ya Engineers!
 
Simkatai mtu. Nawajuwa Wamisri kwa pesa, kuliko wachaga hao. Tulilisema zamani.

Hapo lazima zitutoke tukitaka tusitake.

Point yangu ni, nchi haiendeshwi kwa kujimwambafai.
Wewe usilete ngonjera;Engineer Tito aliyekuwa MD wa TANESCO pamoja na Bodi chini ya Engineer Kyaruzi walianza vizuri Kusimamia kazi,akaja January baada ya kumtoa Kalemani akaunda Bodi ya rafiki zake Bankers wakina Mafuru,Mchechu et al na wakajigamba kwamba wao wanafanya kazi Kisayansi na wana team makini ya Kusimamia mradi,sasa kiko wapi!
Na bado tunapewa umeme wa mgao wakati hizo habari tulishazisahau.
Tulia tu Mama,muongo mpe muda!
 
Zisije zikatolewa sababu za "expansion joint" hapo, katika mradi huo nyeti wa bwawa hilo kubwa la uzalishaji wa umeme. Uwepo wa nyufa hizo inailazimu serikali kutuma timu ya wataalamu, ikewezekana watoke nje ya nchi, ili kuhakiki uimara na ubora wa mradi mzima ili kuona kama unakidhi viwango vilivyowekwa na kukusudiwa kutokana na masharti ya mkataba.

Inawezekana tatizo lilianzia katika kumchagua mkandarasi. Pengine serikali ilimtaka yule wa bei ya chini pasipo kujali ubora na uzoefu katika kuendesha mradi kama huu. Kama sheria ya manunuzi ya umma inabadirishwa ili serikali iweze kununua vitu vya mtumba, inawezekana kabisa mkandarasi alipatikana kwa minajili ya bei ya nusu na robo, hata pasipo kuzingatia ubora na uzoefu wake.
 
WALIVUNJE LOTE WAANZE KUJENGA UPYA PESA SI ZIPO KEDEKEDE

OVA
 
Bado hujapona tu mkuu wangu?
 
Naunga mkono HOJA 🙏🙏.

Ikibidi iwe Tume huru na ihusishe wataalamu Toka nje ya Serikali na nje ya nchi.

Umeme wa Bwawa like waeza saidia hata Nchi Jirani.

Kuhujumu Bwawa ni kuhujumu Vision ya Mwl Nyerere.
 
Nakushauri tunapojadili issues zinazogusa Maslahi ya nchi,

Weka pembeni uchama, udini na ubinafsi tafadhali[emoji120]
Huyu kiumbe huwa nina mwona mimi kama anashida mahari furani,hoja zake zoote zimepinda na kuegemea uchama.
 
Hua unaziamin san hiz kamati? Kwa mfumo ulivyo bana kamati nying huja na yale yakumfurahisha mtawala na ikitokea kuna makosa even yanatokana na mtawala, tambua kamati haitomgusa bali itatafuta chaka lingine!!
 
Yasije yakatokea ya Libya, watu wakasombwa na maji baada ya mabwawa kuvunjika. Naunga mkono hoja.
 
Rejea thread:Bwawa la kufua umeme la Mwl Nyerere, limeanza Kutoa nyufa-Peno hasenagwa. Picha zipo pale.
Mkuu nimerejea hiyo thread na picha nimeona.
Ni normal crazy cracks zinazorekebishika (kulingana na ile picha) otherwise ziliendelea kukata baada ya ile picha.
Cracks kwenye zenge haziepukiki, kinachofanyika ni ku control zile sources za cracks ili zitakazojitokeza zisiwe na effect kwenye structure husika.
Hapo sijaona cracks za kuundiwa tume tena ya bunge. Waliopo site bado wapo capable kuja na appropriately solutions ya u-repair hizo cracks.
Ingelikuwa ni structural failure wesingelithubutu kujaza maji.
 
Nilijua...! Kuna namna...mambo ya kihandisi huwezi kudanganyA. Kumbe ndiyo maana waliwakatalia wahandisi wa Mkoa Fulani wasitembelee JNHP. Walitaka kuficha mapungufu haya nini?
 
Interesting....
Na akikuta hujuma ni ya sukuma gang wenzie aseme Tu bila kuficha...

Hii hujuma iliripotiwa hapa miezi zaidi ya mitatu kabla haijatokea
Hii mada tumeombwa ijadiliwe bila udini wala ukabila sasa mambo ya SUKUMA gang yanatutoa nje ya mada! Hapa inaitakiwa iundwe tume ya uchcunguzi ya wataalam na sio wana siasa ili kujua kama kweli we are getting value for our money in this project!!
 
Natumaini tunaelewana, ni kwamba hali ya nyufa kwenye project kama hizo uwa zinatokea lkn zikiwa zinatokea ndani ya muda wa project kuhisha, basi mkandarasi anakuwa anahusika kuweza kudeal na iyo situation chini ya usimamizi wa mwandishi mshauri wa serikali.. nafikiri tuwaachie wahusika wa hili jambo mpaka tutakapokabidhiwa Mradi ..lkn tukienda zaidi mbele hizo zitakuwa ni Siasa za maji taka.
 
Kwani madam si kuna mkandarasi aliyepewa kujenga hilo bwawa kwanini usimsingizie huyo badala ya mwendazake lakini pia si kuna wizara inayosimamia huo ujenzi? kwanini hao ndio wasilaumiwe kwa kushindwa kusimamia? Yaani mwendazake amekufa ukiwa ujenzi unaendelea alafu leo tunataka aamke aje awakague wajenzi wa bwawa wakati wizara ipo. Kwani mkandarasi aliyepewa tenda ya kujenga hilo bwawa alisaini hadi mkataba wa kutogaguliwa pale anapojenga chini ya kiwango?? Mimi kwa ushauri wangu sisi tulio achiwa mradi ndio tulaumiwe kwakutokujalii. Lakini kutokujali mradi hatari kama huo madhara tutayaona baadaye kama maji yakitoroka kwenye bwawa nakuingia kwenye makazi ya watu.
 
Nilijua...! Kuna namna...mambo ya kihandisi huwezi kudanganyA. Kumbe ndiyo maana waliwakatalia wahandisi wa Mkoa Fulani wasitembelee JNHP. Walitaka kuficha mapungufu haya nini?
R.I.P Mfugale😭
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…