Najua kila siku watu wanakula na kuvaa, ukija kwenye sekta ya Chakula watu wengi wamewekeza huko kuna cafe za kila aina Mjini Canteen za kutosha na kila siku wanapiga hela ata kwa mtaji kidogo wa mama ntilie,
Leo mi nataka nifanye kwa upande wa pili kwa kuwa watu wana kula basi wanavaa pia na ndio maana hauwezi kutana na binadamu anaetembea uchi,
Lengo.
Kufungua kiwanda cha nguo, ninachoitaji ni vitendea kazi vyereani 3 tofauti,mashine ya kuchapa maandishi kwenye t shirt(siyo lazima nianze nayo)
--Kwenye kiwanda changu nitahitaji vijana watatu tu wa ushonaji na hao hao ndio watadili na designing ya mavazi,
--malipo watakuwa wanalipwa kwa mwezi kama wafanyakazi wengine na watakuwa na mikataba ili tubanane vizuri
--Kiwanda changu kitadeal sana na designing ya ushonaji wa nguo za kike na za watoto,kidogo na nguo za vijana wa kiume kwa sababu nafikiri ndio soko lilipo,
--Kiwanda changu kitakuwa cha kisasa nataka nitengeze website Acount mbali mbali kwenye social network eg insta, tweeter N.k zitakazodili na kutangaza bidhaa zinazotoka kiwandani kwangu,
--Nataka kiwe free delivery unaagiza mzigo kutoka kiwandani designing yake unashonewa unapakiwa na kukufikia popote ulipo ndani ya tanzania(siyo leo biashara ikikua kua)
Mtaji nilionao wa kuanzia ni takribani milioni 2 Tsh pesa halali kwa malipo ya kitanzania.
Najua humu kuna Wazoefu naomba mnipe changamoto kama hela niliyonayo inatosha au niongeze ngapi kwa mahitaji ya kiwanda changu.
CC Zero IQ