Ushauri kwa Balozi Mulamula: Mkitaka Tanzania ifaidike na Diaspora suala la uraia pacha haliepukiki

..labda hawa ndugu zetu waliozaliwa Tz na kuchukua uraia wa nje watengenezewe UTARATIBU MAALUM utakao rahisisha mambo yafuatayo.

1. Mirathi.

2. Uwekezaji.

3. Ukaazi.

4. Ajira.

..Mengine mnaweza kuongezea. Na utaratibu huo sio lazima uwe ktk daraja sawa na sisi tunaoendelea kuulinda na kuuhifadhi Uraia wetu wa Tanzania.
 
Yeah, mkuu swala hii inabidi lifanyiwe kazi kwa haraka sana
Dunia saivi imebadlika ni vema tukawa na utaratbu wa Urai pacha
 
Kumbe ni kweli hamuna hoja zaidi ya vihoja na chuki tu.
Mie nilishawagundua siku nyingi Mkuu. Siku moja tulikuwa sehemu sehemu jamaa walikuwa wanabisha eti sie tumesota hapa wao wakakimbia nchi halafu wanataka warudi kututambia! Ndipo nilijua kumbe watu ni chuki na wivu tu vinawasumbua!
 
South Afrika ina uchumi mzuri kuliko Tanzania, lakini bado ikaona umuhimu wa uraia pacha. Tanzania masikini wao ndio wanajifanya ooh uzalendo, ulalama wa nchi. Point off kabisa.
 
Unaona basi usivyo na point? Aina ile ile ya wabishiwa wivu na chuki tu.

Kwanza hao walioukana uraia, wakipewa tena uraia wa Tanzania wewe unaathirikaje, na hasa ukizingatia itawawezesha kuhamisha mitaji kuja Tanzania kirahisi?

Pili, kama hao walioukana uraia wanatamani tena kuwa Watanzania, sio lazima wawe raia pacha. Bado wanaweza kuwa raia wa Tanzania tena, kwa hiyo issue sio hiyo. Uko off kabisa.

Uraia pacha unaingia pale ambapo inakuwa rahisi kwa mtu kuhamisha capital kati ya nchi mbili (repatriation of earnings, profits or capital). Ukitaka kuona ni jinsi gani, hebu nenda Bank waambie ninataka kutuka Dola Elfu mbili kwa rafuiki yangu pale Kenya uone utakavyotolewa nje. Lakini sasa, ukiwa na uraia pacha wa Tanzania na Kenya, utaruhusiwa kirahisi kwa kuwa wewe ni raia wa Kenya pia, kwa hiyo inakubalika kwamba unafanya repatriation of profits. Ndio maana hata makampuni ya kigeni yanaruhusiwa kutoa fedha walizochuma hapa nchini kwenda nje. Ni kwa msingi huo mie nikiwa Kenya na nina uraia pacha na Tanzania, inakuwa rahisi kutuima fedha toka Kenya kuja Tanzania.

Yaani watu mnabisha wakati hivi vitu hamvielewi. Eti uzalendo, usalama, wivu tu na chuki vimewazidi. Uzalendo wako unaisaidia nini Tanzania kama hujawahi kuiingizia nchi hata dola moja toka uzaliwe?
 
Point nzuri, ila watoto wao hawana uraia pacha Mkuu, labda kwa siri. Maana Tanzania bado hairuhusu.
Kuna jamaa yangu alikua akifanya usajili wa vitambulisho kule maeneo ya oysterbay ambapo wengi wao ni watoto was vigogo na vigogo wenyewe.

Sasa wale jamaa wanakuja na passport mbili ya Tanzania na ughaibuni na zote zinataarifa zao sasa hio sio uraia pacha kweli?
 
Mkuu Membe alifanya kazi nzuri sana alipokuwa Foreign Affairs kwenda katika nchi mbali mbali za Africa na Caribbean kukusanya important info ya advantages na disadvantages za uraia pacha katika nchi ambazo zinaruhusu hilo. Nchi zote alizotembelea maoni ya Marais na pia Wizara zao za nje zilifagilia sana uraia pacha na hawakusagia chochote lakini UNAFIKI wa Kikwete baada ya kuona ndani ya ccm linapingwa sana bila ya kuwepo hoja ya msingi ukakwamisha hili kufanikishwa. Nadhani Tanzania katika Africa inaweza kabisa kuwa nchi ya mwisho kuruhusu uraia pacha.
Nasikia leo saa 12 jioni EAT kulikuwa na kikao cha Diaspora na balozi zetu mbali mbali za nchi za nje ambacho Mwenyekiti wa kikao alikuwa Asha Migiro.
Ningewashauri wale wote wanaoona faida za Tanzania kuwa na uraia pacha watoe msisitizo wao kwenye hii thread
 
Hata swala la passport wangepunguza vikwazo na mlolongo, ili vijana wakajimwage mambele ili kujiokotea chochote na kuleta nyumbani
 
Ni mhindi gani wa kuhangaika na ajira za kulipwa milioni kwa mwezi? Labda mhindi koko

Ah aha kumbe wewe hujui...
Nenda vuwanda vya Cement utajua wahindi ni Kina Nani na wanapokea Tsh ngapi?
Unaweza Kupata Ugonjwa wa Moyo ukianbiwa Mshahara wao,
Hata Mimi nilidhani Tsh 5,6M tuuu..
Kumbe duuu...
Nikasema Ahsanteeee Piga Mara 5,6 ya Hizooo
 
Mkuu kuna baadhi ya Watanzania wana chuki za kutisha. Akiona kitu yeye hawezi kukipata basi anaweza kufanya juu chini hata kusema uongo ili mwenzake pia asikipate. NTIMA NYONGO!!!
Kumbe ni kweli hamuna hoja zaidi ya vihoja na chuki tu.
 
Hoja yako kuhusu Wahindi inaonekana msingi wake ni Uhamiaji hawako makini, wanachukua rushwa kutoa vibali.

Hapo ni kuimarisha hii idara iwe na watu makini. Diaspora wengi ni watu weusi kama wewe. Wahindi wanaweza kuwa less than 5%.

Mkuu Wahindi ndio waneshikila Uchumi wetu Mkuu!
Pia Ni ngumu...Nasema ngumu kwa hiyo Taasisi kudhibiti Vibali vya Kazi!
Kwani Hawapendi Hela?
Angalia Work Permit tuu za Makampuni Kama ya cement,Migodini,Simu,nk!
Halafu uwaulize ni Mara ngapi wanatembelea Site au Wameonana na Vyama vya wafanyakazi angaalu kuwahoji?
 
Niambie faida na hasara za uraia pacha. Tuanzie hapa kwanza na asiniambie Hakuna hasara maana Hakuna jambo lolote lisilokuwa na hasara
 
..anaweza kuwekeza kwa kuwatumia wazazi au ndugu zake.

..sokomoko linakuja kukitokea bahati mbaya kuwa aliyeandikishwa mali amefariki.

..au aliyeandikishwa mali amekosa uaminifu huyu diaspora anakuwa hana namna ya kupata haki yake.
Duh! Wacha ni reserve comments zangu tusije kukwazana. Kumbe na wewe ni wale wale tu, Sema una kauli za kinafiki.
 
Duh! Wacha ni reserve comments zangu tusije kukwazana. Kumbe na wewe ni wale wale tu, Sema una kauli za kinafiki.

..Umenielewa vibaya. Mimi nilikuwa namjibu Econometrician.

..Umefanya vizuri ku-reserve comments zako.

..Ungeweza kupata DHAMBI za bure kwa kunituhumu kitu ambacho sicho.

..I am just being realistic here.

..Kama itakupendeza tafuta mrejesho aliofanya muwakilishi wa diaspora ktk bunge maalum la katiba.

..baada ya kumsikiliza nime-conclude kwamba ni afadhali mpiganie kuwa na ukaazi wa kudumu kuliko kuwa na uraia pacha.
 

Lakini hii ni separate issue. Wengi ya hao Wahindi wanaokuja na kuomba vibali wanatoka India. Hapa tunazungumzia Watanzania (wenye asili ya TZ) walioko Ulaya, US na nchi nyingine.
 
Kubwa ni ushamba na ulimbuken wa baadhi ya wenye mamlaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…