Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Siku hao wazee wakifikiwa wataanza nawao kitoa matamko kama kwa maveterani wa Mugabe.Udikteta sio mchezo tutalia machozi ya damu.

QUOTE="king's lawyer, post: 17026535, member: 287834"]Lile BARAZA LA WAZEE LA CHAMA KILEEEEEE[emoji117],huwa linafanya kazi saa ngapi?wako macho?wanaona upepo mkali ukivuma?wanaona mwelekeo wa jahazi?kwakuwa sisi si wazoefu,tunatamani watuhakikishie safari.[/QUOTE]
 
"Hakuna dhambi mbaya kama uoga" Godbless Lema

Acha tuandamane tutapambana barabarani na polisi.

Makamanda tujiandae kuingia barabarani nawaomba Mbowe na Lowassa pamoja na Sumaye tuwe pamoja kwenye maandamano.
Wacha kujifanya kutabiri jua wakati wa kiangazi
 
Reactions: BAK
Hapo kwenye rangi pataanza kupata umaarufu mkubwa nchini kama hali nchini itaendelea kuelekea siko. Tusikubali kukaa kimya huku tukiona nchi inapelekwa gizani na huyu dikteta na vitisho dhidi ya raia, viongozi wa upinzani kila kukicha na kutoheshimu katiba ya nchi.

 
Kwani Katiba inasemaje.Katiba haisemi ni lazima amalize miaka 5. Hata maandamano yanaweza kumng'oa kupitia shinikizo kwa bunge .Nashangaa kuna watu wanatoa povu hapa
 
Kwani Katiba inasemaje.Katiba haisemi ni lazima amalize miaka 5. Hata maandamano yanaweza kumng'oa kupitia shinikizo kwa bunge .Nashangaa kuna watu wanatoa povu hapa
Kumbe lengo lenu ni kumng, oa Rais wetu.. Hakika tunasubiri hiyo tarehe 1
 
Pasco alikuwa ni wa miaka hiyo lkn huyu wa sasa ni Pasco karatasi
Pasco wewe tayari tumesha kustukia kuwa unatumika sasa na watawala hivyo ushauri wako peleka huko huko kwenu lumumba
Mkuu Mmawia, Pasco ni yule yule wa juzi, jana na leo kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa.

Mimi sina kabisa chama, sio mshabiki wala mfuasi ila ni mzalendo na siku zote Natanguliza uzalendo wangu kwa taifa langu! .

Fuatilia threads humu jf uangalie ni mwana jf gani amekomalia udikiteta wa Magufuli kama Pasco wa JF, hivyo kitendo cha kuniita mimi ni wa Lumumba ni kama kunitukana, hata hivyo I'm coming up of an age na the most favourite past time ya retirees ni politics hivyo msishangae mwakani wakati wa mikutano Mkuu wa CCCM nami nikajiunge nikajilie pensheni nono huko kuliko kuendelea kufa njaa huku juani nilipo sasa kwa sababu kujiunga chama chochote sio dhambi.

Pasco
 
Mkuu kawadanganye wasiyo kufahamu au inaelekea wewe ndiye hunijui kwa sababu ya hii ID yangu lkn ni watu tulio wahi kufanya kazi kwa pamoja
 
Hakuna habari ya mwenye nguvu mpishe ingelikuwa hivyo wazee wetu na mwl nyerere wasingetuletea uhuru maana mkoloni mwingereza alikuwa na kila kitu.Kikubwa tunatumia HAKI YA MNYONGE HIARI YA MWENYE NGUVU,hapa ni kutumia maneno kama silaha na ushindi utakao patikana ni ushindi wa nguvu za maneno ndo maana ya kufanya mikutano,lazima kuhakikisha kuwa nguvu ya maneno zinafaulu kupenya ktk masikio yanayotambua na kukiri madai ya maneno hayo wala hajaribiwi mtu,pale mtu mwenye nguvu anapo mpuuza mnyonge.je huyu atafanya nn?
 
Binafsi nitaandamana bila kumuogopa mpuuzi yeyote.. nitakuwa mstali wa mbele.. kama wananiua kama mwangosi na kamanda mawazo waniue..
lakini nikitoka bila kufa nao wajiandae kuuwawa
 
Hivi mnafanya makusudi au ni ukweli upeo wenu ndio umeishia hapo?

Mimi namuunga mkono Rais kwenye vita dhidi ya ufisadi, uzembe kwenye ofisi za umma na kurudisha uwajibikaji.

Ila nitampinga kwa nguvu zote kuingilia haki za raia kujumuika hili halikubaliki hata chembe, hakuna mtu yeyote aliyemzuia Rais asifanye kazi yake.

Otherwise labda unishawishi upya kwamba ilani ya ccm ilisema wakishinda urais watapiga marufuku shughuli za kisiasa.
 
Hiiiiii hapa iko poaaa zaidi
 
Tanzania itaendelea kuwa maskini hivi hivi kwa sababu ina watu wengi waoga! Mfikilie Mandela, J. K. Nyerere, Nkurumah na wengine wengi. Wangeogopa kusimamia hoja zao kwa kuwaogopa waliokuwa na dola, ingekuwaje!?
 
masikini wee muda wa mdanganyika umepotea bure
 
Mkuu Gamba la Nyoka, atakachofanya Magufuli, ni kuwatumia the best of his snipers, wadunguaji wazuri, kwenye maandamano Kikwete alikuwa akishoot randomly ili kuogofya tuu, na waliokuwa wakiuwawa ni akina kaja.. nani!, kiukweli Magufuli, atawashikisha adabu kiukweli kweli haswa, kazi ya wadunguaji ni ku target vinara!, mkuu wa nchi hawezi kufikishwa the Hague kwa ku clear the mess ya kifo kimoja au viwili, na amini usiamini, wakiandamana tuu, watadunguliwa kwa risasi za moto, lakini taarifa ya polisi itasema walitumia rubber bullets, postmortem report itathibitisha hilo na mchezo, utakwisha.

Pasco
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…