Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Serikali ikitenda kwa kukiuka, kutokutenda au kukandamiza, mahakama kupitia powers zake inatoa executive orders, au writs za prohibition, certiorary na mandamus kuiamuru serikali itake isitake!
Pasco, between the law and political science notions there is something practical on how we run the government in the real world. Ninaamini kuwa wanataaluma wengine wakitoa mawazo na uzoefu wao wa kuendesha serikali wataweza kupanua mjadala kufukia hapo katika real world state governance. Hata hivyo umenikumbusha mipango yetu tuliyokuwa tukisuka enzi za DARUSO change miaka hiyo, tukilenga kuishitaki Serikali. Ni bahati mbaya hata washauri wetu, waadhiri wa sheria wa enzi hizo, walikuwa hawaamini we would achieve anything with the ......certiorari, mandamus, et cetra strategies.
 
Mkuu Gamba la Nyoka, atakachofanya Magufuli, ni kuwatumia the best of his snipers, wadunguaji wazuri, kwenye maandamano Kikwete alikuwa akishoot randomly ili kuogofya tuu, na waliokuwa wakiuwawa ni akina kaja.. nani!, kiukweli Magufuli, atawashikisha adabu kiukweli kweli haswa, kazi ya wadunguaji ni ku target vinara!, mkuu wa nchi hawezi kufikishwa the Hague kwa ku clear the mess ya kifo kimoja au viwili, na amini usiamini, wakiandamana tuu, watadunguliwa kwa risasi za moto, lakini taarifa ya polisi itasema walitumia rubber bullets, postmortem report itathibitisha hilo na mchezo, utakwisha.

Pasco

Ushauri mbaya huu maana wakifanya hivi, watakuwa wamefungua cycle ya violence ambayo hawataweza kuizima, kumbuka kule Soweto mauaji ya wale watoto waandamanaji yalivyofungua moto wa Resistance kwa nchi nzima.
Kinachotakiwa hapo ni Kutoa haki kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi.
 
Ushauri mbaya huu maana wakifanya hivi, watakuwa wamefungua cycle ya violence ambayo hawataweza kuizima, kumbuka kule Soweto mauaji ya wale watoto waandamanaji yalivyofungua moto wa Resistance kwa nchi nzima.
Kinachotakiwa hapo ni Kutoa haki kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi.
Wajibu wa vyama vya siasa kanuni zipo wazi kabisa !!
Na kwa upande wa katiba ya jamhuri
ya muungano ipo wazi kuhushu sheria za jamhuri kuzifuata! Soma ibara ya 26
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kutoa ushauri wa bure, huu ni ushauri wa bure kwa Chadema, japo kuandamana na mikutano ya kisiasa ni haki iliyotolewa kihalali ndani ya katiba, nawashauri kwa dhati kabisa, tafadhalini sana msiandamane, na kusitisha hiyo Operesheni UKUTA, ili kuutumia ule msemo wa Kiswahili "Mwenye nguvu mpishe", hata kama una haki, usitake kujipima nguvu kwa kutunishiana misuli na mtu mwenye nguvu zaidi yako, na sio tuu ana nguvu zaidi yako, na tayari, umeishajua ni dikiteta, bali ndio mwenye nguvu ya dola mikononi mwake!.

Misingi ya Katiba na The Rule of Law
Tanzania ni nchi inayofuata misingi ya katiba na sheria, (the rule of law) ambapo inapaswa kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni, na sio kwa matamko ya viongozi yanayokwenda kinyume cha katiba!.

The Separation of Powers & Check and Balance .
Nchi yetu ina mihimili mikuu mitatu, Serikali, (the executive), Bunge (The Legislature) na Mahakama (The Judiciary). Mihimili hii mitatu, ilipaswa kufanya kazi kwa kujitegemea bila mhimili mmoja kuingilia mhimili mwingine (independence), huki kila mhimili uki act as a watchdog wa muhimili mwingine usivuke mipaka ya madaraka au mamlaka yake yaani (The sepaation of powers check and balance).

Serikali yenye Nguvu, Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo!.
Mihimili hii, inaongozwa na viongozi ambao wana mamlaka kuu kuhusu mihimili yao. President ndio mkuu wa the executive, Spika ndio mkuu wa The Legistlatue, na Jaji Mkuu, ndie mkuu wa The Judiciary, lakini pamoja na nia njema kuwa mihimili yote inamamlaka na hakuna mhimili wowote uliokuwa unapaswa kuwa na mamlaka kuliko mhimili mwingine, lakini kiukweli, mhimili wa the executive ndio mhimili mkuu unaomiliki vyombo vya dola na kuitawala mihimili mingine yote!, hivyo mkuu wa the executive, yaani rais, ndio kila kitu!, akisema!, amesema!.

Rais Magufuli na Uvunjaji wa Katiba.
Tuambiane ukweli, tangu rais Magufuli ameingia madarakani, sio mara moja au mbili amekuwa akitoa kauli tata, zinazokwenda kinyume cha katiba, mhimili wa Bunge na Mahakama ilipaswa kuingilia kati kwa kumcheck mkuu wa the executive, lakini vyombo hivyo vimekaa kimya hivyo kumfanya rais ajisikie kuwa he is always right! kwa kanuni ya "the boss is always right!".

Udikiteta wa Magufuli.
Hoja kama Magufuli ni dikiteta au la, haina mjadala, Magufuli ni dikiteta wa ukweli ambaye hana msalie mtume, na alipoingia tuu madarakani, alianza kuonyesha udikiteta wake right away kwa kuliingilia bunge na mahakama kuziweka chini ya amri zake!. Lile katazo lake la watumishi wa umma hawaruhusiwi kusafiri safari za nje bila kibali chake kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, liliwahusu watumishi wote wa serikali, likiwemo bunge na mahakama!, just imagine Jaji Mkuu na Spika wa bunge wakapige magoti kwa rais kuomba kutimiza wajibu wao!.

Baada ya katazo lile, checks and balance zingepaswa kuanzia hapo kwa Jaji Mkuu kumweleza rais huko ni kuingilia uhuru wa mahakama (the independence of the judiciary) hivyo muhimili wa mahakama haukupaswa kujisubmit chini ya the executuve, bali mamlaka hayo ya kuzuia safari za nje, Spika alipaswa kuwa nayo kudhibiti safari za mhimili wa bunge, na Jaji Mkuu alipaswa kuwana nayo kudhibiti safari za mhimili wa mahakama, lakini mihimili hii ilikaa kimya kwa kujisubmit chini ya the executive, hivyo kumfanya rais ndio kila kitu!.

Hivyo sasa rais Magufuli ndio kila kitu, hakuna cha bunge, mahakama, wala katiba, amri ya rais ndio kila kitu na ndio sheria kuu!, hivyo nawashauri Chadema kwa dhati kabisa, wasitishe maandamano yao, wasifanye kabisa mchezo wa kumjaribu Ngosha, wataumia bure!.

Hili la udikiteta wa rais Magufuli, tumeisha lizungumza sana humu
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...
Rais Magufuli, Waliomchagua Wanajuta!, Wasiomchagua Wanamshangilia ...
Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...
Utumbuaji Majipu wa Rais Magufuli: Is It A Right Thing, At The ...
Je, Hizi Terorizing za Ziara za Kushtukiza, Hakutajenga Nidhamu ya ...
Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote | Page ...
Nimetishwa, Kushitushwa na Kuogopeshwa na Kauli Hii ya Rais ...
Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ...
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa ...

Ila kitu kimoja kuzuri kuhusu udikiteta wa rais wetu, ni Rais Magufuli ni dikiteta mzalendo!, mwenye uchungu na umasikini wa nchi hii, mwenye nia njema ya kusafisha uozo wote wa uzembe, rushwa na ufisadi, na kulikomboa taifa letu toka kwenye lindi la umasikini uliotopea na kuwa nchi ya maziwa na asali kupitia uchumi wa gesi na viwanda.

Mungu mbariki Magufuli!.

Mungu ibariki Tanzania.

Wasalaam.

Pasco
Rejea za shauri za bure
Ushauri wa Bure Kwa Lowassa: Kwa Vile ni Magufuli, Kubali Matokeo ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Hata kama ni kweli uliibiwa kura; Kaa ...
Ushauri wa Bure kwa CCM: Hope for the best but get prepared for ...
Ushauri wa Bure kwa Mhe. Lowassa: Ili kuilinda Heshima yako ...
Ushauri wa Bure kwa ZZK!-Congratulations..But,,,!, Be Calm!, Keep ...
Ushauri wa Bure Kwa Hon Dr. Harison Mwakyembe (Mb)-Kwa Hili la ...
Ushauri wa Bure Kwa Mhe. Zitto on Escrow Report: Please Keep Quite ...
Ushauri wa Bure kwa CHADEMA: Heri Nusu Shari Kuliko Shari Kamili ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Magufuli, Futilia Mbali Utawala wa Sheria ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Kikwete, muombe msamaha Lowassa kabla ya ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Usikanyage Arumeru!, Atamponza Sioi!.
Ushauri wa Bure kwa Dr. Shein: Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar ...
Ushauri wa Bure kwa Magufuli, DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es ...
Mimi napenda tuoneshe kuwa nguvu ya umma kamwe haijawahi kushindwa! Chadema tufanye mikutano kila kijiji. kila wilaya, kila mkoa na ngazi ya Taifa tena muda uleule halafu tuone itakavyo kuwa. Haiwezekani watu tulijinyima ili tumtoe Dikteta IDD AMINI halafu mwingine anakuja karne hii kuonesha udikteta wake! haiwezekani.
 
Ushauri mzuri
Chama cha siasa kama taasisi inayojitegemea shughuli zake nini?
Unajua kutofanya mikutano ya hadhara
na maandamano!watakuwa wamepoteza sifa ya kuitwa chama cha siasa?
Ila tu niseme ya kwamba huyo mheshimiwa akipiga marufuku chama tawala kutofanya shughul za kisia mpaka 2020.ni sawa kwa kuwa yeye ndiye mwenyekiti wa hicho chama ila kwa vyama vingine aviache kwani vina
Wenyeviti wao na wasemaji wao.

Na pia kila chama kina m/kiti taifa!
 
Ushauri mbaya huu maana wakifanya hivi, watakuwa wamefungua cycle ya violence ambayo hawataweza kuizima, kumbuka kule Soweto mauaji ya wale watoto waandamanaji yalivyofungua moto wa Resistance kwa nchi nzima.
Kinachotakiwa hapo ni Kutoa haki kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi.
Tuko kwenye the reign of terror nchi haiendeshwi tena kwa sheria na katiba bali kwa kauli na utashi wa rais, siku ile anawaambia polisi mkiwakamata majambazi malizaneni nao wasiinuke ,nitawapandisha vyeo, maadam ameishasema hataki na wala hapendi kujaribishiwa, ndio maana nawashauri jamaa zangu wasijaribu! . Kule Pemba Cuf ilisumbua sana lakini baada ya kuwafyatulia za moto na kuwazika faster kwa kuwatosa baharini mpaka leo hutakaa usikie tena CUF wanaandamana Pemba. Mwenye mamlaka ya nchi akisema hataki ni hataki, atakaye kaidi cha moto atakipata! .

Sisi waona mbali tumeishaiona nia ovu kwenye katazo lile, tumesema humu ili kila mwenye masikio asikie na mwenye macho aone! .

Pasco
 
Wacha kujifanya kutabiri jua wakati wa kiangazi
Tarehe 1 utaingia barabarani kamanda? Najua siku hiyo Mbowe atakuwa amepumzika Mikocheni na Lowassa kapumzika Masaki akisubiri kuona majeruhi kwenye TV au maiti hili wapate mtaji wa siasa.
 
Tarehe 1 utaingia barabarani kamanda? Najua siku hiyo Mbowe atakuwa amepumzika Mikocheni na Lowassa kapumzika Masaki akisubiri kuona majeruhi kwenye TV au maiti hili wapate mtaji wa siasa.
Tunashukuru kwa kutuwekea ukweli kuwa mmejiandaa kuwaua watu...asante sana Ritz
 
Tarehe 1 utaingia barabarani kamanda? Najua siku hiyo Mbowe atakuwa amepumzika Mikocheni na Lowassa kapumzika Masaki akisubiri kuona majeruhi kwenye TV au maiti hili wapate mtaji wa siasa.
Kuhusu kwenda tutaenda
ni lazma kuwa tayari kupamba
na namna yoyote ya uonevu,ukandamizaji.udhalilishaji
na uonevu.
 
Kuhusu kwenda tutaenda
ni lazma kuwa tayari kupamba
na namna yoyote ya uonevu,ukandamizaji.udhalilishaji
na uonevu.
Kamanda nakushauri ukiondoka nyumbani acha kabisa umeandika wosia kuna uwezekano usirudi au ukarudi miguu imevunjika. Huyu siyo JK huyu ni Magu.
 
Kamanda nakushauri ukiondoka nyumbani acha kabisa umeandika wosia kuna uwezekano usirudi au ukarudi miguu imevunjika. Huyu siyo JK huyu ni Magu.
Unamwogopa ww sisi siyo
Lelemama!kama yeye hajaribiwi
na sisi hatujaribu!na hatuogopi vitisho vyako wala vyake!
ina maana endapo tutakuwa tunaogopa
kila kitisho kuna hatari kubwa nchi yetu
kurudi kwenye utawala wa chama kimoja!ambayo si dalili nzuri kwa mutakabali wa nchi
 
WASWAHILI WALISEMA "UOGA NI ADUI WA HAKI"

Chadema wanatakiwa wajifunze misukosuko mbinu ambazo CUF wamepitia hadi wakafanikiwa kuingia katika serikali ya Zanzibar tena kikatiba (ijapokuwa kwa kipindi hichi hawamo)

CUF inao mtaji mzuri sana wa wapenzi na wanachama wake hasa linapokuja suala la kutetea haki yao, mara nyingi huwa hawarudi nyuma pindi wanapoamua kusimamia haki yao hasa viongozi wao wanapokuwa wako nyuma yao.

Ni vijana wa CUF ndio walioondoa kashfa ya vinyesi katika mashule, visima na masoko Pemba pale walipoweka mtego na kuwakamata Polisi na ndoo zao za mavi tayari kuharibu.

Ni vijana wa CUF ndio ambao walipambana kishujaa katika maandamno ya January 2001! Pamoja na athari zote zilizowapata lakini bado wakafanikiwa kugain kitu.

Hivyo basi vijana na wapenzi wa CHADEMA inabidi wasimame imara na kusapoti kwa vitendo kauli za viongozi wao.
 
Unajua kwa tanzania elimu ya siasa na uraia kuna mapungufu sana........
Kiukweli wapinzani pamoja na serikali wote wanamaeneo wanakosea pia wanapatia.........
Nikianza na wapinzani........hawa mlengo wa hoja zao zimekaa kukosoa serikali sio kwa lengo la kuijenga bali kuiharibia ili nao wapate ridhaa ya wananchi katika kuliongoza taifa.....hili si jambo zuri hata kidogo.......huu ni usanii kabisa....

Nitawapa mfano wa inshu ya sukari.........wabunge wengi wa upinzani walichachamaa sana kwa kuwaambia wananchi kuwa serikali haiwatakii mema kwa kuzia uagizaji wa sukari usio fuata taratibu za kisheria za biashara katika manunuzi........nakumbuka walituhadaa wananchi kuwa sukari haitokuja kushuka maana serikali inakosea......leo hapa mimi nipo kilimanjaro nimetoka kununua sukari kilo 1800. Tokea ilipokuwa 3000. Sasa najiuliza huwa wapinzani wakiongea wanatumia taarifa za wapi.......maana ni kama wanapotosha uma.........mimi naona ni kama wanaweka jitihada nyingi kubeza jitihada zinazofanywa na kupotosha uma wa watanzania.......na asilimia kubwa ya watanzania si wafuatiliahi huwa wanajiridhisha na story za kusadikika ama za mtaani au post za facebook ambazo huwa wanaozipost hawajulikani ni akina nani plus wanamalengo gani.......

Swala la elimu......wanabeza sana maamuzi ya kuweka vigezo ambavyo vitarejesha thamani ya elimu sio kama sasa kila mtu anadegree uchwara halafu uwezo zero kazi kupiga domo tu.....wapinzani wanakazana kuropoka tu ili wapate hii popularity kama ya akina wema na diamond kwa kuropoka.......

Me nasema mh.raisi yupo sahihi kukataza hizi kelele zisizo na tija yeyote ........hawa wapinzani si muda wote.wapo sahihi......wanayohaki ya kuikanya......kuirekebisha na kuikosoa serikali.......ila sio kwa staili hii wanavyofanya ya kuibeza na kuikejeli badala ya kuishauri.............wapinzani hawaongei jipya kazi yao ni kubeza .Unapomkosoa mtu......toa suggestion ......au wazo mbadala ila sio unangojea mwenzako akosee ndipo povu likutoke........tena unatoa kauli za kuhatarisha amani na usalama wa raia........

serikali ni kweli inakosea kuwazuia wapinzani kuongea na uma lakini ni kwasababu wamegundua mnaitumia fursa hiyo kuongea vijembe.....na kukejeli serikali ndio maana wanawabana kwa kila namna .......hata ningekuwa mimi nisingeruhusu mtu ambaye hauna ridhaa ya kuendesha nchi uongee maneno ya uchochezi badala ya kutoa ushauri.......hii kitu alishaifanyaga mbatia mara moja tu......aliishauri serikali kuhusu kuhamisha maofisi yao maeneo ya posta na kuyasambaza maeneo mengine ili kupunguza msongamano wa foleni za magari asubuhi watu wanapokwenda makazini maana msongamano huu unaitia serikali hasara kila siku ya mabilioni......na ndio maana kikwete akamkubali sana akampa nafasi ubunge viti maalumu.........mrema huyo hapo amepewa nafasi anashirikiana na serikali......huo ndio upinzani wa ukweli unatakiwa kuwa sio hawa wakina zitto wanakwenda kusoma vitabu na notes za shule wanakuja kutuletea theory za utabiri hapa.....wanaboa sana......
Umetoa maelezo mareeeeefu alafu pointless ndio zimejaa, unaweza ukajiona umeongea logic lakini asilimia kubwa ya hii insha uliotuandikia hapa ni uharo tu...

Labda nikuulize unawelewa nini maana ya upinzani?
Na nini faida na dhamira kuu ya vyama pinzani katika nchi yoyote ile?

Nijibu hapa kisha tuurefushe mjadala ufahamu na makosa yako!!

Na ulivyosema elimu ya kiraia/siasa Tanzania ina mapungufu sana hata ukukosea kwa sababu hata wewe mwenyewe kwa hichi ulichokiandika ni uthibitisho tosha wa kauli yako.
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"


Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!
pole sana,maybe wewe ndo uwe careful
 
Tuko kwenye the reign of terror nchi haiendeshwi tena kwa sheria na katiba bali kwa kauli na utashi wa rais, siku ile anawaambia polisi mkiwakamata majambazi malizaneni nao wasiinuke ,nitawapandisha vyeo, maadam ameishasema hataki na wala hapendi kujaribishiwa, ndio maana nawashauri jamaa zangu wasijaribu! . Kule Pemba Cuf ilisumbua sana lakini baada ya kuwafyatulia za moto na kuwazika faster kwa kuwatosa baharini mpaka leo hutakaa usikie tena CUF wanaandamana Pemba. Mwenye mamlaka ya nchi akisema hataki ni hataki, atakaye kaidi cha moto atakipata! .

Sisi waona mbali tumeishaiona nia ovu kwenye katazo lile, tumesema humu ili kila mwenye masikio asikie na mwenye macho aone! .

Pasco

Wewe naona hujui unaongea kitu gani bali unabwabwaja tu kufurahisha genge.

Wewe huwajui WAPEMBA zaidi ya unaowaona hapa wakifanya biashara.

Serikali zote mbili zinawafahamu vizuri wapemba ninani linapokuja kusimamia suala wanaloliamini, Kama CUF PEMBA hawatakaapo waandamane tena mbona serikali zote mbili zinawagwaya mno wakati Wapemba hata GOBORE hawana!!????

Ulikuwepo wapi wakati wa uchaguzi wa marudio pale serikali zote mbili zilipomimina Pemba Askari kwa maelfu huku wakisapotiwa na silaha nzito nzito zikiwamo gari za kivita!!!!???
25630ea45477c026e4423734caec8f40.jpg
25630ea45477c026e4423734caec8f40.jpg
downloadfile.jpeg

Hawa wote walikuwa njiani kuelekea Pemba na hiyo Gari ya kivita ikivinjari mitaa ya Pemba.

Unajua nikwanini serikali zote mbili ziliwagwaya wapemba wakati wa uchaguzi wa Marudiol!!??? Nikwasababu mara hii wapemba walikuwa na mbinu Mpya za kupambana na vyombo vya dola, msikilize Kijana hapa halafu uje na shombo zako juu ya wapemba.



Kumbuka hivi sasa WAPEMBA wako kimya nikwasababu wanawasikiliza viongozi wao wa juu waliotaka watulie ili wao wapapatue haki yao iliyodhulumiwa!! Wala hawako kimya eti kwa sababu niwaoga!!!!! Hilo haliko kwa Wapemba ambao dini yao inawakataza kumuogopa mtu kupita kiasi.
 
Naisikitikia serikali kwa kujiingiza katika confrontation zisizo za lazima, kwa sababu katiba na sheria za nchi zinaruhusu mikutano ya kisiasa ya chama chochote chenye usajili nchini kufanya mikutano ktk mikoa yote ya nchi!. Hili liko wazi na wala siyo hisani ya mtu yoyote kuguarantee haki hii

Sheria haijasema walioshinda peke yake ndo wafanye mikutano katika majimbo yao.

Kwa jinsi ninavyoona, iwapo Watu wataandamana na ikatokea nguvu kutumika hadi kupoteza maisha ya wananchi, basi kuna hatari watu kupelekwa katika vyombo vya kimataifa kama the Hague kujibu mashtaka, kwa maana wananchi hao wanadai kilicho haki kwa mujibu wa sheria za vyama vya siasa kuhusu haki ya kufanya mikutano!
Ninavyofahamu mimi hakuna mahali po pote ambako majeshi yanatumika kukandamiza wananchi yaliwahi kufanikiwa. Tayari majeshi ya nje yanaingia Burundi kwa kuwa tu Nkuruzinza aliamua kuvunja katiba. Je, sasa ana amani gani? Wananchi wa chama chake na wale wa upinzani wote wanakufa. Marafiki zake wanajeshi nao wanauawa. Furaha ya kutawala iko wapi? Kuna shida gani kufuata kanuni na sheria zinazotawala nchi? Ndugu zangu, VITA HAINA MACHO.
 
Tuko kwenye the reign of terror nchi haiendeshwi tena kwa sheria na katiba bali kwa kauli na utashi wa rais, siku ile anawaambia polisi mkiwakamata majambazi malizaneni nao wasiinuke ,nitawapandisha vyeo, maadam ameishasema hataki na wala hapendi kujaribishiwa, ndio maana nawashauri jamaa zangu wasijaribu! . Kule Pemba Cuf ilisumbua sana lakini baada ya kuwafyatulia za moto na kuwazika faster kwa kuwatosa baharini mpaka leo hutakaa usikie tena CUF wanaandamana Pemba. Mwenye mamlaka ya nchi akisema hataki ni hataki, atakaye kaidi cha moto atakipata! .

Sisi waona mbali tumeishaiona nia ovu kwenye katazo lile, tumesema humu ili kila mwenye masikio asikie na mwenye macho aone! .

Pasco
Sasa Pemba kuna amani? Sawa. Watu watakufa. Je, wenye kuua wenzao hawatakufa? Unadhani mtu akifa ndiyo mwisho wa maisha? Kama alikuwa muuaji ndipo mateso ya milele huanza. Maisha hapa duniani ni mafupi sana.
 
Ushauri wangu ni kwa Chadema kuachana na siasa za uanaharakati, the politics of confrontation, na badala yake wafanye real politics of development, Magufuli ni dikiteta mzalendo mwenye no sense ya busara zozote when it comes kwenye kumjaribu, Huyu ni mwenye nguvu akisema jambo fulani ni hapana na iwe hapana kweli hataki mchezo.

The right thing to do kwa Chadema ni kwenda mahakamani kuiomba mahakama kutoa tafsiri sahihi ya haki ya mikutano, freedom of lawful assembly, freedom of expression, na political activities hivyo kuonyesha tamko la rais ni batili na kinyume cha katiba na sheria lakini sio kumpinga rais kwa mikutano ya hadhara na matamko ya kutishana na kutunishiana misuli! .

Pasco

Wewe Pasco naona unazidi kuchafua hali ya hewa baada ya thread yako na sasa hii comment.

Huo ushauri unaojaribu kutoa hapa ni kutuletea habari za kijima, we unaona sawa tu watu watii kila agizo wanaloambiwa na wasichukue yoyote hata kama ni agizo la kipuuzi? huo ni utwana...

Unasema eti waende mahakamani kuomba tafsri sahihi ya sheria inayohusu maandamano.. hivi unaishi Tanzania wewe?

Mahakama gani hizo? hizi za kibongo ambazo zimewekwa mfukoni na CCM na hata sheria zenyewe zinatafsiriwa kuendana na matakwa ya watawala..!!?

Kama waliweza kufanya amendment ya sheria ya mita 200 hili kuendana na kauli ya raisi, watashindwa nini kutwambia safari hii tena kwa kiongozi huyu aliyopo kwamba "SHERIA INASEMA MAANDAMANO YOYOTE YALE NI KOSA LA JINAI"....?

leo hujawaza kabisa Pasco.
 
Pasco acha hahari zako wengine tunahamu ya kuvunja watu wewe unaleta sanaa za kuwapa ushauri sisi tutapata wapi watu wa kupiga? Acha waje tufanye kazi yetu tupate posho za kazi ya kutukuka.
Eeeh Mungu wa mbinguni msamehe kiumbe wako huyu hajui alisemalo! Amen
 
Back
Top Bottom