Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Wewe Pasco naona unazidi kuchafua hali ya hewa baada ya thread yako na sasa hii comment.

Huo ushauri unaojaribu kutoa hapa ni kutuletea habari za kijima, we unaona sawa tu watu watii kila agizo wanaloambiwa na wasichukue yoyote hata kama ni agizo la kipuuzi? huo ni utwana...

Unasema eti waende mahakamani kuomba tafsri sahihi ya sheria inayohusu maandamano.. hivi unaishi Tanzania wewe?

Mahakama gani hizo? hizi za kibongo ambazo zimewekwa mfukoni na CCM na hata sheria zenyewe zinatafsiriwa kuendana na matakwa ya watawala..!!?

Kama waliweza kufanya amendment ya sheria ya mita 200 hili kuendana na kauli ya raisi, watashindwa nini kutwambia safari hii tena kwa kiongozi huyu aliyopo kwamba "SHERIA INASEMA MAANDAMANO YOYOTE YALE NI KOSA LA JINAI"....?

leo hujawaza kabisa Pasco.
Huyu Pasco anajifanya chizi.
 
Wewe Pasco naona unazidi kuchafua hali ya hewa baada ya thread yako na sasa hii comment.

Huo ushauri unaojaribu kutoa hapa ni kutuletea habari za kijima, we unaona sawa tu watu watii kila agizo wanaloambiwa na wasichukue yoyote hata kama ni agizo la kipuuzi? huo ni utwana...

Unasema eti waende mahakamani kuomba tafsri sahihi ya sheria inayohusu maandamano.. hivi unaishi Tanzania wewe?

Mahakama gani hizo? hizi za kibongo ambazo zimewekwa mfukoni na CCM na hata sheria zenyewe zinatafsiriwa kuendana na matakwa ya watawala..!!?

Kama waliweza kufanya amendment ya sheria ya mita 200 hili kuendana na kauli ya raisi, watashindwa nini kutwambia safari hii tena kwa kiongozi huyu aliyopo kwamba "SHERIA INASEMA MAANDAMANO YOYOTE YALE NI KOSA LA JINAI"....?

leo hujawaza kabisa Pasco.

Mahakama ambazo MAJAJI NA MAHAKIMU wake wanachukua form za kugombea uongozi kupitia tiketi ya CCM pale wanapostaafu.

Refer Jaji Augostino Ramadhani na kuchukua form za kugombea kupitishwa ili awe mgombea wa CCM
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"


Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!
Maneno mazito sana haya ,nadhani hili ulilosema hapa halikua kwenye agenda ya kamati kuu ,wengi wetu tuna hasira kweli ila pia tujizuie na kutafakari kabla ya kusema ama kuandika jambo
 
Ushauri wangu ni kwa Chadema kuachana na siasa za uanaharakati, the politics of confrontation, na badala yake wafanye real politics of development, Magufuli ni dikiteta mzalendo mwenye no sense ya busara zozote when it comes kwenye kumjaribu, Huyu ni mwenye nguvu akisema jambo fulani ni hapana na iwe hapana kweli hataki mchezo.

The right thing to do kwa Chadema ni kwenda mahakamani kuiomba mahakama kutoa tafsiri sahihi ya haki ya mikutano, freedom of lawful assembly, freedom of expression, na political activities hivyo kuonyesha tamko la rais ni batili na kinyume cha katiba na sheria lakini sio kumpinga rais kwa mikutano ya hadhara na matamko ya kutishana na kutunishiana misuli! .

Pasco

Mkuu nyeusi ni nyeusi tu haiwezi kuonekana ni nyeupe hata siku moja ,unashauri watu waende Mahakamani huko huko unaposema kwa sasa pako chini ya boss anaeamua liwe na likawa..Mbona unajichanganya Mkuu.?.Hivi haki kwa vyama vya siasa kufanya siasa namna isiyopingaa na Katiba ni ya kuiombea tafsiri Mahakamani ?...
 
Chadema mbele kwa mbele dar arush mbeya tanga moshi shinyanga mwanza kagera geita wako tayar tunasonga mbele
 
Mkuu Sophist, kwanza nimefarijika sana kwa mchango wako kwa sababu wewe ndio mtu wa kwanza kuchangia kuhusu the separation of powers tena kwa kupangua hoja kwa hoja japo you are not right but you've tried.

Lengo la the principal of the separation of powers and checks and balance ni ili kuuzuia mhimili mmoja usijiinue kupitiliza. Bunge ni mtunga sheria, mahakama mfasiri na serikali mtekelezaji, serikali inapotunga a draconian law na Bunge likaipitisha Mahakama inauwezo wa kuifutilia mbali. Serikali ikitenda kwa kukiuka, kutokutenda au kukandamiza, mahakama kupitia powers zake inatoa executive orders, au writs za prohibition, certiorary na mandamus kuiamuru serikali itake isitake! .

Kitendo cha the executive kuingilia freedom of movement kwa mhimili ya Bunge na Mahakama ni kuingilia the independence ya mihimili hii.

Haki ya vyama vya siasa kukutana na kufanya mikutano ni haki iliyomo kwenye katiba, haki hii sio territorial lakini rais ameingilia haki hii kinyume cha katiba kama ilivyo rais hana mamlaka yoyote ya kupunguza mshahara wa mtumishi yoyote.

Rais Magufuli ametoa kauli kibao za uvunjaji wa katiba Bunge na Mahakama vinaangalia tuu.

Pale kunapotokea kauli za uvunjaji wa katiba au kinyume cha haki za binaadamu kama zilivyoainishwa kwenye katiba, Mahakama ina mamlaka ya ku act kwa mtindo unaoitwa act on suo motto, ni acting on it's own volition na kutoa tafsiri ya katiba ili maandishi nini bila hata kumsubiri yoyote kufungua shauri.

Bunge linapoona rais anatenda ndiyo sivyo lina mamlaka kujadili kauli za rais na kuzitolea azimio la Bunge.

Lakini hebu tusemezane ukweli, Jaji Chande na Spika Ndungai na Naibu Dr. Tulia ni watu wa kutengemewa kumfanyia checks Magufuli huku wengine wamefanywa kubebwa na wengine ni wastaafu siku nyingi wanaendelea na kazi kwa hisani tuu ya Magufuli.

Tanzania tunafuata mfumo wa presidential ambao rais ndio kila kitu, Bunge ni Butu na Mahakama ni Kibogoyo haina meno ya kuingata serikali, ndio maana nawashauri Chadema Mkuu wa the executive akisema hiki usifanye, hata kama wewe ndio mwenye haki, usifanye kwa sababu kauli hiyo ni final na conclusive! . Japo katiba yetu inasisitiza no one's is above the law, rais wetu is over and above the law! . Yeye ndio katiba, ndio Bunge, ndio mahakama na ndiye the law kubali kataa. Mtu wa namna hii akisema hapana ni hapana.

Pasco
Mkuu mada mezani ni kuwashauri CHADEMA mbona umekomalia urais wa dikteta wako na madaraka yanayomzidi kimo.
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"


Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!
[emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15]
 
Tusidharau Watanzania wanachoweza kukifanya!, Jamani tuheshimu sheria, kama Sheria zinaruhusu kufanyika kwa mikutano ya kisiasa basi haina budi kuheshimiwa.

Haina maana kuvunja nyumba zilizo katika hifadhi za barabara kwa kisingizio cha kufuata sheria lakini wakati huohuo hutaki kuiheshimu sheria inayosema kuwa vyama vya siasa vina haki ya kufanya mikutano ya kisiasa nchi nzima.

Tunapoapa kulinda katiba huku umeshika biblia au qur'an huku ukisema " eh Mwenyezi Mungu nisaidie" basi yapasa uwe mkweli wa nia na matendo!
 
Pasco wewe mwenyewe umekiri kwa maandishi yako kweli huyu Raisi dikteta kama unalitambua hilo kunyamaza kimya kunaweza kumpa nguvu kuendelea kuzidisha huo udikteta lazima zikafanyika juhudi za kupinga huo udikteta kwa nguvu zote zinaweza kuzaa mafanikio kiasi kikubwa sana.
Jana Chadema wametoa msimamo kupitia Naibu Katibu Mkuu Salimu Mwalimu maandamano yatafanyika kama yalivyopangwa na maandalizi nchi nzima yanaendelea . Maandamano yatafanyika kama yalivyopangwa
 
Pasco, kuna tatizo kubwa la kimantiki katika post yako. Ili kuona jinsi hoja yako isivyokidhi matakwa ya tafakuri ya kimantiki (logical reasoning), ione jinsi ilivyo katika mizania (syllogistic form): (1) Kitiba inaruhusu vyama vya siasa kufanya mikutano kwa uhuru; (2) Rais Magufuli amepiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa; na (3) Chadema wakae kimya! Kutokana na ulivyojenga hoja yako, hitimisho tu ambalo lingeifanya iwe na mantiki ni hili: "Magufuli amevunja katiba hivyo mamlaka husika (bunge) inapaswa kumchukulia hatua". Kwa upande mwingine, kama Chadema watafanya mikutano na madhara yakatokea, kwa kuzingatia kanuni ya causality (uhusiano wa kisababishi na matokeo), mkosaji (culprit) ni yule aliyekiuka matakwa ya katiba na siyo waliotetea na kulinda haki yao ya kikatiba. Kiuhalisia, umewashauri Chadema wawe wanafiki na wasiozingatia kanuni za kimaadili (unprincipled). "It is better to die with honour than to live with shame".
Shikamoo brother.. Hongera kwa kuandika nondo hiyo[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji111] [emoji111] [emoji111] [emoji111]
 
Kamanda nakushauri ukiondoka nyumbani acha kabisa umeandika wosia kuna uwezekano usirudi au ukarudi miguu imevunjika. Huyu siyo JK huyu ni Magu.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Pasco kuna tofauti kati ya kuandamana na kufanya mikutano. CHADEMA wamedhamiria kufamya mikutano na sio kuandamana!
Mkuu wewe mwenyewe ulimsikia Mwenyekiti wa Chadema, Mhe. Mbowe kwa masikio yako, au ulifanya ulihadithiwa tuu kuwa Mbowe kasema hiki na kile?!, kwa sababu kuna watu wana masikio lakini hawasikii, na kuna watu wana macho lakini hawaoni!.

Sasa kwa kukusaidia wewe na wengine ambao hamkubahatika kumsikia Mwenyekiti wa Chadema, alisema nini, nakuwekea video yake uiangalie na kumsikiliza kwa makini alisema nini, pia nakuwekea na clip ya mwenyenchi mwenyewe, amesema nini, na ni hii clip mkuu wa nchi, ndio imepelekea kunifanya mimi kuutoa ushauri huu kwa Chadema, cho chonde msiandamane, this man mean business!, he mean what he says and will practice what he preach!.

Pasco
 
Hivi tukiangalia hizi clip mbili alizoweka hapa Pasco, halafu tukawa wakweli kabisa na tukamuogopa Mungu kwa kusimama upande wa haki....ni nani kati yao anaitetea katiba ya nchi hii? Ni nani kati yao kwa dhati kabisa anataka wananchi watendewe haki?

Mababa na mababu zetu walisimama kidete kupinga kunyanyaswa na kudhulumiwa, japo hawakukosekana vibaraka walioshirikiana na wakoloni. Ndiyo kusema leo hii kuna hekima mpya imezuka ya kukubali na kuhalalisha watu kufanyiwa dhuluma na kubaguliwa na jamii yote kutakiwa kukaa kimya?!
 
Mkuu wewe mwenyewe ulimsikia Mwenyekiti wa Chadema, Mhe. Mbowe kwa masikio yako, au ulifanya ulihadithiwa tuu kuwa Mbowe kasema hiki na kile?!, kwa sababu kuna watu wana masikio lakini hawasikii, na kuna watu wana macho lakini hawaoni!.

Sasa kwa kukusaidia wewe na wengine ambao hamkubahatika kumsikia Mwenyekiti wa Chadema, alisema nini, nakuwekea video yake uiangalie na kumsikiliza kwa makini alisema nini, pia nakuwekea na clip ya mwenyenchi mwenyewe, amesema nini, na ni hii clip mkuu wa nchi, ndio imepelekea kunifanya mimi kuutoa ushauri huu kwa Chadema, cho chonde msiandamane, this man mean business!, he mean what he says and will practice what he preach!.

Pasco


Kati ya kauli ya mdomo na kauli ya maandishi ipi ina uzito?
 
Hivi tukiangalia hizi clip mbili alizoweka hapa Pasco, halafu tukawa wakweli kabisa na tukamuogopa Mungu kwa kusimama upande wa haki....ni nani kati yao anaitetea katiba ya nchi hii? Ni nani kati yao kwa dhati kabisa anataka wananchi watendewe haki?

Mababa na mababu zetu walisimama kidete kupinga kunyanyaswa na kudhulumiwa, japo hawakukosekana vibaraka walioshirikiana na wakoloni. Ndiyo kusema leo hii kuna hekima mpya imezuka ya kukubali na kuhalalisha watu kufanyiwa dhuluma na kubaguliwa na jamii yote kutakiwa kukaa kimya?!
Kwa mujibu wa hizo clips, mtetezi wa kweli wa katiba ni Mhe. Mbowe, anachofanya Rais Magufuli ni udikiteta tuu per se!, huu udikiteta Magufuli hakuuanza leo, tangu ameanza huu udikiteta, Chadema wamo kwenye chombo cha kumdhibiti, Bunge, badala ya kulitumia bunge ambacho ni chombo rasmi kumdhibiti rais, wenzetu walikuwa wanaenda na kutoka bila kuchangia chochote, mara wanaweka plasta midomoni na vituko hivi na vile, kimya chao, kimemfanya Magufuli kuiweka pembeni katiba, na kutawala kwa kauli na matamko na siku zote wamenyamaza!, japo katiba inaruhusu maandamano, lakini mwenye nchi amesema hataki maandamano, ushauri wangu ni watu wasiandamane, mwenye nguvu mpishe, huyu jamaa yuko serious kweli, wakiandamana, atawatandika kweli!.

Pasco
 
Back
Top Bottom